Tusijidanganye kutatua tatizo la uchumi na ajira bila kuhakikisha walau 70% ya bidhaa tunazozitumia tunazalisha wenyewe

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,820
Siku hizi imekuwa kama sifa kumsikia Mtu akijinadi kuwa yeye ni bingwa wa kuagiza bidhaa kutoka China au sehemu nyingine ya Dunia.

Kwa vyovyote Mtu kama huyu hawezi kufurahi akisikia mipango yoyote ya Nchi kutengeneza bidhaa zake yenyewe, na atafanya kila linalowezekana kuhujumu juhudi kama hizo.

Kama nchi ni lazima kuwe na mikakati mahsusi kuhakikisha nasi tunakuwa Watengenezaji maana ni hakika nguvu ya kupinga inaweza kuzidi nguvu ya kutekeleza.

Inasikitisha ukipita Mtaani unakuta 99% ya bidhaa alizobeba Mmachinga ni bidhaa kutoka nje ya nchi.

Hivi kweli bidhaa kama Soksi, Nguo za ndani, mikanda ya kiunoni, vifaa vya usafi n.k vyote ni mpaka tutengenezewe na Wengine?

Mbali na kutatua tatizo la ajira na uchumi pia ni heshima kwa nchi kama tukijitengenezea bidhaa zetu wenyewe.
 
Tanzania kuna mbao za mninga lakini watu wanaenda madukani kununua vitanda na makabati ya vumbi ya mbao kutoka china,
baada ya mwaka vitanda vimevunjika.
Waafrika IQ ndogo sana huwezi kuwabadiisha bali wachache tu.
Kama Nchi iwe na sera pia kuweka ugumu kwa bidhaa za nje zisizo na ulazima ili hali za kwetu zipo.
 
Donald Trump's one of the best presida amewahi kusema ..waafrika wafanyie uchunguz kama kwel ni normal human being...nchi ina kilaa aina ya madini lakn bado OMBAOMBA
Tunashangilia kuwa China wanatupenda, hivi nani asiyempenda Mteja wake?.

Kama kweli wanawapenda basi wangewafundisha hata namna ya kutengeneza brush za kuogea badala ya kusafirisha kutoka kwao kutuuzia.
 
Umeandika jambo la maana sana.
Yaani kwa sasa kazi tunayoifanya ni kuuziana bidhaa za nje ya nchi huku hatuna mpango wa kuangalia ni namna gani hizi bidhaa tutapunguza uagizaji wake. Vijana wengi wanatoka vyuoni na elimu kubwa wanaishia kupost bidhaa za nje. Sasa kwa hali hii kweli tutafika kama Taifa??
Hizi bidhaa hazitengenezi ajira bali utegemezi. Serikali iangalie kufanya mapinduzi ya Elimu yatakayotusaidia kuthamini vya kwetu na kupunguza uagizaji wa nje. Kwa kufanya hivi itasaidia elimu yetu kutumika hapa ndani vizuri na kuleta ajira kuliko kusoma masomo mengi kwa miaka mingi halafu uje kuuza bidhaa za nje.
 
Tunashangilia kuwa China wanatupenda, hivi nani asiyempenda Mteja wake?.

Kama kweli wanawapenda basi wangewafundisha hata namna ya kutengeneza brush za kuogea badala ya kusafirisha kutoka kwao kutuuzia.
Mkuu unadhani hao wachina kuna taifa lilienda kule kuwafundisha? Hapana, wao ndiyo walienda kuiba technologia na kujifunza wenyewe, sasa tusubiri eti kuna taifa litakuja kutufundisha jinsi ya kutengeneza dodoki la kuogea, sahau kabisa hilo
 
Umeandika jambo la maana sana.
Yaani kwa sasa kazi tunayoifanya ni kuuziana bidhaa za nje ya nchi huku hatuna mpango wa kuangalia ni namna gani hizi bidhaa tutapunguza uagizaji wake. Vijana wengi wanatoka vyuoni na elimu kubwa wanaishia kupost bidhaa za nje. Sasa kwa hali hii kweli tutafika kama Taifa??
Hizi bidhaa hazitengenezi ajira bali utegemezi. Serikali iangalie kufanya mapinduzi ya Elimu yatakayotusaidia kuthamini vya kwetu na kupunguza uagizaji wa nje. Kwa kufanya hivi itasaidia elimu yetu kutumika hapa ndani vizuri na kuleta ajira kuliko kusoma masomo mengi kwa miaka mingi halafu uje kuuza bidhaa za nje.
Kinachotushinda pakubwa ni pamoja na kwenye eneo la gharama za uzalishaji....lakini nina uhakika tukikaa chini kimkakati tunaweza kuja na jibu ya hili....maana hata hao Wachina tunawarahisishia kazi kutokana na kununua kwa wingi.

Hivyo ni suala linalohitaji muda, uvumilivu na malengo.
 
Mkuu unadhani hao wachina kuna taifa lilienda kule kuwafundisha? Hapana, wao ndiyo walienda kuiba technologia na kujifunza wenyewe, sasa tusubiri eti kuna taifa litakuja kutufundisha jinsi ya kutengeneza dodoki la kuogea, sahau kabisa hilo
Hayo maneno nimeyatumia tu lakini lengo ni kuonesha kuwa hawawezi wala hawatotamani tujue namna ya kutengeneza bidhaa wanazotuuzia maana itaathiri viwanda vyao.
 
Hayo maneno nimeyatumia tu lakini lengo ni kuonesha kuwa hawawezi wala hawatotamani ujue namna ya kutengeneza wanachokuuzia maana utaathiri viwanda vyao.
Shida yetu ubongo ulilogwa zamani na Mzungu inawezeka ata wewe ukijitafuta vzr una uwezo mkubwa kuwazidi skills zetu ziko makaburini kwa mababu zetu waliouwawa kinyama enzi za ukoloni ila muumba wetu ni mwema tujitafute
 
Hili lipo wazi kabisa, huwezi kuagiza bidhaa zote zinazotumiwa kwa wingi nchini....utaishia kutengeneza taifa la wachuuzi. Na huu mkenge mlitaka kuuingia kwa kenya.....haya kazi iendelee.
 
Mkuu unadhani hao wachina kuna taifa lilienda kule kuwafundisha? Hapana, wao ndiyo walienda kuiba technologia na kujifunza wenyewe, sasa tusubiri eti kuna taifa litakuja kutufundisha jinsi ya kutengeneza dodoki la kuogea, sahau kabisa hilo
Unachosema ndo kilivyo kwa sisi tuliofanya biashara ndogo ndogo tumejifunza kidogo, sioni Kama tutavuka kwenye hili kabisa la kumkimbia mchina, mganda na mkenya maana hata elimu inayoitwa ya ufundi ni nadhalia tu hakuna kitu.

imagine mtu anasoma mapishi veta lakini hajui kupika chakula chenye hadhi ya kimataaifa, hapo nilichokiona labda serikali iruhusu wachina kufungua kampuni za training za mafunzo ya vitendo au viwanda vyao watu wakafanye kazi huku wakiiba ujuzi maana tumeshachelewa sana vile vitu babu zetu walitengeza wakiwa hawana elimu sisi wenye elimu tulishindwa kuvigeuza kuwa vya kisasa.

Kama vinu sasa zimekuja blender, makalai ya chuma ya mikono sasa zimekuja za kisasa, tenga za nguo na vyombo sasa zimekuja za kisasa, nguo za vitenge sasa zipo za fabric nzuri sana, na hapo hata hivi vidogo vya kusaga karanga na viungo tumeiga hapo kenya lakini tumeshindwa kuiba ujuzi wa vitu vinavyorahisisha kazi Kama mashine za kufua, simu, na vitu vitavyorahishisha kazi kutumia muda mfupi ambavyo vinasoko sana.
 
Uko sahihi kabisa mkuu, ila hata tukiwaita Wachina kwa akili zetu hizi tutaishia kuwa watumwa wao wala hatutotoka na ujuzi wowote, reference ni wanaofanya kazi kwenye viwanda vya wachina mathalani vya kutengeneza tiles, miaka nenda rudi hawawezi iba ujuzi wowote zaidi ya wao kuendelea kuwa vibarua tu.
 
Tanzania kuna mbao za mninga lakini watu wanaenda madukani kununua vitanda na makabati ya vumbi ya mbao kutoka china,
baada ya mwaka vitanda vimevunjika.
Waafrika IQ ndogo sana huwezi kuwabadiisha bali wachache tu.
Sikupingi komenti yako bali maisha ya mwafrika na kipato chake ni sababu mojawapo ya kununua hizo shirt time assets, maana kipato chenyewe ni cha kushtukiza, nk.
 
Tanzania kuna mbao za mninga lakini watu wanaenda madukani kununua vitanda na makabati ya vumbi ya mbao kutoka china,
baada ya mwaka vitanda vimevunjka
Sasa unataka nani aje akutengeneze vitanda vya mninga wa Tanzania, Mchina ?

Kazi yetu kulaumu na kuandika ma comment kwenye mitandao, good for nothing, lazy bums.

Nenda huko unakosema mininga ipo anzisha karakana ya kutengeneza furniture. Watu wataachana na particle board furniture za mchina.
 
Sasa unataka nani aje akutengeneze vitanda vya mninga wa Tanzania, Mchina ?

Kazi yetu kulaumu na kuandika ma comment kwenye mitandao, good for nothing, lazy bums.

Nenda huko unakosema mininga ipo anzisha karakana ya kutengeneza furniture. Watu wataachana na particle board furniture za mchina.
Mbona karana zipo.Kama nawe ni mteja wa kabati za mchina tafuta hoja nyingine sio hio ulioleta. Asset zipo nyingi tu ila ulimbukeni wa wabongo kufikiri mchina anawasaidia kumbe anawaua kiuchumi. Kama haumudu kununnua Huko Dar agiza mkoani kwenu.
Katavi,Tabora,Mbeya zimejaa hizo asset, ukishindwa basi nunua hata syprass ya kitanzania ya mti wa mkambokambo au mlingoti ambao mti wake ni mgumu.
Nakuomba usitetee uzembe wa watanzania wengi.
Ukitaka nikuunganishe na fundi akutumie asset kutoka Tabora uinjoi maisha huko mjini.
 
Back
Top Bottom