Tusemezane: Elimu yetu inaandaa taifa la aina gani?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,196
25,516
Nimeyasikia na kuyafuatilia matokeo ya Kidato cha Nne waliomaliza mwaka jana 2016. Matokeo hayo yalitangazwa jana na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA). Walioongoza wameongoza; walioongozwa wameongozwa; waliofaulu wamefaulu na waliofeli wamefeli.

Binafsi, naamini kuwa ustawi wa elimu Tanzania huonekana kupitia Shule za Serikali. Huko ndiko wanapopatikana watanzania asilia. Huko hupatikana watanzania wa kawaida wanaosoma katika mazingira ya kitanzania hasa. Wanaofaulu huko, hufaulu kweli.

Shule za Sekondari za Serikali, hakika, ni kioo cha ustawi wa elimu Tanzania. Kutokana na uiamara wa Serikali, ilitegemewa kuwa angalau Shule za Serikali zingechomoja hapa kumi bora katika matokeo hayo. Hali inakuwa kinyume kila kukicha. Shule binafsi zinaendelea kutamba.

Shule binafsi, kwa maoni yangu, husheheni watoto wa watu wa tabaka fulani. Kufaulu kwao kwa kiwango cha juu kunaongeza nafasi kati ya tabaka lao na tabaka la wale wasomao Shule za Serikali. Hii si dalili nzuri kinchi. Wale wanaofeli kwa maelfu waelekee wapi?

Kutamba kwa shule binafsi na kufanya vibaya kwa shule za Serikali kunaleta picha gani? Kunaleta picha kuwa Serikali ina kazi ya kufanya katika nyanja ya elimu ya Tanzania. Inapaswa kufanya tafiti kupitia wadau wa elimu kujua tatizo. Ipo haja ya kuangalia na maslahi ya walimu.

Hali hii ikiendelea, maskini wa kitanzania watafeli kwa maelfu kidato cha nne na kutengeneza magenge hatari mitaani. Lengo la elimu ya bure si tu mwanafunzi afike kidato cha nne; afike na kusonga mbele zaidi. Anayefeli kidato cha nne hana tofauti yoyote na darasa la saba.

Nimalize kwa kupongeza shule na wanafunzi waliofanya vyema. Nitoe pole kwa shule na wanafunzi waliofanya vibaya. Kubwa zaidi, Serikali naishauri kutafiti na kujua tatizo linalokumba shule zake hadi kufelisha kwa kiasi kinachotokea. Elimu yetu ni roho ya Taifa letu.
 
Kwa maoni yangu, hali hii imetengenezwa na watawala kwa kuwa hutegemea sana ignorance katika jamii kuendelea kutawala. Wanasiasa wanataka kutengeneza mazingira ambapo watu wanadanganyika kirahisi. Watu ambao hawajaelimika na kupata maarifa ya kutosha, huogopa wanasiasa. Hawajiamini. Hufikiri wanasiasa ndio wanapaswa kutatua matatizo yao na hivyo hujikuta wakinyenyekea wanasiasa badala ya kuwaadhibu. Overall, standard ya viongozi inaathirika sana na accountability inakosekana. Pia, quality ya wafanyakazi sehemu za kazi ni ndogo mno kutokana na aina ya elimu inayotolewa.
 
Kwa maoni yangu, hali hii imetengenezwa na watawala kwa kuwa hutegemea sana ignorance katika jamii kuendelea kutawala. Wanasiasa wanataka kutengeneza mazingira ambapo watu wanadanganyika kirahisi. Watu ambao hawajaelimika na kupata maarifa ya kutosha, huogopa wanasiasa. Hawajiamini. Hufikiri wanasiasa ndio wanapaswa kutatua matatizo yao na hivyo hujikuta wakinyenyekea wanasiasa badala ya kuwaadhibu. Overall, standard ya viongozi inaathirika sana na accountability inakosekana. Pia, quality ya wafanyakazi sehemu za kazi ni ndogo mno kutokana na aina ya elimu inayotolewa.

Una uhakika Mkuu?
 
poor-students-4.jpg
 
Elimu bora ni general knowledge ambayo inapatikana mtaani na kwenye vitabu vya watu waliofanya mambo yakawa. General knowledge inaccount 80% ya maendeleo ya mwanadamu.
Academic education accounts only 20% of human development ndio maana hata darasani tunasoma mambo yaliyobuniwa na watu ambao hawakusoma ila walikomaa wenyewe.
Ni jukumu la wazazi kujua watoto wao wanapassion na nini na kuwasimamia wafikie malengo yao mapema.
Ndio maana Form Four china anaweza kumiliki kiwanda wakati form four afrika anaogopa hata kwenda mkoa jirani.

ELIMU YA KWELI INAANZIA NYUMBANI SIO SHULE.
 
Yaani siku hizi kuisikia kibaha au pugu au tabora boys au kilakala ni nadra hizi shule sijui zimekumbwa na pepo gani,siku hizi zinazoongoza ni hawa academia,tu nnaanza kuamini kuwa hizi shule zinanunua mitihani ya taifa,siwezi ongea sana shule za Govt zinahujumiwa.
 
Woote wenye uwezo hawataki shule za serikali, watoto wao wanawapeleka kuleee kwenye miundo mbinu bora
 
Una uhakika Mkuu?

Or else what "alternative facts" do you have? Sioni sababu nyingine kwa nini elimu yetu imekuwa kama ilivyo. Someone must be benefiting from mass ignorance. Haiwezekani tunajua kabisa waalimu ndio kila kitu halafu we are doing nothing about it. Kama sio makusudi ya kutaka watoto wetu wasipate maarifa ili we raise kuwatawala ni nini? Hivi umeshafika shule kama Mzumbe Secondari siku za karibuni? Ni kama gereza. Pengine hata gereza ni afadhali. Everything is run-down halafu eti ndio shule ya watoto wenye vipaji na mtu anakaa Dar es Salaam anatarajia vijana wa Mzumbe wajifunze kitu na washindane na Feza Boys. [HASHTAG]#Public[/HASHTAG] fiction.
 
Falsafa ya Elimu inayotolewa leo ndio itakuja kuwa Falsafa ya Serikali ya kizazi kijacho.
 
Kama mfumo wa elimu katika taifa hili ungekuwa wa namna inayoleta tija kweli kweli; kwamba watoto si tu kwamba wanafaulu vizuri lakini pia wanaelimika kweli kweli, shule za binafsi ingepata wapi soko? Hata watoto wa mawaziri na wabunge; watoto wa matajiri wakubwa, wangesoma kwenye shule za serikali.

Kwa sasa tuikubali hali ilivyo. Elimu "bure" ilipaswa kuwa "bora" na siyo vinginevyo!
 
Mi naona tatizo ni yale yaliyo ndani ya mitaala yetu na lugha inayotumika kuyafundisha; hayaeleweki kiasi cha kuweza kuwa applied katika mazingira ya kawaida.
Bora serikali ingehakikisha mtu akimaliza Form four anaweza kujenga, kufuga, kulima, kuunda vitu, kuvua, kufanya shughuli za kibiashara..n.k (kutokana na uchaguzi wa mwanafunzi)
atakayefanya vizuri zaidi kwenye project yake anasonga mbele zaidi. Kuliko hali ilivyo sasa mwanafunzi anahitimu form four hana skill yoyote ya maana zaidi ya kukumbuka definitions mbili tatu ambazo hazimsaidii lolote kwenye mazingira yake.
Mf. Waliohitimu mwaka jana walikuwa zaidi ya watu 408,000. kati yao watakaoenda A-level hawazidi 100,000 (na wengine watafeli form 6 hawatakuwa na tofauti na waliofeli o level). Maana yake 300,000 waliobaki wameshakwama na Archimedes principle zao kichwani. Si bora wangekuwa na ujuzi wa kulima, kufuga, kuvua n.k wangekuwa na pa kuanzia.
 
Watu huwa wanadhani ufaulu ni ufaulu tu. Mimi hata uwe T.O bongo wakati huwezi hata kuunga Nyaya kwenye kitasa ili taa ya umeme iwake nakuona kilaza kuliko failure ambaye anayeweza kuunda hicho kitasa .
Swala ni umefaulu nini? Na kitaleta impact gani kwako na kwa jamii yako.
Badala ya kujaza booklets za Necta kupiga porojo, bora tungekuwa tunajaza ardhi,anga na maji kwa matendo halisi ya maisha.
Hata yule mwanafunzi aliyechora mazombi kwenye booklet asingechora kama mitihani ingekuwa ni ya kutekeleza project yake.
Elimu sio kuandaa watu wa kuja kuajiri: kusema uandikishe watoto 1,000,000 primary school halafu miaka 18 baadaye uje uajiri wahitimu 35,000 waliofika chuo kikuu. Wakati huo huo, hao watu 965,000 hukuwafundisha ujuzi wowote wa kukabiliana na changamoto na kutumia fursa zilizopo katika mazingira yao.Sasa nchi itaendeleaje? Yaani mtoto wa kanda ya ziwa akifeli Form six akaamua kurudi Kuvua samaki, anakuwa hana tofauti na baba yake ambaye hakufika hata darasa la 7. Sasa kuna umuhimu gani wa kwenda shule.

Mali haizalishwi kwenye makaratasi kwa maneno. Mali inazalishwa juu ya Uso wa dunia kwa matendo. Kwa hiyo Elimu yetu itufunze njia bora za kuzalisha mali. Sio kujaza makaratasi na kuandika porojo kuombea misaada kwa Wazungu.
 
Naomba nitoe maoni yangu juu ya elimu ya Tanzania. Kwa kuanzia, nimesoma shule ya msingi ya Upanga (1982-1988), shule ya sekondari ya Azania (1989-1992), na shule ya Mzizima (PCM - 1993-1995). Nikaondoka kwenda kusoma chuo Marekani mwaka 1996 na nimesoma na kuishi huku toka wakati huo. Naomba niongelee tofauti ya elimu yetu na ya huku ambayo kwa muangalio wangu utatufanya tuwe tuko nyuma sana hususani kwenye masomo ya sayansi, hesabu, na teknologia.
Toka nasoma msingi mpaka namaliza sekondari, ninaweza kuhesabu kwa kiganja kimoja ni mara ngapi mwalimu aliweka chaki yake chini na kuweza kumuuliza na kumsikilza mwanafunzi juu ya maoni yake binafsi amabayo hayaendani ma alichoandika kwenye ubao (for instance, what is your opinion about the role of Mathematics in the advancement of technology?, what is an alternative method to solving the quadratic equation?, here is a homework to work on building a simple battery-operated circuit, Are there any other ways that you would have used to solve the situation?, etc). Kwa bahati mbaya elimu ya Tanzania ni ya mwalimu kuandika kwenye ubao kuanzia mwanzo hadi mwisho (from the subject definition to adv./disadv. of the subject). Uthubutu kujibu ambavyo mwalimu hakuandika ubaoni hata kama hujakosea uone atakavyokukata maksi na wakati mwingine kuadhibiwa na bakora (wakati wa enzi zangu shuleni). Elimu yetu hairuhusu ubunifu na "utundu" wa mwanafunzi. Kuna watu wangapi tulisoma nao ambao ukikumbukia sasa, ni walikuwa wana akili sana, lakini tulikuwa tunawaita watukutu na watundu?. Walikuwa wanafungua TV, baiskeli, radio, na kujua kuiweka tena pamoja na kuelewa inavyofanya kazi lakini hata wazazi wao walikuwa wanawatandika na kuwaita watundu?.
Nasema yote haya ni kwa sababu nilikuja chuoni huku na pia kupitia kwa watoto wangu shuleni, walimu wa huku wanapenda sana maoni yako kuhusu somo (creativity and free thinking). Hao tunaowaita watundu kwetu, ndio wengi wao (kutokana na walimu wa huku kuwajali na kuwathamini) wanaokuwa innovators, scientists, engineers, doctors, etc. Ndio maana umweke Mtanzania na watu wa nchi mbalimbali, inakuwa vigumu sana kupata kazi. Swali dogo tu (for instance, tell us something about yourself) kwenye kuomba kazi linakuwa tabu sana kwa sababu tumezoea kuambiwa na ku cram vitu tunavyofundishwa.
Elimu ya wenzetu inampa mazingira mazuri sana mwanafunzi kuwa na uimara (confidence) mbele ya wenzake na kuweza kujielezea na kufafanua vitu toka umri mdogo sana. Watoto wangu (miaka 4 and 9) wanapewa homework za sayansi na hesabu ambazo kwetu ingekuwa haiwezekani au vigumu sana kufanya.
Itabidi kuwekeza sana kwenye elimu, kuanzia kwa serikali mpaka kwa wazazi. Ninaelewa uchumi wa nchi zilizoendelea na fedha wanazowekeza kwenye elimu ni mchana na usiku kulinganisha na nchi masikini kama Tanzania. Lakini kama hatujaamua kuwekeza na kubadilisha jinsi tunavyowafundisha wanafunzi, itakuwa ni janga kwa nchi na kwa maendeleo ya taifa.
My 2 cents.
 
Una uhakika Mkuu?

Unataka uhakika gani sasa? Mbona amechambua vizuri na hali halisi ndio iko hivyo? Mtaji wa watawala wa sasa kuendelea kutawala ni ufinyu mdogo wa elimu za Watanzania walio wengi. Hata wale ambao pengine tunaweza tukasema "wameelimika" unakuta ni patupu kwasababu mfumo wa elimu yetu hauhamasishi "critical thinking and analysis" bali ni kukariri kwa kwenda mbeleee. Matokeo yake, mtu ana maliza high school mpaka chuo kikuu lakini bado hajielewi. Hii ni hatari sana!
 
Tusitafute mchawi. Jibu rahisi. Kama shule za serikali zinafeli na binafsi kufaulu ina maana:
X. Shule za serikali hakuna usimamizi kwa mwanafunzi kufanya wajibu wake shuleni
Y. Hakuna usimamizi kwa walimu kutenda wajibu wao shuleni
Z. miundombinu ya kufundishia shule za serikali ni duni/hazitoshelezi/hakuna
N. Maslahi ya walimu shule za serikali na binafsi hazifanani.

Kwa hiyo ukisolve N, Y na Z utapata thamani ya X.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom