Tundu, Zitto wasisitiza chadema ni shwari

TUKUTUKU

JF-Expert Member
Sep 14, 2010
11,765
4,033
Hali ya kisiasa ndani ya CHADEMA imeelezwa kwamba ni shwari na hakuna matafaruku utakaotokea.Mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni,Tindu Lissu,pamoja na Naibu katibu mkuu wa chadema Zitto kabwe walisema hayo kwa nyakati tofauti walipohojiwa kufuatia hatua ya wabunge wa 10,akiwemo naibu katibu mkuu wake,Zitto Kabwe kutokana na kupingana na msimamo wa chama hicho wa kutoka nje ya bunge wakati Rais Kikwete alipokuwa akihutubia bunge.
“Hakuna mgogoro wowote baina ya viongozi wa chama bali kilichopo ni taratibu za kinidhamu na sio mgogoro wala mgongano wowote”alisema.Akizungumza jana,Lissu alisema hakuna mpasuko,mgogoro wala mgongano wowote ndani ya chama hicho na kwamba kilichopo ni masuala ya kawaida yanayojadiliwa na vikao vya chama na kwamba hayawezi kuvuruga mshikamano uliyopo ndani ya chama hicho.
Kwa upande wake zitto kabwe alisema,hakuna mgogoro wowote ndani ya chama hicho na kwamba taratibu za kinidhamu haziwezi kuitwa mgogoro hata siku moja.Zitto alisema watu wengi wanakesha wakikiombea mabaya chama hicho na wengine kufikia hatua ya kusema uongo kwa nia ya kuleta chokochoko ,na akasisitiza haoni mgogoro wowote na kutaka wanaozusha maneno hayo watofautishe tofauti ya mgogoro na taratibu za kinidhamu.Zitto alisema wakati umefika kwa watanzania kujenga tabia ya kuimarisha vyama na sio kubomoa kama ulivyo sasa ambapo jambo dogo linakuzwa.[Mwananchi,6 Desemba 2010,pp 5]

My take
Mnaokodolea macho na kuombea chadema iingie kwenye mgogorona hatimaye kufa kabisa,hamta fanikiwa kamwe!CHADEMA ilikuwepo,ipo na itaendelea kuwepo na kushamiri kwa kasi zaidi,hari zaidi na nguvu zaidi.Mungu ibariki CHADEMA,mungu ibariki Tanganyika.
 
Tunaomba pasiwe na mpasuko japo chokochoko ni nyingi sana. Zinatokea ccm, cuf na nccr. Chadema mnawindwa na kwa bahati nzuri mnalijua hili. Sorry, chadema tunawindwa
 
Bora hata Zitto kaongelea hili suala manake anti-CDM hawalali wakiombea mabaya
 
Tunaomba pasiwe na mpasuko japo chokochoko ni nyingi sana. Zinatokea ccm, cuf na nccr. Chadema mnawindwa na kwa bahati nzuri mnalijua hili. Sorry, chadema tunawindwa

Mkuu ni sawa kuwepo na chokochoko kwa kuwa binadamu hawawezi kukaa sehemu moja bila kutofautiana mawazo,hili ni jambo la kawaida.Ninachokiogopa mimi ni mgogoro kama ule uliyoikumba NCCR MAGEUZI 1996,hule ulikuwa hatari sana na tena ulisababisha chama kudhoofika kwa haraka!CHADEMA itavuka na kufika 2015 ikiwa chama imara kabisa cha upinzani,mungu ni mkubwa!!
 
gazeti la jambo leo linakuza sana migogoro ndani ya vyama vya siasa
 
hayo ni maneno ya kisiasa tu lakini mgogoro upo tu..
tumeona migogoro mingi kwenye serikali za sehemu nyingi nchi mbali mbali..
wanapatana kwa maslai yao binafsi tu ndipo wakija kwetu wananchi wanatudanganya kwa mgongo wa chupa.. sina hakika na wanachokinena. Cha msingi tuombeee mazuri a migogoro isiwepo ili kuwantoa wanaoshikilia nchi kwasasa
 
Aminaah! Inshahlaah! Angalau sasa naweza walau kunywa maji maana hiz chokochoko zlinikosesha amani kabisa.Mola ibariki CHADEMA, Mola ibariki TZ. Wanaoleta fitna ni watu wabaya sana wanataka kutuharibia amani ktk nchi yetu, kuanzia sasa wakome kama walivyokoma ***** yao, na wakizid tutawasomea albadili laana iwafate mpaka kwa vitukuu na vilembwe vyao.
 
hayo ni maneno ya kisiasa tu lakini mgogoro upo tu..
Tumeona migogoro mingi kwenye serikali za sehemu nyingi nchi mbali mbali..
Wanapatana kwa maslai yao binafsi tu ndipo wakija kwetu wananchi wanatudanganya kwa mgongo wa chupa.. Sina hakika na wanachokinena. Cha msingi tuombeee mazuri a migogoro isiwepo ili kuwantoa wanaoshikilia nchi kwasasa

sawaaaaa
 
hayo ni maneno ya kisiasa tu lakini mgogoro upo tu..
tumeona migogoro mingi kwenye serikali za sehemu nyingi nchi mbali mbali..
wanapatana kwa maslai yao binafsi tu ndipo wakija kwetu wananchi wanatudanganya kwa mgongo wa chupa.. sina hakika na wanachokinena. Cha msingi tuombeee mazuri a migogoro isiwepo ili kuwantoa wanaoshikilia nchi kwasasa

Upo mgongano wa mawazo na si mgogoro!ingawa wakati mwingine mgongano wa mawazo huzaa mgogoro!lakini CHADEMA bado haijafika huko!ikifika huko wala haitakuwa siri tena kila mtu atajua kama ilivyokuwa kwa NCCR MAGEUZI 1996.
 
hayo ni maneno ya kisiasa tu lakini mgogoro upo tu..
tumeona migogoro mingi kwenye serikali za sehemu nyingi nchi mbali mbali..
wanapatana kwa maslai yao binafsi tu ndipo wakija kwetu wananchi wanatudanganya kwa mgongo wa chupa.. sina hakika na wanachokinena. Cha msingi tuombeee mazuri a migogoro isiwepo ili kuwantoa wanaoshikilia nchi kwasasa
hivi we ukoje lakini? si wameshasema hakuna migogoro!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Hapo ndipo mchezo wa siasa unapofurahisha! walio ndani wanayafunika kwa nguvu zote, walio nje wanashabikia bila kujua ni lipi sahihi:
mwisho wa siku maneno haya yanakuja:
SIASA NI UONGO WENYE MANUFAA!!
 
Mkuu ni sawa kuwepo na chokochoko kwa kuwa binadamu hawawezi kukaa sehemu moja bila kutofautiana mawazo,hili ni jambo la kawaida.Ninachokiogopa mimi ni mgogoro kama ule uliyoikumba NCCR MAGEUZI 1996,hule ulikuwa hatari sana na tena ulisababisha chama kudhoofika kwa haraka!CHADEMA itavuka na kufika 2015 ikiwa chama imara kabisa cha upinzani,mungu ni mkubwa!!

sure mkuu. We shall make it
 
Back
Top Bottom