Tupeane maujuzi jinsi ya kupata tenda serikalini!

Hata mimi ndio nilikuwa nawaza hivyo mkuu.
Mbongo hajawahi kutenda haki kwa kuufatisha mfumo hata siku moja.
Network Network network


Ndio kila kitu mfumo wa TanePs na GPSA ni mifumo tu mwisho wa siku nyuma ya hiyo mifumo wapo watu.


Kujua utamu wa ngoma ingia ucheze.

Je kampuni yako umeshaisajiri ? Ina muda gani ? Imeshapewa vibali vya GPSA (Vibali vya GPSA hutoka Mara 2 kwa mwaka )..


Kama majibu ya maswali yote hapo juu ni ndio uko sawa kuanza hustles , lakini nakushauri ungeanza na hata sector binafsi. Huko hawahitaji mambo ya GPSA au TanePs na mavibali Yao.


Wewe ni kuwa na Brela incorporation Certificate, Tin number , Bussiness licence , tax clearance na EFD machine tayari tenda unaanza kupiga. Ila huku serikalini daah Mambo mengi muda mchache.


Uliza swali lolote pm au hapa ujibiwe.
 
Mkuu Soma hapo juu nimeandika vizuri documents gani unapaswa kuwa nazo ili iwe timilifu kuanza kubid tender za Serikali. Naomba upitie comment yangu hapo juu nimeeeleza kiundani na ushauri wangu.


Kingine Cha kukushauri eneo lako la kazi inabidi uwe mvumilivu maana Lina kazi chache Sana serikalini. Ningekushauri maeneo mengine ya kufanya kazi ili iwe rahisi kwako kupata kazi ukiwa unaendelea kukua. Nina rafiki yangu ana kampuni inayofanya kazi Kama yako huko serikalini anapata kazi chache Sana Tena kwa mbinde sana. Ndio maana juu hapo nikasema angalia upande wa secta binafsi ( NGO n.k ) . Huko ndiko anapata tenders nyingi.


Nakukumbusha tu kuwa na kampun sio issue ila Jambo la msingi ni kwanini unakuwa na kampuni ? .. Una mikakati gani ? Tender utapata vipi ( Public au private sector ).. Hayo maswali inabidi uwe na majibu kabla hujafungua kampuni kinyume na Hapo utakuwa na kampuni jina tu na hufanyi lolote.

Kumbuka kampuni Ni gharama , kila mwaka Kuna Kodi mbalimbali lazima ulipie kuanzia tra , halmashauri au wizarani wanakotoa bussiness license. Sasa unapokuwa na kampuni hujui utafanyaje kazi lazima utaifunga na itakuingiza hasara na utaifunga.
mkuu umeelezea vyema .hivi kupata tenda private sector naon wana vigezo vingi kuliko government ....mfano kweny mining companies? .

Maan nikipita ''tenda mpya'' website naon vigezo vigumu
 
Nataka tenda ya usafi wa barabara nna kila kitu kasoro konektion tuuu
Sumajkt washaingia huku ..... Kibaya experience na vifaa vinatukosesha tenda ...subiri watangaze manispaa , usisite kwenda kuuliza au kupitia taneps kila siku
 
Ukiomba private sector utapata, ila kwa government sector kuna vigezo vingi haijalishi ni tenda ya usafi
Mimi nilifikiri private sector ndio ina vigezo vingi na kujuana kwa asilimia kubwa sana...

Government vigezo ni documentation ,experience na financial capability kwa NCB , na CUIS ni bei tu kupitia Taneps.

Nafikiria kudeal na private ila nikisoma bidding docs zao naona mambo mengi sana ,hasa lines of credit ,wakati credit exposure yangu ni ndogo nategemea internal financing ya mfukoni ya kula....
 
Kwa wale wajuzi wa mambo tupeane maujuzi ya jinsi ya kupata tenda ndogondogo na kubwa kubwa mfano tenda za ujenzi wa majengo mbalimbali ya serikali kama zahanati katika halmashauri za wilaya zetu.
We mzee eti wanasem siku hizi bila lifti haufiki.
 
Mkuu Soma hapo juu nimeandika vizuri documents gani unapaswa kuwa nazo ili iwe timilifu kuanza kubid tender za Serikali. Naomba upitie comment yangu hapo juu nimeeeleza kiundani na ushauri wangu.


Kingine Cha kukushauri eneo lako la kazi inabidi uwe mvumilivu maana Lina kazi chache Sana serikalini. Ningekushauri maeneo mengine ya kufanya kazi ili iwe rahisi kwako kupata kazi ukiwa unaendelea kukua. Nina rafiki yangu ana kampuni inayofanya kazi Kama yako huko serikalini anapata kazi chache Sana Tena kwa mbinde sana. Ndio maana juu hapo nikasema angalia upande wa secta binafsi ( NGO n.k ) . Huko ndiko anapata tenders nyingi.


Nakukumbusha tu kuwa na kampun sio issue ila Jambo la msingi ni kwanini unakuwa na kampuni ? .. Una mikakati gani ? Tender utapata vipi ( Public au private sector ).. Hayo maswali inabidi uwe na majibu kabla hujafungua kampuni kinyume na Hapo utakuwa na kampuni jina tu na hufanyi lolote.

Kumbuka kampuni Ni gharama , kila mwaka Kuna Kodi mbalimbali lazima ulipie kuanzia tra , halmashauri au wizarani wanakotoa bussiness license. Sasa unapokuwa na kampuni hujui utafanyaje kazi lazima utaifunga na itakuingiza hasara na utaifunga.
Kwa kampuni za nje zilizojisajili nchini kwao zinawezaje kupata tenda za ndani kwa mfano kuwa vendor wa sugar mills parts na agricultural machines?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom