GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,865
Kuna Mwalimu Mkuu mmoja wa Shule ya Upili ( Secondary ) iitwayo Mnazi Mmoja aitwae Jose ambaye inasemekana ana Urafiki wa karibu sana hadi unaoudhi wengine na mmoja wa Viranja wa hiyo Shule. Kinachosikitisha wengi ni kwamba hadi hivi sasa huyo Mwalimu Mkuu ameshawafukuza Kazi Viranja kama Watano hivi kwa makosa ya kawaida mno ila ni hivi majuzi tu huyu Kiranja wake Kipenzi aitwae Chris ametoka kufanya Kosa kubwa ambalo pengine hadi hivi sasa alipashwa awe tu Mwanafunzi wa kawaida na siyo tena Kiranja.
Je unadhani huu ukaribu wa huyu Mwalimu Mkuu Jose ambaye anasifika kwa ukali sana na huyu Kiranja wake Kipenzi Chris kiasi kwamba anampenda na kumlinda unatokana na lipi kati ya haya mambo mawili?
a) Mwalimu Mkuu Jose anaogopa akimuondoa kuwa Kiranja Chris anaweza akachukiwa na Wanafunzi wote kutokana na kwamba ameshajijengea Uadui na Wanafunzi wenzake wengi kutokana na tabia yake ya Kuwaonea hata pasipo sababu yoyote ile
b) Mwalimu Mkuu Jose anaogopa akimuondoa labda huyu Kiranja anaweza akatoa Siri Kali za Mwalimu Mkuu hasa ukizingatia kwamba huyu Kiranja Chris anajua mambo yake mengi ambayo si Walimu wenzake wala Wanafunzi wa hiyo Shule wanayajua hivyo inaweza ikamuathiri katika Ukuu wake wa Shule hiyo.
Nawasilisha.
Je unadhani huu ukaribu wa huyu Mwalimu Mkuu Jose ambaye anasifika kwa ukali sana na huyu Kiranja wake Kipenzi Chris kiasi kwamba anampenda na kumlinda unatokana na lipi kati ya haya mambo mawili?
a) Mwalimu Mkuu Jose anaogopa akimuondoa kuwa Kiranja Chris anaweza akachukiwa na Wanafunzi wote kutokana na kwamba ameshajijengea Uadui na Wanafunzi wenzake wengi kutokana na tabia yake ya Kuwaonea hata pasipo sababu yoyote ile
b) Mwalimu Mkuu Jose anaogopa akimuondoa labda huyu Kiranja anaweza akatoa Siri Kali za Mwalimu Mkuu hasa ukizingatia kwamba huyu Kiranja Chris anajua mambo yake mengi ambayo si Walimu wenzake wala Wanafunzi wa hiyo Shule wanayajua hivyo inaweza ikamuathiri katika Ukuu wake wa Shule hiyo.
Nawasilisha.