Binti Msichana
Senior Member
- Oct 9, 2016
- 109
- 247
Mwendesha kipindi amealika wazungumzaji wawili kila mmoja na mtazamo wake kuhusu siasa za Tanzania.
Anwar Saidi : Anazungumzia upepo wa siasa nchini.Amenukuu msemo wa Abraham Maslow : Ukiwa na nyundo kila tatizo unaliona msumari, amehusisha msemo huu na hatua mbalimbali za serikali za kuleta maadili kwa viongozi kwa hatua ya serikali ya kutumbua majipu bila ya kuangalia njia nyingine ya kinidhamu.Amegusia vilevile visasi na chuki za kisiasa za viongozi kwa watu wanaowapinga, ametoa mfano jinsi gani viongozi wanavyojaribu kunyamazisha wapinzani au watu wenye mawazo kinzani dhidi yao badala ya kufanyia kazi mawazo yao kwa mustakabali ya maendeleo ya watu.Mzungumzaji huyu ametoa mfano wa mataifa mbalimbali yaliyokuwa na hofu na wananchi wake kwa kuminya demokrasia.
Mzee Falijallah : Serikali hii ina uvumilivu wa hali ya juu wa kisiasa, mfano aliyekuwa kada wa CCM aliyehamia CHADEMA alipokuwa na nyadhifa mbalimbali CCM amevurunda sana badala yake amekuwa anasema hovyo kuhusu serikali hata hivyo anavumiliwa.Ameipongeza serikali ya awamu ya tano jinsi inavyopigania maisha ya Watanzania maskini kwa kuleta uadilifu serikalini na kuwawezesha kiuchumi, ametoa mfano hatua ya rais Magufuli kuruhusu wachimbaji wadogo wa dhahabu kuchimba dhahabu mgodi wa Kahama.Vilevile ameipongeza hatua ya Waziri Mkuu kuhamia Dodoma kama mji mkuu wa Tanzania.
Kipindi kinaendelea mengi yanajadiliwa.
Anwar Saidi : Anazungumzia upepo wa siasa nchini.Amenukuu msemo wa Abraham Maslow : Ukiwa na nyundo kila tatizo unaliona msumari, amehusisha msemo huu na hatua mbalimbali za serikali za kuleta maadili kwa viongozi kwa hatua ya serikali ya kutumbua majipu bila ya kuangalia njia nyingine ya kinidhamu.Amegusia vilevile visasi na chuki za kisiasa za viongozi kwa watu wanaowapinga, ametoa mfano jinsi gani viongozi wanavyojaribu kunyamazisha wapinzani au watu wenye mawazo kinzani dhidi yao badala ya kufanyia kazi mawazo yao kwa mustakabali ya maendeleo ya watu.Mzungumzaji huyu ametoa mfano wa mataifa mbalimbali yaliyokuwa na hofu na wananchi wake kwa kuminya demokrasia.
Mzee Falijallah : Serikali hii ina uvumilivu wa hali ya juu wa kisiasa, mfano aliyekuwa kada wa CCM aliyehamia CHADEMA alipokuwa na nyadhifa mbalimbali CCM amevurunda sana badala yake amekuwa anasema hovyo kuhusu serikali hata hivyo anavumiliwa.Ameipongeza serikali ya awamu ya tano jinsi inavyopigania maisha ya Watanzania maskini kwa kuleta uadilifu serikalini na kuwawezesha kiuchumi, ametoa mfano hatua ya rais Magufuli kuruhusu wachimbaji wadogo wa dhahabu kuchimba dhahabu mgodi wa Kahama.Vilevile ameipongeza hatua ya Waziri Mkuu kuhamia Dodoma kama mji mkuu wa Tanzania.
Kipindi kinaendelea mengi yanajadiliwa.