Tundu Lissu, silaha muhimu ya upinzani iliyolenga shabaha sahihi

Zimbabwe is important to us primarily because of major British and western economic and strategic interests in southern Africa, and Zimbabwe’s pivotal position there. Other important interests are investment (£800 million) and trade (£120 million exports in 1982), Lancaster House prestige, and the need to avoid a mass white exodus. Zimbabwe offers scope to influence the outcome of the agonising South Africa problem; and is a bulwark against Soviet inroads… Zimbabwe’s scale facilitates effective external influence on the outcome of the Zimbabwe experiment, despite occasional Zimbabwean perversity.
Mbase, natamani ningekuwa na muda wa kutosha kuongea na wewe, kwa sababu umeyasema mengi, baadhi nikikubaliana nayo, kama hilo la 'interest' za hao jamaa, ambalo kwa kweli sio geni.

Lakini pia uwe unachukua tahadhari kupima na kuchuja taarifa unazozipata. Pana upotoshaji na kila aina ya propaganda siku hizi; usipokuwa mwangalifu utaingia kichwa kichwa kwenye 'campaign' usizofahamu kabisa.

Nakubaliana na wewe moja kwa moja, sisi hatuwezi kamwe kuwategemea hao jamaa wasaidie chochote kuondoa ukandamizaji unaotukabili. Labda tuwaombe tu msaada wa usimamizi huku sisi wenyewe tukijishughulisha na mapambano yetu wenyewe. Kwa mfano. Hizi chaguzi zetu zinazokuja. Hawawezi hata kutupa msaada tu tukajua kwamba uchaguzi wetu umefanyika katika mazingira ya haki na huru kabisa? Hilo tu hawawezi wakatusaidia?

Nilivyosema, natamani ningekuwa na nafasi nzuri ya kutumia muda kujadili nawe, kwani nimeona hoja nzuri katika mchango wako.
 
Mmoja ya wakufunzi wangu Mis Pam Overend juzi alinifunza mada ngumu sana katika uwanja wa mapambano (Module: Psychology GCSE). Alisema uwanja wa mapambano haumilikiwi na mtu mmoja au kikundu kimoja, inapofika uwanja umezingirwa na adui, pigana vita ukitokea nje, akakazia kuwa nje utaungwa mkono na wabia wa umiliki wa uwanja wa vita, hawa wana kura ya turufu kumshinda adui...

Nataka kusema kwamba, upinzani Tanzania uko katika vita takatifu na utawala huu, kwa miezi zaidi ya 36 sasa, sisi wapinzani tumwekwa katika tanuru la moto wa makaa ya mawe tunapambana usiku na mchana na huyu ndugu yetu wa damu kabisa aliyeamua kutubatiza kwa moto na aliahidi kutufuta Tanzania akiamini sisi ni kikwazo kwake kupeleka maji Nkasi, Nyakanazi na maeneo mengine, kwaujumla anaamini upinzani ni kikwako cha maendeleo ya nchi, hakika ahadi yake si ya maneno ni ya vitendo hasaa, mahabusu zimejaa wakosoaji dhidi ya utawala, mahakama zimejaa kesi za uchochezi..

Amefunga kila mwanya wa sisi kupambana nae kwa hoja, amefunga mikutano ya hadhara, amefunga uhuru wa kutoa maoni, amefunga vyombo vya habari visitumulike bali vimmulike yeye tu, amefunga mitandao isimkosoe, na sasa anakwenda kufunga kabisa uweko wa vyama vya siasa kwakuweka sheria ya jehanamu rasmi.

Awali nguvu ya wanaharakati ilipata ahueni baada ya gurudumu la nje kuendeshwa na Bi Mange Kimambi, huyu bahati mbaya yeye si mwanasiasa, akachoka kuwasemea waswahili. Tulifikiri tufuate nyayo za wazee wetu wapigania uhuru akina Nyerere, Nkurumah, Machel, Neto, Mandela nk, Tukaona sasa tutafute nguvu ya kidunia tukiungwa mkono na mataifa huenda ahueni itakuwepo kupunguza kibano hiki, maana kila siku mahabusu au mahakamani, Mataifa wanawasikiliza pale mtakapoeleza masahibu yenu kwa wazi, hata kama wao wanajua kinachoendelea, lakini hawakemeagi au kuchukua hatua kama hamtapaza sauti kutoa kelele za vilio vyenu...

Bahati mbaya viongozi wetu wako jela mwezi wa tatu huu, Mungu si Magufuli wala si Makonda, Kiongozi wetu aliyechakazwa risasi zaidi ya 38 mchana kweupe Tundu Lissu huyooo kasimama na katulia katika uwanja sahihi wa kimataifa wa kuieleza dunia masahibu yaliyomkuta na hali ya mambo nchini,

Ni lazima aeleze, hana sababu ya kunyamaza, kungekuwa na kesi mahakamani dhidi ya washukiwa wa kushambuliwa kwake hakika angenyamaza kutoingilia mahakama, Sasa hakuna aliyekamatwa wala kuhojiwa mwaka wa pili unaenda tangu ashambuliwe, Serikali yenye wajibu huo ilidhani ni upepo utapita, Sasa ni wakati wa kuadhibiwa, amini nakuambia kitakachotokea watajilaumu mara mia heri lisingetokea la Lissu.

Tunaoijua dunia na siasa yake, tunawaeleza kwamba hasara ya wahalifu kwa afanyacho Lissu ni kubwa kuliko kumfunga Mbowe na Matiko, Kuliko mswada wa vyama vya Siasa, Kuliko Membe kugombea urais na kuliko kuruhusu mikutano ya vyama vya siasa, Lissu yupo kwenye laiti traki, anapiga utosini tu na msumari wa nchi sita. Hana cha kupoteza, ati ubunge?? Miezi 18 tu imesalia akachukue fomu, nini kigumu au cha maana mtakachomkwamisha yeye? Anaweza kuzungumza jukwaa lolote duniani bila nembo ya ubunge bali kama manusura wa risasi 38 au Mwanasheria wa Chadema. Anayewashauri anawadhalilisha na kuwachora zaidi...

Hana hasara yoyote, nanyi waharifu hamna faida yoyote kwake, Faida kubwa anayopata Lissu ni kuimarisha upinzani mara mia, na kuongeza mgawanyiko wa ccm mara mia.

Lissu ni silaha muhimu ya upinzani kwa sasa kupambana na hali ya mambo nchini, Songa mbele Lissu umma uliokutibu na unaokuombea siku zote uko nyuma yako, sisi huku home tumewekwa mtu kati, hatupanui hata pua tu sero kumekuwa sebule zetu, segerea kumekuwa kijiweni kwetu, kisutu ndio usiseme kumekuwa kama taarifa ya habari kila siku tuko huko, Sasa hivi kuna mtindo tunaambiwa kama tunabisha tujifanye tunajikuna...

Zingatia kesho jumatatu, 21 Januari 2019 TUNDU LISSU atakuwa BBC katika kipindi maarufu duniani cha HARDTalk, dunia itasinamama kwa dakika 30 mwanamume akizungumza kushambuliwa kwake na hali ya mambo ilivyo Tanzania

Heri ya kuzaliwa kamanda Tundu Lissu.

Na Yericko Nyerere

Updates 21/01/2019.

BBC HARDtalk 21/01/2019 Tundu Lissu MP via YouTube

Ukiamua kutunga kitabu, fanya hivyo na kiweke dukani. TUnachoka kusoma hadithi mpaka za darasani ktk blog. Huna summary? Huna abstract? Ulichotaka ni kumsifu Lissu. Bahati mbaya Interview inasikilizwa na kila mtu siyo wewe tu je, unayaona mapungufu ya Lissu au hukuyaona?

Tulio nje ya ushabiki hatuoni lolote! Kila wakati alikuwa anataka aulizwe hadithi ya kupigwa risasi. Hebu angalia alivyozoea kutukana hadi BBC anataka asikike kwa hayo! Eti kununua ndege ni petty, petty ..... fooool! Nani amekuita kukusikiliza matusi yako. Hard Talk ni mambo yenye substance! Upinzani sasa mtumieni muathirika huyu kupata kura za huruma, lakini nadhani siyo mfano mzuri wa kiongozi.
 
Nashukuru kwa kunielewa mkuu maana nikiandikaga hivi wengi wanadhani sipendi mabadiliko ama mimi ccm. Mimi siyo ccm wala chadema mimi ni free thinker ambaye sipendi siasa zinazoendelea hapa nyumbani pande zote mbili. Lissu na bashe peke yao angalau wsnatupatia matumaini. Ila tatizo hata wao wanikwaza ni kwamba kuna vitu wanakemea lakini wapo partisan zaidi kuliko maslahi ya nchi. Naweza sema Bashe ndiye mwiba zaidi ya Lissu maana anakichana chama chake sijawahi msikia Lissu akikikosoa chama chake. Na Bashe anakosoa ikifika mikutano ya kampeni anaharibu hapo ndiyo matatizo na wanasiasa wa kibongo ni vinyonga na wanafiki.
Mkuu "kuchana" ndiyo mila ianayopendwa na Watanzania wa aina yako. Muhimu kama una itikadi unachoita kuchana ni wajibu; itikadi inatoka kwenye kina cha moyo na si matukio.

Lisu kapata fursa adimu hata kama ni kwa kucharazwa risasi; kwa majaliwa na Mungu wake inaitumia vema fursa hiyo.

NDIYO MAANA TUNASISITIZIWA KUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO.

Mamlaka zote za awamu hii kama hawafikirii matokeo ya TL kwenye media za kimataifa, basi tusubiri kitakachofuata.
 
Vyovyote itakavyo kuwa mwache Lisu aongee dunia ijue kinacho endelea hapa nyumbani.Tulipo si pazuri sana ,tupo wengi tuna mengi ya kuongea lakini,hatuna pakuyasemea.MUNGU MBARIKI TUNDU LISU,MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Siasa na kazi,hakuna jinsi tutajikomboa kisiasa wakati tunaendekeza uvivu ulipindukia.
Katika Afrika,Tanzania tunaongoza kwa uvivu.Hakuna mtu atatuchukulia serious wakati tumepindukia kuwa taifa la wavivu.Fanyeni kazi kwa juhudi na maarifa ndio dawa.
labda mama yako ndio mvivu wananchi asilia 75 wapo vijijin mvua jua kiangazi masika vyote vya wanaamuka saa kumi usiku kurudi saa kuminambili wapo mashambani wavivu unawalisha mumeshindwa kutengeneza ajira serikali ya ccm halafu unatuambia ujinga
 
Ukiamua kutunga kitabu, fanya hivyo na kiweke dukani. TUnachoka kusoma hadithi mpaka za darasani ktk blog. Huna summary? Huna abstract? Ulichotaka ni kumsifu Lissu. Bahati mbaya Interview inasikilizwa na kila mtu siyo wewe tu je, unayaona mapungufu ya Lissu au hukuyaona?

Tulio nje ya ushabiki hatuoni lolote! Kila wakati alikuwa anataka aulizwe hadithi ya kupigwa risasi. Hebu angalia alivyozoea kutukana hadi BBC anataka asikike kwa hayo! Eti kununua ndege ni petty, petty ..... fooool! Nani amekuita kukusikiliza matusi yako. Hard Talk ni mambo yenye substance! Upinzani sasa mtumieni muathirika huyu kupata kura za huruma, lakini nadhani siyo mfano mzuri wa kiongozi.
Mangi muuza duka kaniambia faida 4 billions ...service 13 billions...PHD yake inabidi ichunguzwe
 
Haipo hivyo hilo kampuni ni ya Canada. Mkuu Canada umewaona wapi wanaingilia mambo ya watu? Pili fuatilia sana nchi mbili Sweden na Canada wana uhusiano mzuri sana na Tanzania tangu wakati wa Nyerere.

Ukweli utabaki kuwa hakuna chochote kitakachotokea japo hamtaki kukubali. Last week niliwakumbusha yaliyotokea Zanzibar mpaka Mkapa alibanwa HARDtalk na akawasifu askari wake kwa kuua waandamanaji. Tatizo lenu hamuishi na kukumbuka ya nyuma mnaishi kuangalia ya leo tu.
 
Maslai ya wakubwa!!! mfano mmoja ACACIA karibia migodi yao yote imeathiriea shares zimeshuka - hayo si maslahi ya wakubwa? take it or leave it hao hao wakubwa ndo hivyo unavyoona wanalinda maslahi yao. Hii kitu ya Lissu madhara yake utayaona tu muda si mrefu. Serikali kama ni wajanja waanze kurekebisha mambo haraka hasa haya yanayohusu haki za binadamu, utawala bora ana utawala wa sheria. Soon ama tayari tulishaathirika sana. Inategemea upo wapi na unatazamaje ama umguswaje lkn mwisho wa siku kila mtu ataguswa.
Hakuna madhara yoyote. Hao ACACIA wenyewe wameshakubali yaishe. Halafu ACACIA ni wacanada hawana tabia za majambazi USA NA UK. Endeleeni kujidanganya. Magufuli mnaye mpaka 2025. Ombeni Mungu ccm haitawaletea Magufuli mwingine 2025.
 
Mbase, natamani ningekuwa na muda wa kutosha kuongea na wewe, kwa sababu umeyasema mengi, baadhi nikikubaliana nayo, kama hilo la 'interest' za hao jamaa, ambalo kwa kweli sio geni.

Lakini pia uwe unachukua tahadhari kupima na kuchuja taarifa unazozipata. Pana upotoshaji na kila aina ya propaganda siku hizi; usipokuwa mwangalifu utaingia kichwa kichwa kwenye 'campaign' usizofahamu kabisa.

Nakubaliana na wewe moja kwa moja, sisi hatuwezi kamwe kuwategemea hao jamaa wasaidie chochote kuondoa ukandamizaji unaotukabili. Labda tuwaombe tu msaada wa usimamizi huku sisi wenyewe tukijishughulisha na mapambano yetu wenyewe. Kwa mfano. Hizi chaguzi zetu zinazokuja. Hawawezi hata kutupa msaada tu tukajua kwamba uchaguzi wetu umefanyika katika mazingira ya haki na huru kabisa? Hilo tu hawawezi wakatusaidia?

Nilivyosema, natamani ningekuwa na nafasi nzuri ya kutumia muda kujadili nawe, kwani nimeona hoja nzuri katika mchango wako.
nimekuelewa sana mkuu. mimi na wewe wote tunapenda mabadiliko ya kweli lakini pia tusijidanganye kwa kuona matukio machache yanayoendelea tukadhani yatatua matatizo yetu. mimi ni mtu baye japo sipendi kuyaona yanayotokea nchini lakini hiyo hainisukumi mimi kujiliwaza na mambo ya kufikirika.

wengi wameshangilia sana uwepo wa Lissu BBC lakini mjadala baada ya bbc umetuonyesha kuna makundi. Na ningependa sana kuwaona wanasiasa wetu hasa wa upinzani wanapoenda kuhojiwa na vyombo vya nje wajiandae sana. kuna aadhi ya vyombo vya habari vinaweza kukupandisha ama kukushusha.

Tatizo kub
 
Ukiamua kutunga kitabu, fanya hivyo na kiweke dukani. TUnachoka kusoma hadithi mpaka za darasani ktk blog. Huna summary? Huna abstract? Ulichotaka ni kumsifu Lissu. Bahati mbaya Interview inasikilizwa na kila mtu siyo wewe tu je, unayaona mapungufu ya Lissu au hukuyaona?

Tulio nje ya ushabiki hatuoni lolote! Kila wakati alikuwa anataka aulizwe hadithi ya kupigwa risasi. Hebu angalia alivyozoea kutukana hadi BBC anataka asikike kwa hayo! Eti kununua ndege ni petty, petty ..... fooool! Nani amekuita kukusikiliza matusi yako. Hard Talk ni mambo yenye substance! Upinzani sasa mtumieni muathirika huyu kupata kura za huruma, lakini nadhani siyo mfano mzuri wa kiongozi.
Mkuu kama ulikua kichwani kwangu. Lissu ajiangalie sana na hawa watu wa vyombo vya habari wakati anahojiwa. Akiongea na Sali wa VOA waswshili wenzetu ndiyo aongee vile maana Nsali anajua nini anachokiongea kwa experience hao kina Stephen Sackur wao ni kwena na facts. Kuhusu kupigwa risasi labda watamuelewa lakini kuna vitu vingine alichemka sana. Ndiyo maana siku zote hua nasema wanasiasa wetu ni weupe sana.

Bora ya wale wa wakati wa Nyerere kaiangalie HARDtalk ya Mkapa ambaye alihojiwa na nguli wa hardtalk Tim Sebastian na linganisha ya mwanasheria ni vitu viwili tofauti. Labda sababu Mkapa ni mwandishi wa habari sijui. Kwa Mkapa ilitakiwa iwe ngumu maana alishutumiwa serikali yake na chama kili rig matokeo na mauaji ya wanzanzibar. lakini alimudu.
 
Mkuu kama ulikua kichwani kwangu. Lissu ajiangalie sana na hawa watu wa vyombo vya habari wakati anahojiwa. Akiongea na Sali wa VOA waswshili wenzetu ndiyo aongee vile maana Nsali anajua nini anachokiongea kwa experience hao kina Stephen Sackur wao ni kwena na facts. Kuhusu kupigwa risasi labda watamuelewa lakini kuna vitu vingine alichemka sana. Ndiyo maana siku zote hua nasema wanasiasa wetu ni weupe sana.

Bora ya wale wa wakati wa Nyerere kaiangalie HARDtalk ya Mkapa ambaye alihojiwa na nguli wa hardtalk Tim Sebastian na linganisha ya mwanasheria ni vitu viwili tofauti. Labda sababu Mkapa ni mwandishi wa habari sijui. Kwa Mkapa ilitakiwa iwe ngumu maana alishutumiwa serikali yake na chama kili rig matokeo na mauaji ya wanzanzibar. lakini alimudu.
Lisu bado mshamba sana. Anafikiri dunia nzima watu wana mawazo ya kichadema chadema. Ajue anapoongea BBC anaangaliwa na watu wa mataifa mengi (waafrica wa nchi mbali mbali wakiwemo) sio makamanda tu. Leo kajiabisha, ingawa makamanda wanajifariji kama kawaida yao.
 
Mbona mnahangaika sana kumpangia lissu nini afanye, na nini asifanye, mfano si ameishaonyesha Jiwe alishasema hapangiwi si muufuate na kwa lissu au mkuki kwa nguruwe kijani kibichi.
 
Back
Top Bottom