cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Abdul Nondo amewahi kutekwa na watu wasio julikana,kwa upande wa serikali na wapambe wao na uchunguzi wao hadi kwenye simu na minara wakaja na hoja kuwa Nondo alijiteka mwenyewe
Yaani chombo cha polisi na usalama wa Taifa wakaaminisha Watanzania kuwa Nondo kajiteka mwenyewe,bila kusahau kauli nzito kutoka Lumumba za kejeli na dharau dhidi ya Nondo kuwa amejiteka mwenyewe
Mpaka kuna lugha ngumu imewahi kutolewa na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Mwigulu kwa Abdul Nondo
Nondo kapelekwa mahakamani,pamoja na ushahidi wenye utata mahakamani umemuachia huru mara mbili kuwa Nondo hana hatia
Sasa turudi nyuma Nondo alijiteka au alitekwa?
Vyombo vya serikali kwa makusudi viliwahadaa Watanzania kuwa Nondo alijiteka kumbe wenyewe ndo watekaji?
Wewe kama mtanzania una bado imani na vyombo vya usalama Tanzania ?
IGP Sirro tuambieni nani anahusika na utekaji Tanzania? Intelligensia ya polisi imeshindwa kubaini waliomteka Nondo wakaja na majibu kuwa alijiteka?
Watanzania bado tunajiuliza ni nani alimteka Nondo,
Mwigulu,Lugora na IGP tunasubiri majibu
Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani chombo cha polisi na usalama wa Taifa wakaaminisha Watanzania kuwa Nondo kajiteka mwenyewe,bila kusahau kauli nzito kutoka Lumumba za kejeli na dharau dhidi ya Nondo kuwa amejiteka mwenyewe
Mpaka kuna lugha ngumu imewahi kutolewa na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Mwigulu kwa Abdul Nondo
Nondo kapelekwa mahakamani,pamoja na ushahidi wenye utata mahakamani umemuachia huru mara mbili kuwa Nondo hana hatia
Sasa turudi nyuma Nondo alijiteka au alitekwa?
Vyombo vya serikali kwa makusudi viliwahadaa Watanzania kuwa Nondo alijiteka kumbe wenyewe ndo watekaji?
Wewe kama mtanzania una bado imani na vyombo vya usalama Tanzania ?
IGP Sirro tuambieni nani anahusika na utekaji Tanzania? Intelligensia ya polisi imeshindwa kubaini waliomteka Nondo wakaja na majibu kuwa alijiteka?
Watanzania bado tunajiuliza ni nani alimteka Nondo,
Mwigulu,Lugora na IGP tunasubiri majibu
Sent using Jamii Forums mobile app