Tundu Lissu: Paper Tigers wanatushauri tususie chaguzi zijazo ili CCM wapite bila kupingwa

Naomba na mimi kuchangia mjadala huu kidogo. Na mapema kabisa niwaombe radhi wote nitakaowakwaza, kwa sababu nafikiri nitakachosema kitawakwaza wengi humu.

Nimefuatilia mjadala wa yaliyojiri Korogwe Vijijini na nikiri nimeshuhudia utoto wa kisiasa wa kutisha na kusikitisha sana. Nimeona kile ambacho Lenin alikiita 'an infantile disorder' miaka mia moja iliyopita. Naomba kufafanua.

Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake zinaelekeza kwamba mgombea anatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kabla ya saa kumi ya siku moja kabla ya siku ya uteuzi.

Sheria inasema fomu za uteuzi zitakabidhiwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo. Maadili ya Uchaguzi yameelekeza wazi kwamba Msimamizi wa Uchaguzi anatakiwa awepo ofisini kwake wakati wote anaotakiwa ili kupokea fomu za uteuzi za wagombea.

Kwa hiyo, kitu cha kwanza cha kujiuliza ni je, mgombea wetu alipeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati uliowekwa kisheria au hakufanya hivyo???

Kama alifanya hivyo, je, kwa nini fomu zake hazikupokelewa??? Kama hakufanya hivyo ni kwa nini na lawama iangukie wapi???

Baada ya kupata jibu la swali la kwanza, swali la pili ni je, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo alikuwepo ofisini kwake kwa wakati wote aliotakiwa kuwepo ili kupokea fomu za uteuzi za wagombea???

Kama alikuwepo je, alipokea fomu za uteuzi za wagombea kama inavyotakiwa na Sheria??? Kama hakuwepo, je, ni kwa nini na lawama iangukie wapi???

Kwa ninayoyasoma mitandaoni, mgombea wetu alipeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati muafaka. Na wala hakuwa peke yake, walikuwepo wagombea wa CCM na ACT-Wazalendo.

Kwa ninayoyasoma mitandaoni, wagombea walipofika ofisini kwa Msimamizi wa Uchaguzi wakakuta hayupo ofisini kwake wakati aliotakiwa kuwepo. Inasemekana alikuwa ameitwa kwa Mkuu wa Wilaya.

Fomu za mgombea wetu na wa ACT-Wazalendo hazikupokelewa lakini, somehow, fomu za mgombea wa CCM zikabandikwa ukutani na mara akatangazwa kuwa amepita bila kupingwa!!!!

Je, aliyekosea hapa ni nani??? Je, ni mgombea aliyepeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati??? Je, ni Katibu wa Wilaya ya Korogwe Vijijini au wa Mkoa wa Tanga??? Au Katibu wa Kanda ya Kaskazini huko Arusha??? Au Katibu Mkuu na maafisa wake Dar Es Salaam??? Au Mwenyekiti wa Chama ambaye yuko kortini Kisutu kila siku???

Jibu la baadhi ya 'Marafiki wa BAVICHA Original' humu ndani ni kwamba viongozi wetu, hasa wa juu, ndio waliosababisha yote haya!!! Sio Msimamizi wa Uchaguzi aliyekimbia ofisi wakati anaotakiwa awepo ili kupokea fomu za uteuzi.

Sio Magufuli aliyejaza makada wa CCM walioshindwa uchaguzi uliopita kama Wakurugenzi wa Halmashauri na, kwa hiyo, kuwafanya wasimamizi wa uchaguzi.

Sio mapolisi waliotumwa kwenda kuwatawanya wagombea ambao fomu zao za uteuzi hazikupokelewa.

Wale waliopewa jukumu la kupokea fomu za uteuzi za wagombea wote na Sheria za nchi yetu; na Bosi wao aliyewakataza hadharani kutenda haki, hao hawana lawama.

Wahalifu halisi hawana makosa; waliofanyiwa uhalifu ndio wanaolaumiwa na hawa wanaojiita wanaCHADEMA au marafiki wa BAVICHA Original.

Halafu tukisema kuna watu wanamtumikia shetani kwa kuelewa au kutokujielewa, people take offence.

Halafu 'Marafiki' hawa wanaleta vihoja kwamba haya yanatokea kwa sababu ya Katibu Mkuu wa sasa; hayakuwa yanatokea wakati Dr. Slaa akiwa Katibu Mkuu, etc.

Wenye hoja za aina hii wanafikiria wanajua, ni werevu, wasomi, n.k. Ni wajinga wasiojua wasemalo.

Kabla hamjasema sana muwe mnawauliza akina Tony Komu na Joe Selasini na James Mbatia na wengineo ambao wameshiriki hizi vita tangu kabla ya kuingia mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Au sisi wengine, mimi mmojawapo, ambao tumeshiriki kwenye uchaguzi tangu mwaka '95. Haya ya sasa sio mapya sana.

Hii habari ya wasimamizi wa uchaguzi kukimbia ofisi zao ili wasipokee fomu za uteuzi za wagombea wa upinzani haikuanza Korogwe Vijijini. Ilikuwepo tangu mwaka '95 wakati wa Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi.

Wagombea wetu kuwekewa mapingamizi ya ajabu ajabu na kuenguliwa kiharamia na maCCM kupitishwa bila kupingwa haikuanza na Magufuli na watu wake. Ilianza Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais na Ben Mkapa mgombea Urais.

Wagombea wa CCM kutangazwa kwa nguvu haikuanza na Magufuli. Ilianza Mkapa akiwa Rais na baadae ikarithiwa na Kikwete na imepokelewa na Magufuli. Kumbukeni ya marehemu Shelembi wetu Shinyanga Mjini mwaka '10 na ya David Kafulila mwaka '95 wakati Rais akiwa Kikwete.

Kuna wakati maCCM, wakisaidiwa na mapolisi kama ilivyo sasa, walikuwa wanateka magari ya Tume yenye masanduku ya kura halali na kuyabadilisha na masanduku yenye kura haramu kwa lengo la kuwashindisha wagombea wa CCM.

Wagombea au wabunge wetu kujiuza kama malaya kwa maCCM haikuanza na akina Waitara na ole Kalanga. Tuliwahi kuwa na wabunge kama Makongoro Nyerere na Dr. Masumbuko Lamwai na Danhi Makanga na Daniel Nsanzugwanko huyu huyu wa CCM ya sasa. Nani anayewakumbuka tena???

Tuliwahi kuwa na wanamageuzi maarufu kama Prince Bagenda na Chief Abdallah Fundikira na wengineo wengi walioishia kujiuza CCM.

Licha ya haya yote, hatukuwahi kufikiria kuacha kushiriki kwenye chaguzi za marudio au Uchaguzi Mkuu.

Tulijua uchaguzi ni vita, na vitani kuna kushinda au kushindwa; kuna kufa au kujeruhiwa au kutekwa, na kuna kuua au kujeruhi au kuteka.

Hawa 'Marafiki' waliokuja jana na leo asubuhi wameshuhudia tukipigwa na Magufuli na watu wake wa CCM ya sasa na tayari wanatushauri tunyanyue mikono juu na kusalimu amri mbele ya watesi wetu.

Wanatushauri tususie chaguzi zijazo ili maCCM yapite bila kupingwa kwenye nafasi zote nchi nzima. Wanatumia maneno makali yenye kuonyesha wana msimamo mkali na ujasiri ambao hatujawahi kuona wakiuonyesha kwa vitendo mahali popote.

These are all Paper Tigers, chui wa makaratasi aliowasema Mwenyekiti Mao Zedong. Tukiwasikiliza imekula kwetu na maCCM watachekelea all the way to the bank.

Tufanyeje???

Niliizungumzia hii wiki iliyopita na sina haja ya kuirudia hapa. Tujielewe na tuelewe hali yetu ya sasa relative to hali ya jana na ya juzi.

Tunaelewa hali yetu ya sasa kwa sababu kila mmoja wetu anaona yanayotendeka. Hata hivyo, uelewa wetu wa sasa hautoshi kututabiria kesho yetu.

Ili tuelewe kesho yetu itakuwaje, ni lazima tuelewe jana na juzi yetu ilikuwaje. There's no telling the future without knowing the past and understanding the present.

Tusikubali ujasiri feki na ushauri wa sumu wa hawa wanaojiita 'Marafiki' zetu. Tusikubali kutengenezewa ugomvi wa bure baina yetu na viongozi wetu na hawa wanaojifanya wana uchungu na Chama.

Tusikubali kupotezewa focus kwa kuaminishwa kuwa adui ni Mbowe au Mashinji au Mnyika; wakati adui halisi ni yule aliyemuua Mawazo na kumpoteza Ben Saanane au kumjeruhi Tundu Lissu.

Tuelewe mazingira yetu, tujielewe sisi wenyewe na tuwe na nidhamu ndani na nje ya Chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tundu Lissu the righteousness, brought to this land by Almighty God to guide and teach his fellowmans.
His lips does present the word of God.
 
Mimi sishauri hata mara moja kususia uchaguzi 'under hooks and crooks'. Ni kubanana tu humo humo mpaka kieleweke.

Lakini nimesoma kwa umakini mkubwa taarifa iliyotolewa hapa ili kupata jibu, na sikuliona, wala hata kule kugusia tu sababu zinazofanya matukio yote hayo ya kukanyaga sheria waziwazi kabisa na udhalilishaji kufanywa, lakini wapinzani hawaoni haja ya kwenda mahakamani. Jambo hili silielewi kabisa. Je, kuna siri gani? Ucheleweshaji, au nini!
Je, kuna matatizo gani yanayowazuia kupeleka yote haya mahahakamani? Hata kama mnajua huko pia hakuna haki, lakini kuna shida gani kuyafikisha haya huko ili kuongeza uzito wa ushahidi wanaouona wananchi juu ya kuonewa kwenu? Hebu funua kidogo siri hii kama inawezekana ili tusiendelee kulaumu kwa kutojua.

Vita inakuwa ngumu zaidi unapopigana na adui wa nje anayesaidiwa na unayedhani ni mwezako uliyenae ndani. Vita ya namna hiyo huwezi ukaishinda hata siku moja. 'Malignant cancer' mara nyingi dawa ni kuondoa sehemu inayoliwa kwa haraka. Vinginevyo uhai wa vyama vyenu utapotea, hasa chini ya utawala huu uliojiapiza CCM kutawala milele.
 
Dawa ni kufanya maamuzi magumu.

Bila na wao kupata misukosuko, kamwe hawawezi kuja kwenye meza ya mazungumzo wala kuona umuhimu wa kutusikiliza(these people are callous and therefore they are enjoying what they are doing).

In short, this regime is worse and needs special treatment(they deserve similar treatment).

Taratibu. Soma na uelewe Tanzania na waTanzania ni watu wa namna gani kabla hujaenda huko. Hivi sasa huyo jamaa, mtesi wenu mkubwa hilo ndilo analolisubiri kwa hamu sana ili awamalize. Msimpe mwanya huo kirahisi hivyo. Kufika huko kunahitaji mikakati ambayo haipo kabisa sasa hivi. Kwa hiyo tuliza kichwa upate njia bora zaidi kuliko hiyo. Njia mbadala zipo.
 
Dawa ya ccm ni kutumia akili ya ziada kuliko ile wanayoifikiria wao.Nasema tena kiboko ya ccm ni Jacob meya wa ubungo awe katibu mkuu utaona mapambano yatakavyo kuwa
Bila katiba mpya na wananchi kuwa tayari kusimamia haki yao..hata kiongozi awe nani hakutakuwa na jipya...ukiniuliza safu sahihi ya uongozi,
Mkiti-Tundu lissu
Mmkiti-John Mnyika
Katibu mkuu-John Heche
Katibu msaidizi-Upendo Peneza
 
Hii tabia ya wasimamizi wa chaguzi zetu ktk ngazi za majimbo na kata kukimbia ofisi zao wakati wa mchakato wa urejeshaji fomu za wagombea hususani wa kutoka vyama vya upinzani yafaa kukomeshwa.
 
Naomba na mimi kuchangia mjadala huu kidogo. Na mapema kabisa niwaombe radhi wote nitakaowakwaza, kwa sababu nafikiri nitakachosema kitawakwaza wengi humu.

Nimefuatilia mjadala wa yaliyojiri Korogwe Vijijini na nikiri nimeshuhudia utoto wa kisiasa wa kutisha na kusikitisha sana. Nimeona kile ambacho Lenin alikiita 'an infantile disorder' miaka mia moja iliyopita. Naomba kufafanua.

Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake zinaelekeza kwamba mgombea anatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kabla ya saa kumi ya siku moja kabla ya siku ya uteuzi.

Sheria inasema fomu za uteuzi zitakabidhiwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo. Maadili ya Uchaguzi yameelekeza wazi kwamba Msimamizi wa Uchaguzi anatakiwa awepo ofisini kwake wakati wote anaotakiwa ili kupokea fomu za uteuzi za wagombea.

Kwa hiyo, kitu cha kwanza cha kujiuliza ni je, mgombea wetu alipeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati uliowekwa kisheria au hakufanya hivyo???

Kama alifanya hivyo, je, kwa nini fomu zake hazikupokelewa??? Kama hakufanya hivyo ni kwa nini na lawama iangukie wapi???

Baada ya kupata jibu la swali la kwanza, swali la pili ni je, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo alikuwepo ofisini kwake kwa wakati wote aliotakiwa kuwepo ili kupokea fomu za uteuzi za wagombea???

Kama alikuwepo je, alipokea fomu za uteuzi za wagombea kama inavyotakiwa na Sheria??? Kama hakuwepo, je, ni kwa nini na lawama iangukie wapi???

Kwa ninayoyasoma mitandaoni, mgombea wetu alipeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati muafaka. Na wala hakuwa peke yake, walikuwepo wagombea wa CCM na ACT-Wazalendo.

Kwa ninayoyasoma mitandaoni, wagombea walipofika ofisini kwa Msimamizi wa Uchaguzi wakakuta hayupo ofisini kwake wakati aliotakiwa kuwepo. Inasemekana alikuwa ameitwa kwa Mkuu wa Wilaya.

Fomu za mgombea wetu na wa ACT-Wazalendo hazikupokelewa lakini, somehow, fomu za mgombea wa CCM zikabandikwa ukutani na mara akatangazwa kuwa amepita bila kupingwa!!!!

Je, aliyekosea hapa ni nani??? Je, ni mgombea aliyepeleka fomu zake za uteuzi kwa wakati??? Je, ni Katibu wa Wilaya ya Korogwe Vijijini au wa Mkoa wa Tanga??? Au Katibu wa Kanda ya Kaskazini huko Arusha??? Au Katibu Mkuu na maafisa wake Dar Es Salaam??? Au Mwenyekiti wa Chama ambaye yuko kortini Kisutu kila siku???

Jibu la baadhi ya 'Marafiki wa BAVICHA Original' humu ndani ni kwamba viongozi wetu, hasa wa juu, ndio waliosababisha yote haya!!! Sio Msimamizi wa Uchaguzi aliyekimbia ofisi wakati anaotakiwa awepo ili kupokea fomu za uteuzi.

Sio Magufuli aliyejaza makada wa CCM walioshindwa uchaguzi uliopita kama Wakurugenzi wa Halmashauri na, kwa hiyo, kuwafanya wasimamizi wa uchaguzi.

Sio mapolisi waliotumwa kwenda kuwatawanya wagombea ambao fomu zao za uteuzi hazikupokelewa.

Wale waliopewa jukumu la kupokea fomu za uteuzi za wagombea wote na Sheria za nchi yetu; na Bosi wao aliyewakataza hadharani kutenda haki, hao hawana lawama.

Wahalifu halisi hawana makosa; waliofanyiwa uhalifu ndio wanaolaumiwa na hawa wanaojiita wanaCHADEMA au marafiki wa BAVICHA Original.

Halafu tukisema kuna watu wanamtumikia shetani kwa kuelewa au kutokujielewa, people take offence.

Halafu 'Marafiki' hawa wanaleta vihoja kwamba haya yanatokea kwa sababu ya Katibu Mkuu wa sasa; hayakuwa yanatokea wakati Dr. Slaa akiwa Katibu Mkuu, etc.

Wenye hoja za aina hii wanafikiria wanajua, ni werevu, wasomi, n.k. Ni wajinga wasiojua wasemalo.

Kabla hamjasema sana muwe mnawauliza akina Tony Komu na Joe Selasini na James Mbatia na wengineo ambao wameshiriki hizi vita tangu kabla ya kuingia mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Au sisi wengine, mimi mmojawapo, ambao tumeshiriki kwenye uchaguzi tangu mwaka '95. Haya ya sasa sio mapya sana.

Hii habari ya wasimamizi wa uchaguzi kukimbia ofisi zao ili wasipokee fomu za uteuzi za wagombea wa upinzani haikuanza Korogwe Vijijini. Ilikuwepo tangu mwaka '95 wakati wa Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi.

Wagombea wetu kuwekewa mapingamizi ya ajabu ajabu na kuenguliwa kiharamia na maCCM kupitishwa bila kupingwa haikuanza na Magufuli na watu wake. Ilianza Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais na Ben Mkapa mgombea Urais.

Wagombea wa CCM kutangazwa kwa nguvu haikuanza na Magufuli. Ilianza Mkapa akiwa Rais na baadae ikarithiwa na Kikwete na imepokelewa na Magufuli. Kumbukeni ya marehemu Shelembi wetu Shinyanga Mjini mwaka '10 na ya David Kafulila mwaka '95 wakati Rais akiwa Kikwete.

Kuna wakati maCCM, wakisaidiwa na mapolisi kama ilivyo sasa, walikuwa wanateka magari ya Tume yenye masanduku ya kura halali na kuyabadilisha na masanduku yenye kura haramu kwa lengo la kuwashindisha wagombea wa CCM.

Wagombea au wabunge wetu kujiuza kama malaya kwa maCCM haikuanza na akina Waitara na ole Kalanga. Tuliwahi kuwa na wabunge kama Makongoro Nyerere na Dr. Masumbuko Lamwai na Danhi Makanga na Daniel Nsanzugwanko huyu huyu wa CCM ya sasa. Nani anayewakumbuka tena???

Tuliwahi kuwa na wanamageuzi maarufu kama Prince Bagenda na Chief Abdallah Fundikira na wengineo wengi walioishia kujiuza CCM.

Licha ya haya yote, hatukuwahi kufikiria kuacha kushiriki kwenye chaguzi za marudio au Uchaguzi Mkuu.

Tulijua uchaguzi ni vita, na vitani kuna kushinda au kushindwa; kuna kufa au kujeruhiwa au kutekwa, na kuna kuua au kujeruhi au kuteka.

Hawa 'Marafiki' waliokuja jana na leo asubuhi wameshuhudia tukipigwa na Magufuli na watu wake wa CCM ya sasa na tayari wanatushauri tunyanyue mikono juu na kusalimu amri mbele ya watesi wetu.

Wanatushauri tususie chaguzi zijazo ili maCCM yapite bila kupingwa kwenye nafasi zote nchi nzima. Wanatumia maneno makali yenye kuonyesha wana msimamo mkali na ujasiri ambao hatujawahi kuona wakiuonyesha kwa vitendo mahali popote.

These are all Paper Tigers, chui wa makaratasi aliowasema Mwenyekiti Mao Zedong. Tukiwasikiliza imekula kwetu na maCCM watachekelea all the way to the bank.

Tufanyeje???

Niliizungumzia hii wiki iliyopita na sina haja ya kuirudia hapa. Tujielewe na tuelewe hali yetu ya sasa relative to hali ya jana na ya juzi.

Tunaelewa hali yetu ya sasa kwa sababu kila mmoja wetu anaona yanayotendeka. Hata hivyo, uelewa wetu wa sasa hautoshi kututabiria kesho yetu.

Ili tuelewe kesho yetu itakuwaje, ni lazima tuelewe jana na juzi yetu ilikuwaje. There's no telling the future without knowing the past and understanding the present.

Tusikubali ujasiri feki na ushauri wa sumu wa hawa wanaojiita 'Marafiki' zetu. Tusikubali kutengenezewa ugomvi wa bure baina yetu na viongozi wetu na hawa wanaojifanya wana uchungu na Chama.

Tusikubali kupotezewa focus kwa kuaminishwa kuwa adui ni Mbowe au Mashinji au Mnyika; wakati adui halisi ni yule aliyemuua Mawazo na kumpoteza Ben Saanane au kumjeruhi Tundu Lissu.

Tuelewe mazingira yetu, tujielewe sisi wenyewe na tuwe na nidhamu ndani na nje ya Chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmmmmh
 
Mimi sishauri hata mara moja kususia uchaguzi 'under hooks and crooks'. Ni kubanana tu humo humo mpaka kieleweke.

Lakini nimesoma kwa umakini mkubwa taarifa iliyotolewa hapa ili kupata jibu, na sikuliona, wala hata kule kugusia tu sababu zinazofanya matukio yote hayo ya kukanyaga sheria waziwazi kabisa na udhalilishaji kufanywa, lakini wapinzani hawaoni haja ya kwenda mahakamani. Jambo hili silielewi kabisa. Je, kuna siri gani? Ucheleweshaji, au nini!
Je, kuna matatizo gani yanayowazuia kupeleka yote haya mahahakamani? Hata kama mnajua huko pia hakuna haki, lakini kuna shida gani kuyafikisha haya huko ili kuongeza uzito wa ushahidi wanaouona wananchi juu ya kuonewa kwenu? Hebu funua kidogo siri hii kama inawezekana ili tusiendelee kulaumu kwa kutojua.

Vita inakuwa ngumu zaidi unapopigana na adui wa nje anayesaidiwa na unayedhani ni mwezako uliyenae ndani. Vita ya namna hiyo huwezi ukaishinda hata siku moja. 'Malignant cancer' mara nyingi dawa ni kuondoa sehemu inayoliwa kwa haraka. Vinginevyo uhai wa vyama vyenu utapotea, hasa chini ya utawala huu uliojiapiza CCM kutawala milele.
Tundu Lisu na Mbowe ni CCM original...Wako na mkakati wa kuhakikisha wanaiua Chadema
 
Dawa ni kufanya maamuzi magumu.

Bila na wao kupata misukosuko, kamwe hawawezi kuja kwenye meza ya mazungumzo wala kuona umuhimu wa kutusikiliza(these people are callous and therefore they are enjoying what they are doing).

In short, this regime is worse and needs special treatment(they deserve similar treatment).
Keyboard warrior..
..hakuna wa kumchuuza leo aache familia yake yatima akauawe na polisi eti kwa kuamini yuko hatarini.Hizi wishes zenu za kishetani will never come to pass.hakuna misukosuko popote kwenye Tanzania yetu na wewe na wenzio mkianzisha 'misukosuko' you wont take time before you're made extinct!
Tusitishane na kuharibiana amani hapa eti kwasababu kuna watu wamelewa siasa!!!
 
Mwanasheria wa CHADEMA na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu, aliye kwenye matibabu nchini Ubelgiji, akiongea na Mwananchi, amewakoromea kwa mara nyingine Viongozi na wanachama wa CHADEMA wanaotaka kujitoa kwenye Uchaguzi wa Marudio.

Lissu alisema kuwa, "Tulijua Uchaguzi ni vita na vitani kuna kushinda ama kushindwa; kuna kufa ama kujeruhiwa au kutekwa na kuna kuua au kujeruhi au kuteka." Lissu aliongeza kuwa, "Marafiki waliokuja jana na leo asubuhi, wameshuhudia wakipigwa na sasa tayari wanatushauri tunyanyue mikono juu na kusalimu amri mbele ya watesi wetu." Wanatushauri tususie chaguzi zijazo ila CCM ipite bila kupingwa kwenye nafasi zote Nchi nzima."

Aidha, Lissu Alidai kuwa, (marafiki) ... "Wanatumia maneno makali yenye kuonyesha wana msimamo mkali na ujasiri ambao hatujawahi kuona wakiuonyesha kwa vitendo mahali popote."

Tamko hilo la Lissu limekuja wakati Makamu Mwenyekiti, Prof. Safari akiwa amekishauri CHADEMA kususia chaguzi zote nchini ikiwa ni njia mojawapo ya kudai Tume huru ya Uchaguzi. Hata hivyo, Lissu alikana kuwa tamko lake lilimlenga Prof. Safari kwa kuwa alikuwa hajamsikia.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alifafanua kuwa, CHADEMA inashiriki kwenye Uchaguzi kutokana na wengi kutaka hivyo. "Wapo wanachama wanaodai ukimsusia asiyejali demokrasia kwake ni kicheko."

IMG_6706.JPG
 
72 Reactions
Reply
Back
Top Bottom