Tupitie kidogo hii Makala (Ujasusi wa kidola na kiuchumi))

futurestar

JF-Expert Member
Oct 15, 2014
245
77
Kanali Patrick Karegeya alikuwa mkuu wa wa shirika la ujasusi la Rwanda (NISS) na Apollo Gafaranga alikuwa mmoja wa Informer wake. Karegeya alijaribu kumpindua Kagame ktk jaribio lililoshindwa kabla ya kukimbilia nchini Afrika Kusini kuishi Uhamishoni. Serikali ya Afrika kusini ilimpa ulinzi wa askari na wanausalama ili Kagame asiweze kumfuatilia huko.

Baada ya Karegeya kukimbilia Afrika kusini, haraka sana Kagame akaunda kikosi cha kumfuatilia huko kilichoitwa "Escandot de la Mort" yani kikosi cha kifo. Kagame akamteua Appolo Gafaranga kuwa mmoja wa wajumbe wa kikosi hicho. Huyu ni yule aliyekuwa informer wa Patrick Karegeye.

Kikosi hiko kikapewa mafunzo maalumu na jukumunmoja tu la kumuua Karegeya na washitika wake. Mwaka 2010 Apollo Gafaranga akaanza mawasiliano ya siri na Patrick Karegeye akijifanya anachukizwa sana na utawala wa Kagame. Karegeya akafurahi kuwa amepata mshirika wa kumng'oa Kagame. Wakaendelea kuwasiliana.

Gafaranga akawa anasafiri mara kadhaa kwenda Afrika kusini kukutana na Karegeya na kupanga mipango ya kumpindua Kagame. Mara zote Karegeya alikua na ulinzi wa wana usalama aliopewa na serikali ya Afrika kusini. Gafaranga akamshauri Karegeye awakatae askari hao waliokuwa wakimlinda kwa kuwa wanaweza kutumika kuvujisha siri. Karegeya akapokea ushauri huo na kuomba serikali ya Afrika kusini imuondolee ulinzi huo.

Disemba 25 mwaka 2013 Gafaranga aliwasiliana na Karegeya na akapanga kwenda kumsalimia Afrika kusini. Alifika Afrika kusini na akapokelewa na rafiki yake Karegeya ambaye alikua amemchukulia chumba kwenye hoteli ya Sandton, mjini Johanersburg.

Gafaranga na Karegeya wakawa wanakutana chumbani hapo kupanga namna ya kumpindua Kagame. Disemba 31 Karegeya akaenda chumbani humo. Alipoingia, akaweka kibao "do not disturb". Alipoingia ndani wakati akiongea na rafiki yake, mara wakatokea watu wawili waliokua wamejificha bafuni. Wakampiga risasi kwa kutumia silaha yenye kiwambo cha sauti. Walipohakikisha wamemuua wakamlaza kitandani wakamfunika na kuondoka. Hivyo ndivyo Kagame alivyofanikiwa kuzima uasi wa Karegeya aliyekua mkuu usalama wa taifa la Rwanda (NISS).
____________
Habari hii inapatikana ktk kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kitabu chenye kurasa zaidi ya 700 chenye mengi ya kujifunza.

[HASHTAG]#MyTake[/HASHTAG]:
Habari hii ya Kanali Karegeya inatufundisha kutomuamini yeyote kwenye harakati za mapambano. Karegeye alimuamini Gafaranga kwa sababu tu alikua kijana wake wa kazi. Karegeye hakujua kama kijana huyo aliyemuamini sana ndiye atakayekuja kumuua.

Wakati Karegeya anaasi serikali ya Kagame, na kukimbilia Afrika ya kusini, Gafaranga nae alijifanya kuasi. Akaanza kuwasiliana na Karegeya kwa siri jinsi ya kumpindua Kagame. Kumbe Gafaranga yupo kazini.

Karegeya pamoja na kwamba alishawahi kuwa mkuu wa shirika la ujasusi la Rwanda hakujua kama ule ni mtego. Alidhani Gafaranga ameasi kweli. Akampa siri zote. Gafaranga nae akazifikisha kwa Kagame.

Kagame akaongeza watu wawili nchini Afrika kusini. Watu hao Gafaranga aliwaingiza chumbani kwake na kuwaficha bafuni. Karegeya alipoingia wakaibuka kutoka bafuni na kumuua kabla ya kutokomea.

Na kwa kuwa walikua wanatumia majina bandia haikua rahisi kuwakamata. Walitoroka kwa barabara kwa kupitia mpaka wa Msumbiji na baadae Tanzania kisha Rwanda.

Hili liwe funzo kwetu hasa kwa vijana wanaofanya siasa za upinzani. Vijana wengi wa opposition nchini (hasa Chadema) hutokea sana kuwaamini watu kwa jina tu la "kamanda". Umekutana na mtu siku mbili anajiita Kamanda, unamuamini na kumpa siri zako. Kumbe mwenzio yupo kazini.

Wapo watu wa usalama wengi wanaovaa magwanda, wanashiriki mikutano ya chama, wanachangia chama, na wengine wanakuwa hadi viongozi wa chama lakini ni ma "agent" wapo kazini. Mtu anajiunga na chama chenu kutokea chama kingine, hata miezi miwili hana anapewa nafasi ya kugombea uongozi. Mnamuamini kiasi gani?

Usimuamini mtu kirahisi kwa kigezo tu cha ukamanda. Jipe muda wa kutosha kujiridhisha. Yupo mtu anaweza kuitukana serikali ukadhani ni mwenzio ukaungana nae, kumbe yeye ana kazi maalumu. Ukaingia mtegoni, ukanasa. Be careful.!

Kujifunza haya na mengine mengi tafuta kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kina madini mengi ya kujifunza. Ni kurasa 700 zilizosheheni. Kinapatikana kwa TZS 80,000/= tu. Wasiliana na Yericko kupitia 0715 865 544.

Picha chini ni Kanali Patrick Karegeya enzi akiwa Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Rwanda (NISS).

97d28a8121b10e0486b49e289d9e3992.jpg
 
Nimekusoma mkuu! Pia ukiisoma historia ya dikteta mobutu sese seko wa jamhuri ya kongo enzi hizo ikiitwa zaire utakutana na kisa kinachofanana na hicho, kinamhusu mtu mmoja aliyeitwa alphonce Bangala(colonel bangala) aliyekuwa mkuu wa mkoa wa leopordville(Kinshasa) huyu naye alitumiwa na mobutu kumtrack down hasimu mkubwa wa mobutu kwa kujifanya yupo naye Bega kwa Bega katika harakati za kumngoa mobutu madarakani! Matokeo yake aliwa snitch na kupelekea maafisa kadhaa wa jeshi pamoja na mawaziri maarufu kunyongwa hadharani hadi kufa!! Na kibaraka wa mobutu aliyekuwa na kazi za kutunga na kuimba nyimbo za kumtukuza dikteta mobutu (Franco Lwambo lwanzo makiadi)alitunga wimbo wa kumsifia Bangala kwa u snitch wake! Wimbo unaitwa colonel bangala, colonel bangala,obongise munene na vila ya kinshasa( colonel bangala umifanyia makubwa jiji la kinshasa) huwa namfananisha bangala na bashite(sorry)
 
Nimekusoma mkuu! Pia ukiisoma historia ya dikteta mobutu sese seko wa jamhuri ya kongo enzi hizo ikiitwa zaire utakutana na kisa kinachofanana na hicho, kinamhusu mtu mmoja aliyeitwa alphonce Bangala(colonel bangala) aliyekuwa mkuu wa mkoa wa leopordville(Kinshasa) huyu naye alitumiwa na mobutu kumtrack down hasimu mkubwa wa mobutu kwa kujifanya yupo naye Bega kwa Bega katika harakati za kumngoa mobutu madarakani! Matokeo yake aliwa snitch na kupelekea maafisa kadhaa wa jeshi pamoja na mawaziri maarufu kunyongwa hadharani hadi kufa!! Na kibaraka wa mobutu aliyekuwa na kazi za kutunga na kuimba nyimbo za kumtukuza dikteta mobutu (Franco Lwambo lwanzo makiadi)alitunga wimbo wa kumsifia Bangala kwa u snitch wake! Wimbo unaitwa colonel bangala, colonel bangala,obongise munene na vila ya kinshasa( colonel bangala umifanyia makubwa jiji la kinshasa) huwa namfananisha bangala na bashite(sorry)
Haya mambo ni magumu sana
 
Kanali Patrick Karegeya alikuwa mkuu wa wa shirika la ujasusi la Rwanda (NISS) na Apollo Gafaranga alikuwa mmoja wa Informer wake. Karegeya alijaribu kumpindua Kagame ktk jaribio lililoshindwa kabla ya kukimbilia nchini Afrika Kusini kuishi Uhamishoni. Serikali ya Afrika kusini ilimpa ulinzi wa askari na wanausalama ili Kagame asiweze kumfuatilia huko.

Baada ya Karegeya kukimbilia Afrika kusini, haraka sana Kagame akaunda kikosi cha kumfuatilia huko kilichoitwa "Escandot de la Mort" yani kikosi cha kifo. Kagame akamteua Appolo Gafaranga kuwa mmoja wa wajumbe wa kikosi hicho. Huyu ni yule aliyekuwa informer wa Patrick Karegeye.

Kikosi hiko kikapewa mafunzo maalumu na jukumunmoja tu la kumuua Karegeya na washitika wake. Mwaka 2010 Apollo Gafaranga akaanza mawasiliano ya siri na Patrick Karegeye akijifanya anachukizwa sana na utawala wa Kagame. Karegeya akafurahi kuwa amepata mshirika wa kumng'oa Kagame. Wakaendelea kuwasiliana.

Gafaranga akawa anasafiri mara kadhaa kwenda Afrika kusini kukutana na Karegeya na kupanga mipango ya kumpindua Kagame. Mara zote Karegeya alikua na ulinzi wa wana usalama aliopewa na serikali ya Afrika kusini. Gafaranga akamshauri Karegeye awakatae askari hao waliokuwa wakimlinda kwa kuwa wanaweza kutumika kuvujisha siri. Karegeya akapokea ushauri huo na kuomba serikali ya Afrika kusini imuondolee ulinzi huo.

Disemba 25 mwaka 2013 Gafaranga aliwasiliana na Karegeya na akapanga kwenda kumsalimia Afrika kusini. Alifika Afrika kusini na akapokelewa na rafiki yake Karegeya ambaye alikua amemchukulia chumba kwenye hoteli ya Sandton, mjini Johanersburg.

Gafaranga na Karegeya wakawa wanakutana chumbani hapo kupanga namna ya kumpindua Kagame. Disemba 31 Karegeya akaenda chumbani humo. Alipoingia, akaweka kibao "do not disturb". Alipoingia ndani wakati akiongea na rafiki yake, mara wakatokea watu wawili waliokua wamejificha bafuni. Wakampiga risasi kwa kutumia silaha yenye kiwambo cha sauti. Walipohakikisha wamemuua wakamlaza kitandani wakamfunika na kuondoka. Hivyo ndivyo Kagame alivyofanikiwa kuzima uasi wa Karegeya aliyekua mkuu usalama wa taifa la Rwanda (NISS).
____________
Habari hii inapatikana ktk kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kitabu chenye kurasa zaidi ya 700 chenye mengi ya kujifunza.

[HASHTAG]#MyTake[/HASHTAG]:
Habari hii ya Kanali Karegeya inatufundisha kutomuamini yeyote kwenye harakati za mapambano. Karegeye alimuamini Gafaranga kwa sababu tu alikua kijana wake wa kazi. Karegeye hakujua kama kijana huyo aliyemuamini sana ndiye atakayekuja kumuua.

Wakati Karegeya anaasi serikali ya Kagame, na kukimbilia Afrika ya kusini, Gafaranga nae alijifanya kuasi. Akaanza kuwasiliana na Karegeya kwa siri jinsi ya kumpindua Kagame. Kumbe Gafaranga yupo kazini.

Karegeya pamoja na kwamba alishawahi kuwa mkuu wa shirika la ujasusi la Rwanda hakujua kama ule ni mtego. Alidhani Gafaranga ameasi kweli. Akampa siri zote. Gafaranga nae akazifikisha kwa Kagame.

Kagame akaongeza watu wawili nchini Afrika kusini. Watu hao Gafaranga aliwaingiza chumbani kwake na kuwaficha bafuni. Karegeya alipoingia wakaibuka kutoka bafuni na kumuua kabla ya kutokomea.

Na kwa kuwa walikua wanatumia majina bandia haikua rahisi kuwakamata. Walitoroka kwa barabara kwa kupitia mpaka wa Msumbiji na baadae Tanzania kisha Rwanda.

Hili liwe funzo kwetu hasa kwa vijana wanaofanya siasa za upinzani. Vijana wengi wa opposition nchini (hasa Chadema) hutokea sana kuwaamini watu kwa jina tu la "kamanda". Umekutana na mtu siku mbili anajiita Kamanda, unamuamini na kumpa siri zako. Kumbe mwenzio yupo kazini.

Wapo watu wa usalama wengi wanaovaa magwanda, wanashiriki mikutano ya chama, wanachangia chama, na wengine wanakuwa hadi viongozi wa chama lakini ni ma "agent" wapo kazini. Mtu anajiunga na chama chenu kutokea chama kingine, hata miezi miwili hana anapewa nafasi ya kugombea uongozi. Mnamuamini kiasi gani?

Usimuamini mtu kirahisi kwa kigezo tu cha ukamanda. Jipe muda wa kutosha kujiridhisha. Yupo mtu anaweza kuitukana serikali ukadhani ni mwenzio ukaungana nae, kumbe yeye ana kazi maalumu. Ukaingia mtegoni, ukanasa. Be careful.!

Kujifunza haya na mengine mengi tafuta kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kina madini mengi ya kujifunza. Ni kurasa 700 zilizosheheni. Kinapatikana kwa TZS 80,000/= tu. Wasiliana na Yericko kupitia 0715 865 544.

Picha chini ni Kanali Patrick Karegeya enzi akiwa Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Rwanda (NISS).

97d28a8121b10e0486b49e289d9e3992.jpg
Ok
 
Nimekusoma mkuu! Pia ukiisoma historia ya dikteta mobutu sese seko wa jamhuri ya kongo enzi hizo ikiitwa zaire utakutana na kisa kinachofanana na hicho, kinamhusu mtu mmoja aliyeitwa alphonce Bangala(colonel bangala) aliyekuwa mkuu wa mkoa wa leopordville(Kinshasa) huyu naye alitumiwa na mobutu kumtrack down hasimu mkubwa wa mobutu kwa kujifanya yupo naye Bega kwa Bega katika harakati za kumngoa mobutu madarakani! Matokeo yake aliwa snitch na kupelekea maafisa kadhaa wa jeshi pamoja na mawaziri maarufu kunyongwa hadharani hadi kufa!! Na kibaraka wa mobutu aliyekuwa na kazi za kutunga na kuimba nyimbo za kumtukuza dikteta mobutu (Franco Lwambo lwanzo makiadi)alitunga wimbo wa kumsifia Bangala kwa u snitch wake! Wimbo unaitwa colonel bangala, colonel bangala,obongise munene na vila ya kinshasa( colonel bangala umifanyia makubwa jiji la kinshasa) huwa namfananisha bangala na bashite(sorry)
 
Kachero ni kachero hawabadiriki ni kawaida yao,wanaendelea kutoa taarifa za ukachero hata wakishastaafu kazi yao.
NCCR Mageuzi uanzishwaji wake kama chama cha siasa na watu kama Mabele Marandu kachero nguli aliemtwaga risasi commando Tamimu wa JWTZ,aliedaiwa kupanga mbinu za kumuua Mwl.Nyerere na kupindua serikali yake.
Kulikuwa na kada maarufu wa CCM Lumumba political scientist Prince Bagenda na kurudi kuwa mshauri wa viongozi wakuu wa serikali.
Tunakumbuka mwanasheria mahili Dr Masumbuko Lamwai alivyorejea CCM
Tulimwona Mrema hakuwahi kuanzisha chama bali kusambalatisha vyama NCCR Mageuzi ,TLP akavisambaratisha kila alipokaribishwa,wala hakuwahi kurejesha kadi ya uanachama wa CCM.
Juzi juzi yupo profesa alituhumiwa na tume ya bunge akiwa mjumbe au mwenyekiti wa bodi ya mgodi wa Mwadui,lakini raisi Magu akasema alikuwa under cover yaani kachero wa serikali.
 
Nimekusoma mkuu! Pia ukiisoma historia ya dikteta mobutu sese seko wa jamhuri ya kongo enzi hizo ikiitwa zaire utakutana na kisa kinachofanana na hicho, kinamhusu mtu mmoja aliyeitwa alphonce Bangala(colonel bangala) aliyekuwa mkuu wa mkoa wa leopordville(Kinshasa) huyu naye alitumiwa na mobutu kumtrack down hasimu mkubwa wa mobutu kwa kujifanya yupo naye Bega kwa Bega katika harakati za kumngoa mobutu madarakani! Matokeo yake aliwa snitch na kupelekea maafisa kadhaa wa jeshi pamoja na mawaziri maarufu kunyongwa hadharani hadi kufa!! Na kibaraka wa mobutu aliyekuwa na kazi za kutunga na kuimba nyimbo za kumtukuza dikteta mobutu (Franco Lwambo lwanzo makiadi)alitunga wimbo wa kumsifia Bangala kwa u snitch wake! Wimbo unaitwa colonel bangala, colonel bangala,obongise munene na vila ya kinshasa( colonel bangala umifanyia makubwa jiji la kinshasa) huwa namfananisha bangala na bashite(sorry)
mkuu
mm ni mpenzi mkubwa wa nyimbo za Franco luambo,ni kweli kuwa alikuwa kibaraka wa dikteta Mobutu,mwaka 1984 alimtungia wimbo wa kampeni uitwao candidate na bisso Mobutu
Franco na Mobutu walikuwa wanakosana mda mwingine mfano miaka ya 1970 Franco aliwekwa jela miez kadhaa kwa kutunga nyimbo ya kumkosoa Mobutu kabla hajawa kibaraka wake
Franco alipofariki 1989,Mobutu alitangaza cku 5 za maombolezo msiba wa Franco ulitikisa Africa nzima
Franco hadi anafariki alikuwa na albamu 200 na nyimbo moja moja(single) zaidi ya 1500
dikteta Mobutu mwisho wake ulikuwa mbaya alijapnduliwa 1998 na alifia morocco akazikwa kama mbwa na watu 3
 
Nimekusoma mkuu! Pia ukiisoma historia ya dikteta mobutu sese seko wa jamhuri ya kongo enzi hizo ikiitwa zaire utakutana na kisa kinachofanana na hicho, kinamhusu mtu mmoja aliyeitwa alphonce Bangala(colonel bangala) aliyekuwa mkuu wa mkoa wa leopordville(Kinshasa) huyu naye alitumiwa na mobutu kumtrack down hasimu mkubwa wa mobutu kwa kujifanya yupo naye Bega kwa Bega katika harakati za kumngoa mobutu madarakani! Matokeo yake aliwa snitch na kupelekea maafisa kadhaa wa jeshi pamoja na mawaziri maarufu kunyongwa hadharani hadi kufa!! Na kibaraka wa mobutu aliyekuwa na kazi za kutunga na kuimba nyimbo za kumtukuza dikteta mobutu (Franco Lwambo lwanzo makiadi)alitunga wimbo wa kumsifia Bangala kwa u snitch wake! Wimbo unaitwa colonel bangala, colonel bangala,obongise munene na vila ya kinshasa( colonel bangala umifanyia makubwa jiji la kinshasa) huwa namfananisha bangala na bashite(sorry)
Mkuu huo wimbo colonel bangala upo ktk albamu IPI?
au n ule fc 105 du Gabon?
 
Kanali Patrick Karegeya alikuwa mkuu wa wa shirika la ujasusi la Rwanda (NISS) na Apollo Gafaranga alikuwa mmoja wa Informer wake. Karegeya alijaribu kumpindua Kagame ktk jaribio lililoshindwa kabla ya kukimbilia nchini Afrika Kusini kuishi Uhamishoni. Serikali ya Afrika kusini ilimpa ulinzi wa askari na wanausalama ili Kagame asiweze kumfuatilia huko.

Baada ya Karegeya kukimbilia Afrika kusini, haraka sana Kagame akaunda kikosi cha kumfuatilia huko kilichoitwa "Escandot de la Mort" yani kikosi cha kifo. Kagame akamteua Appolo Gafaranga kuwa mmoja wa wajumbe wa kikosi hicho. Huyu ni yule aliyekuwa informer wa Patrick Karegeye.

Kikosi hiko kikapewa mafunzo maalumu na jukumunmoja tu la kumuua Karegeya na washitika wake. Mwaka 2010 Apollo Gafaranga akaanza mawasiliano ya siri na Patrick Karegeye akijifanya anachukizwa sana na utawala wa Kagame. Karegeya akafurahi kuwa amepata mshirika wa kumng'oa Kagame. Wakaendelea kuwasiliana.

Gafaranga akawa anasafiri mara kadhaa kwenda Afrika kusini kukutana na Karegeya na kupanga mipango ya kumpindua Kagame. Mara zote Karegeya alikua na ulinzi wa wana usalama aliopewa na serikali ya Afrika kusini. Gafaranga akamshauri Karegeye awakatae askari hao waliokuwa wakimlinda kwa kuwa wanaweza kutumika kuvujisha siri. Karegeya akapokea ushauri huo na kuomba serikali ya Afrika kusini imuondolee ulinzi huo.

Disemba 25 mwaka 2013 Gafaranga aliwasiliana na Karegeya na akapanga kwenda kumsalimia Afrika kusini. Alifika Afrika kusini na akapokelewa na rafiki yake Karegeya ambaye alikua amemchukulia chumba kwenye hoteli ya Sandton, mjini Johanersburg.

Gafaranga na Karegeya wakawa wanakutana chumbani hapo kupanga namna ya kumpindua Kagame. Disemba 31 Karegeya akaenda chumbani humo. Alipoingia, akaweka kibao "do not disturb". Alipoingia ndani wakati akiongea na rafiki yake, mara wakatokea watu wawili waliokua wamejificha bafuni. Wakampiga risasi kwa kutumia silaha yenye kiwambo cha sauti. Walipohakikisha wamemuua wakamlaza kitandani wakamfunika na kuondoka. Hivyo ndivyo Kagame alivyofanikiwa kuzima uasi wa Karegeya aliyekua mkuu usalama wa taifa la Rwanda (NISS).
____________
Habari hii inapatikana ktk kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kitabu chenye kurasa zaidi ya 700 chenye mengi ya kujifunza.

[HASHTAG]#MyTake[/HASHTAG]:
Habari hii ya Kanali Karegeya inatufundisha kutomuamini yeyote kwenye harakati za mapambano. Karegeye alimuamini Gafaranga kwa sababu tu alikua kijana wake wa kazi. Karegeye hakujua kama kijana huyo aliyemuamini sana ndiye atakayekuja kumuua.

Wakati Karegeya anaasi serikali ya Kagame, na kukimbilia Afrika ya kusini, Gafaranga nae alijifanya kuasi. Akaanza kuwasiliana na Karegeya kwa siri jinsi ya kumpindua Kagame. Kumbe Gafaranga yupo kazini.

Karegeya pamoja na kwamba alishawahi kuwa mkuu wa shirika la ujasusi la Rwanda hakujua kama ule ni mtego. Alidhani Gafaranga ameasi kweli. Akampa siri zote. Gafaranga nae akazifikisha kwa Kagame.

Kagame akaongeza watu wawili nchini Afrika kusini. Watu hao Gafaranga aliwaingiza chumbani kwake na kuwaficha bafuni. Karegeya alipoingia wakaibuka kutoka bafuni na kumuua kabla ya kutokomea.

Na kwa kuwa walikua wanatumia majina bandia haikua rahisi kuwakamata. Walitoroka kwa barabara kwa kupitia mpaka wa Msumbiji na baadae Tanzania kisha Rwanda.

Hili liwe funzo kwetu hasa kwa vijana wanaofanya siasa za upinzani. Vijana wengi wa opposition nchini (hasa Chadema) hutokea sana kuwaamini watu kwa jina tu la "kamanda". Umekutana na mtu siku mbili anajiita Kamanda, unamuamini na kumpa siri zako. Kumbe mwenzio yupo kazini.

Wapo watu wa usalama wengi wanaovaa magwanda, wanashiriki mikutano ya chama, wanachangia chama, na wengine wanakuwa hadi viongozi wa chama lakini ni ma "agent" wapo kazini. Mtu anajiunga na chama chenu kutokea chama kingine, hata miezi miwili hana anapewa nafasi ya kugombea uongozi. Mnamuamini kiasi gani?

Usimuamini mtu kirahisi kwa kigezo tu cha ukamanda. Jipe muda wa kutosha kujiridhisha. Yupo mtu anaweza kuitukana serikali ukadhani ni mwenzio ukaungana nae, kumbe yeye ana kazi maalumu. Ukaingia mtegoni, ukanasa. Be careful.!

Kujifunza haya na mengine mengi tafuta kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI cha Yericko Nyerere. Kina madini mengi ya kujifunza. Ni kurasa 700 zilizosheheni. Kinapatikana kwa TZS 80,000/= tu. Wasiliana na Yericko kupitia 0715 865 544.

Picha chini ni Kanali Patrick Karegeya enzi akiwa Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Rwanda (NISS).

97d28a8121b10e0486b49e289d9e3992.jpg

Sio kweli.. Wala haikuwa hivyo. mambo mengi yamepotoshwa hapo.. Yericko Nyerere ulitakiwa kufanya research ya kutosha kabla hujaandika kuhusu kisa cha Karegeya
 
Back
Top Bottom