Lihakanga
JF-Expert Member
- Dec 17, 2016
- 4,829
- 6,376
Asalam Aleikum, Bwana apewe sifa, tumsifu Yesu Kristo. Nakusalimuni nyote kila mmoja kwa imani yake.
Ninaitwa Britho Lihakanga, ninaishi Tabata. Najua mtashangaa kuona leo ninaanika details zangu wazi. Sina uhakika na kesho yangu.
Kwa kifupi ni kwamba nina siku ya tano leo, nikipigania kesho yangu. Si kwa maana ya juma lijalo, la hasha ni siku inayofuata baada ya leo.
Ninajifukiza usiku usiku na mchana, mara ninapata nafuu, mara ninazidiwa. Sijakata tamaa, ninapigania uzima, japo ni Mungu tu ndiye anayeninusuru.
Nipo kitandani, sina hata hamu ya kuangalia TV, nikiulizia taarifa za habari zimebeba jambo gani zito, ninaambiwa misiba sana na karibu kila kona ya nchi ni misiba inayotokana na kushindwa kupumua vizuri.
Nimepata wazo kuwa tutakwisha huku mamlaka zimekaa kimya. Ni misiba ya wakubwa tu inatangazwa. Nina uhakika digidigi huku chini tutakuwa tunapukutika.
Tupaze sauti, vinginevyo tutakwisha. Tumwabie baba Jesca, lockdown haikwepeki, japo ni ile ya kiaina, shule zifungwe, tupunguze msongamano usio wa lazima na kila mmoja aseme wazi kwamba covid 19 is back and it is in another level.
Nikipona nitakuja kuandika tena. Vinginevyo, BuURIANI nyote ndani na nje ya JF.
Ninaitwa Britho Lihakanga, ninaishi Tabata. Najua mtashangaa kuona leo ninaanika details zangu wazi. Sina uhakika na kesho yangu.
Kwa kifupi ni kwamba nina siku ya tano leo, nikipigania kesho yangu. Si kwa maana ya juma lijalo, la hasha ni siku inayofuata baada ya leo.
Ninajifukiza usiku usiku na mchana, mara ninapata nafuu, mara ninazidiwa. Sijakata tamaa, ninapigania uzima, japo ni Mungu tu ndiye anayeninusuru.
Nipo kitandani, sina hata hamu ya kuangalia TV, nikiulizia taarifa za habari zimebeba jambo gani zito, ninaambiwa misiba sana na karibu kila kona ya nchi ni misiba inayotokana na kushindwa kupumua vizuri.
Nimepata wazo kuwa tutakwisha huku mamlaka zimekaa kimya. Ni misiba ya wakubwa tu inatangazwa. Nina uhakika digidigi huku chini tutakuwa tunapukutika.
Tupaze sauti, vinginevyo tutakwisha. Tumwabie baba Jesca, lockdown haikwepeki, japo ni ile ya kiaina, shule zifungwe, tupunguze msongamano usio wa lazima na kila mmoja aseme wazi kwamba covid 19 is back and it is in another level.
Nikipona nitakuja kuandika tena. Vinginevyo, BuURIANI nyote ndani na nje ya JF.