Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,586
- 217,977
Aliyekuwa Meya wa Tunduma kupitia Chadema Mh. Ally Mwafongo alikamatwa na Polisi kwa tuhuma za kutengenezwa kiwandani za mauaji kabla ya uchaguzi na kuwekwa selo yeye na viongozi wengine lundo wa Chadema , lengo la unyama huo lilikuwa kumzuia kugombea tena udiwani ili kuirahisishia ccm ushindi .
Mwafongo pamoja na lundo la viongozi wa Chadema leo wanatimiza siku 143 gerezani kwa tuhuma za uongo kwa sababu za kisiasa , kwa vile Mungu si Athumani basi tunaamini Mwafongo na wenzake wataachiwa huru na kila aliyeshiriki kutenda unyama huu wa kishamba atalipwa kwa kiasi kile kile alichotenda .
Leo kuna watu nchi hii wanataka tufanye maridhiano na watu wenye roho za kishetani namna hii , hili jambo haliwezekani hata kwa mtutu wa bunduki .
Mungu ibariki Chadema