Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,793
- 71,206
Nimegundua kuwa kuna jambo moja Mheshimiwa sana Tundu Lissu, msemaji wetu asiye na chembe ya unafiki amesahau kuliweka wazi mbele ya dunia. Jambo hilo ni ruhusa iliyotolewa kwa askari Polisi na Amiri jeshi mkuu kuwa wanaweza kuua mshukiwa yeyote na hataki kusikia afanyaye hivyo akishtakiwa kijeshi au kiraia kwa kufanya mauaji. Nadhani sasa inataka kuwa kama Nchi moja kule mashariki ya mbali.
Nimekumbuka hili ili nimkumbushe asisahahu kuliweka hadharani kwani ni ukosefu wa utawala wa sheria na dunia nzima inapiga vita tabia lakini kwetu hata jana huko Arusha kijana kapigwa risasi kituo cha Polisi akiwa chini ya ulinzi na RPC wa huko anatoa majibu kama wameua mbwa wa mtaani kwani kinga wanayo.
Nimekumbuka hili ili nimkumbushe asisahahu kuliweka hadharani kwani ni ukosefu wa utawala wa sheria na dunia nzima inapiga vita tabia lakini kwetu hata jana huko Arusha kijana kapigwa risasi kituo cha Polisi akiwa chini ya ulinzi na RPC wa huko anatoa majibu kama wameua mbwa wa mtaani kwani kinga wanayo.