Tundu Lissu on KLH News Exclusive!

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Baada ya kama saa moja hivi (sawa na saa tisa EST), saa nane CST karibu sawa na saa nne EAT mwanasheria na mwanaharakati wa mazingira Bw. Tundu Lissu atakuwa nami moja kwa moja toka jijini Dar tukizungumzia mambo mbalimbali. Bw. Lissu ndiye ambaye ameuchambua Mkataba wa Buzwagi kimahiri na kuonesha ni jinsi gani una mapungufu na ni kwanini haujaweka maslahi ya Taifa mbele. Wiki ijayo tutajitahidi kupata msemaji wa serikali kuweza kuzungumza nasi kwani majaribio yote ya kufanya hivyo leo yamekuwa magumu.

Matangazo hayo yatarushwa moja kwa moja kupitia http://www.bongoradio.com

Hakikisha ukiingia kwenye bongoradio, chagua player yako lakini tumia "low" setting ili kuwezesha wasikilizaji wengi kuweza kusikia bila matatizo yoyote. Kama tayari ulikuwa unasikiliza basi kata na fungua tena katika "low".

M. M.
 
Baada ya kama saa moja hivi (sawa na saa tisa EST), saa nane CST karibu sawa na saa nne EAT mwanasheria na mwanaharakati wa mazingira Bw. Tundu Lissu atakuwa nami moja kwa moja toka jijini Dar tukizungumzia mambo mbalimbali. Bw. Lissu ndiye ambaye ameuchambua Mkataba wa Buzwagi kimahiri na kuonesha ni jinsi gani una mapungufu na ni kwanini haujaweka maslahi ya Taifa mbele. Wiki ijayo tutajitahidi kupata msemaji wa serikali kuweza kuzungumza nasi kwani majaribio yote ya kufanya hivyo leo yamekuwa magumu.

Matangazo hayo yatarushwa moja kwa moja kupitia http://www.bongoradio.com

Hakikisha ukiingia kwenye bongoradio, chagua player yako lakini tumia "low" setting ili kuwezesha wasikilizaji wengi kuweza kusikia bila matatizo yoyote. Kama tayari ulikuwa unasikiliza basi kata na fungua tena katika "low".

M. M.


Mwanakijiji,

Huyu jamaa kwasasa pia si ni kiongozi wa CHADEMA? Ingebidi utaje vyeo vyake vyote kwenye introduction yako hasa anapozungumzia suala la kisiasa.
 
Huyu jamaa kwasasa pia si ni kiongozi wa CHADEMA? Ingebidi utaje vyeo vyake vyote.

Whaaaat? Kumbe ni kiongozi wa Chadema, sio mwanasheria wa uharakati? ebo! Mkuu MMJ, mtafute na Mgasi tuone upande wa pili wa shillingi mkuu!
 
Jamani, Tundu Lissu ni mwanasheria mahiri na mwanaharakati wa mazingira, amekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wanyonge, hasa wachimba madini wadogo wadogo, na mtetezi wa maslahi ya umma kwenye sekta ya madini. anasemekana ana ujuzi mkubwa wa masuala ya mikataba na mambo ya kisheria.
 
Mwanakijiji,

Nina uhakika unajua wazi kwamba Tundu Lisu ni mkurugenzi wa sheria, haki na katiba wa CHADEMA. Ni haki kuelezea vyeo vyake vyote ili kuwapa wananchi nafasi ya kumuelewa kabla ya kuanza kujadili uchambuzi wake.
http://www.chadema.net/uongozi/sekreta.php

Hata mimi ambaye uandishi uko mbali sana najua hiyo ni requirement moja hasa pale suala analojadili lina uhusiano na hicho cheo chake ambacho umekificha.

Pamoja na kutokuwa na wasiwasi na integrity ya Tindu Lisu na kuheshimimu mchango wake huko nyuma hasa kwenye suala la wananchi wanaodhaniwa kufukiwa kwenye mashimo ya madini Mwanza, lakini ni vizuri kujua katika hili suala anazungumza kama nani.

Mwanakijiji, unatisha, sioni kama una tofauti na akina Rweyemamu.
Sikutegemea hata siku moja niliseme hili Mwanakijiji juu yako kwani kuna michango yako asilimia kama 80 ninaiheshimu sana.

Lakini haya mambo ya kuficha ukweli makusudi, ni uwongo ambao ukiachiwa utaendelea kukua siku hadi siku.
 
Jamani, Tundu Lissu ni mwanasheria mahiri na mwanaharakati wa mazingira, amekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wanyonge, hasa wachimba madini wadogo wadogo, na mtetezi wa maslahi ya umma kwenye sekta ya madini. anasemekana ana ujuzi mkubwa wa masuala ya mikataba na mambo ya kisheria.

Mkuu,

Nalijua hilo lakini hata hili hapa chini nalo ni sahihi:

Mkurugenzi Sheria, Katiba na Haki
Tundu Lissu (38)
Kutoka Singida
lissu@chadema.net
 
MKJJ
Tunakusikia wewe, Tundu Lisu hatumsikii, sijui vipi....au ni computer yangu ndio mbovu, sauti yake inasikika kwa mbaaali sana
 
Ni kweli MKJJ kuwa "Haogopwi" wala "kupendwa" mtu katika kuchambua issues hapo KLH,lakini pia nafikiri ni Busara na Haki kutaja vyeo vyote vya Bwana Tundu Lissu wakati wa kumtambulisha KLH.Kutokufanya hivyo kunazua maswali mengi!.Kwa mtazamo wangu jambo hilo alozua Mtanzania si siri?sasa kwa nini hutaki kumtambulisha kwa cheo chake!.MKJJ naomba uangalie hayo matangazo,kwani Tundu anasikika kwa mbali mno!!
 
MKJJ

Muulize pia kabla hujamalizia mazungumzo yako kuwa, atueleze Nafasi yake yeye Tundu Lissu ni ipi ktk CHADEMA
 
MKJJ muulize Ndg Tundu Lissu.Je? watachukua hatua gani kisheria kama serikali itaendelea kupuuza shutuma dhidi ya watendaji wake waandamizi?
 
Mwanakijiji,

Nina uhakika unajua wazi kwamba Tundu Lisu ni mkurugenzi wa sheria, haki na katiba wa CHADEMA. Ni haki kuelezea vyeo vyake vyote ili kuwapa wananchi nafasi ya kumuelewa kabla ya kuanza kujadili uchambuzi wake.
http://www.chadema.net/uongozi/sekreta.php

Hata mimi ambaye uandishi uko mbali sana najua hiyo ni requirement moja hasa pale suala analojadili lina uhusiano na hicho cheo chake ambacho umekificha.

Pamoja na kutokuwa na wasiwasi na integrity ya Tindu Lisu na kuheshimimu mchango wake huko nyuma hasa kwenye suala la wananchi wanaodhaniwa kufukiwa kwenye mashimo ya madini Mwanza, lakini ni vizuri kujua katika hili suala anazungumza kama nani.

Mwanakijiji, unatisha, sioni kama una tofauti na akina Rweyemamu.
Sikutegemea hata siku moja niliseme hili Mwanakijiji juu yako kwani kuna michango yako asilimia kama 80 ninaiheshimu sana.

Lakini haya mambo ya kuficha ukweli makusudi, ni uwongo ambao ukiachiwa utaendelea kukua siku hadi siku.


We Mtanzania,

Mbona unaweweseka?

Watu wenye vyeo vingi hutambulishwa vyeo kutokana na mazingira. Haiwezekani Lissu akazungumza kama Mwanasheria wa LEAT ukataka atambulishwe kama Mkurugenzi wa CHADEMA.

Lissu hajifichi. Nimesoma kwenye vyombo vya habari, kwenye mambo ya chama chake hujitambulisha kama CHADEMA. Kwenye harakati zake hujitambulisha kama Mwanasheria.

Ni kama Baregu, wakati mwingine huzungumza kama Profesa wa Chuo Kikuu na wakati mwingine kama Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA.

Mbona hamuulizi Karamagi akihojiwa kama Waziri kwamba kwa nini asijitambulishe pia kama mmiliki wa Makampuni yake ya kifedhuli?

Kila kitu na mahali pake. Inategemea yeye na mwanakijiji walikubaliana anahojiwa kama nani.

Kama maneno yake yamekuchoma meza nyembe...halo halo halo.

Mtajiju mwaka huu

Asha
 
We Mtanzania,

Mbona unaweweseka?

Watu wenye vyeo vingi hutambulishwa vyeo kutokana na mazingira. Haiwezekani Lissu akazungumza kama Mwanasheria wa LEAT ukataka atambulishwe kama Mkurugenzi wa CHADEMA.

Lissu hajifichi. Nimesoma kwenye vyombo vya habari, kwenye mambo ya chama chake hujitambulisha kama CHADEMA. Kwenye harakati zake hujitambulisha kama Mwanasheria.

Ni kama Baregu, wakati mwingine huzungumza kama Profesa wa Chuo Kikuu na wakati mwingine kama Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA.

Mbona hamuulizi Karamagi akihojiwa kama Waziri kwamba kwa nini asijitambulishe pia kama mmiliki wa Makampuni yake ya kifedhuli?

Kila kitu na mahali pake. Inategemea yeye na mwanakijiji walikubaliana anahojiwa kama nani.

Kama maneno yake yamekuchoma meza nyembe...halo halo halo.

Mtajiju mwaka huu

Asha


Asha,

Suala la mkataba ni la kisiasa na limeibuliwa na vyama vya siasa. Kwahiyo nafasi ya Lisu kwenye siasa ni muhimu mno kwenye hili suala kuliko hata hicho cheo cha mazingira.
 
Excellent MKJJ kwa swali la utambulisho........na pia nimependa jibu

ya kwamba ni HOJA ndio ya kuangaliwa na sio mtu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom