Tundu Lissu: Sitarudi tena Tanzania hadi nihakikishiwe Usalama wangu

H
Kama amekua hatarudi kwann amekuwa anadai kulipwa posho na mishahara Yale ya ubunge pia kwann kafungua kesi ya kunyang'anywa ubunge kauli zake Ni Kama kumpa Kiki ndugai kuwa aliona mbali kuwa watu wa Jimbo lake hawana mwakilishi

Hayo yamefanyika baada ya ndugai na serikali yake kupoka ubunge wake.

Ndipo suala la usalama wake likatamalaki
 
Akihojiwa na Sauti ya Amerika kutoka Marekani, mwanasheria Mkuu wa CHADEMA na mbunge wa Zamani wa Singida Mashariki amesema hawezi kurudi tena Tanzania kwani wasiojulikana bado hawajapatikana.

Pia amesema ametishwa na mwandishi Cyprian Musiba kwenye mitandao.

Nilichopenda leo hajaongea kwa kufoka foka na mikwara km tulivyozoea labda ameanza kubadilika kimtazamo


huyo ashaishiwa siasa
 
Hata mimi sipendi arudi mpaka mwaka kesho watakapo mtimua huyu mbaya wake, akija wakamtwanga risasi atatuliza wengi sasa matokeo Lisu 1-0wasiojulika ubao usome hivyohivyo
 
amechukuwa uhamuzi wa busara sana, kuna kiongozi mstaafu pia amemshauri kwasasa asirejee had uyu baba amalize muda wake mwakani
Eenh, nimeipenda hiyo "hadi huyu baba amalize muda wake mwakani,' hata kama najua kwamba tutasubiri sana.
Amekwishatangaza yeye mwenyewe kwamba "hawezi kutoka madarakani na kuacha kazi za ujenzi wa 'mavitu' aliouanza."

Maana ya maneno hayo ni kwamba hawezi kutoka madarakani hadi 'adondoke chini', na hakuna ajuae Mungu kampa siku ngapi hapa duniani.
 
sababu aliyotoa ni ya hovyo na haina mashiko. Viongozi wake watawezaje kumhakikishia usalama wake wakati sio vyombo vya ulinzi na usalama
Wewe unaweza kuiita "sababu ya ovyo," lakini inawezekana usijue maana yake ni nini katika kuyasema hayo maneno.
 
Hakuna Jambo limefanya niwachukie watz Kama ishu ya lisu ishu ya lisu imenifanya niwachukie Sana wenye mamlaka na praise power team yao yani msemakweli na mtetea haki ya kidemokrasia mnamtwanga risasi mnampokonya ubunge halafu mnafurahia na kumkejeli ushetani ulioje?
Kuna mambo mengi ya kujifunza ndani ya jambo hili la Lissu na walio madarakani kuhusu waTanzania.

Inaonekana dhahiri anayetawala nchi anazijua vizuri sana tabia zao.
 
Naunga hoja kabisa pambana ukiwa huko huko.Hata wana frelimo ANC walipambana wakiwa tanzania
Apambane against nini? Against SGR, STIGLERS GORGE, FLY OVERS, NDEGE, BARABARA ZA LAMI TANZANIA NZIMA, MELI TANO: NYASA, TANGANYIKA NA VICTORIA, UPANUZI WA BANDARI: DAR, TANGA NA MTWARA, MABASI YA MWENDO KASI, COMMUTER TRAIN, REA UMEME VIJIJINI, UDHIBIT WA RASILIMALI ZETU, UVUVI HOLELA, MIGOGORO YA ARDHI, NIDHAM KWA WATUMISHI WA SERIKALI, HOSPTALI, ELIMU BURE, VIWANJA VYA NDEGE, RELI YA ARUSHA, TERMINAL III AIR PORT DAR, VIWANDA, UCHUMI WA KATI, AMANI, KUTOKOMEZWA KWA RUSHWA na kadhalika na kadhalika?
 
Naona mimamluki ya Jiwe yamejazana humu..sio wengi ila wana ac nyingi sana unaweza kudhani unabishana na zaidi ya watu mia kumbe wanne tu...anyway kwa mtu mwenye ubinadamu na utu..hawezi kukejeli,kudhihaki wala kuchekelea kitendo alichofanyiwa Lissu..ni pale tu unapokuwa na roho mbaya ya kishetani itakayokutuma uchekelee hicho kitendo hata kama huna dini!..
 
Maneno ya Tundu Lissu siku zote yanaonekana kuwa mepesi lakini kwa watu wenye uelewa watatambua kuwa Tundu Lissu hajawai kukosea katika comments zake. Huwa anaongea huku akifahamu fika impacts za kile anachokisema. Sasa usipokuwa makini unaweza kumwelewa kiwepesi wepesi tu wakati yeye akimaanisha matokeo makubwa mbeleni.

MUNGU AKUBARIKI TUNDU ANTIPAS LISSU


Ni ngumu sana kwa Prise Lumumba kukuelewa. Mimi ni binadamu unyama ukatili aliofanyiwa Hon. Tundu Lissu ni wa aibu kwa Taifa. watu wanachukulia juu juu tuu
 
Walimnyang'anya ubunge hili iwe rahisi kumdhibiti ,kawapiga chenga ya mwili watesi wake.
 
Jikalie ujiponeee huko achana na huku kuanzia Uongozi wa juu mpk chini huku ni unafiki mtupu hata ndani ya chama chako chenyewe
 
Hata mimi sipendi arudi mpaka mwaka kesho watakapo mtimua huyu mbaya wake, akija wakamtwanga risasi atatuliza wengi sasa matokeo Lisu 1-0wasiojulika ubao usome hivyohivyo
Alivyosema anarudi mkakenua meno na kumuita shujaa na tshirt za lissu welcome back mkauziwa.
Leo kasema harudi mnakenua tena, nyie ni zaidi ya minyumbu
 
Naona mimamluki ya Jiwe yamejazana humu..sio wengi ila wana ac nyingi sana unaweza kudhani unabishana na zaidi ya watu mia kumbe wanne tu...anyway kwa mtu mwenye ubinadamu na utu..hawezi kukejeli,kudhihaki wala kuchekelea kitendo alichofanyiwa Lissu..ni pale tu unapokuwa na roho mbaya ya kishetani itakayokutuma uchekelee hicho kitendo hata kama huna dini!..
Mi nakejelu na namdhihaki pumbavu huyo lissu! Vutu lake
 
Hakuna Jambo limefanya niwachukie watz Kama ishu ya lisu ishu ya lisu imenifanya niwachukie Sana wenye mamlaka na praise power team yao yani msemakweli na mtetea haki ya kidemokrasia mnamtwanga risasi mnampokonya ubunge halafu mnafurahia na kumkejeli ushetani ulioje?

Usipate taabu kwa hilo. Hii nchi ilijengwa kwa misingi ya ujanja ujanja wa kuvizia fursa. Nchi ya “watoto wa mjini”. Utu na “kujali wanyonge” ni kauli za kudanganyia mazoba. It’s a cruel society.

Nilishawahi kuwaambia jamaa zangu kuwa tunaishi kwenye nchi ya hatari. Wakafikiri utani. Hata Mwangosi, Ulimboka na Arusha miaka ile havikuwashtua. Awamu hii inazidi kudhihirisha ukweli huo. Watetezi wa ukatili nao wanashindana bila soni kuonyesha umahiri wao kwa vipande vya shekeli. It’s a bizarre country. On the way to the dogs.
 
Watu Kama lissu huzaliwa 1 baada ya 100 ndio huzaliwa mwingine Tena lissu ni asset kubwa Sana kwa watanzania ila tunashindwa kuitumia
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom