Tundu Lissu, unakuwaje Rais wa nchi bila kukemea Rushwa, bila kuongelea suala la maji, miundombinu na Elimu?

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,899
Tundu Lissu umetoa hotuba dhaifu sana kuwahi kutolewa na mgombea yeyote kuwahi kutokea nchini mwetu umeongea mambo mepesi ambayo najua mambo hayo ni ya mazingira ya Marekani na nchi zilizoendelea.

Tundu Lissu tunaonewa na wala Rushwa wanaoiba Mali zetu na kutufanya tuishi maisha ya kifukara na mateso makubwa badili mfumo wa Sera zako zijikite kwenye mazingira halisi ya nchi yetu inayohitaji. Maji, umeme, afya bora uonevu tunaofanyiwa wananchi wa kunyimwa huduma za msingi za kijamii ndo tunaotaka uukemee.

Mheshimiwa Tundu Lissu unaosema wameonewa ni wale ambao wanatuibia na kutuoñea wananchi sisi wananchi tumeteseka muda mrefu tumepata Rais Magufuli anayewabana unaowaita wanaonewaa kwa manufaa ya ya wengi masikini wanaopita kwenye barabara mbovu wanaokunywa maji machafu hawa Magufuli ameamua kula nao sahani moja.

Kaeni na Chama chenu mudraft upya Sera zako Sera ulizooñgea ni dhaifu sana to be the Head of state.

Tuambie mambo ya kuijenga nchi lakini Personal attack zako kwa kweli hafu za uongo na kutunga ukipata kura hats laki moja kati ya wapiga kura una bahati. Umewaangusha wafuasi wako wamenywea, weakest speech ever.
 
Bado mko kizamani sana. Mpaka mtajiwe zahanati, rushwa, ufisadi nk ndio mnaona kuna kitu.

Kwa taarifa yako, unaposema utasimamia utawala wa sheria hilo limemaliza yote maana unazungumzia rushwa wakati IPO mamlaka husika na wewe kama Rais ni wajibu wako kuipa uwezo tuu iwajibike? Zahanati wizara ya Afya unaipa budget yake 100% na inatimiza mipango yake?

Madaraja unahakikisha fedha zilizotengwa zinaenda na kila jambo mamlaka husika yanatimiza wajibu.
Tunataka strong institutions na sio strong persons katika kujenga nchi.

Sio utatuzi wa mambo usubiri msafara wa Rais uje apewe mic na kamera ya TBC1 ndio unapatikana. Hayo mambo ya stone age hatutaki ni ushamba wahed
 
Lissu ni mkora tu kama wakora wengine,hafai hata kidogo ,twendeni na Magufuli 2020 October
 
Bado mko kizamani sana. Mpaka mtajiwe zahanati, rushwa, ufisadi nk ndio mnaona kuna kitu.

Kwa taarifa yako, unaposema utasimamia utawala wa sheria hilo limemaliza yote maana unazungumzia rushwa wakati IPO mamlaka husika na wewe kama Rais ni wajibu wako kuipa uwezo tuu iwajibike? Zahanati wizara ya Afya unaipa budget yake 100% na inatimiza mipango yake?

Madaraja unahakikisha fedha zilizotengwa zinaenda na kila jambo mamlaka husika yanatimiza wajibu.
Tunataka strong institutions na sio strong persons katika kujenga nchi.

Sio utatuzi wa mambo usubiri msafara wa Rais uje apewe mic na kamera ya TBC1 ndio unapatikana. Hayo mambo ya stone age hatutaki ni ushamba wahed
Ndugu Rushwa ni ajenda namba moja huwezi ukaongea kienyeji kienyeji tu hafu ukabaki salama Rushwa ni ya kuikemea kwa ukali na bila kupepesa Tanzania haina wasomi wa kuelewa mambo kwa hiyo Rushwa Rushwa Rushwa ndiye Sera namba moja ya kupambana na kiongozi
 
Ndugu Rushwa ni ajenda namba moja huwezi ukaongea kienyeji kienyeji tu hafu ukabaki salama Rushwa ni ya kuikemea kwa ukali na bila kupepesa Tanzania haina wasomi wa kuelewa mambo kwa hiyo Rushwa Rushwa Rushwa ndiye Sera namba moja ya kupambana na kiongozi
Bila kujenga mamlaka au taasisi za kitaaluma za kupambana na rushwa itabaki kuwa kelele za debe tupu kama za Jiwe. Mara mahakama maalumu, Mara mapambano moto ilimradi ulaghai mtupu na miaka mitano imekata
 
Naanza na kukupa pole Mheshimiwa Mbowe kwa kushambuliwa na wasiojulikana. Naamini Mwenyezi Mungu atakulinda na utaendeea vema na pia ukirudi ulingoni utakuwa umeimarika sana na utatuchachafya vya kutosha WanaCCM.

Ili nilnachotaka kuonesha leo ni kuwa nimesikitika sana kwa sababu Tundu Lisu hakuongelea chochote kuhusu maslahi ya wafanyakazi jana - wale watumishi wa Umma na hata wa Sekta Binafsi. Wafanyakazi hawa wa nchi wamekosa mtetezi kabisa. Miaka mitano hii wamenyanyasika sana. Kubwa zaidi ya yote ni kutoonesha hata nia tu ya kuwaongezea mishahara au kuboresha maisha yao. Tundu Lisu umeongea vema kuhusu kunyanyaswa kwa wafanyabiashara.

Lakini pia hata wafanyakazi sekta ya Sheria miaka hii wamenyanyasika sana. Ama wanasheria wa Umma ama wale mawakili wa kujitegemea. Wamenyanyasika sana. Inawezekana hujawaongelea kwa sababu inajuliana na wanasiasa wote kuwa wafanyakazi wanatengeneza segment ndogo sana ya wapiga kura wa Tanzania ndiyo maana wanasiasa hawana mpango nao kabisa.

JPM ndiyo mbaya zaidi sababu manake aliona akiwatoa wale wenye vyeti feki anatengeneza kick - lakini huyo huyo JPM alishindwa kutambua kuwa huko nyuma Serikali yenyewe ilikuwa na mifumo mibovu ya kutambua udanganyifu na makosa ya Serikali yenyewe ikajikuta inaajiri watu wa hivyo. Wamewaondoa bila hata kuzingatia haki zao wakati hata Magu mwenyewe kuna uwezekanao mkubwa aliwahi kufundishwa na Mwal aliyekuwa kafoji vyeti. Mbaya sana! Magu kaonesha wazi double standard - kaacha wanasiasa ambao wanajinadi wana elimu fulani kwa kutumia majina ya watu wengine kwa ajili tu ya kutetea maslahi ya kisiasa.

Labda kwa kumalizia tu - msifikiri kura za Wafanyakazi hazina impact kwenye Uchaguzi - endeleeni tu kuwaongelea wafanyabiasha ambao kwa sasa mnaha-ha kuwabembeleza ili wawawezeshe kwenye Kampeni zenu. Ipo siku mtatambua nguvu ya wafanyakazi.
 
Angeongelea wafanyakazi angekuja mlemavu angesema hajagusiwa walemavu,angefanya hivyo angekuja mchimbaji madini aseme kuwa hajagusia wachimbaji wadogo, etc etc. Alitakiwa atoe speech ya muda gani ili aongelee yote?
 
Wafanyakazi wa Tanz hawajitambui. Fuatilia vikao vyao kupitia vyama vyao. Vyama vile vimekuwa upande wa Waajiri huku Wafanyakazi wakiachwa bila Watetezi. Juzi nilisikitika sana kuona chama cha waalimu Tanz wakisifu na kuishangilia serikali wakati wengi wa wajumbe wale walichangiwa nauli kuhudhuria kikao kile.
 
Nigrastratatract,

Huu ni mwaka wa 59 tangu tupate Uhuru.Tunahitaji miaka mingapi zaidi ili kero ya maji,barabara na umeme viwe historia? Unadhani kwanini in 59 years ya Uhuru tumeshindwa kuwapa watu wetu maji Safi? majibu yake yako kwenye hotuba ya Lissu.
 
Muda wa kuongelea hayo haujafika, akipitishwa Kuna mengi mengi atayaongelea na kuyatolea ufafanuzi.
 
Hili lilihisiwa na wengi kuwa HOTUBA yake inakuwa ya hisia kwa yaliyomtokea zaidi.

Kutekwa watu na kupotea
Kupigwa risasi. Hapa nampa mpole
Kuonewa wapinzani

Mambo ya Muhimu kama
Elimu, Uchumi, ukwepaji wa kodi na Rushwa
Usimamizi wa rasilimali n.k hajagusa
Hotuba ilikuwa dhaifu. Natamani kama akipange atoe labda nyingine.
 
Unataka Lissu aongelee matatizo yote yanayowakumba Watanzania? Unajua akianza kuongelea matatiizo ya wabongo anaweza live stream mwezi mzima na asimalize. Muda wa kampeni bado, jana ni kutangaza nia tu, anatoa summary picha itafata baadaye.
 
Back
Top Bottom