Tatizo lako haunifahamu mrembo. Ungenifahamu usingekuwa unakurupuka hivi. Nimeshazoea kuhamishwa vyama kutokana na mada zangu.Ona bushlawyer uyu, wanasheria wenzio huwa wanajadili vitu vya msingi kama mitandao kuwaibia wateja wawekapo salio,
Umebakia kwenye korido za mazuzu wa lumumba kutafta cheo
Hata utoke utetezi wa aina gani na kwanini, sasa sio wakati sahihi wa Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa cdm. Ni vyema tukaweka utaratibu wa kupokezana vijiti hiyo ndio demokrasia makini. Kiongozi yoyote mzuri hapaswi kukaa madarakani zaidi ya miaka 10, huyo Mbowe ana zaidi ya miaka 10 na sasa muda sio rafiki tena. Ni vyema akakaa pembeni akatoa nafasi kwa mtu mwingine.
Mbowe anahitajika sasa kuliko nyakati zote alizowahi kuwa mwenyekiti.Nimesoma mada ya ndugu na Rafiki yangu Molemo inayodai kuwa maelfu ya wanachama wa CHADEMA wamejitokeza kuchangia fedha kwa ajili ya kumchukulia na kumpelekea fomu ya kugombea Uenyekiti wa Taifa Mwenyekiti wa sasa Mhe. Freeman A. Mbowe. Fomu husika, kwa uchaguzi wa Disemba, inagharimu shilingi milioni moja za kitanzania.
Mkuu Molemo anajaribu kuonyesha kuwa wanachama wa CHADEMA kwa maelfu bado wanamtaka Mbowe ili 'awavushe'. Mbowe amekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka kumi akichukua uongozi baada ya Hayati Bob Makani. Sikubaliani na hoja kuwa Mbowe analazimishwa na wanachama kugombea Uenyekiti.
Ingawa mimi si mwanasiasa, ufuatiliaji wangu wa siasa katika vyama vyote umenifahamisha kuwa siasa ni mkusanyiko wa maigizo, ulaghai na utapeli ulio na chembechembe ndogo za ukweli. Kwenye siasa, 9 husemwa 6 na sifuri na o zaweza kutotofautishwa kirahisi. Kwenye siasa, ambamo Mbowe yumo, kunaweza kuigizwa jambo hadi watu wakaamini.
Nasema kuwa Mbowe (kama itaonekana amechangiwa na kupelekewa fomu) anataka mwenyewe kuendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Haya maigizo ya kuchangiwa na kubembelezwa kugombea nayakataa. Walishawahi kuwepo wanasiasa waliotembelewa na kuombwa kugombea katika aina hii hii ya maigizo.
Mbowe amefanya mengi na makubwa. Anapaswa kukaa benchi la washauri wa chama na kuachia wengine wakiongoze chama. Aliyoyafanya wakati wa uongozi wake yatamfanya akumbukwe na kuheshimika kuliko aendelee na kundelea kusemwa kama mlafi wa madaraka kwenye chama chake.
Sisi wana Chadema ndiyo tunataka aendelee. Wanaopiga kelele kutaka Mbowe asiendelee ni wana CCM, sasa tukichagua mwingine itakuwa kama tumetii matakwa ya CCM.Nimesoma mada ya ndugu na Rafiki yangu Molemo inayodai kuwa maelfu ya wanachama wa CHADEMA wamejitokeza kuchangia fedha kwa ajili ya kumchukulia na kumpelekea fomu ya kugombea Uenyekiti wa Taifa Mwenyekiti wa sasa Mhe. Freeman A. Mbowe. Fomu husika, kwa uchaguzi wa Disemba, inagharimu shilingi milioni moja za kitanzania.
Mkuu Molemo anajaribu kuonyesha kuwa wanachama wa CHADEMA kwa maelfu bado wanamtaka Mbowe ili 'awavushe'. Mbowe amekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka kumi akichukua uongozi baada ya Hayati Bob Makani. Sikubaliani na hoja kuwa Mbowe analazimishwa na wanachama kugombea Uenyekiti.
Ingawa mimi si mwanasiasa, ufuatiliaji wangu wa siasa katika vyama vyote umenifahamisha kuwa siasa ni mkusanyiko wa maigizo, ulaghai na utapeli ulio na chembechembe ndogo za ukweli. Kwenye siasa, 9 husemwa 6 na sifuri na o zaweza kutotofautishwa kirahisi. Kwenye siasa, ambamo Mbowe yumo, kunaweza kuigizwa jambo hadi watu wakaamini.
Nasema kuwa Mbowe (kama itaonekana amechangiwa na kupelekewa fomu) anataka mwenyewe kuendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Haya maigizo ya kuchangiwa na kubembelezwa kugombea nayakataa. Walishawahi kuwepo wanasiasa waliotembelewa na kuombwa kugombea katika aina hii hii ya maigizo.
Mbowe amefanya mengi na makubwa. Anapaswa kukaa benchi la washauri wa chama na kuachia wengine wakiongoze chama. Aliyoyafanya wakati wa uongozi wake yatamfanya akumbukwe na kuheshimika kuliko aendelee na kundelea kusemwa kama mlafi wa madaraka kwenye chama chake.
Halafu mkuu kama issue ni ku over stay kwemye uongozi wa siasa. Kuna majina tunasikia toka tukiwa watoto wa shule za msingi enzi hizo tukilazimishwa kukipenda chama, mpaka leo hao watu wapo na ni viongozi.
Wachache wao ni Mangula na Wasira. Jeeee huko hakuna watu wengine wa kushika hivyo vyeo vyao
Kuna mtu anaitwa Mrema, mbona humuongelei
Kuna Lipumba, mbona humuongelei
Tunataka maendeleo na uhuru wa kuelezea mawazo yetu hata kama ni ya hovyo. Tusikilizeni na mtujibu
Hivi kuna nyuma ya CCM kutofanya uchaguzi wa mwenyekiti wa Chama na kusubiri wananchi tumchague Rais kupitia CCM na moja kwa moja akawa mwenyekiti wa Chama chao? Kwa nini huwa wanatumia fedha za umma na nguvu kazi ya umma kumchagua mwenyekiti wa chama chao? haya si matumizi mabaya ya fedha za umma?Nimesoma mada ya ndugu na Rafiki yangu Molemo inayodai kuwa maelfu ya wanachama wa CHADEMA wamejitokeza kuchangia fedha kwa ajili ya kumchukulia na kumpelekea fomu ya kugombea Uenyekiti wa Taifa Mwenyekiti wa sasa Mhe. Freeman A. Mbowe. Fomu husika, kwa uchaguzi wa Disemba, inagharimu shilingi milioni moja za kitanzania.
Mkuu Molemo anajaribu kuonyesha kuwa wanachama wa CHADEMA kwa maelfu bado wanamtaka Mbowe ili 'awavushe'. Mbowe amekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka kumi akichukua uongozi baada ya Hayati Bob Makani. Sikubaliani na hoja kuwa Mbowe analazimishwa na wanachama kugombea Uenyekiti.
Ingawa mimi si mwanasiasa, ufuatiliaji wangu wa siasa katika vyama vyote umenifahamisha kuwa siasa ni mkusanyiko wa maigizo, ulaghai na utapeli ulio na chembechembe ndogo za ukweli. Kwenye siasa, 9 husemwa 6 na sifuri na o zaweza kutotofautishwa kirahisi. Kwenye siasa, ambamo Mbowe yumo, kunaweza kuigizwa jambo hadi watu wakaamini.
Nasema kuwa Mbowe (kama itaonekana amechangiwa na kupelekewa fomu) anataka mwenyewe kuendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Haya maigizo ya kuchangiwa na kubembelezwa kugombea nayakataa. Walishawahi kuwepo wanasiasa waliotembelewa na kuombwa kugombea katika aina hii hii ya maigizo.
Mbowe amefanya mengi na makubwa. Anapaswa kukaa benchi la washauri wa chama na kuachia wengine wakiongoze chama. Aliyoyafanya wakati wa uongozi wake yatamfanya akumbukwe na kuheshimika kuliko aendelee na kundelea kusemwa kama mlafi wa madaraka kwenye chama chake.
Uko sahihi kabisa katika andikp lako, Mbowe siasa za zama za Magufuli haziwezi, ningewaona vijana wa chadema wanazo akili kama wangemchulia fomu John Heche na Tundu Lisu, hawa ndio wenye uwezo wa kufanya siasa anazozitaka Magufuli. Jino kwa jino.Mbowe kashakuwa Lipumba na mrema wa Chadema na hili ni kosa la kiufundi wanalifanya Chadema
Mbowe ni bora apumzike
Vipi kuhusu kuhofia mamluki kupenyezwa wagombee huo uenyekiti pindi Mbowe akiachia ngazi?Viongozi hawako tayari kupoteza uongozi wao
Jiulize wanag'ang'ania nini kwenye uongozi
Je hatuna mwingne anae weza kuwa kiongozi
Je wanaanda vipi viongozi makini kama wao wanavyo jijua kuwa wako makini
Tujiulize Kwanin watu tunamwona kiongozi tulie nae ni bora
Kuna wakati viongozi makini huandaa viongozi makini
Ila tunapo pata kiongozi mbovu husimama na kuonekana bila yeye hakuna kitu
Mbowe alipaswa kuachia kiti akiwa bado na nguvu awacoach vijana kama mzee wa chama
Hivi ni kwa nini CCM na washirika wake wanamwogopa sana Mbowe? Hivi kwa nini Vyama vingine wenyeviti wao ni wa miaka na miaka lakini watu hawawasemi kuwa wawaachie wengine bali Mbowe tu? Nani aliwahi kusikia uchaguzi wa mwenyekiti wa TLP ya Mrema?Akivunja katiba itakuwa siyo sawa, lakini 0kama katiba inaruhusu ashindane akishinda itakuwa sawa tu.
Ndungu mwanasheria wa mtaondaoni