Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,883
TUNDU LISU RUDI NYUMBANI, RAIS MAGUFULI ATIMIZE AHADI YAKE.
Na, Robert Heriel
Sisi wote ni wanadamu, kila mmoja anamapungufu yake ambayo anahangaika kuyaweka sawa ili tuwe wakamilifu. Hatuwezi kuwa na tabia zile zile mbaya zinazowaumiza wengine, ni lazima tuziondoe ili kulifanya taifa hili kuwa sehemu salama.
Hatuwezi kuendekeza jeuri na viburi vyetu vya uzima ambavyo kimsingi havitusaidii, ni wakati wa kujishusha, kujinyenyekeza kabla mwenye nguvu hajatunyenyekeza. Licha ya kuwa tuna sifa na hadhi tofauti, lakini haiondoi ukweli kuwa sisi ni sawa mbele za Mungu.
Nichukue nafasi hii kumuomba Lisu arudi nchini, nakuomba Tundu Lisu Rudi nchini tuijenge nchi yetu, pengine huenda tumekukosea, pengine huenda tumekuumiza, pengine huenda tumeufanya moyo wako umejawa na uchungu mwingi ndani ya nafsi yako. Sisi ni ndugu zako, haijalishi tumekosana kwa kiasi kipi, haijalishi tumejeruhiana mioyo yetu, akili zetu na miili yetu kwa kiasi kipi. Tunaomba utusamehe ikiwa ndivyo ilivyo.
Sisi ni binadamu, tunaweza kukosea kwa tamaa zetu, au kiburi chetu, au hata kujigeuza miungu.
Sisi kama ulitukosea, tumeshakusamehe, Rudi Nyumbani, huna haja ya kutanga tanga huko duniani.
Ikiwa wewe ni Mtu wa Dini, basi utafahamu kisa cha Nabii Yusufu na nduguze kumi na Moja, walivyotaka kumuua, lakini kwa nasibu na rehema za Mungu wakimuuza kwa Waishmael kisha baadaye akauzwa Misri kama Mtumwa, Baadaye Mungu akambariki na kumstawisha sana mpaka akawa sehemu ya watoa maamuzi wenye mamlaka katika nchi ya Misri, Mwishowe aliwasamehe ndugu zake licha ya kutaka kumuua na kumuuza.
Sasa huenda sisi ndugu zako watanzania tukawa mfano wa ndugu za Yusuph, nakusihi ufungue moyo wako kutusamehe Urudi Nyumbani tuijenge nchi. Kiukweli hatufurahii unayoyafanya huko, bila shaka nawe hufurahii mambo hayo.
Nawe Mhe. Rais, nakuomba uwe kama Baba kwa kijana wake, kwa vile wewe ni mtu wa dini pia, bila shaka unafahamu kisa cha Mwana Mpotevu katika kitabu cha Luka 15. Fungua moyo wako, haijalishi amekukosea au umemkosea, huo ni ubinadamu, lakini umungu ni kusameheana, mchukulie kama Mwana mpotevu.
Kwa bahati nzuri Mhe,. Rais kwenye kampeni zake alishasema kuwa yupo tayari kumpokea Tundu Lisu na kumpa kazi alitumikie taifa. Bila shaka Rais alikuwa anamaanisha kile alichokuwa akikisema. Sasa ni muda wa Lisu kurudi nyumbani, kumalizana katika yale anayoona tumemkosea nasi ametukosea.
Ninachoomba ni kuwa Tundu Lisu asiwe kama mwana Mkaidi akashupaza shingo kwa Kiburi cha Uzima. Arudi ajinyenyekeze kama Rais Magufuli alivyojinyenyekeza kwa kumuambia atampa kazi ndogo ya kufanya,
Rais Magufuli kusema hivyo sio kwamba hana watu wengine wa kuwapa cheo lakini ni dalili ya kuonyesha unyenyekevu kwa Tundu Lisu na kuhisi vile Lisu anavyohisi.
Nafahamu wapo watu watakaoumia na kurudi kwa Tundu Lissu na kupewa cheo na Mhe. Rais, wapo watakaokuwa kama yule mwana wa nyumbani aliyemuonea wivu mdogo wake(mwana mpotevu) kwa kufanyiwa sherehe ya kufa mtu na Baba yake.
Nafahamu wapo ambao watajisikia vibaya wakimuona Magufuli akimteua Lisu wakati wao wamekitumikia chama siku nenda Rudi. Hiyo haitaondoa ukweli kuwa, siku Lisu na Magufuli watakapo kutana na kuyajenga itakuwa siku kubwa sana ndani ya taifa hili.
Naomba Tundu Lisu, au watu wa karibu yake waanze mchakato wa kumsihi Lisu aache ukaidi, wamtafute Mhe. Rais wayamalize, kisha Lisu arudi nchini aendelee na ujenzi wa nchi.
Pia namuomba Mhe. Rais, awe kama yule Baba kwenye kisa cha mwana mpotevu ambaye kila ilipofika jioni alikuwa akisimama nje ya njia kuona kama mwanaye anarudi, au jinsi yule Baba alivyokuwa akituma watu kwenda miji ya mbali kumtafuta mwanaye.
Lisu acha ukaidi, Siasa za uchaguzi ulizifanya kwa kiwango chako na uelewa wako na uwezo wako. Uliyokosea tumekusamehe, waliyokukosea nawe wasamehe.
Samehe nafasi ikiwepo, usisubiri nafasi ikiwa haipo.
Tundu Lisu Rudi nchini, Mhe Rais Atimize ahadi yake. Ujeuri, kiburi na ukaidi havitasaidia.
Hata usipopewa cheo usije umia lakini tunakuhitaji nyumbani.
Nimalize kwa kusema, Heri waliowapatanishi kwa maana hao watamuona MUNGU.
Wale mnaopenda mifarakano mjue wazi kuwa haitasaidia kwa lolote lile.
Ulikuwa nami;
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar esa salaam
Na, Robert Heriel
Sisi wote ni wanadamu, kila mmoja anamapungufu yake ambayo anahangaika kuyaweka sawa ili tuwe wakamilifu. Hatuwezi kuwa na tabia zile zile mbaya zinazowaumiza wengine, ni lazima tuziondoe ili kulifanya taifa hili kuwa sehemu salama.
Hatuwezi kuendekeza jeuri na viburi vyetu vya uzima ambavyo kimsingi havitusaidii, ni wakati wa kujishusha, kujinyenyekeza kabla mwenye nguvu hajatunyenyekeza. Licha ya kuwa tuna sifa na hadhi tofauti, lakini haiondoi ukweli kuwa sisi ni sawa mbele za Mungu.
Nichukue nafasi hii kumuomba Lisu arudi nchini, nakuomba Tundu Lisu Rudi nchini tuijenge nchi yetu, pengine huenda tumekukosea, pengine huenda tumekuumiza, pengine huenda tumeufanya moyo wako umejawa na uchungu mwingi ndani ya nafsi yako. Sisi ni ndugu zako, haijalishi tumekosana kwa kiasi kipi, haijalishi tumejeruhiana mioyo yetu, akili zetu na miili yetu kwa kiasi kipi. Tunaomba utusamehe ikiwa ndivyo ilivyo.
Sisi ni binadamu, tunaweza kukosea kwa tamaa zetu, au kiburi chetu, au hata kujigeuza miungu.
Sisi kama ulitukosea, tumeshakusamehe, Rudi Nyumbani, huna haja ya kutanga tanga huko duniani.
Ikiwa wewe ni Mtu wa Dini, basi utafahamu kisa cha Nabii Yusufu na nduguze kumi na Moja, walivyotaka kumuua, lakini kwa nasibu na rehema za Mungu wakimuuza kwa Waishmael kisha baadaye akauzwa Misri kama Mtumwa, Baadaye Mungu akambariki na kumstawisha sana mpaka akawa sehemu ya watoa maamuzi wenye mamlaka katika nchi ya Misri, Mwishowe aliwasamehe ndugu zake licha ya kutaka kumuua na kumuuza.
Sasa huenda sisi ndugu zako watanzania tukawa mfano wa ndugu za Yusuph, nakusihi ufungue moyo wako kutusamehe Urudi Nyumbani tuijenge nchi. Kiukweli hatufurahii unayoyafanya huko, bila shaka nawe hufurahii mambo hayo.
Nawe Mhe. Rais, nakuomba uwe kama Baba kwa kijana wake, kwa vile wewe ni mtu wa dini pia, bila shaka unafahamu kisa cha Mwana Mpotevu katika kitabu cha Luka 15. Fungua moyo wako, haijalishi amekukosea au umemkosea, huo ni ubinadamu, lakini umungu ni kusameheana, mchukulie kama Mwana mpotevu.
Kwa bahati nzuri Mhe,. Rais kwenye kampeni zake alishasema kuwa yupo tayari kumpokea Tundu Lisu na kumpa kazi alitumikie taifa. Bila shaka Rais alikuwa anamaanisha kile alichokuwa akikisema. Sasa ni muda wa Lisu kurudi nyumbani, kumalizana katika yale anayoona tumemkosea nasi ametukosea.
Ninachoomba ni kuwa Tundu Lisu asiwe kama mwana Mkaidi akashupaza shingo kwa Kiburi cha Uzima. Arudi ajinyenyekeze kama Rais Magufuli alivyojinyenyekeza kwa kumuambia atampa kazi ndogo ya kufanya,
Rais Magufuli kusema hivyo sio kwamba hana watu wengine wa kuwapa cheo lakini ni dalili ya kuonyesha unyenyekevu kwa Tundu Lisu na kuhisi vile Lisu anavyohisi.
Nafahamu wapo watu watakaoumia na kurudi kwa Tundu Lissu na kupewa cheo na Mhe. Rais, wapo watakaokuwa kama yule mwana wa nyumbani aliyemuonea wivu mdogo wake(mwana mpotevu) kwa kufanyiwa sherehe ya kufa mtu na Baba yake.
Nafahamu wapo ambao watajisikia vibaya wakimuona Magufuli akimteua Lisu wakati wao wamekitumikia chama siku nenda Rudi. Hiyo haitaondoa ukweli kuwa, siku Lisu na Magufuli watakapo kutana na kuyajenga itakuwa siku kubwa sana ndani ya taifa hili.
Naomba Tundu Lisu, au watu wa karibu yake waanze mchakato wa kumsihi Lisu aache ukaidi, wamtafute Mhe. Rais wayamalize, kisha Lisu arudi nchini aendelee na ujenzi wa nchi.
Pia namuomba Mhe. Rais, awe kama yule Baba kwenye kisa cha mwana mpotevu ambaye kila ilipofika jioni alikuwa akisimama nje ya njia kuona kama mwanaye anarudi, au jinsi yule Baba alivyokuwa akituma watu kwenda miji ya mbali kumtafuta mwanaye.
Lisu acha ukaidi, Siasa za uchaguzi ulizifanya kwa kiwango chako na uelewa wako na uwezo wako. Uliyokosea tumekusamehe, waliyokukosea nawe wasamehe.
Samehe nafasi ikiwepo, usisubiri nafasi ikiwa haipo.
Tundu Lisu Rudi nchini, Mhe Rais Atimize ahadi yake. Ujeuri, kiburi na ukaidi havitasaidia.
Hata usipopewa cheo usije umia lakini tunakuhitaji nyumbani.
Nimalize kwa kusema, Heri waliowapatanishi kwa maana hao watamuona MUNGU.
Wale mnaopenda mifarakano mjue wazi kuwa haitasaidia kwa lolote lile.
Ulikuwa nami;
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar esa salaam