Tusijidanganye hakuna Rais aliyewaletea maendeleo watu wake wakamuombea mabaya

Lituye

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
1,862
5,680
Miaka 20 iliyopita tarehe 14 Oktoba 1999 Taifa lilikuwa katika majonzi mazito. Kipindi hicho nikiwa na miaka 20 hivi namaliza kidato cha nne mkoani Mbeya.

Tangazo la Mh. Benjamin W. Mkapa kuwa Baba wa Taifa Mwl. J.K.Nyerere hatunaye tena ilikuwa kama ni ndoto za alinacha na hakuna raia aliyetaka kuzikubali taarifa zile kupitia ITV.

Wakati Mh. Mkapa anasisitiza wananchi kuwa watulivu amani itadumu na kila kitu kiko under control nilikuwa natamani asiendelee kutupa habari hizo maana ananipa woga na simanzi zaidi. Sikuwa naona kitu mbele zaidi ya Giza na hofu.

Nyerere hakuwa Rais, ila uwepo wake, ushauri wake, Matendo yake Uzalendo wake na Maono yake, kwa taifa yalikuwa ni zaidi ya kuwa kiongozi wa taifa.

Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu.
Tutampata wapi mtu kama Nyerere atakaye weza kushauri, kukosoa kuonya na kutupa matumani mahali ambapo tumekosa Matumaini?

Nyerere alikuwa na kipaji cha kipekee sana. Hii iliwafanya watu wengi tuamini maisha bila Nyerere ilikuwa haiwezekani. Matendo yake na maneno yake yalifanana hasa anapozungumzia maendeleo, utu haki na usawa.

Giza lile nililokuwa nikiliona na kulihofu miaka ishirini iliyopita sasa linaonekana dhahiri kutamalaki katika nchi yetu ya Tanzania. Utu umetoweka na umebakia unyama unyama tuu.

Taratibu taifa letu limeanza kufurahia unyama na matendo ya uovu kwa binadamu wenzetu. Amepigwa Risasi Tundu Lissu kinyama sana wapo watu walioshangilia unyama huo. Na hakuna hata Nzi aliye kamatwa mpaka sasa kuhusika na tukio hilo. Ametenguliwa ubunge Tundu Lissu pia wapo watu wameshangilia haki yake hiyo kupotea.

Juzi na jana zilizuka taarifa ya hali ya afya ya kiongozi wa nchi kuwa mbaya. Wapo watu walidiriki kuombea kusikia amekufa tena wakishangilia na kusubiria kwa haamu kupewa uhakika wa tukio.

Hili sio jambo la kawaida katika siasa za Dunia ya ustaarabu na utu. Kuna nyufa zimeonekana na tukiendelea kuzitikisa sisi sote tupo hatarini hakuna wa kupona.

Hii ina maana sasa hivi watu wakisikia ikulu imelipuliwa hawatajali kabisa zaidi watauliza tuu fulani kafa? Ni kwa nini tumefika hapa?

Tusijidanganye kuwa chuki hii inatokana na wahujumu uchumi au sijui mafisadi ambao taifa linapambana nao. Huo ni uongo na unafiki uliutukuka.

Hakuna kiongozi aliye pambana na mafisadi kama Nyerere mpaka kuweka Azimio la Arusha. Kwa miaka mingi aliyo ongoza Nyerere angepaswa kuwa na Maadui wananchi wengi kuliko kiongozi yeyote yule hapa Tanzania. Hakuna wa kujifananisha na Nyerere na hata kumfikia kwa robo tuu.

Viongozi wa sasa wanahamasisha chuki na ubaguzi miongoni mwetu raia na Matunda ya chuki hiyo tumeanza kuyachuma na kuyala sasa.

Tutampata wapi Nyerere kwa sasa aweze kutuonya, kutukaripia, kutusahihisha? Nyerere alikuwa na Kariba ya kipekee ya kiuongozi.

Kikwete alijaribu kuongea kidogo tu hivi karibuni katika Nyerere Day alicho kipata anakijua. Mtu kama Ally Hapi anajitutumua na kutaka kujibizana na Rais mstaafu huku akijiapiza kuwa yupo tayari kupambana na kiongozi mkuu wa nchi aliyestaafu.

Tusipo ziba ufa tutajenga ukuta.
 
Katafute Uzi wa Jk alipoumwa uone matusi na dua mbaya za wapinzani hadi Mods waliufunga


Acha kutishwa na hawa watu wachache wenye chuki na madaraka waliopo tweeter na jf ,ndio hao hao hawana vitambulisho vya kupigia kura na ndio hao hao wanaosemaga wameibiwa kura ,ni watu wachache sana.


Wanaomuombea mema JPM ni wengi kulinganisha na kundi la kina kigogo2014
 
Katafute Uzi wa Jk alipoumwa uone matusi na dua mbaya za wapinzani hadi Mods waliufunga


Acha kutishwa na hawa watu wachache wenye chuki na madaraka waliopo tweeter na jf ,ndio hao hao hawana vitambulisho vya kupigia kura na ndio hao hao wanaosemaga wameibiwa kura ,ni watu wachache sana.


Wanaomuombea mema JPM ni wengi kulinganisha na kundi la kina kigogo2014
Jiulize kwanini kuna hao wachache?
 
Nyerere alikuwa na kipaji cha kipekee sanaa. Hii iliwafanya watu wengi tuamini Maisha bila Nyerere ilikuwa haiwezekani. Matendo yake na Maneno yake yalifanana hasa anapozungumzia Maendeleo, Utu haki na usawa.

Namnukuu TUNDU LISU ".......Mwl. Nyerere hakukataa hoja ya Muungano kwa sababu safi kabisa, bali aliwaweka kizuizini wale waliohoji Muungano. Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uwongo na hakuweza kusema kweli"
 
Ha ha! Ninachokishuhudia ni kwamba taifa linaviongozi wana siasa na wananchi ambao bado hawajafikia hadhi ya siasa hizo!!.. michezo ya kisiasa ipo mingi na wanaozurika na siasa hizo ni wananchi,tunapelekwa kinyumbunyumbu! Na ndio maana tunayafata mapigo ya wanasiasa!.. muda mwengine Jambo ni dogo ila wanalolikuza ni wananchi,wanasiasa wao wakikutana wanakula gambe we unalia hovyo!.. Kama wananchi tunatakiwa tujue tunataka nini na tu focus hapo alasivyo tutaendeshwa na upepo hata wa feni.
 
Maendeleo ni nini kwanza? ukijua kutofautisha maendeleo ya vitu na ya watu ndio utajua utofauti. Magufuli kawegeza kwenye maendeleo ya vitu badala ya maendeleo ya watu.

watu wanahitaji elimu bora, bima bora,ajira bora, kuondoa vikwazo vya kufanya biashara, kupunguza garama za maisha na mfumuko wa bei. ukiwagusa watu apa Hutasikia kelele sana lakini madege, reli haziwezi kuwa kipimo cha maendeleo.
 
Jiulize kwanini kuna hao wachache?
We ni mgeni na hawa chadema aisee, soma kwa makink mstari kwa mstari siku hii ambapo kikwete alianguka jukwaani ndipo utajua kuwa chadema ni wapumbavu na wajinga. Hadi admins wakaamua kuufunga uzi
 
Mkuu labda mgeni wa siasa za Tanzania na tabia za watanzania.
Ilipotangazwa kwenye taarifa ya habari maalumu kifo cha Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine,tukisikia kwenye radio RTD tulipata mshutuko mkubwa,lakini kuna matajiri waliokuwa wanahujumu uchumi walishangilia wazi wazi kwa macho yangu pale mtaa wa Jamhuri. Hadi polisi ikawaweka ndani lakini cha ajabu ilitoka amri kutoka juu wale wote waliokamatwa kwa kushangilia kifo cha Sokine nchi nzima waliachiwa huru.
Hata dalala walishangilia kwa kuwa Sokione alikataza kunyanyasa wanafunzi wakikatazwa kupanda mabasi hayo.
 
Katafute Uzi wa Jk alipoumwa uone matusi na dua mbaya za wapinzani hadi Mods waliufunga


Acha kutishwa na hawa watu wachache wenye chuki na madaraka waliopo tweeter na jf ,ndio hao hao hawana vitambulisho vya kupigia kura na ndio hao hao wanaosemaga wameibiwa kura ,ni watu wachache sana.


Wanaomuombea mema JPM ni wengi kulinganisha na kundi la kina kigogo2014
Ok ni wachache kweli nami nakubaliana na wewe japo huonyeshi takwimu bali utashi wako tu! swali la kujiuliza ni hao wachache kwa sasa wametokana na nini, je wataendelea kubaki wachache? maana life is dynamic sio static! je tuendelee kusubiri wawe wengi (critica massl)? Na itakuwaje wakiwa wengi au tufanyeje?!
 
Wanadamu hata uwafanyie nini,
Nabii Issa tu alikiona cha moto,kabla Mungu kutumia nguvu zake,itakua Rais wetu mpendwa?
 
Kiujumla kwa sasa taifa letu limekosa viongozi Wa kuliunganisha taifa, kilichofanyika kwa tundu lissu hakikubaliki kamwe.serikali ilishindwa kutimiza wàjibu wake kikamilifu...
 
Katafute Uzi wa Jk alipoumwa uone matusi na dua mbaya za wapinzani hadi Mods waliufunga


Acha kutishwa na hawa watu wachache wenye chuki na madaraka waliopo tweeter na jf ,ndio hao hao hawana vitambulisho vya kupigia kura na ndio hao hao wanaosemaga wameibiwa kura ,ni watu wachache sana.


Wanaomuombea mema JPM ni wengi kulinganisha na kundi la kina kigogo2014
Na akitaka kuona aende kwenye uzi wa Zitto aone watu walivyofura kwa ujinga aliofanya. Hao anaowasema walikuwa sijui watu wangapi, na walikuwa wakikomenti kwenye kila uzi, wakiongozwa na Mchawi Mshana JR, Bibi kizee SKY ECLAT, na maboya watatu James 88, Hustling na Nevada. Ukiangalia Hawa wote wako very frustarated, tangu jamaa aingie Kuna mambo yao yamebuma. Sasa hawa Kungu---ru wangapi ndo wamekufanya ufikie holo hitimisho!
 
Hakukuwahi kutokea kiongozi yeyote wa nchi duniani ambaye hana wapinzani na watu wanaomchukia. Viongozi wetu wakuu wa imani Mohammed (S.AW) alipingwa na mpaka leo anapingwa. Yesu Kristo alipingwa vibaya mpaka akasulubiwa na mpaka sasa anapingwa. Mungu mwenyewe anapingwa na wanadamu hawahawa

Nikusaidie tu mkuu. Kupingwa sio ishara kwamba unafanya mabaya. Ujenzi wowote ule wa ustawi wa taifa hukanyaga maslahi mapana ya baadhi ya watu. Unataka wafurahie? Hili ni jambo lililo wazi kabisa kwa yeyote mwenye akili

Watanzania wengi wanaelewa JPM anafanya nini. Taarifa za kuumwa kwake zilifanya mitaa kuzizima. Usijidanganye kiasi hicho mkuu
 
Na akitaka kuona aende kwenye uzi wa Zitto aone watu walivyofura kwa ujinga aliofanya. Hao anaowasema walikuwa sijui watu wangapi, na walikuwa wakikomenti kwenye kila uzi, wakiongozwa na Mchawi Mshana JR, Bibi kizee SKY ECLAT, na maboya watatu James 88, Hustling na Nevada. Ukiangalia Hawa wote wako very frustarated, tangu jamaa aingie Kuna mambo yao yamebuma. Sasa hawa Kungu---ru wangapi ndo wamekufanya ufikie holo hitimisho!
The hate is real usifanye mzaha!! Ila kwa nyie msio na uwezo wa kuchanganua mambo hamuwezi kuiona.

Hebu mwambie aache uhuru wa vyombo vya habari waandike kama wakati wa Awamu ya 4 na aruhusu vyama vya upinzani vifanye kazi yake kadri ya katiba. Nakuhakikishia Magufuri hawezi kupata hata 10%.
Hiyo 10% Ni watu wa Mkoa wa Geita na sehemu kidogo ya lake zone na Watanzania wachache waliozoea kuchagua CCM.

Unajidanganya sana kwa kuwa watu wanaogopa kusema chuki zao wazi wazi kwa kuwa wamekuwa wanatekwa na kuuliwa. Na vyombo vya habari vinashtakiwa au kufungiwa leseni.

MAGUFURI HAKUBALIKI, believe me nguvu yake inategemea Police, TPDF na NEC
 
Miaka 20 iliyopita tarehe 14 Oktoba 1999 Taifa lilikuwa katika majonzi mazito. Kipindi hicho nikiwa na miaka 20 hivi namaliza kidato cha nne mkoani Mbeya.

Tangazo la Mh. Benjamin W. Mkapa kuwa Baba wa Taifa Mwl. J.K.Nyerere hatunaye tena ilikuwa kama ni ndoto za alinacha na hakuna raia aliyetaka kuzikubali taarifa zile kupitia ITV.

Wakati Mh. Mkapa anasisitiza wananchi kuwa watulivu amani itadumu na kila kitu kiko under control nilikuwa natamani asiendelee kutupa habari hizo maana ananipa woga na simanzi zaidi. Sikuwa naona kitu mbele zaidi ya Giza na hofu.

Nyerere hakuwa Rais, ila uwepo wake, ushauri wake, Matendo yake Uzalendo wake na Maono yake, kwa taifa yalikuwa ni zaidi ya kuwa kiongozi wa taifa.

Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu.
Tutampata wapi mtu kama Nyerere atakaye weza kushauri, kukosoa kuonya na kutupa matumani mahali ambapo tumekosa Matumaini?

Nyerere alikuwa na kipaji cha kipekee sana. Hii iliwafanya watu wengi tuamini maisha bila Nyerere ilikuwa haiwezekani. Matendo yake na maneno yake yalifanana hasa anapozungumzia maendeleo, utu haki na usawa.

Giza lile nililokuwa nikiliona na kulihofu miaka ishirini iliyopita sasa linaonekana dhahiri kutamalaki katika nchi yetu ya Tanzania. Utu umetoweka na umebakia unyama unyama tuu.

Taratibu taifa letu limeanza kufurahia unyama na matendo ya uovu kwa binadamu wenzetu. Amepigwa Risasi Tundu Lissu kinyama sana wapo watu walioshangilia unyama huo. Na hakuna hata Nzi aliye kamatwa mpaka sasa kuhusika na tukio hilo. Ametenguliwa ubunge Tundu Lissu pia wapo watu wameshangilia haki yake hiyo kupotea.

Juzi na jana zilizuka taarifa ya hali ya afya ya kiongozi wa nchi kuwa mbaya. Wapo watu walidiriki kuombea kusikia amekufa tena wakishangilia na kusubiria kwa haamu kupewa uhakika wa tukio.

Hili sio jambo la kawaida katika siasa za Dunia ya ustaarabu na utu. Kuna nyufa zimeonekana na tukiendelea kuzitikisa sisi sote tupo hatarini hakuna wa kupona.

Hii ina maana sasa hivi watu wakisikia ikulu imelipuliwa hawatajali kabisa zaidi watauliza tuu fulani kafa? Ni kwa nini tumefika hapa?

Tusijidanganye kuwa chuki hii inatokana na wahujumu uchumi au sijui mafisadi ambao taifa linapambana nao. Huo ni uongo na unafiki uliutukuka.

Hakuna kiongozi aliye pambana na mafisadi kama Nyerere mpaka kuweka Azimio la Arusha. Kwa miaka mingi aliyo ongoza Nyerere angepaswa kuwa na Maadui wananchi wengi kuliko kiongozi yeyote yule hapa Tanzania. Hakuna wa kujifananisha na Nyerere na hata kumfikia kwa robo tuu.

Viongozi wa sasa wanahamasisha chuki na ubaguzi miongoni mwetu raia na Matunda ya chuki hiyo tumeanza kuyachuma na kuyala sasa.

Tutampata wapi Nyerere kwa sasa aweze kutuonya, kutukaripia, kutusahihisha? Nyerere alikuwa na Kariba ya kipekee ya kiuongozi.

Kikwete alijaribu kuongea kidogo tu hivi karibuni katika Nyerere Day alicho kipata anakijua. Mtu kama Ally Hapi anajitutumua na kutaka kujibizana na Rais mstaafu huku akijiapiza kuwa yupo tayari kupambana na kiongozi mkuu wa nchi aliyestaafu.

Tusipo ziba ufa tutajenga ukuta.
Umeongea ukweli mtupu na hekima,ila utashangaa Watanzania wenzako waliojibatiza uzalendo watakavyokusasambua kwa vijembe vyao.
Tunatakiwa kama Taifa tutafute muafaka kupitia maridhiano na Katiba ya wananchi kwa ajili ya wananchi,tuidai hima.
 
Back
Top Bottom