Tunapowaambia nyie ni wajinga muwe mnaelewa? Nani amekwambia mimi ni Chadema? nani amekwambia ninachokiandika mimi ni cha Chadema? Huu wako hauwezi kuwa ni ujinga? Unaweza kuthibitisha kuwa Lowasa alipitishwa Chadema kwa kutoa mabulungutu? Huu wako tena hauwezi kuwa ujinga na uroporopo? Unadhihirisha ujinga pia kujaribu kuonyesha ni Dk Slaa pekee yake aliyeing'arisha Chadema. Bungeni wakati huo, kama ulikuwa hujaanza kufuatilia bunge, hoja zilijengwa na akina Zitto, hoja zilijengwa na akina Mnyika, hoja ziliendelea kujengwa na akina Halima Mdee, hoja zilijenmgwa na akina Lisu na hoja zilijengwa na akina Lema. Unamjua Wenje wewe?Kama matusi na kejeli yangekuwa sera, Chadema mgekubalika kila kona. Leo hii mmeshasahau Lowassa alikuja na maburungutu ya fedha na akapitishwa kwa kura za kunyanyua mikono juu. Mmeshasahau Dr. Slaa aliyejenga hoja karibu zote bungeni na kukifanya chama kikubalike nje ya ngome yake ya kaskazini. Chadema kilikuwa ni chama cha wafanyabiashara na matajiri, masikini hakuwa na nafasi kwenye chama. Leo hii hata huko kaskazini kuanza kupuputika.
Hakuna mtu hata mmoja aliyetoka Chadema iwe kwa hiyari yake au kwa kufukuzwa anajutia huo uamuzi. Nashukuru Nyalandu amejitahidi kubadili lugha inayotumiwa na viongozi wa Chadema wa sasa, ni tofauti sana na ilivyokuwa miaka michache iliyopita ya nguvu nyingi kuliko akili. Tatizo ni nyinyi ambao bado mna elements za kizamani.
Ni kaskazini ipi ambako Chadema imepukutika? Au mauzo ya Meya wa Arusha ndio yameongeza ujima kichwani mwako? Nyie ndo mnapokea propaganda rahisi za manunuzi ya madiwani na wabunge, umeona wananchi wanaombatana na hao wasaka tonge? kwa taarifa yako wao wewenyewe wanaponunuliwa wanawaogopa wananchi, hawana ujasiri wa kuwashawishi..kalaghabaho!