Tusiligeuze Taifa letu kuwa la wamachinga, huu ni mtego mbaya wa umaskini

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,339
45,659
Wiki hii na mwaka huu vimetia fora kuhusu habari za wamchinga. Bungeni wamejadiliwa, Ofisi namba moja imezungumza kuwahusu na leo Morogoro watu wametumbuliwa kwa sababu yao, RC wa Dar bado anagugumia na kiswahili kingi cha kuwapanga wasizibe mitaro iweze kufanyiwa usafi.

Hizi ni sehemu tu suala hili lilipopata nafasi sehemu ya mbele ya vyombo vya habari lakini kupo kwingi ambapo hapajaweza kumulikwa.

Kuzidi kushamiri kwa wamachinga na zaidi sana wakiwa wanauza bidhaa za Wachina ni dalali mbaya ya uchumi dhaifu na usio endelevu.
Wanapozidi kuongezeka wamachinga ndivyo ndoto za uchumi wa viwanda zinazikwa taratibu, ndivyo mifumo ya biashara rasmi inazidi kuparanganyika, ndivyo ukusanyaji wa kodi utakuwa mgumu zaidi na ndivyo mazingira ya miji yataharabiwa kabisa.

Ili nchi iwe na uchumi imara na endelevu sehemu kubwa ya raia nchi inahatajika wawe wanafanya kazi katika sekta za uzalishaji kama viwanda, madini, ujenzi na huduma kama utalii sio kuchuuza bidhaa hafifu za nchi nyingine barabarani na kuuza malighafi.

Watunga sera wanaolipwa kwa kodi za wananchi wanao wajibu mkubwa na wa haraka kulikwamua taifa kutoka katika mtego huu mbaya wa umaskini na uharibifu kwa taifa. Watimize wajibu wao kabla maji hayajakorogeka zaidi.
 
Wiki hii na mwaka huu vimetia fora kuhusu habari za wamchinga.Bungeni wamejadiliwa, Ofisi namba moja imezungumza kuwahusu na leo Morogoro watu wametumbuliwa kwa sababu yao, RC wa Dar bado anagugumia na kiswahili kingi cha kuwapanga wasizibe mitaro iweze kufanyiwa usafi.

Hizi ni sehemu tu suala hili lilipopata nafasi sehemu ya mbele ya vyombo vya habari lakini kupo kwingi ambapo hapajaweza kumulikwa.

Kuzidi kushamiri kwa wamachinga na zaidi sana wakiwa wanauza bidhaa za Wachina ni dalali mbaya ya uchumi dhaifu na usio endelevu.
Wanapozidi kuongezeka wamachinga ndivyo ndoto za uchumi wa viwanda zinazikwa taratibu, ndivyo mifumo ya biashara rasmi inazidi kuparanganyika, ndivyo ukusanyaji wa kodi utakuwa mgumu zaidi na ndivyo mazingira ya miji yataharabiwa kabisa.

Ili nchi iwe na uchumi imara na endelevu sehemu kubwa ya raia nchi inahatajika wawe wanafanya kazi katika sekta za uzalishaji kama viwanda, madini, ujenzi na huduma kama utalii sio kuchuuza bidhaa hafifu za nchi nyingine barabarani na kuuza malighafi.

Watunga sera wanaolipwa kwa kodi za wananchi wanao wajibu mkubwa na wa haraka kulikwamua taifa kutoka katika mtego huu mbaya wa umaskini na uharibifu kwa taifa. Watimize wajibu wao kabla maji hayajakorogeka zaidi.
Umeandika point mkuu

Mheshimiwa Makalla anaonesha kabisa alishaingia ubaridi kwenye hili suala la wamachinga, kifupi inaonesha kabisa hana maamuzi

Na hili lilitokea leo kwa viongozi wa Morogoro ndio kabisaaa litafifisha juhudi za kuwaondoa wamachinga.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Labda wabadilishwe jina wasiitwe ^wamachinga!!!^ Hilo jina lenyewe kisheria linawafungeni nyie vipapanuksi wa maendeleo ya taifa. Umaskini hauondoki kwa kuukana bali kuukabili kishujaa. Wanaolikataa kishabiki & kishamba jina la ^wanyonge,^ wakati obviously ^Watanzania zaidi ya milioni 14 wanaishi chini ya kiwango kisichokubalika cha umaskini^ (according to VP Dkt Mpango), wanapaswa kupimwa akili -- siyo kujua iwapo wana akili timamu -- bali kujua iwapo hata hiyo akili yenyewe wanayo ama la.
 
Labda wabadilishwe jina wasiitwe ^wamachinga!!!^ Hilo jina lenyewe kisheria linawafungeni nyie vipapanuksi wa maendeleo ya taifa. Umaskini hauondoki kwa kuukana bali kuukabili kishujaa. Wanaolikataa kishabiki & kishamba jina la ^wanyonge,^ wakati obviously ^Watanzania zaidi ya milioni 14 wanaishi chini ya kiwango kisichokubalika cha umaskini^ (according to VP Dkt Mpango), wanapaswa kupimwa akili -- siyo kujua iwapo wana akili timamu -- bali kujua iwapo hata hiyo akili yenyewe wanayo ama la.
Unajikuta sana kumbe ni hamnazo Mataga wewe.
 
Acha roho mbaya
Machinga ni mtu wa mhimu sana katika ujenzi wa taifa..

Wengi wao ni wale waliokosa ajira leo muanze kuwanyanyasa kweli? Hiyo haikubaliki kabisa..

Rais kaza kamba kwa viongozi wajinga wajinga wasio thamini machinga
 
Labda wabadilishwe jina wasiitwe ^wamachinga!!!^ Hilo jina lenyewe kisheria linawafungeni nyie vipapanuksi wa maendeleo ya taifa. Umaskini hauondoki kwa kuukana bali kuukabili kishujaa. Wanaolikataa kishabiki & kishamba jina la ^wanyonge,^ wakati obviously ^Watanzania zaidi ya milioni 14 wanaishi chini ya kiwango kisichokubalika cha umaskini^ (according to VP Dkt Mpango), wanapaswa kupimwa akili -- siyo kujua iwapo wana akili timamu -- bali kujua iwapo hata hiyo akili yenyewe wanayo ama la.
Aisee hizi Pumba huwa unazitowa wapi?
 
Labda wabadilishwe jina wasiitwe ^wamachinga!!!^ Hilo jina lenyewe kisheria linawafungeni nyie vipapanuksi wa maendeleo ya taifa. Umaskini hauondoki kwa kuukana bali kuukabili kishujaa. Wanaolikataa kishabiki & kishamba jina la ^wanyonge,^ wakati obviously ^Watanzania zaidi ya milioni 14 wanaishi chini ya kiwango kisichokubalika cha umaskini^ (according to VP Dkt Mpango), wanapaswa kupimwa akili -- siyo kujua iwapo wana akili timamu -- bali kujua iwapo hata hiyo akili yenyewe wanayo ama la.
Umechangia kama mwimba taarabu wa vichochoroni, hujui hata unaunga mkono au unapinga!! Zero brain
 
Umachinga uliokithiri, boda boda na mama ntilie hadi kwenye mitaro ni ishara ya udhaifu mkubwa katika uchumi kutoa fursa za kazi bora, rasmi na endelevu. Inawezekana kwenda kwenye uchuuzi na uzalishaji rasmi bila kupitia umachinga, wamachinga wengi pia hawafiki kwenye uchuuzi rasmi.
Wanahitajika machinga wanaolipa kodi. Machinga wanaoweza kuratibiwa ili waingie kwenye mfumo rasmi wa uchuuzi au uzalishaji
 
Hakuna taifa lililowahi kujengwa na wamachinga wanaouza bidhaa za Kichina na bodaboda, labda hili la kwetu ndio litakuwa la kwanza.
Acha roho mbaya
Machinga ni mtu wa mhimu sana katika ujenzi wa taifa..

Wengi wao ni wale waliokosa ajira leo muanze kuwanyanyasa kweli? Hiyo haikubaliki kabisa..

Rais kaza kamba kwa viongozi wajinga wajinga wasio thamini machinga
 
Umachinga uliokithiri, boda boda na mama ntilie hadi kwenye mitaro ni ishara ya udhaifu mkubwa katika uchumi kutoa fursa za kazi bora, rasmi na endelevu. Inawezekana kwenda kwenye uchuuzi na uzalishaji rasmi bila kupitia umachinga, wamachinga wengi pia hawafiki kwenye uchuuzi rasmi.
Uko sahihi ila kwangu mimi naona kama ni dalili chanya ya vijana kufanya kazi,kujituma na kupambana kujitafutia riziki. Jitihada zao ziratibiwe ili ziipatie kodi serekali na kuwarasimisha na kuwainua kimitaji ili taifa liwe na strong private sector itakayotoa ajira.
 
Umeandika point mkuu

Mheshimiwa makalla anaonesha kbsa alishaingia ubaridi kwenye hili suala la wamachinga, kifupi inaonesha kbsa hana maamuzi

Na hili lilitokea leo kwa viongozi wa morogoro ndio kbsaaa litafifisha juhudi za kuwaondoa wamachinga.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Mtaalam hata wewe ungekuwa wewe usingeingia? itabidi wabaki tu kama walivo utafanyaje
 
Wiki hii na mwaka huu vimetia fora kuhusu habari za wamchinga.Bungeni wamejadiliwa, Ofisi namba moja imezungumza kuwahusu na leo Morogoro watu wametumbuliwa kwa sababu yao, RC wa Dar bado anagugumia na kiswahili kingi cha kuwapanga wasizibe mitaro iweze kufanyiwa usafi.

Hizi ni sehemu tu suala hili lilipopata nafasi sehemu ya mbele ya vyombo vya habari lakini kupo kwingi ambapo hapajaweza kumulikwa.

Kuzidi kushamiri kwa wamachinga na zaidi sana wakiwa wanauza bidhaa za Wachina ni dalali mbaya ya uchumi dhaifu na usio endelevu.
Wanapozidi kuongezeka wamachinga ndivyo ndoto za uchumi wa viwanda zinazikwa taratibu, ndivyo mifumo ya biashara rasmi inazidi kuparanganyika, ndivyo ukusanyaji wa kodi utakuwa mgumu zaidi na ndivyo mazingira ya miji yataharabiwa kabisa.

Ili nchi iwe na uchumi imara na endelevu sehemu kubwa ya raia nchi inahatajika wawe wanafanya kazi katika sekta za uzalishaji kama viwanda, madini, ujenzi na huduma kama utalii sio kuchuuza bidhaa hafifu za nchi nyingine barabarani na kuuza malighafi.

Watunga sera wanaolipwa kwa kodi za wananchi wanao wajibu mkubwa na wa haraka kulikwamua taifa kutoka katika mtego huu mbaya wa umaskini na uharibifu kwa taifa. Watimize wajibu wao kabla maji hayajakorogeka zaidi.
Asante JF, kuna vitu navipata humu nisingeweza kuvipata popote
 
Back
Top Bottom