SoC01 Tusikifumbie Kiingereza kana kwamba huo ndiyo uzalendo

Stories of Change - 2021 Competition

cilla

JF-Expert Member
Jul 15, 2011
369
296
UTANGULIZI

Pamekuwa na mijadala na minong’ono mingi juu ya kuporomoka kwa uelewa wa lugha ya kiingereza. Tafiti mbalimbali zimefanywa na watu pamoja na taasisi mbalimbali zikionyesha kushuka kwa umahiri wa kuzaungumzwa kwa lugha ya kiingereza. Na sababu kubwa kabisa ambayo imekuwa ikitajwa ni msingi mbaya wa elimu katika kumfanya mtoto kuwa mahiri katika lugha hii maarufu duniani.

Sababu hii ya msingi mbaya wa lugha katika mfumo wetu wa elimu pia ndio sababu inayotajwa kusababisha wanafunzi wengi kufanya vibaya lakini pia kutumia muda mwingi kukariri kuliko kuelewa. Na kwasababu kukariri ni kwingi kuliko kuelewa matokeo yake tunapata wahitimu wasio na ujuzi unaokusudiwa.

Hii inaonyesha kuwa wanafunzi wengi wanaofanikiwa kufaulu kidato cha nne na sita haina maana kuwa wanauwezo sana kuliko waliofeli isipokuwa wengi hufaulu kutokana na uwezo mkubwa walionao wa kukariri na sio kuelewa.

Wanafunzi mwenye msingi mzuri walugha ya kiingereza hatumii nguvu kubwa sana katika kujisomea kwasababu anasoma kwa kuelewa na si kukariri.

Tusikikimbie kiingereza tuwe wazi na tukubali tumekosea tujirekebishe ikiwezekana tukope ujuzi kwa waliotuzidi.

MSINGI MBAYA WA LUGHA YA KIINGEREZA NI SABABU YA AFYA DUNI YA AKILI YA WATOTO WETU

Kitendo cha mwanafunzi kutoka shule ya msingi na kuingia sekondari hajui kiingereza huwasababisha wanafunzi wengi kuwa na msongo wa mawazo unaowasababishia afya duni ya akili .Unaweza kuona mwanafunzi kabla ya kuingia sekondari anajiamini, amechangamka lakini ghafla anapoingia sekondari anabadilika,kujiamini kunaondoka na baadhi huchukia shule kabisa na kukata tamaa.Walimu wanapoingia madarasani uchangamfu wa waanafunzi hupotea. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA CHANZO CHA WENGI KUKIMBIA MAARIFA.

Umuhimu wa lugha ya kiingereza upo katika kupata maarifa mbalimbali.Maarifa mbalimbali duniani yapo katika lugha ya kiingereza.Huwezi kuwa mahiri katika fani mbalimbali kama hujajizoeza kusoma na kutafuta maarifa katika dunia ya wanaotumia kiingereza.Chanzo kikuu cha wasomi wetu kushindwa kujinoa katika maarifa mbalimbali ,tatizo ni uwelewa mdogo wa lugha ya kiingereza kwasababu maarifa mengi yamefichwa kwenye kimombo ambacho leo hii tunashawishiwa tukiache libaki tu kama somo.Swali la kujiuliza ikiwa sasa tunasomo la kiingereza kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba lakini bado kiingereza kinatupiga chenga ? Vile vile tunajifunza masomo yote ya sekondari kwa kiingereza isipokuwa Kiswahili inakuwaje bado kiingereza ni tatizo kwa watoto wetu? Bilashaka kwa maswali haya mawili utagundua tatizo lipo katika msingi wa lugha yenyewe inayochangiwa na mfumo mbaya wa elimu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA UMETUFANYA TUSIJIAMINI KIMATAIFA

Pasipo kufahamu lugha kuu za kimataifa ni vigumu hata kufikiria kutafuta fursa nje ya nchi yako.Serikali inaposema itaongeza ajira kwa watanzania inapaswa kuangalia na uwezekano wa mtanzania kuajiriwa nje ya nchi yake anapokosa fursa hapa nchini.Kwasababu ya kutokujua vizuri lugha hii ya kimombo tumejikuta wengi tumejifungia hapa hapa ndani kwakukosa ujasiri wakutafuta ajira au fursa nje ya nchi yetu.Zinapotangazwa fursa mbalimbali ajira katika jumuya zetu kama EAC na SADC ni watanzania wachache sana wenye uthubutu wakuomba kwasababu tunajijua wenyewe shida ilipo.Kwa mfano hata kwenye fursa za kufundisha Kiswahili nje ya nchi bado kigezo namba moja uwe unauwezo wakuzungumza na kuandika kiingereza na wenzetu wakenya wanafaidi hiyo fursa kwasababu ya umahiri wao katika hiyo lugha. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

HALI YA KIINGEREZA KATIKA SHULE ZA SERIKALI

Walimu wanashindwa kuhusiana vizuri na wanafunzi wakati wa ufundishaji .Unakuta mwalimu anashindwa kuwashirikisha vizuri wanafunzi kwasababu akiuliza swali kwa kiingereza wachache ndio wanaojibu.Akiruhusu mwanafunzi aulize swali wachache ndio wanaouliza.Hali kama hii huondoa hari ya mwalimu kufundisha na kuwasaidia wanafunzi.Walimu wengi wanauliza maswali mengi ya kutaja(mention na definition) kuliko ya kujieleza wakati wa kufundisha kwasababu wanaelewa watoto wetu hawawezi kujieleza kwasababu ya uelewa mdogo wa lugha ya kiingereza.

Pia baadhi ya walimu wanachangamoto ya umahiri katika kutumia lugha ya kiingereza katika ufundishaji.Hatuwezi kushangaa kwa hilo kwasababu walimu ni zao la mfumo wetu wa elimu hii inayozalisha walimu.Kiingereza ni tatatizo hadi vyuo vikuu.Wahadhiri baadhi lugha kwao ni tatizo kama ilivyo kwa walimu katika shule zetu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

TAFITI ZINASEMA NINI?

Tafiti mbalimbali zilizofanywa nchini Tanzania (Mlama na Matteru, 1978; Mvungi 1982; Tume ya Rais, 1982, 1983; Criper na Dodd, 1984; Roy-Campbell na Qorro, 1987; Simmonds na wenzie, 1991; Kadeghe, 2000, 2003; Brock-Utne, 2004, 2005, 2007; Galabawa na Lwaitama, 2005; Galabawa na Senkoro, 2006; 2003, 2007; Qorro, 1999, 2005; Vuzo, 2002, 2005, 2007; kwa kutaja chache tu), zote zimebainisha kuwa kiwango cha ufahamu wa wanafunzi katika lugha ya Kiingereza kwa shule za sekondari nchini Tanzania ‘hakifai kabisa kwa ufundishaji na ujifunzaji wa masomo mengine...’ (yaani, kama lugha ya kufundishia) ‘... kiasi kwamba suala hili halina budi kushughulikiwa haraka’ (Criper na Dodd, 1984: 72).. Hali hii inaonyesha kwamba kuna haja ya kufanya mapitio ya tafiti muhimu katika eneo hili ili kupata uelewa wa jumla wa matokeo na mapendekezo ya tafiti mbalimbali; na kuangalia uzito wa njia mbalimbali zilizopendekezwa katika kutatua tatizo hili.

NAMNA YA KUKUZA KIINGEREZA

Kiingereza na lugha zingine za kimataifa bado ni ajira kwa vijana wetu hata kama ni kidato cha nne.Kupitia mitandao kama utube na kozi za online kijana anaweza kujifunza mambo mazuri na kujiajiri kama atakuwa anauelewa mzuri wa lugha ya kiingereza.Kijana ambaye amemaliza kidato cha nne na anajua lugha ya kiingereza vizuri ,si rahisi kumkuta hana ajira labda awe na matatizo yake mengine.Binafsi nazishukuru shule za michipuo ya kiingereza nazile za kibinafsi kwakufanya kazi kubwa yakuokoa jahazi kwasababu vinginevyo hali ingekuwa mbaya sana.

Serikali ifanye nini kutatua tatizo hili la vijana wetu kutojua vizuri lugha ya kiingereza.

  • Serikali ikiri bado tuna upungufu wa walimu wazuri wa lugha ya kiingereza. Ninaposikia serikali inadai ina walimu wa kutosha wa masomo ya sanaa binafsi huwa sikubaliani na jambo hilo kwasababu ni ukweli kwamba walimu ni wengi lakini umahiri katika kuzungumza kiingereza ni mdogo.Kwa hiyo serikaliinapaswa kuanza kuajiri walimu wa lugha ya kiingereza kwa kufanya usahili utakao zingatia uwezo wa mtu kimatamshi(pronunciation ) ,mtiririko katika kuzungumza(fluently) , misamiati inayoeleweka katika kuzungumza na kuandika pia.
  • Walimu wa masomo mengine ya sekondari isipokuwa kiswahili nao inafaa sana wakifanyiwa usahili kujua uwezo wao katika kufundisha kwa kutumia kiingereza.Mwalimu mwenyewe akiwa na kiingereza kizuri na rahisi wanafunzi kujifunza kwake kwa njia ya kusikia lakini kitawavutia pia wanafunzi kuongea kiiingereza tofauti na sasa ambapo baadhi ya walimu wanamatamshi yasiyovutia hata kumsikiliza lakini hawawezi kuongea kiingereza kwa kutiririka hata dakika moja.
  • Tukiona ni vigumu kuwapata walimu wenye sifa za kuongea kiingereza vizuri basis i vibaya tukiamua kuomba walimu kutoka mataifa mengine ambao wanaweza kufundisha na kuongea vizuri lugha ya kiingereza.
  • Tunaweza kubadilisha utaratibu.kwamba wanafunzi wasome mpaka darasa la sita alafu darasa la saba liwe darasa maalumu kwa mwanafunzi kujiandaa na sekondari ,kwamba kwa mwaka mzima atakuwa anajifunza kiingereza tu na serikali iajiri waalimu maalumu mahiri na wenye ujuzi wakufundisha kiingereza kuanzia chini (bigginners) na kuendelea.Serikali ijenge madarasa ya kisasa kama Lab za lugha ambayo inaweza ikawa na vifaa vya kujifunzia lugha kama computer zenye software au video maalumu kwaajili ya kufanyia mazoezi ya kusikia na kuongea kiingereza.
  • Tutafute waandishi wazuri au vitabu vizuri vya kujifunzia lugha ya kiingereza mashuleni tofauti na hivi vya sasa ambavyo vinaonekana ni vigumu kwa mtu anayeanza kujifunza lugha na hasa shule ya msingi kwasababu ya misamiati migumu na wakati mwingine mwanafunzi mwenyewe ni wa darasa la tatu au la nne.Kitabu kinapaswa kuwa na stori au hadithi chache na mazoezi mengi ya kuongea na kuandika kiingereza.
  • Changamoto ya mtaala wetu wa shule za msingi ni kujikita kwenye sheria nyingi za lugha.Wanafunzi wanakazaniwa sana kujua grammer,tenses,structure na wakati hata lugha ya kunywea maji hata hajaijua bado.Kwa nini tusijikite kwenye kumfundisha mwanafunzi kujua kuongea kiingereza hata kama ni broken English alafu madarasa ya juu ndipo aanze kujifunza namna ya mpangilio ,sarufi n.k?Lugha yoyote watu huanza kujifunza kwa kukosea kosea ndipo hufuata ya kujifunza sheria na kanuni ya lugha husika,
  • Watunga sera hawana budi kuchunguza upya malengo ya kufundisha lugha ya Kiingereza nchini Tanzania na kuyatofautisha na matumizi ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia. Wanapaswa kutangamanisha malengo hayo na sera ya lugha na mpango lugha ili sera na malengo hayo yaendane na ufundishaji madarasani
TUSIKITUPE KIINGEREZA KWA SABABU TUMESHINDWA KUKIFUNDISHA NA KUJIFICHA KWENYE UZALENDO WA LUGHA.
 
Kwa mfano hata kwenye fursa za kufundisha Kiswahili nje ya nchi bado kigezo namba moja uwe unauwezo wakuzungumza na kuandika kiingereza na wenzetu wakenya wanafaidi hiyo fursa kwasababu ya umahiri wao katika hiyo lugha.
Asanteee. Umenena mkuu 🙏
 
UTANGULIZI

Pamekuwa na mijadala na minong’ono mingi juu ya kuporomoka kwa uelewa wa lugha ya kiingereza. Tafiti mbalimbali zimefanywa na watu pamoja na taasisi mbalimbali zikionyesha kushuka kwa umahiri wa kuzaungumzwa kwa lugha ya kiingereza. Na sababu kubwa kabisa ambayo imekuwa ikitajwa ni msingi mbaya wa elimu katika kumfanya mtoto kuwa mahiri katika lugha hii maarufu duniani.

Sababu hii ya msingi mbaya wa lugha katika mfumo wetu wa elimu pia ndio sababu inayotajwa kusababisha wanafunzi wengi kufanya vibaya lakini pia kutumia muda mwingi kukariri kuliko kuelewa. Na kwasababu kukariri ni kwingi kuliko kuelewa matokeo yake tunapata wahitimu wasio na ujuzi unaokusudiwa.

Hii inaonyesha kuwa wanafunzi wengi wanaofanikiwa kufaulu kidato cha nne na sita haina maana kuwa wanauwezo sana kuliko waliofeli isipokuwa wengi hufaulu kutokana na uwezo mkubwa walionao wa kukariri na sio kuelewa.

Wanafunzi mwenye msingi mzuri walugha ya kiingereza hatumii nguvu kubwa sana katika kujisomea kwasababu anasoma kwa kuelewa na si kukariri.

Tusikikimbie kiingereza tuwe wazi na tukubali tumekosea tujirekebishe ikiwezekana tukope ujuzi kwa waliotuzidi.

MSINGI MBAYA WA LUGHA YA KIINGEREZA NI SABABU YA AFYA DUNI YA AKILI YA WATOTO WETU

Kitendo cha mwanafunzi kutoka shule ya msingi na kuingia sekondari hajui kiingereza huwasababisha wanafunzi wengi kuwa na msongo wa mawazo unaowasababishia afya duni ya akili .Unaweza kuona mwanafunzi kabla ya kuingia sekondari anajiamini, amechangamka lakini ghafla anapoingia sekondari anabadilika,kujiamini kunaondoka na baadhi huchukia shule kabisa na kukata tamaa.Walimu wanapoingia madarasani uchangamfu wa waanafunzi hupotea. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA CHANZO CHA WENGI KUKIMBIA MAARIFA.

Umuhimu wa lugha ya kiingereza upo katika kupata maarifa mbalimbali.Maarifa mbalimbali duniani yapo katika lugha ya kiingereza.Huwezi kuwa mahiri katika fani mbalimbali kama hujajizoeza kusoma na kutafuta maarifa katika dunia ya wanaotumia kiingereza.Chanzo kikuu cha wasomi wetu kushindwa kujinoa katika maarifa mbalimbali ,tatizo ni uwelewa mdogo wa lugha ya kiingereza kwasababu maarifa mengi yamefichwa kwenye kimombo ambacho leo hii tunashawishiwa tukiache libaki tu kama somo.Swali la kujiuliza ikiwa sasa tunasomo la kiingereza kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba lakini bado kiingereza kinatupiga chenga ? Vile vile tunajifunza masomo yote ya sekondari kwa kiingereza isipokuwa Kiswahili inakuwaje bado kiingereza ni tatizo kwa watoto wetu? Bilashaka kwa maswali haya mawili utagundua tatizo lipo katika msingi wa lugha yenyewe inayochangiwa na mfumo mbaya wa elimu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA UMETUFANYA TUSIJIAMINI KIMATAIFA

Pasipo kufahamu lugha kuu za kimataifa ni vigumu hata kufikiria kutafuta fursa nje ya nchi yako.Serikali inaposema itaongeza ajira kwa watanzania inapaswa kuangalia na uwezekano wa mtanzania kuajiriwa nje ya nchi yake anapokosa fursa hapa nchini.Kwasababu ya kutokujua vizuri lugha hii ya kimombo tumejikuta wengi tumejifungia hapa hapa ndani kwakukosa ujasiri wakutafuta ajira au fursa nje ya nchi yetu.Zinapotangazwa fursa mbalimbali ajira katika jumuya zetu kama EAC na SADC ni watanzania wachache sana wenye uthubutu wakuomba kwasababu tunajijua wenyewe shida ilipo.Kwa mfano hata kwenye fursa za kufundisha Kiswahili nje ya nchi bado kigezo namba moja uwe unauwezo wakuzungumza na kuandika kiingereza na wenzetu wakenya wanafaidi hiyo fursa kwasababu ya umahiri wao katika hiyo lugha. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

HALI YA KIINGEREZA KATIKA SHULE ZA SERIKALI

Walimu wanashindwa kuhusiana vizuri na wanafunzi wakati wa ufundishaji .Unakuta mwalimu anashindwa kuwashirikisha vizuri wanafunzi kwasababu akiuliza swali kwa kiingereza wachache ndio wanaojibu.Akiruhusu mwanafunzi aulize swali wachache ndio wanaouliza.Hali kama hii huondoa hari ya mwalimu kufundisha na kuwasaidia wanafunzi.Walimu wengi wanauliza maswali mengi ya kutaja(mention na definition) kuliko ya kujieleza wakati wa kufundisha kwasababu wanaelewa watoto wetu hawawezi kujieleza kwasababu ya uelewa mdogo wa lugha ya kiingereza.

Pia baadhi ya walimu wanachangamoto ya umahiri katika kutumia lugha ya kiingereza katika ufundishaji.Hatuwezi kushangaa kwa hilo kwasababu walimu ni zao la mfumo wetu wa elimu hii inayozalisha walimu.Kiingereza ni tatatizo hadi vyuo vikuu.Wahadhiri baadhi lugha kwao ni tatizo kama ilivyo kwa walimu katika shule zetu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

TAFITI ZINASEMA NINI?

Tafiti mbalimbali zilizofanywa nchini Tanzania (Mlama na Matteru, 1978; Mvungi 1982; Tume ya Rais, 1982, 1983; Criper na Dodd, 1984; Roy-Campbell na Qorro, 1987; Simmonds na wenzie, 1991; Kadeghe, 2000, 2003; Brock-Utne, 2004, 2005, 2007; Galabawa na Lwaitama, 2005; Galabawa na Senkoro, 2006; 2003, 2007; Qorro, 1999, 2005; Vuzo, 2002, 2005, 2007; kwa kutaja chache tu), zote zimebainisha kuwa kiwango cha ufahamu wa wanafunzi katika lugha ya Kiingereza kwa shule za sekondari nchini Tanzania ‘hakifai kabisa kwa ufundishaji na ujifunzaji wa masomo mengine...’ (yaani, kama lugha ya kufundishia) ‘... kiasi kwamba suala hili halina budi kushughulikiwa haraka’ (Criper na Dodd, 1984: 72).. Hali hii inaonyesha kwamba kuna haja ya kufanya mapitio ya tafiti muhimu katika eneo hili ili kupata uelewa wa jumla wa matokeo na mapendekezo ya tafiti mbalimbali; na kuangalia uzito wa njia mbalimbali zilizopendekezwa katika kutatua tatizo hili.

NAMNA YA KUKUZA KIINGEREZA

Kiingereza na lugha zingine za kimataifa bado ni ajira kwa vijana wetu hata kama ni kidato cha nne.Kupitia mitandao kama utube na kozi za online kijana anaweza kujifunza mambo mazuri na kujiajiri kama atakuwa anauelewa mzuri wa lugha ya kiingereza.Kijana ambaye amemaliza kidato cha nne na anajua lugha ya kiingereza vizuri ,si rahisi kumkuta hana ajira labda awe na matatizo yake mengine.Binafsi nazishukuru shule za michipuo ya kiingereza nazile za kibinafsi kwakufanya kazi kubwa yakuokoa jahazi kwasababu vinginevyo hali ingekuwa mbaya sana.

Serikali ifanye nini kutatua tatizo hili la vijana wetu kutojua vizuri lugha ya kiingereza.

  • Serikali ikiri bado tuna upungufu wa walimu wazuri wa lugha ya kiingereza. Ninaposikia serikali inadai ina walimu wa kutosha wa masomo ya sanaa binafsi huwa sikubaliani na jambo hilo kwasababu ni ukweli kwamba walimu ni wengi lakini umahiri katika kuzungumza kiingereza ni mdogo.Kwa hiyo serikaliinapaswa kuanza kuajiri walimu wa lugha ya kiingereza kwa kufanya usahili utakao zingatia uwezo wa mtu kimatamshi(pronunciation ) ,mtiririko katika kuzungumza(fluently) , misamiati inayoeleweka katika kuzungumza na kuandika pia.
  • Walimu wa masomo mengine ya sekondari isipokuwa kiswahili nao inafaa sana wakifanyiwa usahili kujua uwezo wao katika kufundisha kwa kutumia kiingereza.Mwalimu mwenyewe akiwa na kiingereza kizuri na rahisi wanafunzi kujifunza kwake kwa njia ya kusikia lakini kitawavutia pia wanafunzi kuongea kiiingereza tofauti na sasa ambapo baadhi ya walimu wanamatamshi yasiyovutia hata kumsikiliza lakini hawawezi kuongea kiingereza kwa kutiririka hata dakika moja.
  • Tukiona ni vigumu kuwapata walimu wenye sifa za kuongea kiingereza vizuri basis i vibaya tukiamua kuomba walimu kutoka mataifa mengine ambao wanaweza kufundisha na kuongea vizuri lugha ya kiingereza.
  • Tunaweza kubadilisha utaratibu.kwamba wanafunzi wasome mpaka darasa la sita alafu darasa la saba liwe darasa maalumu kwa mwanafunzi kujiandaa na sekondari ,kwamba kwa mwaka mzima atakuwa anajifunza kiingereza tu na serikali iajiri waalimu maalumu mahiri na wenye ujuzi wakufundisha kiingereza kuanzia chini (bigginners) na kuendelea.Serikali ijenge madarasa ya kisasa kama Lab za lugha ambayo inaweza ikawa na vifaa vya kujifunzia lugha kama computer zenye software au video maalumu kwaajili ya kufanyia mazoezi ya kusikia na kuongea kiingereza.
  • Tutafute waandishi wazuri au vitabu vizuri vya kujifunzia lugha ya kiingereza mashuleni tofauti na hivi vya sasa ambavyo vinaonekana ni vigumu kwa mtu anayeanza kujifunza lugha na hasa shule ya msingi kwasababu ya misamiati migumu na wakati mwingine mwanafunzi mwenyewe ni wa darasa la tatu au la nne.Kitabu kinapaswa kuwa na stori au hadithi chache na mazoezi mengi ya kuongea na kuandika kiingereza.
  • Changamoto ya mtaala wetu wa shule za msingi ni kujikita kwenye sheria nyingi za lugha.Wanafunzi wanakazaniwa sana kujua grammer,tenses,structure na wakati hata lugha ya kunywea maji hata hajaijua bado.Kwa nini tusijikite kwenye kumfundisha mwanafunzi kujua kuongea kiingereza hata kama ni broken English alafu madarasa ya juu ndipo aanze kujifunza namna ya mpangilio ,sarufi n.k?Lugha yoyote watu huanza kujifunza kwa kukosea kosea ndipo hufuata ya kujifunza sheria na kanuni ya lugha husika,
  • Watunga sera hawana budi kuchunguza upya malengo ya kufundisha lugha ya Kiingereza nchini Tanzania na kuyatofautisha na matumizi ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia. Wanapaswa kutangamanisha malengo hayo na sera ya lugha na mpango lugha ili sera na malengo hayo yaendane na ufundishaji madarasani
TUSIKITUPE KIINGEREZA KWA SABABU TUMESHINDWA KUKIFUNDISHA NA KUJIFICHA KWENYE UZALENDO WA LUGHA.
Kifupi, mwandishi ametoka nje ya "context". Mjadala wa matumizi ya Kiswahili kufundishia hauhusu uzalendo au la. Wala matumizi ya Kiswahili siyo kigezo cha uzalendo kama ambavyo matumizi ya Kiingereza siyo kigezo cha kutokuwa mzalendo.
Mjadala unahusu matumizi ya lugha ambayo itapandisha uelewa wa walengwa.
Mimi naamini matumizi ya lugha wanayotumia wanafunzi kila siku kufundishia inaongeza uelewa wa wanafunzi!
Mwandishi anaamini kwamba kuongeza uelewa katika Kiingereza ndiyo suluhisho la kuongeza uelewa kwa wanafunzi! Naamini lugha sahihi ya kufikisha uelewa kwa mlengwa ni ile anayoitumia kila siku! Wajerumani wanatumia lugha yao kufundishia na ndiyo uchumi mkubwa zaidi Ulaya. Kiingereza wanakijua pia. Finland wanaongoza duniani katika utoaji wa elimu bora, wanatumia lugha yao lakini Kiingereza au kichina wavizifahamu pia!
Tuache kuamini kwamba kujua Kiingereza ndiyo kuelimika!
Tuache kuamini kwamba kutumia Kiswahili ni dalili ya kutoendelea na kutumia Kiingereza ni kuelimika! Sana inatufanya "wasomi" kuwa mbali zaidi ya wananchi kwa kutumia lugha wasiyoielewa na kuwa karibu zaidi na nchi yenye lugha yake, bila kuwa karibu!
 
Kifupi, mwandishi ametoka nje ya "context". Mjadala wa matumizi ya Kiswahili kufundishia hauhusu uzalendo au la. Wala matumizi ya Kiswahili siyo kigezo cha uzalendo kama ambavyo matumizi ya Kiingereza siyo kigezo cha kutokuwa mzalendo.
Mjadala unahusu matumizi ya lugha ambayo itapandisha uelewa wa walengwa.
Mimi naamini matumizi ya lugha wanayotumia wanafunzi kila siku kufundishia inaongeza uelewa wa wanafunzi!
Mwandishi anaamini kwamba kuongeza uelewa katika Kiingereza ndiyo suluhisho la kuongeza uelewa kwa wanafunzi! Naamini lugha sahihi ya kufikisha uelewa kwa mlengwa ni ile anayoitumia kila siku! Wajerumani wanatumia lugha yao kufundishia na ndiyo uchumi mkubwa zaidi Ulaya. Kiingereza wanakijua pia. Finland wanaongoza duniani katika utoaji wa elimu bora, wanatumia lugha yao lakini Kiingereza au kichina wavizifahamu pia!
Tuache kuamini kwamba kujua Kiingereza ndiyo kuelimika!
Tuache kuamini kwamba kutumia Kiswahili ni dalili ya kutoendelea na kutumia Kiingereza ni kuelimika! Sana inatufanya "wasomi" kuwa mbali zaidi ya wananchi kwa kutumia lugha wasiyoielewa na kuwa karibu zaidi na nchi yenye lugha yake, bila kuwa karibu!
NAFIKIRI HUJASOMA VIZURI.NAOMBA URUDIE KUSOMA UPYA .ASANTE
 
Ahsante mkuu nimegundua kwa nini baadhi ya vijana huchanganyikiwa na kuvurunda kwenye masomo ilhali hapo mwanzoni walikuwa ni wazuri tu katika elimu, kumbe mabadiliko ya lugha yanawapa wakati mgumu sana.
 
Tunapaswa kutumia Kiswahili kufundishia masomo yote kwa ngazi zote za elimu. Sio kwa sababu kutumia Kiswahili ni uzalaendo bali ni kwa sababu ndio njia bora zaidi ya kufikia malengo ya elimu.

Haya sio tu maoni yangu bali ni ukweli wa kisayansi na kitafiti. Kwa hiyo advocates wa Kiingereza watakiwa kutupatia matokeo ya kitafiti yakionesha kwamba, kwa mazingira ya nchi yetu, watu wataelimika zaidi wakitumia Kiingereza kuliko Kiswahili.

Naomba pia niseme kuwa ufundishaji wa Kiingereza kama somo hauepukiki. Tunapaswa kubadilisha namna ya kufundisha Kiingereza. Tuhame kutoka kwenye kuweka mkazo kwenye technicalities na tuweke mkazo kwenye umahiri wa kusoma na kukizungumza kiingereza, maarifa ambayo Watanzania wengi ndio haswa wanahitaji.

Tusidumaze taifa letu kwa kung'ang'ania nguo ya kuazima wakati ya kutusitiri ipo.
 
Kifupi, mwandishi ametoka nje ya "context". Mjadala wa matumizi ya Kiswahili kufundishia hauhusu uzalendo au la. Wala matumizi ya Kiswahili siyo kigezo cha uzalendo kama ambavyo matumizi ya Kiingereza siyo kigezo cha kutokuwa mzalendo.
Mjadala unahusu matumizi ya lugha ambayo itapandisha uelewa wa walengwa.
Mimi naamini matumizi ya lugha wanayotumia wanafunzi kila siku kufundishia inaongeza uelewa wa wanafunzi!
Mwandishi anaamini kwamba kuongeza uelewa katika Kiingereza ndiyo suluhisho la kuongeza uelewa kwa wanafunzi! Naamini lugha sahihi ya kufikisha uelewa kwa mlengwa ni ile anayoitumia kila siku! Wajerumani wanatumia lugha yao kufundishia na ndiyo uchumi mkubwa zaidi Ulaya. Kiingereza wanakijua pia. Finland wanaongoza duniani katika utoaji wa elimu bora, wanatumia lugha yao lakini Kiingereza au kichina wavizifahamu pia!
Tuache kuamini kwamba kujua Kiingereza ndiyo kuelimika!
Tuache kuamini kwamba kutumia Kiswahili ni dalili ya kutoendelea na kutumia Kiingereza ni kuelimika! Sana inatufanya "wasomi" kuwa mbali zaidi ya wananchi kwa kutumia lugha wasiyoielewa na kuwa karibu zaidi na nchi yenye lugha yake, bila kuwa karibu!
kenge kwenye mamba

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
UTANGULIZI

Pamekuwa na mijadala na minong’ono mingi juu ya kuporomoka kwa uelewa wa lugha ya kiingereza. Tafiti mbalimbali zimefanywa na watu pamoja na taasisi mbalimbali zikionyesha kushuka kwa umahiri wa kuzaungumzwa kwa lugha ya kiingereza. Na sababu kubwa kabisa ambayo imekuwa ikitajwa ni msingi mbaya wa elimu katika kumfanya mtoto kuwa mahiri katika lugha hii maarufu duniani.

Sababu hii ya msingi mbaya wa lugha katika mfumo wetu wa elimu pia ndio sababu inayotajwa kusababisha wanafunzi wengi kufanya vibaya lakini pia kutumia muda mwingi kukariri kuliko kuelewa. Na kwasababu kukariri ni kwingi kuliko kuelewa matokeo yake tunapata wahitimu wasio na ujuzi unaokusudiwa.

Hii inaonyesha kuwa wanafunzi wengi wanaofanikiwa kufaulu kidato cha nne na sita haina maana kuwa wanauwezo sana kuliko waliofeli isipokuwa wengi hufaulu kutokana na uwezo mkubwa walionao wa kukariri na sio kuelewa.

Wanafunzi mwenye msingi mzuri walugha ya kiingereza hatumii nguvu kubwa sana katika kujisomea kwasababu anasoma kwa kuelewa na si kukariri.

Tusikikimbie kiingereza tuwe wazi na tukubali tumekosea tujirekebishe ikiwezekana tukope ujuzi kwa waliotuzidi.

MSINGI MBAYA WA LUGHA YA KIINGEREZA NI SABABU YA AFYA DUNI YA AKILI YA WATOTO WETU

Kitendo cha mwanafunzi kutoka shule ya msingi na kuingia sekondari hajui kiingereza huwasababisha wanafunzi wengi kuwa na msongo wa mawazo unaowasababishia afya duni ya akili .Unaweza kuona mwanafunzi kabla ya kuingia sekondari anajiamini, amechangamka lakini ghafla anapoingia sekondari anabadilika,kujiamini kunaondoka na baadhi huchukia shule kabisa na kukata tamaa.Walimu wanapoingia madarasani uchangamfu wa waanafunzi hupotea. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA CHANZO CHA WENGI KUKIMBIA MAARIFA.

Umuhimu wa lugha ya kiingereza upo katika kupata maarifa mbalimbali.Maarifa mbalimbali duniani yapo katika lugha ya kiingereza.Huwezi kuwa mahiri katika fani mbalimbali kama hujajizoeza kusoma na kutafuta maarifa katika dunia ya wanaotumia kiingereza.Chanzo kikuu cha wasomi wetu kushindwa kujinoa katika maarifa mbalimbali ,tatizo ni uwelewa mdogo wa lugha ya kiingereza kwasababu maarifa mengi yamefichwa kwenye kimombo ambacho leo hii tunashawishiwa tukiache libaki tu kama somo.Swali la kujiuliza ikiwa sasa tunasomo la kiingereza kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba lakini bado kiingereza kinatupiga chenga ? Vile vile tunajifunza masomo yote ya sekondari kwa kiingereza isipokuwa Kiswahili inakuwaje bado kiingereza ni tatizo kwa watoto wetu? Bilashaka kwa maswali haya mawili utagundua tatizo lipo katika msingi wa lugha yenyewe inayochangiwa na mfumo mbaya wa elimu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

UWEZO MDOGO WA LUGHA YA KIINGEREZA UMETUFANYA TUSIJIAMINI KIMATAIFA

Pasipo kufahamu lugha kuu za kimataifa ni vigumu hata kufikiria kutafuta fursa nje ya nchi yako.Serikali inaposema itaongeza ajira kwa watanzania inapaswa kuangalia na uwezekano wa mtanzania kuajiriwa nje ya nchi yake anapokosa fursa hapa nchini.Kwasababu ya kutokujua vizuri lugha hii ya kimombo tumejikuta wengi tumejifungia hapa hapa ndani kwakukosa ujasiri wakutafuta ajira au fursa nje ya nchi yetu.Zinapotangazwa fursa mbalimbali ajira katika jumuya zetu kama EAC na SADC ni watanzania wachache sana wenye uthubutu wakuomba kwasababu tunajijua wenyewe shida ilipo.Kwa mfano hata kwenye fursa za kufundisha Kiswahili nje ya nchi bado kigezo namba moja uwe unauwezo wakuzungumza na kuandika kiingereza na wenzetu wakenya wanafaidi hiyo fursa kwasababu ya umahiri wao katika hiyo lugha. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

HALI YA KIINGEREZA KATIKA SHULE ZA SERIKALI

Walimu wanashindwa kuhusiana vizuri na wanafunzi wakati wa ufundishaji .Unakuta mwalimu anashindwa kuwashirikisha vizuri wanafunzi kwasababu akiuliza swali kwa kiingereza wachache ndio wanaojibu.Akiruhusu mwanafunzi aulize swali wachache ndio wanaouliza.Hali kama hii huondoa hari ya mwalimu kufundisha na kuwasaidia wanafunzi.Walimu wengi wanauliza maswali mengi ya kutaja(mention na definition) kuliko ya kujieleza wakati wa kufundisha kwasababu wanaelewa watoto wetu hawawezi kujieleza kwasababu ya uelewa mdogo wa lugha ya kiingereza.

Pia baadhi ya walimu wanachangamoto ya umahiri katika kutumia lugha ya kiingereza katika ufundishaji.Hatuwezi kushangaa kwa hilo kwasababu walimu ni zao la mfumo wetu wa elimu hii inayozalisha walimu.Kiingereza ni tatatizo hadi vyuo vikuu.Wahadhiri baadhi lugha kwao ni tatizo kama ilivyo kwa walimu katika shule zetu. Tusione haya kukubali kuwa kiingereza kimetuacha,Tusifumbe macho kwakukwepa wajibu wetu na kujificha kwenye uzalendo .

TAFITI ZINASEMA NINI?

Tafiti mbalimbali zilizofanywa nchini Tanzania (Mlama na Matteru, 1978; Mvungi 1982; Tume ya Rais, 1982, 1983; Criper na Dodd, 1984; Roy-Campbell na Qorro, 1987; Simmonds na wenzie, 1991; Kadeghe, 2000, 2003; Brock-Utne, 2004, 2005, 2007; Galabawa na Lwaitama, 2005; Galabawa na Senkoro, 2006; 2003, 2007; Qorro, 1999, 2005; Vuzo, 2002, 2005, 2007; kwa kutaja chache tu), zote zimebainisha kuwa kiwango cha ufahamu wa wanafunzi katika lugha ya Kiingereza kwa shule za sekondari nchini Tanzania ‘hakifai kabisa kwa ufundishaji na ujifunzaji wa masomo mengine...’ (yaani, kama lugha ya kufundishia) ‘... kiasi kwamba suala hili halina budi kushughulikiwa haraka’ (Criper na Dodd, 1984: 72).. Hali hii inaonyesha kwamba kuna haja ya kufanya mapitio ya tafiti muhimu katika eneo hili ili kupata uelewa wa jumla wa matokeo na mapendekezo ya tafiti mbalimbali; na kuangalia uzito wa njia mbalimbali zilizopendekezwa katika kutatua tatizo hili.

NAMNA YA KUKUZA KIINGEREZA

Kiingereza na lugha zingine za kimataifa bado ni ajira kwa vijana wetu hata kama ni kidato cha nne.Kupitia mitandao kama utube na kozi za online kijana anaweza kujifunza mambo mazuri na kujiajiri kama atakuwa anauelewa mzuri wa lugha ya kiingereza.Kijana ambaye amemaliza kidato cha nne na anajua lugha ya kiingereza vizuri ,si rahisi kumkuta hana ajira labda awe na matatizo yake mengine.Binafsi nazishukuru shule za michipuo ya kiingereza nazile za kibinafsi kwakufanya kazi kubwa yakuokoa jahazi kwasababu vinginevyo hali ingekuwa mbaya sana.

Serikali ifanye nini kutatua tatizo hili la vijana wetu kutojua vizuri lugha ya kiingereza.

  • Serikali ikiri bado tuna upungufu wa walimu wazuri wa lugha ya kiingereza. Ninaposikia serikali inadai ina walimu wa kutosha wa masomo ya sanaa binafsi huwa sikubaliani na jambo hilo kwasababu ni ukweli kwamba walimu ni wengi lakini umahiri katika kuzungumza kiingereza ni mdogo.Kwa hiyo serikaliinapaswa kuanza kuajiri walimu wa lugha ya kiingereza kwa kufanya usahili utakao zingatia uwezo wa mtu kimatamshi(pronunciation ) ,mtiririko katika kuzungumza(fluently) , misamiati inayoeleweka katika kuzungumza na kuandika pia.
  • Walimu wa masomo mengine ya sekondari isipokuwa kiswahili nao inafaa sana wakifanyiwa usahili kujua uwezo wao katika kufundisha kwa kutumia kiingereza.Mwalimu mwenyewe akiwa na kiingereza kizuri na rahisi wanafunzi kujifunza kwake kwa njia ya kusikia lakini kitawavutia pia wanafunzi kuongea kiiingereza tofauti na sasa ambapo baadhi ya walimu wanamatamshi yasiyovutia hata kumsikiliza lakini hawawezi kuongea kiingereza kwa kutiririka hata dakika moja.
  • Tukiona ni vigumu kuwapata walimu wenye sifa za kuongea kiingereza vizuri basis i vibaya tukiamua kuomba walimu kutoka mataifa mengine ambao wanaweza kufundisha na kuongea vizuri lugha ya kiingereza.
  • Tunaweza kubadilisha utaratibu.kwamba wanafunzi wasome mpaka darasa la sita alafu darasa la saba liwe darasa maalumu kwa mwanafunzi kujiandaa na sekondari ,kwamba kwa mwaka mzima atakuwa anajifunza kiingereza tu na serikali iajiri waalimu maalumu mahiri na wenye ujuzi wakufundisha kiingereza kuanzia chini (bigginners) na kuendelea.Serikali ijenge madarasa ya kisasa kama Lab za lugha ambayo inaweza ikawa na vifaa vya kujifunzia lugha kama computer zenye software au video maalumu kwaajili ya kufanyia mazoezi ya kusikia na kuongea kiingereza.
  • Tutafute waandishi wazuri au vitabu vizuri vya kujifunzia lugha ya kiingereza mashuleni tofauti na hivi vya sasa ambavyo vinaonekana ni vigumu kwa mtu anayeanza kujifunza lugha na hasa shule ya msingi kwasababu ya misamiati migumu na wakati mwingine mwanafunzi mwenyewe ni wa darasa la tatu au la nne.Kitabu kinapaswa kuwa na stori au hadithi chache na mazoezi mengi ya kuongea na kuandika kiingereza.
  • Changamoto ya mtaala wetu wa shule za msingi ni kujikita kwenye sheria nyingi za lugha.Wanafunzi wanakazaniwa sana kujua grammer,tenses,structure na wakati hata lugha ya kunywea maji hata hajaijua bado.Kwa nini tusijikite kwenye kumfundisha mwanafunzi kujua kuongea kiingereza hata kama ni broken English alafu madarasa ya juu ndipo aanze kujifunza namna ya mpangilio ,sarufi n.k?Lugha yoyote watu huanza kujifunza kwa kukosea kosea ndipo hufuata ya kujifunza sheria na kanuni ya lugha husika,
  • Watunga sera hawana budi kuchunguza upya malengo ya kufundisha lugha ya Kiingereza nchini Tanzania na kuyatofautisha na matumizi ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia. Wanapaswa kutangamanisha malengo hayo na sera ya lugha na mpango lugha ili sera na malengo hayo yaendane na ufundishaji madarasani
TUSIKITUPE KIINGEREZA KWA SABABU TUMESHINDWA KUKIFUNDISHA NA KUJIFICHA KWENYE UZALENDO WA LUGHA.
Kinadharia,hoja ya kujikita zaidi kujenga lugha yetu ya Kiswahili,ilikuwa nzuri lakini utafiti ulifanyika Kwa kiwango gani kwamba Kiswahili kitatusaidia?
Ukiacha oxygen ambayo tunaipata Kwa Neema ya Mungu,Sisi hatuna kingine tunaweza kufanya bila kuwategemea wazungu na kiingereza chao.sasa mtu anapojikita kwenye hoja ya kujikita kwenye kuimarisha Kiswahili,ni unafiki tu.
Sasa angalia,madaktari,mainjinia,wanasheria,na wana sayansi wote, kama huna kiingereza hutoboi. kiingereza ni lugha ya dunia tangu kabla ya Uhuru,halafu Leo Kwa kuwa tumeshindwa kujifundisha kiingereza,tunajifanya kutaka kuendeleza kiswahili,ambacho nacho kinatusumbua utadhani lugha ya kimila.kuna kizazi kinakuja baada ya hiki kitakuja upya juu ya lugha ya kiingereza na mtazamo chanya.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Kinadharia,hoja ya kujikita zaidi kujenga lugha yetu ya Kiswahili,ilikuwa nzuri lakini utafiti ulifanyika Kwa kiwango gani kwamba Kiswahili kitatusaidia?
Ukiacha oxygen ambayo tunaipata Kwa Neema ya Mungu,Sisi hatuna kingine tunaweza kufanya bila kuwategemea wazungu na kiingereza chao.sasa mtu anapojikita kwenye hoja ya kujikita kwenye kuimarisha Kiswahili,ni unafiki tu.
Sasa angalia,madaktari,mainjinia,wanasheria,na wana sayansi wote, kama huna kiingereza hutoboi. kiingereza ni lugha ya dunia tangu kabla ya Uhuru,halafu Leo Kwa kuwa tumeshindwa kujifundisha kiingereza,tunajifanya kutaka kuendeleza kiswahili,ambacho nacho kinatusumbua utadhani lugha ya kimila.kuna kizazi kinakuja baada ya hiki kitakuja upya juu ya lugha ya kiingereza na mtazamo chanya.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Mkuu umekosea sana. Suala la lugha limefanyiwa tafiti sana na Kiswahili ndio kinafaa kutumika kufundishia kwa mazingira ya Tanzania. Tena tafiti zimefanyika tangu miaka ya 70 huko hadi miaka ya karibuni na papers zipo kibao unaweza kuzigoogle.

Kosa kubwa wanalofanya watu wengi wanaoongelea hili suala ni kutokusema the extent at which hili jambo limesomwa. Suala la Kiswahili sio suala la kukiendeleza, sio la uzalendo na wala sio mapenzi ya Kiswahili. Hili ni suala la uhitaji, kama tunataka elimu itakayoboresha viwango vya maisha yetu na kuwafikia watanzania wengi, wenye nacho na wasio nacho, lazima tutumie Kiswahili.

Wachina, Wakorea, Wajapan, Waindonesia na wengine walianza kutumia lugha zao hata walivyokuwa masikini. Hoja ya kuwa hatuwezi kuelimika na kujikwamua bila Kiingereza ni hoja dhaifu.
 
Asanteee. Umenena mkuu
Sasa mkuu tufanyeje, sina uwezo wa kumpeleka mtoto english media akajue chiingereza, atasomea kayumba hizi hisi, mimi kila siku najifunza kiingereza na kimenisaidia kusoma mavitabu makubwa makubwa ya kiingereza yenye maarifa adimu. Nafikiri kujifunza kiingereza ni nia na akili ya mtu. Unaweza peleka mtoto huko english media na mtoto akawa zuzu tu
 
Back
Top Bottom