Tupe uzoefu wako!!!!

mwallu

JF-Expert Member
Sep 5, 2013
6,787
4,207
Nashukuru Mungu kampeni dhidi ya ukatili wa kijinsia imepamba moto,pengine itasaidia kufuta kabisa ukatili dhidi ya wanawake na watoto.Mie nachukia sana ukatili dhidi ya mtu yeyote bila kujali jinsia.

Kuna huu ukatili kwa mwanamke kipindi cha ujauzito: kuna wanawake wengi wamepitia ukatili huu kwa namna tofauti tofauti..(kutokumjali mjamzito ni ukatili wa hali ya juu sana)

Dada yangu mie alipobeba ujauzito wake wa pili shemeji yetu alibadilika sana,kwanza akwa mkali kama pilipili kichaa,dada akimuomba amletee ukwaju anakataa,ubuyu hataki ,hata zile ice cream za bakhresa akawa mbishi kuleta.Tukimuuliza kwa nini anamfanyia hivyo mwenzie anasema dada anatumia mimba kumpanda kichwani.

Hakuna siku iliniuma sana kama ile dada alipomfumania shemeji akiwa restaurant ya jirani na nyumbani kwao,mida ya saa moja jioni,yuko na mwanamke wanalishana kwa midomo,cha ajabu shemeji wala hakushtuka,ndo kwaanza akaanza kumgombeza dada kafata nini hapo,dada alipoanza kugomba pale aliambulia makofi na mateke ya kumtosha tu hadi akazimia.

Alizinduka baada ya masaa matatu akiwa hospitali..na shemeji hakuonekana nyumbani wiki nzima.
Ilibidi dada arudi nyumbani..mpaka amejifungua,hataki tena kurudi kwa shemeji.Wakina mama wanamshauri arudi tu kwa mumewe maana huyo ni mumewe.
Baada ya Kujifungua Shemeji anakuja nyumbani kila jioni..na zawadi nyingi nyingi tu.

Wewe,jirani,ndugu jamaa yako,je alishawahi kupitia ukatili wowote au changamoto zozote kutoka kwa mwenzi wake kipindi cha ujauzito? alikabiliana nazo vipi? baada ya ukatili huo ndoa ama mahusiano yaliendelea?

cc:mad:Kaizer ladyfurahia Passion Lady Lady Docto Arushaone Erickb52 Sungura2013 Mapi amu Husninyo Heaven on Earth DEMBA miss strong Baba V Mentor Excel Mamndenyi Ablessed Kongosho Rich woman kiwatengu shansarie miss chagga et al
 
Last edited by a moderator:
Kuna huu ukatili kwa mwanamke kipindi cha ujauzito: kuna wanawake wengi wamepitia ukatili huu kwa namna tofauti tofauti..(kutokumjali mjamzito ni ukatili wa hali ya juu sana)

Dada yangu mie alipobeba ujauzito wake wa pili shemeji yetu alibadilika sana,kwanza akwa mkali kama pilipili kichaa,dada akimuomba amletee ukwaju anakataa,ubuyu hataki ,hata zile ice cream za bakhresa akawa mbishi kuleta.Tukimuuliza kwa nini anamfanyia hivyo mwenzie anasema dada anatumia mimba kumpanda kichwani.

Mkuu umemsema dada yako tu, na hapa umesema wengi hupitia ukatili huu. Je ni wajawazito wangapi husalitiwa na kupigwa?

Ice cream, ubuyu, ukwaju ni lazima mumeo alete? Kwani huwezi kumuagiza mtu mwingine ama zikipita ununue?
 
dah! mi najua cases za wanawake kuchukia wanaume zao. wakati nasoma nikahisi labda huyo baba kaichukia tu mimba ila mpaka kufumaniwa jamani na kutwangana makofi!!! too much.
 
Mkuu umemsema dada yako tu, na hapa umesema wengi hupitia ukatili huu. Je ni wajawazito wangapi husalitiwa na kupigwa?

Ice cream, ubuyu, ukwaju ni lazima mumeo alete? Kwani huwezi kumuagiza mtu mwingine ama zikipita ununue?

ujue mambo madogo madogo tu yanaweza mpa furaha mkeo. kuletewa na mume kuna raha yake bana hata kama waweza nunua mwenyewe.
 
Hili swali liko strategic sana.

Mkuu umemsema dada yako tu, na hapa umesema wengi hupitia ukatili huu. Je ni wajawazito wangapi husalitiwa na kupigwa?

Ice cream, ubuyu, ukwaju ni lazima mumeo alete? Kwani huwezi kumuagiza mtu mwingine ama zikipita ununue?
 
Mwallu mi nasikiaga but I do wish to hear more hum ndani.......

I cant imagine dada alivyokuwa hurted baada ya kumfumania shemeji
 
Mkuu umemsema dada yako tu, na hapa umesema wengi hupitia ukatili huu. Je ni wajawazito wangapi husalitiwa na kupigwa?

Ice cream, ubuyu, ukwaju ni lazima mumeo alete? Kwani huwezi kumuagiza mtu mwingine ama zikipita ununue?

What If unaishi na mumeo tu!!!!!!!!!lets say unapenda ubuyu wa mama mwaj....

na unapouzwa ni njia ambayo mumeo huwa anapita kila siku..INAKUWAJE!!!!
 
nimemtumia dada yangu kama mfano..yanayomkuta najua kuna wengi yamewakuta,pengine zaidi ya hayo..kuhusu ubuyu na ukwaju,ushawahi kuona mjamzito anakaa na shati la mumewe? kila wakati anavuta harufu yake? kwa nini asikae na shati la mwingine?
Mkuu
umemsema dada yako tu, na hapa umesema wengi hupitia ukatili huu. Je ni
wajawazito wangapi husalitiwa na kupigwa?

Ice cream, ubuyu, ukwaju ni lazima mumeo alete? Kwani huwezi kumuagiza
mtu mwingine ama zikipita ununue?
 
yaani huyu,halafu hana aibu hata karibia na nyumbani anafanyia uwehu wake?
dah! mi najua cases za
wanawake kuchukia wanaume zao. wakati nasoma nikahisi labda huyo baba
kaichukia tu mimba ila mpaka kufumaniwa jamani na kutwangana makofi!!!
too much.
 
ujue mambo madogo madogo tu yanaweza mpa furaha mkeo. kuletewa na mume kuna raha yake bana hata kama waweza nunua mwenyewe.

Bi dada unaongea tu,
Mimi nilishapeleka ubuyu umeandikwa wa zanzibar kabisa nikijua leo ntalala kwa amani nikaambiwa sitaki huu nataka unaouzwa dukani kwa fulani! Huyo fulani simjui na nnajua mke wangu kuelekeza ni mzito....first month

Sometimes nahisi mnatukomoa. Nunueni tu ubuyu wenu wenyewe.


Hili swali liko strategic sana.

Kiukweli nachukia sana ubuyu!
 
Hakuna kipindi kigumu wanawake wanapitia ni kipindi cha ujauzito, ukichunguza sana kipindi hiki akina baba huwa ndio kasi ya nyumba ndgo inaongezeka sana, hawajali tena familia zao ukiuliza sababu ohhh, mke wangu hataki kuniona, ananichukia na sababu nyingine nyingi lakini hazina ukweli wowote. Kwa mwanaume anayejitambua na kutambua thamani ya mke ni kipindi ambacho anatakiwa awekaribu mno na familia yake. Akina baba amkeni jamani!
 
alikua so hurt yani..ukizingatia alikua anatamani kila wakati awe karibu nae
Mwallu mi nasikiaga but I do wish to hear more hum ndani.......

I cant imagine dada alivyokuwa hurted baada ya kumfumania shemeji
 
Hapa kuna vitu viwili, Umeoanisha cheating na ukatili wa wanawake wajawazito. Mi binafsi naona haihusiani kwa kuwa huyo shemeji angeweza kufumaniwa hata kama mkewe si mjamzito. Kicheche ni kicheche tu sema this time alicheat openly akijua dada yako hatoki nyumbani oftenly.

Kutoletewa ubuyu sioni kama unyanyasaji wa kijinsia. Matatizo yalikuja kwa kufumaniwa and not otherwise.
 
nimemtumia dada yangu kama mfano..yanayomkuta najua kuna wengi yamewakuta,pengine zaidi ya hayo..kuhusu ubuyu na ukwaju,ushawahi kuona mjamzito anakaa na shati la mumewe? kila wakati anavuta harufu yake? kwa nini asikae na shati la mwingine?

Kwa ukatili kweli thats too much. Ila mama mbona mi sikumuona anasumbua hivyo? Ama nilikuwa too young to notice?
Pinga ukatili and i am right there with u ila ubuyu!!
 
sijawah ona anaenyanyaswa mwallu ...hvo vijitabia wakati wa mimba vinasumbuaaa! Mara ooh nataka supu ya pweza, nataka chipsi za kwa a'su'mani, makande ya magadi..vikiletwa hali. Inakera sana kwa wengne na ni furaha kwa wengne... Kumpiga mama mwenye mimba ni zaidi ya kuwa na mtindio wa ubongo, haisameheki asilani. Humtaki mwache aende zake.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna kipindi kigumu wanawake wanapitia ni kipindi cha ujauzito, ukichunguza sana kipindi hiki akina baba huwa ndio kasi ya nyumba ndgo inaongezeka sana, hawajali tena familia zao ukiuliza sababu ohhh, mke wangu hataki kuniona, ananichukia na sababu nyingine nyingi lakini hazina ukweli wowote. Kwa mwanaume anayejitambua na kutambua thamani ya mke ni kipindi ambacho anatakiwa awekaribu mno na familia yake. Akina baba amkeni jamani!
Bora mimba ikuchukie aisee
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom