share
JF-Expert Member
- Nov 22, 2008
- 6,062
- 10,459
Tangu aanze kampeni mikutano ya hadhara ya Mhe. Lissu inajaza watu wenye hamasa kila kona. Wananchi wanakuja wenyewe kwa maelfu huku kukiwa hakuna matumbuizo ya wasanii, wanamuziki, wachekeshaji, wala ubebaji wa watu kwa malori kutoka sehemu nyingine.
Hii inaashiria kukubalika kwake. Ana mvuto wa kikarisma. Isitoshe, anachozungumza ni madini tupu yanayogusa ubongo na uhalisia. Haijawahi kutokea katika kampeni za urais nchi hii chini ya siasa za vyama vingi.
Historia yake pia ni ya kipekee. Kuna kitu Mungu anataka kuifundisha Tanzania. Tusikaze migumu mioyo yetu.
Hii inaashiria kukubalika kwake. Ana mvuto wa kikarisma. Isitoshe, anachozungumza ni madini tupu yanayogusa ubongo na uhalisia. Haijawahi kutokea katika kampeni za urais nchi hii chini ya siasa za vyama vingi.
Historia yake pia ni ya kipekee. Kuna kitu Mungu anataka kuifundisha Tanzania. Tusikaze migumu mioyo yetu.