Tundu Lissu: Tutanyolewa bila maji suala la mchanga wa madini, tusikurupuke

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu ameibuka na kuishauri serikali jambo la kufanya kutokana na matokeo ya uchunguzi wa mchanga wa madini uliofanywa na kamati ilyoundwa na Rais John Magufuli.

Tundu Lissu

Tundu Lissu anasema Tanzania ni mwanachama wa 'The MIGA Convention' hivyo ukiwa mwanachama ukachukua mali za wawekezaji wao utapelekwa kwenye mahakama za kimataifa na kwenda kushughulikiwa huko, hivyo Tundu Lissu ametoa ushauri wa namna nzuri ya kushughulika na watu

"Sisi Tanzania ni wanachama wa kitu kinaitwa 'The MIGA Convention' Multilateral Investment Guarantee Agency ya benki ya dunia, ukiwa mwanachama wawekezaji wakileta mali zao kwako, ukichukua mali zao kama walivyochukuliwa mali zao namna hii utapelekwa kwenye mahakama zao za kimataifa unaenda kushughulikiwa huko, tumesaini mkataba wa ulinzi wa wawekezaji na mataifa wanayotoka wawekezaji hao Marekani, Canada, Uingereza wote ni mabosi wakubwa makampuni ambayo Rais ameyakamatia mali zao yanatoka kwenye hizi nchi tuna 'bilateral investment treaties ambazo zinalinda mikataba hii" alisema Tundu Lissu

Makontena ya mchanga wenye madini yaliyozuiliwa bandarini

Tundu Lissu anasema hili suala tusipokuwa makini nalo linaweza kuleta matatizo makubwa huku akimtaja muhusika wa mikataba iliyolifikisha taifa katika hasara iliyobainika katika uchunguzi huo.

"Rais anajiingiza kwenye mgogoro mkubwa, akimkamata Dalali Kafumu peke yake, tutamwambia kwanini siyo Gray Mwakalukwa mikataba yote hii imeingia wakati wa Mr. Gray Mwakalukwa, kwanini siyo Daniel Yona, kwanini siyo Jakaya Kikwete sababu alikuwa Waziri na mimi nina mkataba wa Bulyankulu na kwanini siyo mawaziri wote, kwa sababu mikataba iliingiwa wakiwa mawaziri" alisema Tundu Lissu

Rais Magufuli akipokea ripoti ya kamati

Lakini mbali na kusema yote hayo Tundu Lissu alitoa ushauri wake katika suala hilo...

"Kama unataka kufanya haya unayoyafanya elewa hali halisi ilivyo, tatizo liko wapi kama tatizo ni kwamba tunapata mapato kidogo na kweli wanatupiga kweli kweli ila kama utaka kufanya mambo kweli kweli kajiondoe kwanza MIGA ili hao wawekezaji wasikushtaki kwenye hizo mahakama za huko, maana wakikushtaki kule unanyolewa bila maji, hakuna ndege ya Tanzania itakanyaga hizo nchi wataikamata, hakuna hela tutaweka kwenye nanii za kimataifa watazikamata, kwa sababu tunavunja mikataba ya kimataifa inayolindwa na sheria za kiwekezaji za kimataifa, kwa hiyo anzia huko juu ukimaliza mikataba ya kimataifa, njoo kwenye mikataba kati ya nchi na nchi ondoa hiyo mikataba ukishaondoa hiyo hushtakiki nje, baada ya hapo njoo ndani sababu bado unaweza kushtakiwa ndani" alisisitiza Tundu Lissu


The issue on the table at the moment ni wrong declaration of the true value of the export value with an intent of tax avoidance and royality ambayo ipo govern na income tax act yetu na makataba wetu na wao ambao unawataka walipe royality kutokana na thamani ya export value na hii haihusiani na kushikilia Mali za Mtu in contrary to mega agreement. Hivyo tunakuomba tushirikiane ili tuweze kupata kilicho chetu, la hutaki kushirikiana na sisi sawa basi kaa kimya tufanye kazi.
 
Lisu aache kuhadaa watanzania. Nani alisema hiyo miga conversion inalinda wezi. Ni vema akafanya mambo kadhaa.
Kwanza. Aache rais atekeleze wajibu wake. Pili. Aombe kuiwakilisha acacia kwelye suala hili maana anajua sana. Tatu, anaponda kila kitu kinachofanywa na serikali, aiache iafenye kazi yake. Muda wake ukifika akaingia madarakani atafanya yale anayoona yamafaa. Mwisho. Atuambie kalipwa kalipwa shs ngapi na accacia? Ajue bomu limeshalipuka.
 
Umfano ni taarifa ya kamati iliyochunguza ule mchanga

Ile taarifa ya kamati sasa haina maana yeyote imechelewa sana, ilitakiwa ichunguze huo mchanga kabla ya hiyo mikataba hapo awali sasa ni kama mumejitoa fahamu muliposign mikataba na sasa mnatia mpira kwapani., It is good for nothing.

Halafu hii taarifa ya kamati ime-base upande wa faida kwa serikali tu na kwa Wtz haikuangalia upande mwengine ambao wawekezaji kisheria ndio wenye mali kwa mujibu wa mikataba ambayo muliingia hapo kabla.
 
MAZINGATIO : UCHUNGUZI WA MCHANGA WA MADINI

Kuna tofauti za kimtazamo baina ya pande mbili za kisiasa juu ya zoezi hili la uchunguzi wa mchanga wa madini.
Ukitafkari kwa kina juu ya mvutano huu wa wanasiasa katika jambo hili utabaini kuwa; Upande mmoja upo kwa Muamerika na upande wa pili upo kwa Muingereza.

Ilianza kama BARRICK GOLD miaka ya 1983 nchini Canada chini ya himaya (commonwealth) ya Muingereza ambayo ni koloni lake toka miaka ya 1763 kupitia mkataba wa Paris(Treaty of Paris), mwaka 2000 ikahamisha makao yake mjini London na kubadili jina na kuitwa ACACIA.

Kwa kipindi kirefu sasa athari za siasa ya Muingreza zinaendelea kupotea ndani ya nchi wanachama wa EU na ndani ya makoloni yake madogo, bali zinaelekea kuzorota kifikra na kumakinika zaidi siasa ya Muamerika kuliko siasa kongwe ya Muingereza aliyekuwa na hazina kubwa ya mali kwenye makoloni yake hasa Afrika.
Dalili ya kuzorota huku ni pamoja na Muingereza mwenyewe kuathirika zaidi na urasilimali akitaka apumue kutokana na mzigo wa hasara na kuchoshwa kula mifupa hatimaye kutaka kujiengua(BREXIT) katika umoja huu ikiwa mapendekezo aliyoyaainisha kwenye Article 50 hayatopitishwa na European council , huku kila mwanachama kibaki akilinda maslahi yake, akishirikiana na yeyote mwenye nguvu ili alinde mali zake dhidi himaya ya Malkia Elizabeth ll.

Kuzorota kifikra na kuporomoka kiuchumi na kinguvu kwa Muingereza; na kuimarika kinguvu na kiuchumi kwa Muamerika kipindi kirefu dhidi ya Muingereza; imefikia hatua ya kunyang'anyana hazina za makoloni kwa kupitia vita vya wakaazi(civilians) ambapo kwenye baadhi ya maeneo hutumiwa mbinu za siasa kali, ugaidi,maendeleo, haki za binadam na demokrasia.

Libya, Iraq na Afghanistan zinapata maumivu haya mpaka leo, licha ya ahadi lukuki za muingereza na Muamerika kuwa angewapelekea haki za binadam, demokrasia ya kweli, maendeleo ya kijamii na kukomesha biashara haramu , Opium trade (hususan Afghanistan) Lakini ile dhana ya amani imekuwa ni kitendawili miaka na miaka sasa kwa maeneo haya.
Mamilioni ya watu wanakufa, hali ya uchumi ni mbaya, usalama umekuwa mdogo, amani hakuna, na uzalishaji wa opium umeongezeka kuliko ilivyokuwa awali, kadhalika na kuendelea kuzoa rasilimali za madini na mafuta tani kwa tani bure kabisa!

Wanaokubali au kukosoa zoezi la uchunguzi wa mchanga na maamuzi yake baada ya uchunguzi inatakiwa kwanza wafahamu kimsingi wapi walipoegemea,je ni kwa upande wa Muamerika au Muingereza?
Kitu ambacho kitaawangusha,ikiwa si kwa Kenge basi kwa Mamba!
 
Tundu lissu anashindwa kuelewa kuwa kudeclare kiasi cha madini tofauti na kilichopo katika makontena ni kuvunja mkataba!?...hivyo automatically Acasia wamekuwa wakivunja hiyo mikataba ambayo tobo lisu anadhani itatushinda.
Embu jiulize kwanza kabla ya kukataa ushauri .mfano enzi ya Nyerere alikamata Mali na mashamba ya mzungu tajiri mkoani Arusha kwa jina Stein maharufu kwa jina bwana ugoro alikuwa anamiliki mashamba ekari laki 3 na 60 elfu.alikamatwa kwa kosa lakukutwa na shilingi milioni 24 ndani ya ndege yake alipotua nchini Kenya.wakati huo 24 milioni ni pesa mengi sana.bajeti ya Mwaka wakati huo ni 580 milioni.Nyerere alipopata habari hiyo kutoka polisi Kenya.mzungu alipo rudi Tanzania akakamatwa akawekwa ndani uhujumu uchumi .na Mali zake zote zika zuiwa .mfano ya haya makontena ya mchanga Leo.baada ya masiku kadha wakampa dhamana wakazuia na pass yake.lakini mzungu alitoraka nchi wakati huo huo.akaenda kwao holand .akafungua kesi kwenye mahakama hi hii Lisu anayosema .Nyerere kwa ubabe huu huu unao jidai nao.akaongeza zaidi akataifisha Mali zote mashamba ,ndege ,magari akafanya shamba la serikali .wakati huo mzungu anaendelea na kesi huko majuu.huku Tanzania tumegomea ataa tulipoitwa mahakani utukwenda tuligoma.kesi ikawa inaendelea huko majuu .mfano Wa kesi ya Iptl kwa Leo,mahakama huko majuu wakatoa hukumu mzungu alipwe pesa zake zote.serikali ikataarifiwa kulipa ikagoma.Mahakama huko ikatoa amri serikali ya Tanzania ikamatiwe Mali zake popote zilipo duniani .Wakati huo Tanzania hawana habari nikama waliamua hakuna kitu watatufanya ikapita na muda ikawa tumesahau hivi.Mara ghafla ikaja taarifa meli ya Tanzania na shehena ya sukari imekamatwa ikipita kwenye pwani ya uholanzi na inapigwa bei mnadani na sukari yake meli ya takoshili wakati huo kama sijakosea jina na ilikuwa ni Mali ya ubia kati ya China na Tanzania.Ndio Mara ghafla Tanzania ikajikuta inanyolewa bila maji.Ghafla Warioba wakati huo Waziri sheria.akatumwa haraka uholanzi .matokeo yake mzungu alipidi abembelezwa akarudishiwa shamba lakini wakati huo tayari serikali ilishagawa baadhi ya mashamba kwa wananchi kutoka ekari laki 3 na 60 elfu mpaka kubakiwa na ekari 60 elfu .ikabidi wambembeleze mzungu apoke hiyo elfu 60 ambayo mpaka Leo hii ni Mali ya huyo mzungu.pamoja mabilioni taslimu na kuombwa kuendelea kulipwa pole pole na riba kila Mwaka tena kwa makubaliano deni liingizwe kwenye bajeti Tanzania likilipwa kila Mwaka.na hili deni limekuwepo kwenye bajeti Enzi ya Nyerere,Mwinyi,na Mkapa .kwa Kikwete sikupata kusikia labda itakuwa deni limekwisha ,kwa hiyo ushauri ushauri Wa Lisu niwakuzingatia
 
  • Thanks
Reactions: Ebe
Lissu huyuhuyu wa mwembeyanga na list of shame au mwingine?!!!
Stick to the point you fool. Kama hujui namna ya kujenga hoja za mada husika kuna majukwaa ya size yako pia humu kama la photos na celebrities. Tunahitaj hoja za je hii hatua ya pendekezo la lisu inaweza kutatua tatizo? Je madhara yake kitaifa na kimataifa ni yap? Je kuna mbadala? Tunachokubaliana wote ni ..lazima tuondokane na unyonyaj huu. Next is HOW?
 
Elewa kuwa acacia wamesaini mkataba wa kuchimba dhahabu. Kikawaida hata ukiokota jiwe mtaani ni composition ya minerals nyingi mno. Hivyo uwekezaji hutegemea what is your mineral of interest. Sidjani kama hayo madini yote yalioorodheshwa ni muhimu katika biashara ya dhahabu. Otherwise walipaswa kuzuia usafirishaji from day one
Mkataba unakutaka uniambie percentage ya madini fulani katika mchanga,wewe kwa ujanja wako ukaniambia yaliyopo ni 10% wkt ukweli ni 30%,mimi nilivyoshituka nikazuia huo mchanga,sasa hapo nani alianza kuvunja mkataba!?
 
Ujifunze kupembua vitu vizuri unakurupuka tu kama Rais wako.. Subiri uone jtatu wanafungua kesi mahakama ya, biashara.. Swali la kwanza wameuliza maabara zilizotunika ziko cerfified kimataifa kufanya hiyo kazi? Tayari gumi la pua round ya, kwanza tu..
Haya chief Mangungo,naona uko mstari wa mbele kuwatetea wafadhili wako!
 
Taratibu zinaongizwa na kanuni , ambazo mawaziri wajiwekea na zilikuwa zinatumika.mm nimesafirisha sana shaba ufi, kikanuni ulikuwa unadeckre unachosafirisha na si kila element, inayolipiwa mrabaha ilikuwa ni unachosafirisha, na ndo mawaziri wote na mamishina wa madini walikuwa wakizingatia.
Hivyo kama ni kulifabya liwe kisa tubadirishe kanuni na taratibu na si hivi ilivyo sasa.
Wewe ulikuwa unadeclare amount sahihi!?
 
Mheshimiwa, kwa mujibu wa mkataba wao declaration halali ni ile inayotokana na assaying iliyofanywa na chombo cha serikali kiitwacho TMAA, kwa hiyo hadi sasa Acacia hawajasema uongo, kisheria. Ingekuwa TMAA wametoa jibu halafu Acacia wakafoji, au kama TMAA wakikana viwango vilivyoandikwa kwenye containers, hapo kwa mujibu wa mkataba ndipo watakuwa wamedanganya. Lakini hadi sasa, reference figure ambayo kimkataba ni halali ni ile iliyoandikwa na TMAA na kukubaliwa nao kabla ya kufunga (seal) container. Na mkataba wao unasema kama hiyo figure inabishaniwa, basi kuna arbitration sample ambayo inapaswa kupelekwa kwa independent lab, in the presence of representatives from both Tanzania Government and Acacia. Kilichofanyika hadi sasa ni kuwa mlalamikaji (serikali yetu) amejichukulia sheria mkononi akachukua samples zake bila kuwepo uwakilishi wa mlalamikiwa, na amezifanyia analysis kwenye lab yake mwenyewe, siyo independent, kinyume na mkataba. Sijui mnanielewa wakuu?

Wametuibia kweli, lakini tumechukua hatua ambazo zitatuumiza zaidi. Tumempa mwizi wetu nafasi ya kutupiga zaidi badala ya sisi kumpiga.
Unataka kusema kuwa km TMAA walihongwa then the gvmnt haipaswi kuchukua hatua?
 
Sheria ni mchezo kwa sehemu kubwa. Wezi wanaijua hii michezo kuliko 'watakatifu'...
Sijui 'kliarensi reti' ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu, kama iko ninavyodhani basi ushauri wa Rais wa TLS kwa Rais mwenzake sio wa kubeza hata kidogo.
Prof Kabudi and associates lazima wapange timu nzuri hapo
 
Tatizo Wise Comedian,mwenzio anajua kilichopo ndani ya hiyo mikataba ni upupu mtupu ndiyo sababu anaeleza hivyo.Mikataba yetu imejengwa katika UOVU mtupu wa kujilimbikizia mali kwa wachache.Anachoshauri kifanyike mengine yanaendelea.
Mkataba ni tatizo ndio bt haiwezi kuwa ndio ukuta wa kuzuia haki yetu,km haikuwa sawa its high time now kunegotiate better deals
 
Lisu amesema anayo mikataba ya bulyankulu kwa hiyo anajua inasema nini. Pia anauelewa wa hiyo mikataba ya kimataifa inasema nini kuhusu hilo. Wakoloni huwa wanajua wanachokifanya. Kabla hawajaja kuwekeza miaka mingi nyuma walikuja na mradi wa reforms za sector ya madini. Mradi huu waliuleta kama msaada ambapo ulirekebisha sheria zetu nyingi kwa kisingizio cha kuvutia wawekezaji humo humo ndio waliweka mitego.
Lisu anapaswa kuwa real patriot kwa kuonyesha way forward kwa hapa tulipofikia na sio kujifanya mamlaka ya hali ya hewa kwa kubashiri yajayo!
 
Kwao hao maprofessor na Phd zao hawajui? Kama hawajui bora warudi chuoni wakafundishe, sioni umhimu Wa kuongozwa na wasomi katika hii nchi !!
Kama hawajui, na warudi vyuoni, tutaishia na wahimu wa namna gani?
 
Back
Top Bottom