Tupo wawili peke yetu.

Consigliere

JF-Expert Member
Sep 9, 2010
12,037
24,595
Padri amekaa katika ki-box cha kuungamisha, kanisani hakuna mtu. Mara muumini mmoja akaingia, akapiga magoti upande wa pili na kufanya ishara ya msalaba akaanza kuungama.

"padri naungama dhambi zangu, leo nimefanya dhambi kubwa sana" "endelea"

"bosi wangu aliniita nyumbani kwake akaniambia amegundua nimeiba shilingi milioni 50, akasema nisipotoa maelezo ya kutosha atanipeleka polisi. Sasa ukweli mimi naogopa kufungwa, nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikachomoa bastola nikamuua. Je, Yesu atanisamehe?"

"utasamehewa" Padri alijibu

"Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango unafunguliwa, kutazama loh, mke wa bosi. Akaniuliza nimemfanya nini mume wake. Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikamuua na yeye. Je, Yesu atanisamehe na hiyo?"

"utasamehewa" Padri alijibu

"nikatoka nje, nikawasha gari niondoke lakini mlinzi akakataa kufungua geti akasema amesikia kama kishindo hivi! Nikaona ananiwekea kiwingu.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. Je, Yesu atanisamehe?"

"utasamehewa" Padri alijibu

"nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi akabisha hodi nikawaza mambo gani tena. Akasema amerudi nyumbani na kukuta yaliyotokea, lakini akanionyesha diary ya baba yake inayoonesha kuwa nilikuwa na appointment naye kabla hajafa. Nikamuuliza nani mwingine anajua, akasema ameanzia kwangu kisha atakwenda polisi.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. Diary nikaichoma moto. Je, Yesu atanisamehe na hilo?"

- kimya........

"padri, Yesu atanisamehe kwa hilo?"

- kimya.........

Jamaa kutazama kwenye kibox padri hayupo. Lakini kwenye kona moja akaonavazi jeupe linamalizia kona, akamfukuzia na kumpata the akamuulia. " Baba vipi mbona umekimbia na kuniacha peke yangu?"

Padri akajibu "niligundua kuwa tupo wawili peke yetu"



"nilitazama huku na huku nikagundua kuwa tuko wawili peke yetu........"
 
Kuangalia huku na huku, nikaona nipo mimi na simu yangu, nikacheeeka!
Hihiihihiihihhhiiiiiiiii!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom