Tusibomoe ili tusijenge au tubomoe ili tujenge

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,632
40,790
Serikali kuipitia mamlaka yake tanzu ya Rahco inaendelea na bomoa bomoa ili kupisha mradi wa ujenzi wa reli ya kiwango yaani SGR.

Bomoa bomoa hiyo inahusiana na majengo yote yaliyopo ndani ya hifadhi ya reli yaliyopo ndani ya mita 15-30.

Pamoja na nia njema ya Serikali kuipitia mradi huo ambao una manufaa kwa Taifa sasa na kwa vizazi vijavyo bado mradi huo umepata pingamizi kubwa toka kwa wahanga na t taasisi mbali mbali zinazopigania haki za binadamu wote hawa wakisimamia haki ya msingi ya kuwa na makazi.

Swala linalokuja hapa ni kujaribu kuweka Katika mizani faida za mradi na haki ya kupata makazi.

Je tusibomoe ili tusijenge au tubomoe ili tujenge.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom