Tundu Lissu: Utaratibu wa Matibabu ya Mbunge umewekwa na Sheria ya Bunge

Ipo siku hawa wauaji watakuja kuumbuka. Ni vigumu mtu akusudie kukuua ukinusurika kifo aidhinishe pesa za matibabu yako. Kwa kuwa malengo ya CCM kumuua Lissu yaligonga ukuta usitarajie watatoa fedha za matibabu. La hasha!
More exactly..!!
 
Hebu kiscan utuwekee hapa KAMANDA! ili tumsute spika mpaka aone aibu na uongo wake.
Yawezekana hakipo ktk maandishi. Uwepo wa viongozi wa serekali walotajwa katka kikao cya majadiliano ya kupelekwa Nairobi pamoja na uwanja wa ndege wa dodoma kuruhusu ndege itue kinyume na utaratibu ni kibali tosha.
 
Nafkiri matatizo ya akili pia yanachangia kwaiyo lisu alivojeruhiwa ni sawa na anaeumwa na mafua dahh... "RIP ."
Kwnini lakini mnang'ang'ania lisu angeenda muhimbili ?
Mmekipanga nini huko? au mlitaka kukamilisha mession?
Mbona mmeshindwa kuwatafuta waliompiga risasi na mkazuia watu wa nje pia kufanya uchunguzi..? Dahhhh jamani mbona mna roho mbaya hivi .......?
Naam, kwa jinsi swala la Lisu lilivyo kuwa handled na serikali nashawishika kuamini kuwa rufaa ya Muhimbili ilikuwa ni mwendelezo wa kujenga mazingira ya kuhakikisha Lissu anaaga dunia.
Lkn tutarajie nini zaidi ya dhamira ovu ya serekali ya Magufuli dhidi ya Lissu???....kama kuvaa nguo iloandikwa mwombee Lisu ni kosa linalo tosha kukuweka ndani na kunyimwa dhamana kabisa!!!.
 
Hivi huyu msaliti ana ka wehu ka aina fulani eeh?!
Tumeshamwambia alie na mfalme mbowe aliyekiuka utaratibu wa matibabu ya nje kwa wabunge, yeye mbona haelewi? Anadhani pesa ya serikali ya awamu ya tano inatolewe ovyo ovyo kama chadema wanavyokula ruzuku bila kutoa taarifa yoyote?
Huyu jamaa ni mbinafsi sana; EL alitoa mshiko mrefu ili awe mgombea 2015 na 2020, yeye kwa ubinafsi wake akataka kufanya mapinduzi ya ndani kwa ndani! Alie na ubinafsi wake.
Kwa nini asitibiwe na wale wezi wa madini aliotusaliti kwao kwa kuwapa msaada wa ushauri wa kisheria? Kwenye nchi msaliti, kwenye chama msaliti, sijui ataponea kwa jirani gani?!
 
UTAFITI HURU UMEBAINI KWAMBA MH TUNDU LISSU NDIYE MWANASHERIA BORA KABISA KUWAHI KUWEPO KWENYE ENEO LA MAZIWA MAKUU TANGU KUUMBWA KWA MBINGU NA ARDHI
Mkuu, ukiendelea hivi nakushauri ukamwone psychiatric haraka sana ili upate kusaidiwa kabla hujaanza kubonga chande na kuokota makopo.
 
Hivi huyu msaliti ana ka wehu ka aina fulani eeh?!
Tumeshamwambia alie na mfalme mbowe aliyekiuka utaratibu wa matibabu ya nje kwa wabunge, yeye mbona haelewi? Anadhani pesa ya serikali ya awamu ya tano inatolewe ovyo ovyo kama chadema wanavyokula ruzuku bila kutoa taarifa yoyote?
Huyu jamaa ni mbinafsi sana; EL alitoa mshiko mrefu ili awe mgombea 2015 na 2020, yeye kwa ubinafsi wake akataka kufanya mapinduzi ya ndani kwa ndani! Alie na ubinafsi wake.
Kwa nini asitibiwe na wale wezi wa madini aliotusaliti kwao kwa kuwapa msaada wa ushauri wa kisheria? Kwenye nchi msaliti, kwenye chama msaliti, sijui ataponea kwa jirani gani?!
How old are you?
 
Utaratibu wa matibabu ya mbunge umewekwa na sheria ya Bunge iitwayo Sheria ya Uendeshaji wa Bunge ya 2008. Kifungu cha 24(1) cha Sheria hiyo kinasema "matibabu ya mbunge yatagharamiwa na Bunge ndani na nje ya Tanzania."

Kwa utaratibu wa sasa ulivyo, Bunge linalipia gharama za tiba na gharama za kujikimu za mbunge na ndugu anayemuuguza.

Sheria ya Uendeshaji wa Bunge haijaweka masharti anayoyazungumzia Spika Ndugai. Hakuna kifungu chochote kinachozungumzia kibali cha Muhimbili au cha Magufuli.

Ukweli ni kwamba kauli ya Spika Ndugai inathibitisha jinsi ambavyo Bunge limepoteza mamlaka na hadhi yake chini ya uongozi wake dhaifu. Hata masuala ambayo Sheria haijampa Rais mamlaka, Spika Ndugai ameyakabidhi kwa Magufuli.

Kauli hiyo ni uthibitisho pia wa jinsi ambavyo Bunge linaendeshwa bila kufuata sheria, kwa chuki na upendeleo wa kisiasa chini ya uongozi wa Spika Ndugai.

Yeye amekwenda India mara nyingi kutibiwa kabla na baada ya kuwa Spika kwa gharama za Bunge. Mimi mbaya wao niliyepigwa risasi nikiwa nahudhuria vikao vya Bunge ninakataliwa matibabu kwa sababu zisizokuwa na msingi wowote.

Tatu, wala sio kweli kwamba sikufuata utaratibu, kama maana ya neno hilo ni utaratibu uliowekwa na sheria.

Katika mazingira ya jaribio la mauaji dhidi yangu, utaratibu pekee uliokuwa unawezekana ulikuwa ni kunihamisha nchini kwa dharura.

Nilikuwa nimeumizwa vibaya, mifupa imevunjwa kila mahali, nimepoteza damu nyingi na risasi zimejaa tumboni.

Kusema nisubiri kibali cha Bunge au cha Muhimbili au cha Magufuli ilikuwa ni kunitakia kifo cha wazi. Pengine ndicho Spika Ndugai na wakubwa wake walichokitaka. Mungu aliwakatalia, sasa wamenuna.

Na hivi ni kweli sikupata kibali cha kupelekwa Nairobi???

Uamuzi wa kunipeleka Nairobi ulifanywa kwenye kikao kilichofanyika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Spika Ndugai na Naibu wake walikuwepo kwenye kikao hicho. Katibu wa Bunge wakati, Dr. Tom Kashililah, alikuwepo. Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na Katibu Mkuu wake Dr. Ulisubisya Mpoki walikuwepo. Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba alikuwepo. Na Mwenyekiti Mbowe na wabunge kadhaa walihudhuria pia.

Baada ya kukubaliana kwamba napelekwa Nairobi, ndege ililetwa Dodoma saa sita za usiku. Uwanja wa Ndege wa Dodoma hauruhusu ndege kuruka au kutua baada ya saa 12 jioni. Nani aliyeruhusu ndege iliyonichukua kutua na kuruka saa sita usiku kama hakukuwa na kibali cha Bunge???

Lakini waovu waliotaka kuniua wanazidi kujidhihirisha. Nilipigwa risasi masaa mawili baada ya Magufuli kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kulinda rasilimali za nchi hata kama vitavunja sheria za nchi yetu.

Mazingira ya tukio yanadhihirisha njama za mauaji yaliyopangwa au kuelekezwa kutoka juu: ulinzi wote uliondolewa mahali ninapoishi; na barabara za maeneo yote ya jirani zilifungwa.

Baada ya tukio CCTV ya kwenye jengo ninamokaa iliondolewa na Jeshi la Polisi kimya kimya na haijawahi kutolewa maelezo yoyote.

Hakuna uchunguzi wala upelelezi wowote uliofanywa na polisi. Hata kidanganyio cha kuja kunihoji mimi na dereva wangu Nairobi kiliwashinda. Wanajua mpango mzima.

Sasa, baada ya dana dana nyingi, Spika Ndugai anasema sijatibiwa na Bunge kwa sababu sikupata kibali cha Jiwe Magufuli!!! Of course Jiwe hawezi kutoa kibali hicho. Alitaka niuawe, atatoaje kibali cha kunitibu?!?!?!

Kuhusu kupatiwa matibabu na Serikali ya Ujerumani, huu ni uongo usiokuwa tofauti na wa yule mtu anayeitwa Musiba.

Spika Ndugai ametoa kauli hii kwa sababu ukweli ni kwamba hajui na hajawahi kujua natibiwaje. Angeuliza angepewa taarifa sahihi, lakini hajawahi kuuliza.

Ukweli ni huu. Gharama zote za tiba zinagharamiwa na bima ya afya ya Ubelgiji ambayo mimi na mke wangu tulijiunga mara baada ya kufika hapa.

Gharama za bima, ambazo kwa hapa sio kubwa sana, nimelipia mwenyewe.

Gharama za kujikimu kama kupanga nyumba, chakula, usafiri, n.k. ni michango ya Wasamaria Wema Watanzania na wasio Watanzania. Ni wengi sana na wengi wao sijawahi hata kuwaona au kuwafahamu.

Hawa ndio wameniwezesha mimi na mke wangu kuishi hapa Ubelgiji kwa miezi yote ambayo tumekuwa hapa na sijawahi kuacha kuwatambua na kuwashukuru kwa wema na upendo wao.

Hii habari ya tiba ya Wajerumani ni mwendelezo wa propaganda dhaifu kwamba CHADEMA inatumiwa na Wajerumani. Ni ujinga mtupu.
Tundu Lissu.
Aibu yaoo.
 
kutibiwa kwa mbunge siyo hisani ya mtu wala jiwe aka malaika mkuu ni sheria ndio inasema hivyo
Mwambie TUNDU LISSU nae anatakiwa kuona AIBU....mtu unatibiwa na NCHI YA UJERUMANI lakini bado unaendelea kulilia hizi PESA ZA WALALA HOI huu ndio tunaoita UBINAFSI NA UNAFIKI WA KIWANGO CHA JUU....achana na hizi pesa ambazo SERIKALI kupitia BUNGE wameshindwa kukuidhinishia baada ya hao waliokudanganya KUSHINDWA KUFATA UTARATIBU.....zinaweza hata kutumika KUOKOA MAISHA YA WENGINE.....hapa unachokifanya na CHAMA CHAKO ni kutaka hii pesa kwa maslahi yenu8 BINAFSI na kuendelea kuijipatia UMAARUFU WA KISIASA
Hoja, hoja kubwa hapo Ni utawala wa sheria na sio hisani!

Tuelewe, tutambue na tuwajibike ktk sheria ambazo tumezitunga kwa kuingia gharama!

Sheria ndiyo msingi wa kuongoza nchi.
Sheria ya binge inasemaje!!?????
 
Waseme ukweli kwamba hospitals zote walizoenda hakuna hata mija iliyoko kwenye bima za wabunge.
Wenye bima za afya wanajua hili kama bima haina mkataba na hospital husika huwezi kutibiwa.

Pia waache ujeuri walisema wanampeleka wanakoona kuna usalama na huko India wanakopelekwa wabunge wenzie akiwemo spika alienda akaacha kutibiwa?
 
Yawezekana hakipo ktk maandishi. Uwepo wa viongozi wa serekali walotajwa katka kikao cya majadiliano ya kupelekwa Nairobi pamoja na uwanja wa ndege wa dodoma kuruhusu ndege itue kinyume na utaratibu ni kibali tosha.
Spika anadhani kamanda Lissu alikuwa hajitambui.
Ndugai muongo sana! kawataja wote waliokuwepowakati wa majadiliano isipokuwa kamanda Lissu, wakati mgonjwa mhusika alishuhudia mwenyewe majadiliano hadi serikali inatoa kibali?
Kuna haja ya kufungua kesi.
 
Hoja, hoja kubwa hapo Ni utawala wa sheria na sio hisani!

Tuelewe, tutambue na tuwajibike ktk sheria ambazo tumezitunga kwa kuingia gharama!

Sheria ndiyo msingi wa kuongoza nchi.
Sheria ya binge inasemaje!!?????

We vipi?
Sie tunataka UTAWALA wa sheria kwenye kuandamana tu.
Kwenye maslahi yetu hata akikiuka haina shida.
 
Back
Top Bottom