Slim5
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 28,074
- 37,545
Wakati DSTv wakiwa peke yao Ktk dunia ya kidigitali hapa bongo, wakaamua kuleta msamiati unaitwa "DIKODA" ambapo kikazoeleka Kiasi hata BAKITA walipofafanua kuwa kifaa husika sio dikoda, ni KISIMBUSI, imekuwa Kazi watu kuzoea!
Kosa lingine tukalifanya kwenye PASSWORD, tulichelewa na matokeo yake Hata tulipoambiwa ni NYWILA bado tumekuwa wazito!
Sasa huko duniani Kuanzia WC, Bundesliga, La liga kote huko VAR imeshika kasi, naomba tujiandae endapo ikifika hapa kwetu, badala ya VAR, sisi waswahili tutaiitaje hii teknolojia? Au ndio tutatohoa na kuitwa hivo hivo?
Nawakaribisha kwa mapendekezo!
Kosa lingine tukalifanya kwenye PASSWORD, tulichelewa na matokeo yake Hata tulipoambiwa ni NYWILA bado tumekuwa wazito!
Sasa huko duniani Kuanzia WC, Bundesliga, La liga kote huko VAR imeshika kasi, naomba tujiandae endapo ikifika hapa kwetu, badala ya VAR, sisi waswahili tutaiitaje hii teknolojia? Au ndio tutatohoa na kuitwa hivo hivo?
Nawakaribisha kwa mapendekezo!