Mdaiwa-Sugu
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 284
- 910
Japokuwa sikubaliani na Tundu kwa vitu vingi lakini kitendo cha kushambuliwa kwake kilinisononesha sana
Shambulio lake halikuwa la kibinadamu- ulikuwa ni unyama tena unyama uliopitiliza.
Ingawa_pamoja na madhira yote hayo. Tundu ameendelea kuwa jasiri-haonyeshi hali ya kukata tamaa, majonzi wala masononeko. Sura yake imejawa na tabasamu muda wote. Hadi najiuliza:
Waliomshambulia
Wanajisikiaje kumwona akiwa ni mwenye kujawa na uso wa furaha?
Wanajisikiaje kumwona akiwa hai?
Waliwaza nini juu ya familia yake ambayo angeiacha?
Ungekuwa wewe ungejisikiaje endapo ni ndugu yako anapigwa risasi zote zile?
Wanajisikiaje kumwona akiwa anatembea kwa kuchechemea mguu mmoja huku wao wakitembea kwa miguu miwili?
Ndugu Watanzania wenzangu, tujitahidi kutenda kadri ya inavyompendeza Mungu ipo siku tutahukumiwa sawa sawa na matendo yetu.
Shambulio lake halikuwa la kibinadamu- ulikuwa ni unyama tena unyama uliopitiliza.
Ingawa_pamoja na madhira yote hayo. Tundu ameendelea kuwa jasiri-haonyeshi hali ya kukata tamaa, majonzi wala masononeko. Sura yake imejawa na tabasamu muda wote. Hadi najiuliza:
Waliomshambulia
Wanajisikiaje kumwona akiwa ni mwenye kujawa na uso wa furaha?
Wanajisikiaje kumwona akiwa hai?
Waliwaza nini juu ya familia yake ambayo angeiacha?
Ungekuwa wewe ungejisikiaje endapo ni ndugu yako anapigwa risasi zote zile?
Wanajisikiaje kumwona akiwa anatembea kwa kuchechemea mguu mmoja huku wao wakitembea kwa miguu miwili?
Ndugu Watanzania wenzangu, tujitahidi kutenda kadri ya inavyompendeza Mungu ipo siku tutahukumiwa sawa sawa na matendo yetu.