TUONGEE KIUME: Mwenzetu aliletewa watoto wake baa na mkewe...

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Apr 15, 2020
1,664
2,517
Kama una kawaida ya kwenda baa utakuwa unaelewa kuwa hiyo ndiyo sehemu hutokea mambo ya kushangaza zaidi ya sehemu yoyote ile. Nina uhakika ukiwa huko umewahi kushuhudia mzee mtu mzima akiwa amelewa chakari, amevua shati liko mabegani, anacheza wimbo wa ‘chizi karogwa tena’.

Lakini nakuhakikishia, katika mambo yote ya kushangaza niliyowahi kuyaona baa hakuna kitakachozidi siku nilipoona mwanamume ameletewa watoto wake baa na mke wake; nitakusimulia.

Mwanamume kuletewa mtoto sehemu isiyostahili sio jambo jipya kwangu. Nimewahi kuona mwanamume amepelekewa mtoto wake ofisini. Yaani jamaa alizaa na mwanamke ambaye hawaishi pamoja. Kumbe alikuwa na kawaida ya kupiga chenga kumhudumia. Siku hiyo yuko ofisini hana hili wala lile, mara anakuja kuambiwa kuna mgeni wako. Anashangaa mgeni wangu? Nani? Anakwenda mapokezi anamkuta mwanamke, mtoto wake wa miaka mitano na begi lenye nguo za mtoto. Mwanamke akamwambia “kama umeshindwa kumhudumia mtoto wako, nimekuletea umtafutie kazi ili ajihudumie.”

Lakini ya baa sikuwahi kuifikiria. Jamaa tuko naye hapa kila siku, tunakunywa naye, tunatazama mpira pamoja na wakati mwingine, hasa mwisho wa wiki tunamuacha hapa hapa.

Lakini kumbe jamaa nyumbani kwake ni kama sehemu ya kubadilishia nguo tu, yaani anarudi usiku mnene kutoka baa na anatoka majogoo kwenda kazini. Anarudi anakuta watoto wamelala, anaondoka hawajaamka.


Siku hiyo ilikuwa mwisho wa wiki, tulianza naye vizuri, tukanywa lakini mida mida tukaamua tubadilishe kijiwe, tukahamia baa nyingine. Basi mishale ya saa sita usiku hivi, hatuna hili wala lile tunashangaa mwanamke anakuja kwenye meza yetu akiwa na watoto wawili, mmoja mdogo wa miaka mitatu kambeba mwingine wa miaka sita anatembea mwenyewe.

Aisee, sijawahi kuona mwanamke kauzu kama huyo. Alipofika katusalimia tu, za saa hizi shemeji, kisha akamshusha mtoto aliyembeba huku anamwambia nenda kwa baba. Sasa jamaa yetu kabaki kaduwaa tu, haelewi nini kinaendelea, wala hajui afanye nini, ikabidi ampokee mtoto.

Basi ‘waifu’ wake akamwambia neno moja tu, ukirudi nyumbani utakuja nao. Jamaa ikabidi aulize ‘kulikoni mama Junio? Kuna tatizo gani?’

Akaambiwa wewe kila siku kurudi nyumbani unakuta watoto wamelala unaondoka hawajaamka, na sio kwamba upo bize na kazi, hapana, upo baa unapombeka. Muda kama huu ulitakiwa uwe nyumbani na familia yako. Mwisho watoto watakusahau, uje wakuite mjomba, kwa hiyo ili tusifike huko, nimekuletea watoto ukae nao hapa ili wasimsahau baba yao.

Alivyomaliza hotuba yake, akageuka, akaondoka zake. Basi mwenzetu ikabidi ainuke na watoto wake amfuate mke wake, na usiku huo hakurudi tena baa.

Ninachoweza kukwambia ni ile ilikuwa ni njia ya ajabu sana, lakini ilifanya kazi na inafaa kuwanyoosha baba wote wanaodhani jukumu lao ni kutoa pesa tu, sio kukaa karibu na familia zao.



©Mwananchi
 
kila nikiandika nafuta!
ila wanaume tuwe karibu na familia zetu tusiendekeze soka halina maana kabisa.
hata beer sio za kunywa daily sio afya.
saa 6 usiku uko bar unaangalia soka really!? kwanini tusinunue king'amuzi tukaangalia soka home au beer kadhaa tukaweka kwa fridge?
tujirekebishe
 
Yaani mpira uangalie home,lile vibe utapataje,hata bia hainogi nyumbani bhana,ni Kama unakunywa dawa ya kienyeji

Lakini uzi nimeupenda sana umenikumbusha kitu,naona wazi Kuna tafsida huyo mama aliitumia

Suala si watoto,jamaa kutokana na kurudi akiwa kalewa hakuwa anamkuna shemeji vizuri
 
Mi sipendi kelele nyingi ,mziki au kelele kibao. Kwahiyo mara nyingi nakaa home na take away zangu naangalia mpira
 
Maisha ya kuishi wawili Ni shida Sana ngoja nikupe mfano.

Rafiki yangu: Yeye tukiwa baa akisiaga wimbo wa chege ule sijui nini jiweke down Yan ule wimbo unamkuna sana tafsiri yake hapo hujue huko nyumbani wife n mtata.

Huyo mzee: mleta uzi kasimulia Kuna mzee anacheza chiz kalogwa tena mpaka kavua shati hapo ujue huyo mzee aliamua kumuheshimu mkewake akatulia akafanya kila kitu amfurahishe mkewe Ila shida mkewe kanyea kambi tena Sasa huyo mzee kaamua kurudi kwenye maisha yake.

Wanaume tunapitia mengi na maxito kwenye malezi ya watoto wetu hasa kuishi na hawa wanawake zetu Mimi sikuletewa bali nilienda kuwachukua mwenyewe na bila hvyo naamini ingekuwa n mwisho wa kupata elimu Bora na malezi Bora kutoka kwababa yao.

Sisi wababa ukiona mkeo anaurafiki na mwanamke au ndugu yake aliechika hapo ndugu yangu hesabu si muda kinawaka mbaya.

Joyce kiria yule dada na aliempa idhini ya kurusha kile kipindi sijui Kama bado kipo kile kipindi aisee kimewapoteza wanawake wengi sana kwenye ndoa na mahusiano yao.

Turudi kwenye bia: Aisee sie wanaume tuachage ujinga bia kunywa sawa Ila jiwekee kiwango Kama vp Anza mapema ili mapema uwe nyumbani kama n Mpira funga screen kubwa weka kingamuzi kizuri ongeza sauti kubwa ujisikie Kama upo uingereza yan hata watoto wakiwa wanacheza usiwasikie Mpira ukiisha punguza sauti waachie screen yao chukua bia zako mbili toa kitu nje kula bia Mdogo Mdogo.

Ila wanawake aisee n pasua kichwa Yan mwanamke mwenye akili n Mama yako tuu labda na dada zako Ila Hawa tunaokutana nao aisee n balaa.
 
Maisha ya kuishi wawili Ni shida Sana ngoja nikupe mfano.

Rafiki yangu: Yeye tukiwa baa akisiaga wimbo wa chege ule sijui nini jiweke down Yan ule wimbo unamkuna sana tafsiri yake hapo hujue huko nyumbani wife n mtata.

Huyo mzee: mleta uzi kasimulia Kuna mzee anacheza chiz kalogwa tena mpaka kavua shati hapo ujue huyo mzee aliamua kumuheshimu mkewake akatulia akafanya kila kitu amfurahishe mkewe Ila shida mkewe kanyea kambi tena Sasa huyo mzee kaamua kurudi kwenye maisha yake.

Wanaume tunapitia mengi na maxito kwenye malezi ya watoto wetu hasa kuishi na hawa wanawake zetu Mimi sikuletewa bali nilienda kuwachukua mwenyewe na bila hvyo naamini ingekuwa n mwisho wa kupata elimu Bora na malezi Bora kutoka kwababa yao.

Sisi wababa ukiona mkeo anaurafiki na mwanamke au ndugu yake aliechika hapo ndugu yangu hesabu si muda kinawaka mbaya.

Joyce kiria yule dada na aliempa idhini ya kurusha kile kipindi sijui Kama bado kipo kile kipindi aisee kimewapoteza wanawake wengi sana kwenye ndoa na mahusiano yao.

Turudi kwenye bia: Aisee sie wanaume tuachage ujinga bia kunywa sawa Ila jiwekee kiwango Kama vp Anza mapema ili mapema uwe nyumbani kama n Mpira funga screen kubwa weka kingamuzi kizuri ongeza sauti kubwa ujisikie Kama upo uingereza yan hata watoto wakiwa wanacheza usiwasikie Mpira ukiisha punguza sauti waachie screen yao chukua bia zako mbili toa kitu nje kula bia Mdogo Mdogo.

Ila wanawake aisee n pasua kichwa Yan mwanamke mwenye akili n Mama yako tuu labda na dada zako Ila Hawa tunaokutana nao aisee n balaa.
Hahahaha Hahaha

Ova
 
Bia za nyumbani sio tamu....soka la nyumbani halinogi!!!!
kila nikiandika nafuta!
ila wanaume tuwe karibu na familia zetu tusiendekeze soka halina maana kabisa.
hata beer sio za kunywa daily sio afya.
saa 6 usiku uko bar unaangalia soka really!? kwanini tusinunue king'amuzi tukaangalia soka home au beer kadhaa tukaweka kwa fridge?
tujirekebishe
 
Kumbuka....


Hata mama yako.na dada zako kuna watu wanawaona hawana akili kama ulivyoona wa wenzio
Maisha ya kuishi wawili Ni shida Sana ngoja nikupe mfano.

Rafiki yangu: Yeye tukiwa baa akisiaga wimbo wa chege ule sijui nini jiweke down Yan ule wimbo unamkuna sana tafsiri yake hapo hujue huko nyumbani wife n mtata.

Huyo mzee: mleta uzi kasimulia Kuna mzee anacheza chiz kalogwa tena mpaka kavua shati hapo ujue huyo mzee aliamua kumuheshimu mkewake akatulia akafanya kila kitu amfurahishe mkewe Ila shida mkewe kanyea kambi tena Sasa huyo mzee kaamua kurudi kwenye maisha yake.

Wanaume tunapitia mengi na maxito kwenye malezi ya watoto wetu hasa kuishi na hawa wanawake zetu Mimi sikuletewa bali nilienda kuwachukua mwenyewe na bila hvyo naamini ingekuwa n mwisho wa kupata elimu Bora na malezi Bora kutoka kwababa yao.

Sisi wababa ukiona mkeo anaurafiki na mwanamke au ndugu yake aliechika hapo ndugu yangu hesabu si muda kinawaka mbaya.

Joyce kiria yule dada na aliempa idhini ya kurusha kile kipindi sijui Kama bado kipo kile kipindi aisee kimewapoteza wanawake wengi sana kwenye ndoa na mahusiano yao.

Turudi kwenye bia: Aisee sie wanaume tuachage ujinga bia kunywa sawa Ila jiwekee kiwango Kama vp Anza mapema ili mapema uwe nyumbani kama n Mpira funga screen kubwa weka kingamuzi kizuri ongeza sauti kubwa ujisikie Kama upo uingereza yan hata watoto wakiwa wanacheza usiwasikie Mpira ukiisha punguza sauti waachie screen yao chukua bia zako mbili toa kitu nje kula bia Mdogo Mdogo.

Ila wanawake aisee n pasua kichwa Yan mwanamke mwenye akili n Mama yako tuu labda na dada zako Ila Hawa tunaokutana nao aisee n balaa.
Mjifunze kuvumiliana na kuchukuliana!!!!!!
 
Ila kuna wanaume wapole nyie mimi kabisa Ghati abebe watoto aje aniachie kisa haaaaaa sachi ndo atanitambua mi kwa kweli acha niishi kibabe tu nafuu naiona
 
Kweli kabisa ni ungese huchelewi kuanza kutukana ikifungwa, heri utoe stress za kufungwa ukiwa bar ukirudi home unakausha. Na huo ndio uanaume.

Uanaume kazi jamani, nyumba unajenga wewe Ila huifaidi hata kidogo, imagine being a man, no make up, no wigs no lipstick and you still rock and bounce them butts it's not easy (by lucky dube)

Wakati mwingine nao watuache tu watuelewe. Tatizo unakutana na limwanaume eti linasema mwanangu ukipigwa rudo nyumbani, mnalea Malaya bila sababu, mpe makavu, kama umeamua kuolewa mwenyewe please deal na mambo yako na nyumba yako ukishindwa usiniambie we pambana ukitaka kuondoka usiniambie mie baba yako nipo na mke wangu wewe ushaondoka kujenga mji wenu acha kabisa ungese.
soka na beer kunywea home hainogi
 
Back
Top Bottom