Wana JF,
Kumekuwa na watu wanaodhani baadhi ya viongozi CCM ni waadilifu na wapiganaji wa maslahi ya wananchi. Watu wengine wamefikia hatua ya kuwaita wanaowakosoa hao malaika wao wa CCM kuwa ni watu wanaotumiwa na mafisadi kuwadhoofisha.
Tunaotaka ukweli usichanganywe na kitu chochote tunawaona watu kama Samwel Sita, Maghufuli na wengine kuwa si lolote si chochote au ni lolote lakini hawajafikia viwango vya kuitwa wapiganaji. Hawawezi kujibandua CCM kwani wanapenda maslahi wanayopata huko kuliko kuwatumikia wananchi kwa kukemea maovu. Yaani ni watu wanaouma na kupuliza. Uoga umewatawala na hawawezi kufanya jambo lolote linalohatarisha ulaji wa cha chao CCM kwani na wenyewe wanakula humo ndani.
Jana bunge limepitisha muswada wa katiba mpya unaompa Rais na watumishi wa serikali mamlaka ya kuhodhi namna mchakato huo utakavoendeshwa kupata katiba mpya. Hili si jambo zuri hata kidogo kwani tunajua fika kuwa serikali wala CCM hawajawahi hata cku moja kuota ndoto ya kutunga katiba mpya itakayoboresha maslahi ya nchi yetu, kulinda haki za raia na kuweka msingi mzuri wa maendeleo yetu kwa miaka mingi inayokuja. Hivo CCM kutaka kuchukua mchakato wa katiba kuuongoza ni makusudio ya kutaka kupindisha mchakato kuleta ndicho sicho katiba kulinda maslahi yake kukaa madarakani na kuendeleza ufisadi kama kawa.
Kwa mantiki hiyo kama Sita, Maghufuli na wengine wanaotaka tuamini ni watetezi wa maslahi ya nchi tunataka kuona uzalendo wenu kwa kupinga Muswada uliopitishwa na bunge la CCM. Tunataka kuwaona mkiungana na wanachi wazalendo, vyama vya kiraia, wanaharakati na mashirika ya dini kupinga ubabe huu wa CCM. Vinginevo ile imani yetu kuwa Sita, Maghufuli na wale wanaotaka tuamini kuwa ni wapiganaji wetu WANAFIKI, lao na mafisadi ni moja tu ila wanagombana tu kwa kuwa mafisadi wamewazidia ujanja kula minofu.
Kumekuwa na watu wanaodhani baadhi ya viongozi CCM ni waadilifu na wapiganaji wa maslahi ya wananchi. Watu wengine wamefikia hatua ya kuwaita wanaowakosoa hao malaika wao wa CCM kuwa ni watu wanaotumiwa na mafisadi kuwadhoofisha.
Tunaotaka ukweli usichanganywe na kitu chochote tunawaona watu kama Samwel Sita, Maghufuli na wengine kuwa si lolote si chochote au ni lolote lakini hawajafikia viwango vya kuitwa wapiganaji. Hawawezi kujibandua CCM kwani wanapenda maslahi wanayopata huko kuliko kuwatumikia wananchi kwa kukemea maovu. Yaani ni watu wanaouma na kupuliza. Uoga umewatawala na hawawezi kufanya jambo lolote linalohatarisha ulaji wa cha chao CCM kwani na wenyewe wanakula humo ndani.
Jana bunge limepitisha muswada wa katiba mpya unaompa Rais na watumishi wa serikali mamlaka ya kuhodhi namna mchakato huo utakavoendeshwa kupata katiba mpya. Hili si jambo zuri hata kidogo kwani tunajua fika kuwa serikali wala CCM hawajawahi hata cku moja kuota ndoto ya kutunga katiba mpya itakayoboresha maslahi ya nchi yetu, kulinda haki za raia na kuweka msingi mzuri wa maendeleo yetu kwa miaka mingi inayokuja. Hivo CCM kutaka kuchukua mchakato wa katiba kuuongoza ni makusudio ya kutaka kupindisha mchakato kuleta ndicho sicho katiba kulinda maslahi yake kukaa madarakani na kuendeleza ufisadi kama kawa.
Kwa mantiki hiyo kama Sita, Maghufuli na wengine wanaotaka tuamini ni watetezi wa maslahi ya nchi tunataka kuona uzalendo wenu kwa kupinga Muswada uliopitishwa na bunge la CCM. Tunataka kuwaona mkiungana na wanachi wazalendo, vyama vya kiraia, wanaharakati na mashirika ya dini kupinga ubabe huu wa CCM. Vinginevo ile imani yetu kuwa Sita, Maghufuli na wale wanaotaka tuamini kuwa ni wapiganaji wetu WANAFIKI, lao na mafisadi ni moja tu ila wanagombana tu kwa kuwa mafisadi wamewazidia ujanja kula minofu.