Tungekomaa na Ujamaa bila kuikumbatia SAP labda sasa hivi tungekuwa mbali

Ujamaa ulishindwa na Nyerere mwenyewe alikiri.

Ujamaa wa Nyerere aliutengeneza mwenyewe na hakuambilika juu ya namna ya kuuendesha. Ulikuwa ni Ujamaa wa kutafuta wahanga na watu wa kuwaangushia jumba bovu. Kuanzia Utaifishaji wa Mashirika na viwanda, Uanzishaji wa Vijiji vya Ujamaa, Operesheni maduka nk.

Ujamaa haukuwashirikisha Wadau Bali mtu mmoja au,kikundi cha watu ndiyo waliamua nini kifanyike. Hata pale wananchi walipoungana kuunda ushirika wao wa kijamaa walivurugwa kama ilivyotokea Ruvuma Development Association.

Sera za SAP hazikuwa mbaya na si kwamba ndiyo zimetukwamisha, zile zilikuwa sera za waliozitunga na ambao walitoa fedha. Tungekuwa na Uongozi wenye maono hiyo ingekuwa chachu ya kujikwamua zaidi.
kudos
 
china wana apply mixed economy(which is more capitalist than socialist) wao wenyew ujamaa wao ulifeli na zaid ya watu milion 50 walikufa kwa njaa kutokana na kufeli kwa policy mbovu za kisocialist.alvokufa mao akaja rais mpya ambaye aka-liberalise uchumi (yani akau capitalise) kwanzia miaka ya 70 na kuanzia apo ndo CHINA ikaanza kureally develop.kiufupi socialism ni ABOMINATION SYSTEM ambayo at the end of day inapelekea ku-collapse kwa nchi husika mfano USSR ilicollapse kutokana na weakness kibao associated with the system.infact wat u claim to be modern socialism is 75% capitalism kwa mfano kweny socialism hakutakiwi kuwa na mabilionea ambao wanaonexha presence of income inequality but look at china na urusi wana more billioneaz after USA.na iyo ina prove absence of true socialism.
GENERALLY,nchi yoyote inayoapply true socialism (not like china na urus) itaixhia kucollapse mfano mzuri NORTH KOREA leo wananch wananjaa af kim ana kaz ya kuruxha mabomu angani
Sio kweli mkuu
 
Ujamaa haujawahi fanikiwa popote duniani, ujamaa ni mfumo wa utawala na sio mfumo wa uchumi, kwenye uchumi umefeli.
Lengo kuu la ujamaa ni kutawala watu kwa maslai binafsi ya mtawala au kikundi cha walamba asali wachache katika jamii.
Ujamaa unalenga kumiliki akili za watu kupitia uchumi kwa maana mtu binafsi asimiliki mali kuzidi anaemtawala Ili iwe rahisi kumtawala.
Mwanadamu hawezi kuwa mjamaa ni hadi aushinde ubinafsi. Jamii ikiweza kuushinda ubinafsi ujamaa utawezekana.
Ubinafsi na shauku ya kutaka zaidi uchochea maendeleo.
 
Hakuna sehemu yeyeto Mwalimu alichochea uchumi bali alitumia hazina mali na pesa alizoachiwa na mkoloni ambazo nazo alizitapanya kwenye ukombozi wa nchi za afrika pamoja na vita vya Uganda Ili amrudishe madarakani swahiba wake Obote, kumbuka Mwalimu na Amini zilikuwa haziivi, akamtengeneza propaganda Amin ikiwemo ya uvamizi kagera Ili apate sababu ya kumrejesha madarakani Obote.
 
Kosa kubwa tulilofanya kama nchi ni kuzikumbatia sera za kipuuzi na angamivu za SAP hizi ndo zilikua kaburi kwa nchi yetu

Labda tungekomaa na ule ujamaa wa nyerere bila kupinda popote labda leo tungekua tumepiga hatua

Wenzetu China walikomaa na ujamaa na walivyopata matokeo na kufikia mahali pazuri sasa wakaruhusu ubepari sisi tulianguka mapema sana

Sasa hivi hata hatujui tupo kwenye dira gani nashindwa kujua mwelekeo wa nchi yetu kiuchumi ni aibu sana hadi leo tunategemea misaada

Sera za kishenzi za SAP ndo zimetufikisha hapa, alaaniwe aliyeasisi SAP huu ulikua ndo mwisho wa uchumi wa nchi yetu

Imagine ndo anakuambia ushushe thamani ya hela yako ambayo ilikua sawa na dola ya marekani leo hii hiyo dola ndo tunatumia kuagiza bidhaa nje yaani wanatupiga mara 2305 kwa dola moja daaah

Hii nchi sijui kama itakaa iendelee
Ujamaa ni ushetani.
 
Kosa kubwa tulilofanya kama nchi ni kuzikumbatia sera za kipuuzi na angamivu za SAP hizi ndo zilikua kaburi kwa nchi yetu

Labda tungekomaa na ule ujamaa wa nyerere bila kupinda popote labda leo tungekua tumepiga hatua

Wenzetu China walikomaa na ujamaa na walivyopata matokeo na kufikia mahali pazuri sasa wakaruhusu ubepari sisi tulianguka mapema sana

Sasa hivi hata hatujui tupo kwenye dira gani nashindwa kujua mwelekeo wa nchi yetu kiuchumi ni aibu sana hadi leo tunategemea misaada

Sera za kishenzi za SAP ndo zimetufikisha hapa, alaaniwe aliyeasisi SAP huu ulikua ndo mwisho wa uchumi wa nchi yetu

Imagine ndo anakuambia ushushe thamani ya hela yako ambayo ilikua sawa na dola ya marekani leo hii hiyo dola ndo tunatumia kuagiza bidhaa nje yaani wanatupiga mara 2305 kwa dola moja daaah

Hii nchi sijui kama itakaa iendelee
Nchi itaendelea iwapo watu watajitolea kwa ajili ya nchi. Shida yetu kubwa ni matangazo ya tutafanya hivi au tunategemea kufanya hivi. Lakini pia ni ile false consciouness tuliyo nayo kwamba bila msaada hatuendi na bila kuwa na wa kufikiri kwa ajili yetu hatuwezi kupiga hatua. Ubungo farm implements tuliua bila kufikiria. Kwa maisha ya kipindi kile tungetumia products za UFI kwenye kilimo leo tungekuwa na kiwanda cha ku assemble matrekta kama si kuunda! Mpaka leo hatujui tunataka nini hasa. Fine, tuliuacha ujamaa je tumefaidika na nini? Kuna haja ya kutakari kama nchi na kuamua mwelekeo sahihi. Tunata kukimbia bila hata kutambaa japo kwa wiki moja?!
 
Back
Top Bottom