Tundu Lissu: Prof. Kabudi anajipendekeza na kujikomba kwa wanasiasa walioko madarakani miaka yake yote

Lisu naye ni wale wale tu, alikuwa anajipendekeza kwa wazungu kwa kututishia kuwa tukiwachukulia hatua yeyote ile watatushitaki Miga.
 
Profess kabudi katengeneza ajira kwa watanzania nje wakati Yeye Tundu Lisu anazurura na bakuli kuwaomba walioajiriwa wamchangie pesa ya kula,pango,nguo na ada za kusomesha watoto!!! Anayeaibisha hapo? Ni Nani Ni Lisu.Tabia ya kuomba omba sio ya wanyaturu.Lisu ndie omba omba wa kwanza mnyaturu Mimi kumwona toka nizaliwe.Sijawahi kutana na omba omba wa kinyaturu zaidi ya Tundu Lisu
Kumbe na wewe ni mpumbavu!!
 
Kuna Professor kutoka jalalani (UDSM) aliongoza uchunguzi wa makinikia na masuala ya madini akaja na report ya tume aliyoiongoza. Tundu Lissu alipoisoma hakukaa kimya, ali comment kwa kuiita Professorior Rubbish.

Wote tunatambua na kukubaliana kuwa Rubbish kwake ni jalalani. Inakuwaje hivi sasa watu wanatumia nguvu nyingi kumuandama Prof. Kabudi kwa kukiri kwake kuwa ameokotwa kutoka Jalalani (UDSM)? Ina maana mara hii wamesha sahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshangilia Tundu Lissu?

Kwa wale wanaomtetea Prof. Kabudi hivi sasa ina maana na wao mara hii wamesahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshambulia Tundu Lissu kwa kuthubutu kumsema Professor kuwa alichokifanya kilikuwa ni Professorior Rubbish?

Hebu makundi haya mawili yakae chini na kushikana mikono, kwani hadi hivi sasa mshindi ni Tundu Lissu, ninyi mashabiki hakuna mshindi kati yenu, mmetoshana nguvu.
 
Kuna Professor aliongoza uchunguzi wa makinikia na masuala ya madini akaja na report ya tume aliyoiongoza. Tundu Lissu alipoisoma hakukaa kimya, ali comment kwa kuiita Professorior Rubbish.

Wote tunatambua na kukubaliana kuwa Rubbish kwake ni jalalani. Inakuwaje hivi sasa watu wanatumia nguvu nyingi kumuandama Prof. Kabudi kwa kukiri kwake kuwa ameokotwa kutoka Jalalani? Ina maana mara hii wamesha sahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshangilia Tundu Lissu?

Kwa wale wanaomtetea Prif. Kabydi hivi sasa ina maana na wao mara hii wamesahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshambulia Tundu Lissu kwa kuthubutu kumsema Professor kuwa alichokifanya kilikuwa ni ProfessoriorbRubbish?

Hebu makundi haya mawili yakae chini na kushikana mikono, kwani hadi hivi sasa mshindi ni Tundu Lissu, ninyi mashabiki hakuna mshindi kati yenu, mmetoshana nguvu.
Umewaza mbali na sahihi kabisa. Bravo!
 
Kuna Professor aliongoza uchunguzi wa makinikia na masuala ya madini akaja na report ya tume aliyoiongoza. Tundu Lissu alipoisoma hakukaa kimya, ali comment kwa kuiita Professorior Rubbish.
Wote tunatambua na kukubaliana kuwa Rubbish kwake ni jalalani. Inakuwaje hivi sasa watu wanatumia nguvu nyingi kumuandama Prof. Kabudi kwa kukiri kwake kuwa ameokotwa kutoka Jalalani? Ina maana mara hii wamesha sahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshangilia Tundu Lissu?
Kwa wale wanaomtetea Prif. Kabydi hivi sasa ina maana na wao mara hii wamesahau kuwa wakati fulani waliwahi kumshambulia Tundu Lissu kwa kuthubutu kumsema Professor kuwa alichokifanya kilikuwa ni ProfessoriorbRubbish?

Hebu makundi haya mawili yakae chini na kushikana mikono, kwani hadi hivi sasa mshindi ni Tundu Lissu, ninyi mashabiki hakuna mshindi kati yenu, mmetoshana nguvu.
Nafikiri unapaswa kuelewa hili.

Kuna utofauti wa kimuktadha, Proffesor Kabudi kama sehemu ya kamati ni tofauti na Proffesor Kabudi kama mtu binafsi.

Lisu ali attack ripoti ya kamati na opinions zake zilikuwa professionally , Kabudi yeye amejizungumzia personally na experience yake.

Ni sawa na mwanaume kama mume wa mke na mwanaume kama baba wa familia ni mazingira tofauti, mtu huyo mmoja anaweza kufanya jambo lile lile lakini tafsiri ikawa tofauti kwasababu amefanya ktk nafasi tofauti za kimamlaka.

Every situation is situational.
 
Nimekumbuka zamani jinsi ambavyo mitaani tulioishia darasa la saba tulivyokuwa tunawaogopa watu wanaoitwa maprofesa. Anapita Profesa akitembea kwa miguu mtaani kwenu, tunanong’onezana ‘profesa huyo!’.

Unadhani ni kwa nini ilikuwa hivyo? Zamani tuliwaheshimu maprofesa kwa elimu yao. Wengi hawakuwa matajiri. Tulihofia zaidi akili zao. Tulifikiria jinsi ambavyo walikuwa wana uwezo wa kufikiria mambo kwa upana zaidi bila ya kuyageuka siku za usoni.

Kadri siku zinavyosonga sisi tulioishia elimu ya darasa la saba Shule ya Msingi Mapambano na kwingineko hatuna hofu sana wala wivu juu ya akili zao. Wala hatuna wivu sana kwamba lazima tufike walikofika.

Wengi, hasa walioingia katika siasa, akili zao ni sawa na zetu wa darasa la saba. Unamkuta Profesa uliyekuwa unamheshimu sana anaongea vitu vya ajabu. Afadhali angekuwa anaongea hayo huku akiwa ni msimamo wake wa muda mrefu uliopita. Hapana, ni mtu ambaye miezi 36 nyuma alikuwa anaongea lugha nyingine. Unajiuliza ni huyu huyu Profesa Njaakali au mwingine?

Kuna watu ambao majina yao yanaanzia na Dk yaani dokta, nao ni hivyohivyo. Unamshangaa mtu ambaye miezi 36 uliiamini akili yake. Ulikuwa unapenda kumuona akiongoza mijadala. Leo ghafla akili yake na mimi wa darasa la saba zimefanana. Mara nyingi katika ubongo wa mwanadamu akili huanzia chini kwenda juu. Ukibakia darasa la saba unabakia hivyo hivyo. Lakini siku hizi kuna watu ambao akili zao zinatoka juu zinakuja chini. Zinatukuta darasa la saba kama walivyotuacha.

Nadhani akili zao tungeendelea kuziheshimu kama wangeachwa wafanyie kazi mambo waliyosomea. Wakiingia katika siasa wanarudi kuwa darasa la saba. Mtu ambaye majuzi alidai Katiba ni lazima halafu leo anasema sio lazima, ana tofauti gani na mimi darasa la saba ambaye sijui kama Katiba ni lazima au sio lazima?

Matokeo yake ule wivu wetu kwa maprofesa umeondoka. Wivu wetu kwa madokta haupo. Wakati mimi wa darasa la saba nipo katika kituo cha basi nikikaba abiria na kuchomoa pochi zao na wao kumbe ni kama wanakaba tu katika maeneo mengine ya heshima kwa ajili ya kusaka riziki. Acha maisha yaendelee.
 
Profess kabudi katengeneza ajira kwa watanzania nje wakati Yeye Tundu Lisu anazurura na bakuli kuwaomba walioajiriwa wamchangie pesa ya kula,pango,nguo na ada za kusomesha watoto!!! Anayeaibisha hapo? Ni Nani Ni Lisu.Tabia ya kuomba omba sio ya wanyaturu.Lisu ndie omba omba wa kwanza mnyaturu Mimi kumwona toka nizaliwe.Sijawahi kutana na omba omba wa kinyaturu zaidi ya Tundu Lisu
Ajira zipi mkuu, hata miezi mitatu hajamaliza wizara ya mambo ya nje,au na wewe ndiyo wale wapumbavu wa Magufuli
 
*Inaandikwa na Mhe Tundu Lissu*


Katika kitabu chake 'Intellectuals at the Hill' (kilichapishwa miaka ya kati ya '90), Prof. Issa G. Shivji aliwahi kusema kuwa kuna tabia ya wasomi wetu kujipendekeza na kujikomba kwa watawala na kufanya mambo ya hovyo kuliko warasimu wa kawaida, hasa wanapopewa vyeo vya uteuzi na Rais.

Prof. Pala Kabudi ni mfano mzuri wa wasomi wa aina hii. Ni mtu ambaye amejipendekeza na kujikomba kwa wanasiasa walioko madarakani miaka yake yote ya kitaaluma.

Ukiachia msimamo wake akiwa kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambao mimi binafsi niliushangaa sana, Prof. Kabudi hana historia yoyote ya msimamo huru katika masuala muhimu ya nchi.

Ana akili za kitaaluma nyingi sana, lakini ana tabia ya kujikomba na kujipendekeza inayotia kinyaa na kufuta sifa zote za usomi wake.

Alitumiwa sana na Serikali ya Jakaya Kikwete na ya Ben Mkapa kabla ya hapo kama consultant wa masuala mbali mbali ya kisheria. Kwa hiyo anahusika kwa kiasi fulani na uchafu wa Kikwete na Mkapa ambao yeye na Magufuli wanajifanya kuukataa sasa.

Alikuwa mwandishi habari wa Uhuru/Mzalendo wakati wa Vita ya Kagera na, aliwahi kutuambia akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya LEAT, alitunukiwa zawadi na Mwalimu Nyerere kwa uandishi wa makala za propaganda zilizokuwa zinahusu Vita hiyo.

Prof. Kabudi amekuwa Chuo Kikuu cha Dar, kama mwanafunzi na kama mwalimu, tangu mwaka '80 hadi alipostaafu mwaka '16. Amekaa Ujerumani na kusomea Frei Universiteit Berlin, mojawapo ya vyuo vikuu maarufu kabisa barani Ulaya na duniani, kwa miaka 9.

Amekuwa Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar, na mjumbe wa Tume ya Katiba aliyeteuliwa na Rais Kikwete.

Huyu mtoto wa Mchungaji wa Kanisa la Anglican, sio mtu aliyezaliwa kwenye vumbi na kuishi kwenye ufukara. Hakutolewa jalalani kokote na Rais Magufuli. Amekuwa na bado ni sehemu ya top elite ya Tanzania.

Alichokisema mbele ya Rais Magufuli sio cha kweli hata kidogo, lakini ni ishara kamili ya hulka yake ya kujidhalili na kujikomba ili aendelee kutumikia Jimbo lake kuu la uchaguzi: tumbo lake.

Pamoja na kuwa ni Mgogo, Prof. Pala Kabudi ni Msingida mwenzetu. Bibi yake ni Mnyaturu wa kwetu. Baba na Mama yake ni wazaliwa wa Kilimatinde, na yeye mwenyewe amesomea shule ya msingi mojawapo ya Singida mjini.

Kujikomba na kujidhalili mbele ya Rais Magufuli kumechafua sifa na hadhi ya wasomi wetu kwa ujumla. Kwa sisi Wasingida wenzake, ametushushia heshima yetu sana. Tuna kila sababu na haki ya kumzodoa na kumkanya kwa upumbavu wake huu.
Maelezo haya nayakubali na ni vizuri kutoa changamoto kwa viongozi ambao wanapotoka. Lakini Kabudi sasa hivi ni mwanasiasa kama alivyo Lissu. Je, Lissu mwenyewe ni mkweli kiasi anachokitaka? Nauliza tena Lissu ni mkweli kiasi cha kumporomoshea mwenzake matusi na kumpa sifa ya kujikomba?

Ktk uandishi huu Lissu anajionyesha kwamba alimjua sana Kabudi tangu siku za nyuma na kwamba msimamo wake ktk tume ya katiba aliushangaa. Naamini huo ni uongo. Kwa mdomo wa Lissu, kama angeushangaa basi angesema wakati ule. Lissu ni mtu asiye na 'kaba' ya miaka 5 hadi leo ndo atoe maelezo ya tabia ya Kabudi kwa miaka 5 iliyopita. Ni kutafuta sifa asizokuwa nazo yeye mwenyewe.
 
Tukianzisha timu ya mpira wa miguu ya maprofesa itakuwaje?
Key players ni; Golini analinda Dr Benson Bana, wakati beki mstaarabu ni Profesa Kitila Mkumbo, midfielder anakiputa propesa Lipumba na striker Kabudi mwenyewe!
Hiyo yaweza kuwa na slogan ya KUFUNGWA TWAFUNGWA LAKINI CHENGA TWAWALA
 
hata siku moja Lissu hawezi kumuita wala kuita kilichoandikwa na prof.Kabudi rubbish , huyo Lissu anaijua shughuli ya profesa vizuri. Mabeberu waijua shughuli ya Kabudi na wameanza kutumia vibeberu kumtikisa, ule ni mwamba wa win-win situation
 
Profess kabudi katengeneza ajira kwa watanzania nje wakati Yeye Tundu Lisu anazurura na bakuli kuwaomba walioajiriwa wamchangie pesa ya kula,pango,nguo na ada za kusomesha watoto!!! Anayeaibisha hapo? Ni Nani Ni Lisu.Tabia ya kuomba omba sio ya wanyaturu.Lisu ndie omba omba wa kwanza mnyaturu Mimi kumwona toka nizaliwe.Sijawahi kutana na omba omba wa kinyaturu zaidi ya Tundu Lisu
Kabla hayajashambuliwa alikuwa anamwomba nani? Au kabudi nae kashambuliwa?(compromised) tuwe wakweli ili nchi iende mbele Rais apate watu sahihi!.
 

Similar Discussions

63 Reactions
Reply
Back
Top Bottom