Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 322
- 645
MH TUNDU NI MUONGO AU ANA ALZHEIMER'S?
Na Elius Ndabila
Alzheimer's ni moja ya visababishi au dalili ya mtu kuwa na ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu *(DEMENSHIA)*. Kwa kawaida ugonjwa wa DEMENSHIA kisayansi huwapata zaidi watu wenye umri wa kuanzia miaka 65, ijapo hata chini ya umri huo mtu anaweza kuwa nao. Ugonjwa huu hautibiki, ila dalili zake yaani *ALZHEIMER'S* hutibika.
Nilishawahi kuandika kuwa kwa namna Tundu alivyokuwa amejuruhiwa na Mungu kumunusuru kuwa hai hadi sasa alipaswa apate muda zaidi wa kupumzika kutibu afya yake kikamilifu kuliko kugombea Urais. Nilisema afya ya Tundu ni muhimu kuliko nafasi ya Urais anayoitafuta ilihali anajua na chama chake kinajua kuwa hawezi kupata.
Kuonyesha kuwa afya ya Mh Tundu haijatengamaa akiwa Katavi aliudanganya umma kuwa Katavi walidanganya kuwa kutakuwa na safari ya treni ya Dar -katavi. Akasema CCM waliwadanga hii haiwezekani. Alisema treni haiwezi kuja Katavi kwa kuwa hata reli haijakarabatiwa.
Wakati Tundu akisema hivyo, ukweli wa mambo ni kuwa Katavi kuna safari ya treni ambayo husafiri zaidi ya mara tatu.
Maneno ya Tundu kuwa hakuna safari ya treni Katavi yaliendelea ku-cement hoja yangu kuwa Tundu anatakiwa kupata muda mrefu wa mapumziko kuliko kuhangaika na Urais.
Wakati Watanzania hatujasahau kauli yake ya Katavi, jana akiwa Bunda amesema kuwa Mgombea wa CCM ambaye pia ni Rais wa JMT amewaita Wakurugenzi wa halmashauri nchi nzima kwenda Dodoma. Nilisikitika kusikia kauli hiyo kwa kuwa wakati anasema kauli hiyo mimi nilikuwa mahali nimekaa na Mkurugenzi wa halmashauri moja hapa nchini. Huu nao ulikuwa mwendelezo wa uongo na leo Wizara ya TAMISEM imejibu na CCM imejibu kupitia kwa msemaji wake Humprey Polepole. Maneno haya kutoka kinywani kwa Tundu mimi yananishangaza kwa kuwa tangu nianze kufuatilia siasa za Tundu nilikuwa ninajua ni mtu wa facts, sikuwahi kufikiria kuwa naye ni muongo. Mpaka sasa ninaandika sijui kama Tundu ni *Muongo au ALZHEIMER'S*? Ninaamini wasomaji mtanipa jibu sahihi kuwa Tundu ni Muongo au ana ALZHEIMER'S?
Binafsi ninaendelea kushauri kuwa Tundu anahitaji kuendelea kupata matibabu, kwani mikiki mikiki hii ya Kampeni inaweza kumfanya kupata matatizo ikiwepo tatizo la kupoteza kumbukumbu() na kumfanya kuwa mropokaji kwa kuwa anakuwa hakumbuki.
Afya yake ni mhimu kuliko nafasi anayoitafuta ambayo hata hivyo hawezi kuipata. Kuendelea na hili tatizo linaweza kumfanya kuwa sugu na ikawa shida kulitibu
Na Elius Ndabila
Alzheimer's ni moja ya visababishi au dalili ya mtu kuwa na ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu *(DEMENSHIA)*. Kwa kawaida ugonjwa wa DEMENSHIA kisayansi huwapata zaidi watu wenye umri wa kuanzia miaka 65, ijapo hata chini ya umri huo mtu anaweza kuwa nao. Ugonjwa huu hautibiki, ila dalili zake yaani *ALZHEIMER'S* hutibika.
Nilishawahi kuandika kuwa kwa namna Tundu alivyokuwa amejuruhiwa na Mungu kumunusuru kuwa hai hadi sasa alipaswa apate muda zaidi wa kupumzika kutibu afya yake kikamilifu kuliko kugombea Urais. Nilisema afya ya Tundu ni muhimu kuliko nafasi ya Urais anayoitafuta ilihali anajua na chama chake kinajua kuwa hawezi kupata.
Kuonyesha kuwa afya ya Mh Tundu haijatengamaa akiwa Katavi aliudanganya umma kuwa Katavi walidanganya kuwa kutakuwa na safari ya treni ya Dar -katavi. Akasema CCM waliwadanga hii haiwezekani. Alisema treni haiwezi kuja Katavi kwa kuwa hata reli haijakarabatiwa.
Wakati Tundu akisema hivyo, ukweli wa mambo ni kuwa Katavi kuna safari ya treni ambayo husafiri zaidi ya mara tatu.
Maneno ya Tundu kuwa hakuna safari ya treni Katavi yaliendelea ku-cement hoja yangu kuwa Tundu anatakiwa kupata muda mrefu wa mapumziko kuliko kuhangaika na Urais.
Wakati Watanzania hatujasahau kauli yake ya Katavi, jana akiwa Bunda amesema kuwa Mgombea wa CCM ambaye pia ni Rais wa JMT amewaita Wakurugenzi wa halmashauri nchi nzima kwenda Dodoma. Nilisikitika kusikia kauli hiyo kwa kuwa wakati anasema kauli hiyo mimi nilikuwa mahali nimekaa na Mkurugenzi wa halmashauri moja hapa nchini. Huu nao ulikuwa mwendelezo wa uongo na leo Wizara ya TAMISEM imejibu na CCM imejibu kupitia kwa msemaji wake Humprey Polepole. Maneno haya kutoka kinywani kwa Tundu mimi yananishangaza kwa kuwa tangu nianze kufuatilia siasa za Tundu nilikuwa ninajua ni mtu wa facts, sikuwahi kufikiria kuwa naye ni muongo. Mpaka sasa ninaandika sijui kama Tundu ni *Muongo au ALZHEIMER'S*? Ninaamini wasomaji mtanipa jibu sahihi kuwa Tundu ni Muongo au ana ALZHEIMER'S?
Binafsi ninaendelea kushauri kuwa Tundu anahitaji kuendelea kupata matibabu, kwani mikiki mikiki hii ya Kampeni inaweza kumfanya kupata matatizo ikiwepo tatizo la kupoteza kumbukumbu() na kumfanya kuwa mropokaji kwa kuwa anakuwa hakumbuki.
Afya yake ni mhimu kuliko nafasi anayoitafuta ambayo hata hivyo hawezi kuipata. Kuendelea na hili tatizo linaweza kumfanya kuwa sugu na ikawa shida kulitibu