Tuntemeke Sanga: Mbunge aliyekuwa na elimu ya Shahada 7, aliyechachafya miaka ya zamani

Hizi,ndizo habari tulizokuwa tukizisikia! Na ya kwamba,alikuwa anautaka "UNYERERE"!Alipokuwa Mbunge,kuna chombo kimoja cha habari kilishawahi kumuuliza kuhusiana na hilo,alikataa! Bado tuna maswali,ni ya kweli hayo ya kukataa kazi yoyote,mpaka apewe Urais(U-NYERERE)?
hizo ni propaganda tu. Kumbe propaganda zilianza zamani. Ninachojua ni mtu aliekuwa smart kichwani. Alikuwa anaona mbali.
 
Ukweli utajulikana nadhani kwa greater thinker hapashindikani kitu...
 
Assume wewe ndiye raisi wa nchi na anakuja mwananchi mwenzako toka masomoni, unamuuliza anataka kazi gani, yeye anakujibu nafasi inayonifaa ni kuwa raisi tu.
Kama hutomshughulikia mtu huyo ili asubiri hadi muda muafaka wa uchaguzi basi uwe tayari kumpisha ofisi za magogoni mtu huyo muda huo huo!

Mwita,

Kwanini nimshughulikie. Kila binadamu ana haki ya kutoa mawazo yake na kufikiri destiny ya maisha yake.
 
Mwita,

Kwanini nimshughulikie. Kila binadamu ana haki ya kutoa mawazo yake na kufikiri destiny ya maisha yake.


Wakati anafikiria destiny ya maisha yake asisahau kufikiria na destiny ya maisha ya wengine.

Na kwakuwa ni msomi alipaswa kufahamu kwamba nafasi ya uraisi haitolewi kienyeji, kuna utaratibu wa kupita kwenye uchaguzi.

Sasa kwa mtu anayetafuta short cut, na wakati huo huo tunaambiwa ni msomi basi hatuna sababu ya ku question uamuzi wa mwalimu Nyerere kumshughulikia!
 
Jamaa wakati wa kampeni za ubunge alikuwa haombi kura kwa wananchi alikuwa anasema ''nimekuja kuwatembelea tu, kama utanichagua sawa kama hutaki sawa tu..mimi ndio mbunge wa makete hata kama hutaki "
 
Wakati anafikiria destiny ya maisha yake asisahau kufikiria na destiny ya maisha ya wengine.

Na kwakuwa ni msomi alipaswa kufahamu kwamba nafasi ya uraisi haitolewi kienyeji, kuna utaratibu wa kupita kwenye uchaguzi.

Sasa kwa mtu anayetafuta short cut, na wakati huo huo tunaambiwa ni msomi basi hatuna sababu ya ku question uamuzi wa mwalimu Nyerere kumshughulikia!

Kama kuna utaratibu wa kuchaguliwa ni sawa. Kwani Tunte alikataa kuwa kwenye utaratibu huo? Na kama utaratibu ulikuwepo , kwanini Nyerere hakufuata utaratibu kwa miaka 23 ya utawala wake?

Anyway, kubishana na watu waliozoe maisha kama wapo North Korea ni kupoteza muda tu.
 
Hii ni dhahiri kuwa Nyerere hakupenda wasomi. Yeye alipenda sana kufanya kazi na vilaza na watu waliowaoga katika maamuzi yao. Hii ndio sifa moja ya Nyerere na ndio Tz ameifikisha hapo mlipo.

Tuntemeke Sanga pamoja na Usomi wake hakuweza hata kuandika makala za kitaaluma kwa ajili ya kunufaisha waTz na sio wa Tz bali aliishia kuwekewa kizuizi kwao makete.

Kuna Engineer mmoja maarufu sana alikuwa akiitwa Kazibure. Huyu ni mmoja wa wanasayansi wazuri sana wa Tanzania lakini alitofautiana na Nyerere naye alifungiwa pale Kibaha na kuishia kufundisha shule ya sec Kibaha kama mwl wa Physics na mathematics.

Sikupi mfano mwingine wa Idd Simba na wengine kibaaaao.

Enzi za Nyerere nchi ilikuwa ya vilaza na wasomi makondooooooo tu
Kwa hiyo na wewe ulikuwa kilaza na kondoo kwa sababu kuna mahali ulishasema kuwa ulifanya kazi enzi za Nyerere.
Aah, ndio maana mara nyingi unaandika pumba tu humu ukumbini? Now I know
 
So far, sijaona chochote kipya au cha uhakika kuhusu Sanga zaidi ya tetesi zile zile za utotoni...kasoma kuzidi Nyerere, ana degree nane, alifungiwa kijijini, aliingia bungeni na shati la kitenge, alimwambia Nyerere nataka Urais... kwa kweli ni nonsense tupu.

Alisoma degree nane, akazifanyia nini?


Degree nane zipi, tutajieni vyuo, shahada gani, na mwaka.


Alimwambia Nyerere ampe Urais wake, now that's bull ---- kwa sababu Urais humwombi Rais aliyeko madarakani.


Alikuwa Mbunge makini, alifanya nini? Kuna nini Mafia?


Alifungwa kijijini halafu akaomba msamaha akaachiwa, ina maana alikuwa hana principle!


Alifungwa kwa kitu gani? Kwa documented evidence gani?


Oooh, kasoma kuzidi Nyerere, kwani Nyerere ndio gold standard ya wasomi?

Yani vi story vile vile vya darasa la pili, bunch of b.s.
ur very smart thing alive,ila nahisi penye mbunge na amelifanyia nn taifa nadhani sio kila struggle inapaswa kuwa na notable result hata lumumba hajalifanyia kitu taifa la congo alikufa akistruggle,pia pia kuhusu kumwambia nataka urahisi ? nadhani ni wazi kila mtu anahaki ya kutaka kuwa rais na kwa kipindi hicho nchi haikuwa ya kidemokrasia hivo huwezi kuwa raisi bila matakwa ya aliyepo kama China ilivo ,na elimu huwa si tu kwa ajili ya kutatua matatizo ni kwa afya ya fikra pia sio lazma usome degree ya uhandisi halafu ujenge daraja waweza soma ku-xperience tu au 4 adventure au you just think u must know,but ofcourse nakubaliana na ww tuntemeke seems was not a serious guy to discuss
 
Wadau nimekuwa nasikia kulikuwa na msomi Tuntemeke Sanga. Msomi huyu alikuwa na degree zaidi ya sita. Naomba kujua historia fupi ya msomi huyo.
 
Inasemakana baada kurudi toka USA alikopata madigri yake na kuonekana ni kati wasomi wachache wa juu sana wa nchi hii.
Nyerere alimuuliza unataka nafasi gani ndani ya nchi hii yeye akajibu nataka nafasi yako hiyo.

Nyerere kwa hasira akamuweka kizuizini jimboni kwake makete maeneo ya Bulongwa. Akamruhusu akiamua kutembea mwisho Mbeya ndio mkoa alioruhusiwa.

Hizo ni stori za utotoni huku Makete, ila ngoja waje magwiji watakupa taarifa kamili.
 
Alikuwa na mke mzungu inasemekana alianza kuuza ulanzi hali ilipozidi kuwa mbaya mkewe akatoroka Tuntemeke akawa tapeli kiana anakupa mkataba mzuri umjeengee nyumba anaweka mitego ya kisheria ukimaliza hakulipi ukienda polisi wanamwogopa yy anasema muende mahakamani mkifika huko anakushinda na fidia unamlipa but kuishia mbeya kulimnyima raha mwishoe akaomba msamaha kwa nyerere akasamehewa na1980 akagombea ubunge alipita akisema ataweka mabomba makete yatatoa maziwa wanasema alikuwa na degree za sheria 2 uchumi1 politicalsciance1nasaikologia hadi ya sayansi tukiwa watoto miaka ya80 Huko Iringa na mbeya kila mtu alimyua na hakika alifariki 1995hapo dar niliona kwa macho yangu mkapa akiingia msibani hapo posta town kwa mdogo wake naye alikua katibu mkuu simba naye marehemu
 
Back
Top Bottom