chambulilo
JF-Expert Member
- Aug 19, 2013
- 217
- 38
Ndugu wana jamii forum, kumekuwa na malumbano makubwa sana kuhusiana na mafanikio ya ziara zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa na makatibu wakuu wawili wa vyama vikubwa vya siasa hapa nchini, CCM na CHADEMA.
Hivi karibuni Katibu mkuu wa CCM, ndugu Kinana, alikuwa na ziara ya mikoa ya Ruvuma, Mbeya na Njombe. Tayari ndugu Kinana ameisha maliza ziara yake hiyo.
Katibu mkuu wa CHADEMA, Dr. Slaa anaendelea na ziara yake kwa mikoa ya Shinyanga, Kgoma, Tabora na Singida. Tayari Dr. Slaa ameishamaliza ziara yake katika mikoa ya Shinyanga na Kigoma.
Ndugu wana jamiiforum, niawaomba sasa tutumie vigezo vifuatavyo kupima mafanikio ya ziara za makatibu wa kuu hawa wawili katika mikoa miwili tu; yaani Ruvuma na Mbeya kwa Kinana; Shinyanga na Kigoma kwa Dr. Slaa.
VIGEZO
Ndugu wana jamiiforum naomba niishie hapa. Nimatumaini yangu tutatumia vigezo hivi kikamilifu na kwa uaminifu mkubwa bila kupendelea upande wowote. Majadiliano mema!
Hivi karibuni Katibu mkuu wa CCM, ndugu Kinana, alikuwa na ziara ya mikoa ya Ruvuma, Mbeya na Njombe. Tayari ndugu Kinana ameisha maliza ziara yake hiyo.
Katibu mkuu wa CHADEMA, Dr. Slaa anaendelea na ziara yake kwa mikoa ya Shinyanga, Kgoma, Tabora na Singida. Tayari Dr. Slaa ameishamaliza ziara yake katika mikoa ya Shinyanga na Kigoma.
Ndugu wana jamiiforum, niawaomba sasa tutumie vigezo vifuatavyo kupima mafanikio ya ziara za makatibu wa kuu hawa wawili katika mikoa miwili tu; yaani Ruvuma na Mbeya kwa Kinana; Shinyanga na Kigoma kwa Dr. Slaa.
VIGEZO
- Vurugu katika mikutano (mfano:- kurushwa mawe, mabomu ya machozo na mabango)
- Wingi wa kupokea wanachama wapya; kutoka vyama hasimu au watu wasio na chama
- Idadi ya mashina ya wakereketwa yaliyofunguliwa
- Ukamilifu wa ratiba (Yaani kufuata ratiba ilivyo pangwa kikamilifu)
- Kuvunjika kwa mikutano
- Idadi ya watu waliohudhuria mikutano ya hadhara
Ndugu wana jamiiforum naomba niishie hapa. Nimatumaini yangu tutatumia vigezo hivi kikamilifu na kwa uaminifu mkubwa bila kupendelea upande wowote. Majadiliano mema!