Tunduma panahitaji macho zaidi ya Serikali

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
714
1,137
Sijui kwanini Ujerumani walijigawia Tanganyika wakati wa kuligawa bara la Afrika. Lakini Wajerumani walikuwa wana akili sana na waliona mbali sana.

Tanzania ni nchi kubwa sana jamani lakini pia ina kila kitu.

Nimepata bahati ya kukaa kwa siku kadhaa katika mji wa Tunduma. Ni mji mkubwa sana kushinda miji mingi sana.

Tunduma ni mji wa harakati nyingi sana kulinganisha na miji mingine. Tunduma kuna hela sana kiasi kwamba karibia mabenki yote yana matawi hapa.

Pamoja na umuhinu wote wa mji wa Tunduma huduma za afya naona kama bado ziko chini ukilinganisha na idadi kubwa ya watu hapa lakini pia na umuhimu wake katika uchumi wa nchi yetu.

Hata kituo cha Polisi naona kama ni kidogo sana kwani hapa ni mpakani na uhalifu huwa ni jambo la kawaida sana.

Mji huu pia haukupangwa vizuri japo unakua kwa kasi ya ajabu. Sijui huwa tunashindwa nini kupanga miji yetu.

Tunduma Tanzania na Nakonde Zambia ni vigumu kutenganisha watu wa pande hizi mbili. Muingiliana usiofuata sheria ni mkubwa sana.

Mzambia kulala Tanzania na kumiliki nyumba Tanzania ni jambo la kawaida sana. Mtanzania pia kulala na kumiliki nyumba Zambia simple sana.

Na ukiwa mgeni huwezi jua kama uko upande mwingine wa nchi.

Kwa mfano ukiwa sehemu moja wanapaita BLACK utajikuta uko nchi nyingine kinachoweza kukushangaza ni vibanda vya simu za MTN ambazo huku Tanzania hatuna mtandao huo.

Magari ya Zambia hujikuta yapo Tanzania bila kutegemea, hivyo hivyo kwa magari ya Tanzania.

Watu wake wanaelewa sana kana kwamba wote ni wa nchi moja.

Hapa kwenye mambo ya usalama sijui inakuaje.

Vijana wa Tunduma wanafanya sana biashara ya fedha. Tunduma ndiko sehemu ya Tanzania ambako vijana wanaujua uchumi kwa vitendo kwa maana Exchange rate za fedha zote uzijuazo ziko vichwani mwao.

Lakini pia Tunduma kama kumeendelea sana kuliko Nakonde japo ni majirani. Population kubwa ya watu na majumba mengi yako Tunduma kuliko Nakonde.

Kuna sehemu wananchi wa pande zote walijenga mpaka mpakani na hivyo ikawa vigumu kujua mipaka ya nchi mbili za Tanzania na Zambia. Naona bomoa bomoa ilipita kidogo uwazi wa mpaka unaonekana kidogo.

Kabla ya bomoa bomoa hiyo Mtanzania aliweza kutumia umeme wa Zambia kama kawaida kana kwamba nae ni Mzambia.

Kuna mambo mengi sana Tunduma ukipata muda Tembelea Tunduma upate kujua mengi kuhusu nchi yako.

Na hapa ndipo ile dhana ya Diplomacy mbaya kati ya nchi majirani huwa zinatengenezwa na viongozi lakini wananchi wala hawana shida hata kidogo wanaishi kana kwamba kahuna mipaka.

TANZANIA THE BLESSED NATION.
 
Umetia chumvi sana bro! Ungesema labda Tunduma ndo boarder town kubwa na iliochangamka kuliko zote Tanzania. Alafu biashara ya kubadilisha fedha serikali imeiuwa ni kama hakuna, benki kuna NBC na NMB zingine 2 ni kama mini branches tu.
 
Umetia chumvi sana bro! Ungesema labda Tunduma ndo boarder town kubwa na iliochangamka kuliko zote Tanzania. Alafu biashara ya kubadilisha fedha serikali imeiuwa ni kama hakuna, benki kuna NBC na NMB zingine 2 ni kama mini branches tu.

Kuna ile bank ya posta, nadhani atakua anamaanisha na hiyo
 
Umetia chumvi sana bro! Ungesema labda Tunduma ndo boarder town kubwa na iliochangamka kuliko zote Tanzania. Alafu biashara ya kubadilisha fedha serikali imeiuwa ni kama hakuna, benki kuna NBC na NMB zingine 2 ni kama mini branches tu.
Tawi la CRDB na tawi la Azania Bank ni matawi makubwa tu mbona. Hajatia chumvi popote. Amesema ukweli mtupu.
 
Umetia chumvi sana bro! Ungesema labda Tunduma ndo boarder town kubwa na iliochangamka kuliko zote Tanzania. Alafu biashara ya kubadilisha fedha serikali imeiuwa ni kama hakuna, benki kuna NBC na NMB zingine 2 ni kama mini branches tu.
Kuna TPB, BOA pia
 
Tunafeli sana kwenye mipango miji nchi hii lakini miji ya Mbeya na Tunduma zimetia fora kwa miji yote niliyowahi kutembelea. Mbeya itabaki sana na sura mbaya sana na haitapata retail business kubwa kubwa kwa sababu tu ya mipangilio mibaya na ujenzi wa hovyo hovyo hasa katika maeneo ya NZOVWE, SIMIKE, ISANGA, MWANJELWA, ILOMBA, MAMA JOHN, MAFIAT, AIRPORT YA ZAMANI, MWAKIBETE, IYUNGA NA SAE.
 
Tunafeli sana kwenye mipango miji nchi hii lakini miji ya Mbeya na Tunduma zimetia fora kwa miji yote niliyowahi kutembelea. Mbeya itabaki sana na sura mbaya sana na haitapata retail business kubwa kubwa kwa sababu tu ya mipangilio mibaya na ujenzi wa hovyo hovyo hasa katika maeneo ya NZOVWE, SIMIKE, ISANGA, MWANJELWA, ILOMBA, MAMA JOHN, MAFIAT, AIRPORT YA ZAMANI, MWAKIBETE, IYUNGA NA SAE.
Ongezea nanenane, uyole ya katoli, igawilo, iganzo, nsalaga, Mlima nyoka,,,, Yani mbeya siyo jiji bali ni Kijiji kikubwa
 
Kw
Tunafeli sana kwenye mipango miji nchi hii lakini miji ya Mbeya na Tunduma zimetia fora kwa miji yote niliyowahi kutembelea. Mbeya itabaki sana na sura mbaya sana na haitapata retail business kubwa kubwa kwa sababu tu ya mipangilio mibaya na ujenzi wa hovyo hovyo hasa katika maeneo ya NZOVWE, SIMIKE, ISANGA, MWANJELWA, ILOMBA, MAMA JOHN, MAFIAT, AIRPORT YA ZAMANI, MWAKIBETE, IYUNGA NA SAE.
Kwa kifupi kwenye mipango miji Tanzania nzima ni takataka na aibu kubwa. Kuna uzi jukwaa la Hoja mchanganyiko aliuleta Kada wa CCM humu Barbarosa watu wamefunguka sana.

Tanzania tunaitaji reformation kubwa sana kwenye suala la makazi na mipango miji na sioni hili likifanyika chini ya serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Tunaitaji Chama Mbadala na viongozi wapya wenye maono na exposure kimaendeleo kulipa ya hili. Ndo mana nimeamua ku support Chadema na kuachana na Chama cha Mapinduzi.

Ukienda mataifa ya wenzetu alafu ukifanya ulinganisho na Tanzania kwenye suala la mipango miji na makazi unaweza kutoa machozi mwezi mzima. Ni uchafu mtupu
 
Niliwahi kufanya kazi Tunduma.

Shopping tulikuwa tunafanya kwenye supermarket za Zambia. Tunatoa Tsh wanarudisha Tsh. Supermarket zilikuwa zinapokea pesa zote.

Bata tulikuwa tunakula Zambia na kuna baadhi ya wafanyakazi wa serikali walikuwa raia wa zambia niliwahi fanya kazi nao.

Tatizo kubwa la Tunduma ni Usalama. Ukitaka kutoa hela nyingi lazima ukazichukue Mbeya mjini.

Ila ukitoa kwenye hizo benki za hapo mpakani, lazima upigwe tukio.

Na kuna baadhi ya vijiji vipo upande wa Tanzania ila ukitaka kuja Tunduma mjini lazima ukazungukie upande wa Zambia ambapo kuna barabara nzuri.
 
Tunduma ya sasa hivi ni tofauti na Tunduma ya miaka 15 iliyopita!
Kwasasa Tunduma ni salama na huduma zote muhimu zinapatika!
Tunduma ndo sehemu pekee ambapo watu wanashika hela mkononi bila hofu yoyote!
Karibuni sana Tunduma!
 
Tunafeli sana kwenye mipango miji nchi hii lakini miji ya Mbeya na Tunduma zimetia fora kwa miji yote niliyowahi kutembelea. Mbeya itabaki sana na sura mbaya sana na haitapata retail business kubwa kubwa kwa sababu tu ya mipangilio mibaya na ujenzi wa hovyo hovyo hasa katika maeneo ya NZOVWE, SIMIKE, ISANGA, MWANJELWA, ILOMBA, MAMA JOHN, MAFIAT, AIRPORT YA ZAMANI, MWAKIBETE, IYUNGA NA SAE.
Iyunga majengo mapya wamepaconstruct vzuri sana aisee

nina ghorofa moja pale
 
Sijui kwanini Ujerumani walijigawia Tanganyika wakati wa kuligawa bara la Afrika. Lakini Wajerumani walikuwa wana akili sana na waliona mbali sana.

Tanzania ni nchi kubwa sana jamani lakini pia ina kila kitu.

Nimepata bahati ya kukaa kwa siku kadhaa katika mji wa Tunduma. Ni mji mkubwa sana kushinda miji mingi sana.

Tunduma ni mji wa harakati nyingi sana kulinganisha na miji mingine. Tunduma kuna hela sana kiasi kwamba karibia mabenki yote yana matawi hapa.

Pamoja na umuhinu wote wa mji wa Tunduma huduma za afya naona kama bado ziko chini ukilinganisha na idadi kubwa ya watu hapa lakini pia na umuhimu wake katika uchumi wa nchi yetu.

Hata kituo cha Polisi naona kama ni kidogo sana kwani hapa ni mpakani na uhalifu huwa ni jambo la kawaida sana.

Mji huu pia haukupangwa vizuri japo unakua kwa kasi ya ajabu. Sijui huwa tunashindwa nini kupanga miji yetu.

Tunduma Tanzania na Nakonde Zambia ni vigumu kutenganisha watu wa pande hizi mbili. Muingiliana usiofuata sheria ni mkubwa sana.

Mzambia kulala Tanzania na kumiliki nyumba Tanzania ni jambo la kawaida sana. Mtanzania pia kulala na kumiliki nyumba Zambia simple sana.

Na ukiwa mgeni huwezi jua kama uko upande mwingine wa nchi.

Kwa mfano ukiwa sehemu moja wanapaita BLACK utajikuta uko nchi nyingine kinachoweza kukushangaza ni vibanda vya simu za MTN ambazo huku Tanzania hatuna mtandao huo.

Magari ya Zambia hujikuta yapo Tanzania bila kutegemea, hivyo hivyo kwa magari ya Tanzania.

Watu wake wanaelewa sana kana kwamba wote ni wa nchi moja.

Hapa kwenye mambo ya usalama sijui inakuaje.

Vijana wa Tunduma wanafanya sana biashara ya fedha. Tunduma ndiko sehemu ya Tanzania ambako vijana wanaujua uchumi kwa vitendo kwa maana Exchange rate za fedha zote uzijuazo ziko vichwani mwao.

Lakini pia Tunduma kama kumeendelea sana kuliko Nakonde japo ni majirani. Population kubwa ya watu na majumba mengi yako Tunduma kuliko Nakonde.

Kuna sehemu wananchi wa pande zote walijenga mpaka mpakani na hivyo ikawa vigumu kujua mipaka ya nchi mbili za Tanzania na Zambia. Naona bomoa bomoa ilipita kidogo uwazi wa mpaka unaonekana kidogo.

Kabla ya bomoa bomoa hiyo Mtanzania aliweza kutumia umeme wa Zambia kama kawaida kana kwamba nae ni Mzambia.

Kuna mambo mengi sana Tunduma ukipata muda Tembelea Tunduma upate kujua mengi kuhusu nchi yako.

Na hapa ndipo ile dhana ya Diplomacy mbaya kati ya nchi majirani huwa zinatengenezwa na viongozi lakini wananchi wala hawana shida hata kidogo wanaishi kana kwamba kahuna mipaka.

TANZANIA THE BLESSED NATION.
 
sheria ya kimataifa kuhusu mipaka yakimataifa ndo inawalinda kwamba boda yeyote ile wananchi wanatakiwa kufanya shughuli zakiuchumi nakijamii bilakubughudhiwa umbali wa kilomita 14 kila upande waboda....ila utakavokua umezidi 14km lazima uonyeshe vielelezo
 
Tunafeli sana kwenye mipango miji nchi hii lakini miji ya Mbeya na Tunduma zimetia fora kwa miji yote niliyowahi kutembelea. Mbeya itabaki sana na sura mbaya sana na haitapata retail business kubwa kubwa kwa sababu tu ya mipangilio mibaya na ujenzi wa hovyo hovyo hasa katika maeneo ya NZOVWE, SIMIKE, ISANGA, MWANJELWA, ILOMBA, MAMA JOHN, MAFIAT, AIRPORT YA ZAMANI, MWAKIBETE, IYUNGA NA SAE.
Katika upangaji wa miji ninamlaumu Rais wa kwanza, Mwalim Julias Kambarage Nyerere. Rais Nyerere alianza vizuri sana na ujenzi wa miji hasa jiji la Dar es salaam na National Housing. Walipanga mitaa vizuri sana.

Lakini baada ya kuanza harakati za kuikomboa Afrika hapo ndipo mambo yalipo anza kuharibika. Mwalim Nyerere hakuwa na wazo na watanzania tena. Mawazo yote yalilengwa kwa wakimbizi na ukombozi wa Afrika.

Dar es salaam ikaanza kuingiwa na matindiga kutoka mikoani bush na kuanza kuuvuruga mji kwa kununua viwanja holela bila kuzingatia kanuni na usataarabu. Huko kwao bush hawajazoea nyumba za kupangwa kwa mpangilio.

Ameuharibu sana mji wetu Mzaanaki yule!
 
Kuna unafuu katika miji ya TANGA, MOSHI, DODOMA, SUMBAWANGA, MPANDA NA IRINGA.
Hakuna unafuu wowote kote ni takataka. Tanzania tunaitaji opereshi makazi bora na mipango miji kama ilivyokuwa Kilimo kwanza ili miji yetu ipendeze.

Huko unaposema ni kama Regent Estate tu. Mbele kumepangwa ukigeuka mtaa wa pili nyuma tu unakuta kinondoni Shamba na Msasani Bonde la mpunga. Mpangilio mbovu na uchafu mtupu.

Tanzania nzima tunaitaji mabadiriko makubwa sana tena sana ili tupangilie makazi yetu na miji yetu.

Kielelezo cha kwanza cha CCM kushindwa kuiendeleza vizuri nchi yetu ni kufeli kwao vibaya kwenye makazi bora na mipango miji
 
Back
Top Bottom