mbenge
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 4,572
- 9,808
Sote tu mashahidi ya kwamba cheche za hoja zenye mashiko ya nguvu na zikishadadishwa na mantiki za kimdahalo, na hata kuibua mijadala yenye tija ktk kuhamasisha na kuwalazimisha makada wa CCM walazimike kumjibu TAL. Hii ni kuashiria cha wazi ni YEYE ndiye mwenye kuwakilisha wapinzani makini wa serikali iliyopo madarakani.
Mwaka 2015 ingawaje ENL aliwakilisha "icon" ya UKAWA lakini alikuwa ni kiongozi dhaifu kuweza kusimamia dhuluma ya kidemokrasia iliyofanyika dhidi ya maamuzi halali ya umma ya kuikataa CCM. Mwaka huu kimeeleweka, nasema tena kimeeleweka. Huku Tanganyika tunaye TAL na kule Zanzibar ndio tu Maalim Seif.
Upuuzi wowote ule wa kutaka kuchakata matokeo ya uchaguzi yatapatiwa tiba mbadala. Umefika wakati muhimu sasa, kumbukumbu zote za CCM zikatafutwe kule jumba la makumbusho ya taifa.
Mwaka 2015 ingawaje ENL aliwakilisha "icon" ya UKAWA lakini alikuwa ni kiongozi dhaifu kuweza kusimamia dhuluma ya kidemokrasia iliyofanyika dhidi ya maamuzi halali ya umma ya kuikataa CCM. Mwaka huu kimeeleweka, nasema tena kimeeleweka. Huku Tanganyika tunaye TAL na kule Zanzibar ndio tu Maalim Seif.
Upuuzi wowote ule wa kutaka kuchakata matokeo ya uchaguzi yatapatiwa tiba mbadala. Umefika wakati muhimu sasa, kumbukumbu zote za CCM zikatafutwe kule jumba la makumbusho ya taifa.