Tundu Lissu na Zitto Kabwe ni wanasiasa wa upinzani waliojitoa na wanaojituma sana na kwa hakika wanabeba sana upinzani kwa sasa

Nimefanya tathimini yangu kwa muda sasa na nimeona kuwa Tundu Lissu na Zitto Kabwe ndio wanasiasa wawili wanaojituma sana kuikabili hii serikali Bungeni,nje ya Bunge na kupitia mitandao kuliko wanasiasa wengine wote wa upinzani hasa katika kupambana na kufanya siasa nje ya Bunge.

Wanasiasa wengi wa upnzani hujituma zaidi ndani ya Bunge katika kuikosoa na kuishauri serikali na Bunge likiishi basi huwasikii tena na hata mitandaoni sio active kama walivyo Zitto na Lissu na hili ni tatizo ambalo wapnzani inawezekana hawalioni.

Ni Zitto na Lissu ndio ambao mara kwa mara wataandika makala ndefu mitandaoni wakati wanasiasa wenzao huishia tu kuandika tweets fupi fupi(baadhi ni wavivu hata kutumia mitandao) lakini sio kuandika makala ndefu na zenye uchambuzi wa kina za ama kukosoa au kushauri hii serikali.

Yaani Lissu alie mgonjwa na aliyoko nje ya nchi ndio wakati mwingine hutumia muda wake kuandika makala mbalimbali mitandaoni ila hawa wazima wa humu nchini wao wakijitahidi sana ni kuandika tweets fupi fupi tu basi!!

Na ukiacha Lissu ambae ni amekuwa mgonjwa,Zitto kwa sasa ndio naweza kusema ni mwanasiasa wa upinzani anaejituma sana kutumia mitandao kuikosoa hii serikali na hii ni moja ya sababu ya Zitto kwa sasa kuonekana ni mwiba kwa hii serikali kama alivyo Lissu.

MfanO,hivi sasa hata ukiingia katika account yake ya twitte, utakuta teyari ameshafanya uchambuzi(kama alivyowahi kufanya kupitia hapa JF) na kuonyesha mapungufu ya makubaliano baina ya serikali na Barrick, jambo ambalo hata wanasiasa wengine wa upinzani wanapaswa kulifanya ili kukabiliana na propaganda za sasa kuwaaminisha watanzani kuwa makubaliano yaliyofikiwa ni ushinda kwa JPM na Taifa kumbe ndani yake kumejaa mapungufu kibao tena ya kusikitisha.

Naelewa wanasiasa wengine wa upinzani watahoji na kukosoa makubaliano haya kati ya serikali na kampuni ya Barrick lakini wengi watafanya hivyo zaidi ndani ya Bunge na Bunge likiisha ndio basi huwasikii tena japo kuna wachache nao hupenda ku-tweets mara moja moja ila sio kuandika makala ndefu mitandaoni mfano facebook,Instagram na hata hapa JF.

Kwakweli Zitto na Tundu Lissu wanajituma sana katika kutumia mitandao kukosoa na kushauri serikali kama wanavyofanya ndani ya Bunge na kwa hakika kwa sasa wanasiasa hawa wawili ndio wanabeba upinzani nje ya Bunge na CCM kwa kulijua hili, ndio maana wameanzisha propaganda za kutaka kuwavuruga/kuwachonganisha na zaidi kutaka Zitto asiaminike na upinzani kwa ujumla kwa kutuletea habari za zilipendwa kuhusu Zitto.

Hongereni sana Zitto na Lissu mnafanya kazi kubwa sana kubebea upinzani na kuwafanya watanzani waelewe ni nin kinaendelea awamu hii ambacho pengine bila nyinyi na wapinzani wenzenu tusingeyajua, mfano kukamatwa kwa ndege yetu huko Canada wakati ule,utata kuhusu matumizi ya shlingi trilioni 1.5 na mengine mengi.

Bahati mbaya sana, upinzani kwa sasa mnapata support ndogo sana ya media na isingekua mitandao ya kijamii,basi mengi tusingeyajua au tungeyajua juu juu tu.
Umemsahau Mbowe!
 
Too low for you Salary slip. Your are not of this caliber when it comes to the analysis of political dynamics. How can you trust Zito so easily just because of the tweets? Has Zito's ability increased more than when he used to be a Chadema party member? Think twice unless you are not a hardcore Chadema member.
Huu ndio udhaifu tulinao sisi wapinzani.Hivi,ukiacha Lissu,kwa sasa kuna mwanasiasa mwingine anaeumbua huu utawala kama Zitto?

Sio tweets tu,Zitto ameandika makala nyingi tu hapa JF,facebook na kwenye mitandao mingine makala zinazosumbua watawala hivyo sisi hii kwetu ni fursa na si kukariri tu kuwa Zitto haaminiki na hata akibadilika teyari ameshasababisha damage kubwa tu kwa CCM.

Wanasiasa kubadilika, hasa wa hapa kwetu, ni jambo la kawaida japo linaboa ila lisitufunge kiasi hicho.

Hamuoni jInsi CCM hii navyotumia wapinzani hata wale ilikuwa ikiwaona ni hatari kuliko ukoma kujinufaisha kisiasa bila kujali historia zao?

Lowassa na Dr.Slaa leo CCM haiwatumii kwa faida yao?

Hamuoni hata Musiba alivyogeukwa leo hii?

Msishangae hata Kinana,Mzee Makamba na Membe kushikana mikono na Magu kabla ya 2020 ingawa leo hii mtu kama Membe anaonekana/anatajwa kuwa karibu na wapinzani.

Sisi ni wepesi kugombanishwa/kufanywa kutoaminiana wakati wenzetu ni wepesi wa kubadili gia angani mradi tu wameona kuna fursa ya kisiasa bila kujali ya jana yalikuwaje na wanajua sana kutengeneza propaganda hata za kubadili fikra za watu ambao ni wepesi kudanganyika.

Msifikiri CCM wanapenda kuona CHADEMA wanashirikiana na Zitto, bali wanapenda zaidi kuona kinyume chake.
 
Huu ndio udhaifu tulinao sisi wapinzani.Hivi,ukiacha Lissu,kwa sasa kuna mwanasiasa mwingine anaeumbua huu utawala kama Zitto?

Sio tweets tu,Zitto ameandika makala nyingi tu hapa JF,facebook na kwenye mitandao mingine makala zinazosumbua watawala hivyo sisi hii kwetu ni fursa na si kukariri tu kuwa Zitto haaminiki na hata akibadilika teyari ameshasababisha damage kubwa tu kwa CCM.

Wanasiasa kubadilika, hasa wa hapa kwetu, ni jambo la kawaida japo linaboa ila lisitufunge kiasi hicho.

Hamuoni jInsi CCM hii navyotumia wapinzani hata wale ilikuwa ikiwaona ni hatari kuliko ukoma kujinufaisha kisiasa bila kujali historia zao?

Lowassa na Dr.Slaa leo CCM haiwatumii kwa faida yao?

Hamuoni hata Musiba alivyogeukwa leo hii?

Msishangae hata Kinana,Mzee Makamba na Membe kushikana mikono na Magu kabla ya 2020 ingawa leo hii mtu kama Membe anaonekana/anatajwa kuwa karibu na wapinzani.

Sisi ni wepesi kugombanishwa/kufanywa kutoaminiana wakati wenzetu ni wepesi wa kubadili gia angani mradi tu wameona kuna fursa ya kisiasa bila kujali ya jana yalikuwaje na wanajua sana kutengeneza propaganda hata za kubadili fikra za watu ambao ni wepesi kudanganyika.

Msifikiri CCM wanapenda kuona CHADEMA wanashirikiana na Zitto, bali wanapenda zaidi kuona kinyume chake.
Sioni mantiki ya ya hoja hii bwana Salary slip. Unataka kusema kuwa upinzani hawajui au hawajawahi kutumia fursa za wanasiasa wa upande wa pili ili kujinufaisha zaidi kisiasa? Kwani Slaa alitolewa wapi sio CCM, Lowasa alitolewa wapi sio CCM, Bulaya alitolewa wapi sio CCM, Marehemu mzee Kingunge alitolewa wapi sio CCM? Sumaye alitolewa wapi sio CCM? Naje kwani hawakusaidia kuiinua Chadema kwa njia moja au nyingine? Jibu ni kuwa wamesaidia pakubwa tu hata kama baadhi yao walikengeuka baadae. Kwa hoja hii hujawatendea haki wapinzani hususani Chadema na usitake kulazimisha eti lazima washirikiane na Zito. Wao ni taassisi yenye watu wenye uwezo tu wanaoweza kukaa na kuamua kama ni liablity au asset ikiwa watashirikiana au hawatoshirikiana na huyo unayempigia debe. Kugeuzia gia angani haina maana ya kumbakumba bila mpango bwana ati kwa sababu mtu mmoja anaweza kutweet au kuandika makala.
 
Sioni mantiki ya ya hoja hii bwana Salary slip. Unataka kusema kuwa upinzani hawajui au hawajawahi kutumia fursa za wanasiasa wa upande wa pili ili kujinufaisha zaidi kisiasa? Kwani Slaa alitolewa wapi sio CCM, Lowasa alitolewa wapi sio CCM, Bulaya alitolewa wapi sio CCM, Marehemu mzee Kingunge alitolewa wapi sio CCM? Sumaye alitolewa wapi sio CCM? Naje kwani hawakusaidia kuiinua Chadema kwa njia moja au nyingine? Jibu ni kuwa wamesaidia pakubwa tu hata kamq baadhi yao walikengeuka baadae. Kwa hoja hii hujawatendea haki wapinzani hususani Chadema na usitake kulazimisha eti lazima washirikiane na Zito. Wao ni taassisi yenye watu wenye uwezo tu wanaoweza kukaa na kuamua kama ni liablity au asset ikiwa watashirikiana au hawatoshirikiana na huyo unayempigia debe. Kugeuzia gia angani haina maana ya kumbakumba bila mpango bwana ati kwa sababu mtu mmoja anaweza kutweet au kuandika makala.
Msingi wa mada yangu ilikuwa ni kuwapongeza Zitto na Lissu kwa kutumia vizuri mitandao tofauti na wenzao ila wewe unaonekana labda una tatizo binafsi na zitto.

Hakuna mahali nimesema ni lazima washirikiane na Zitto ila nimeshauru umuhimu wa wapinzani kushirkiana badala ya kuruhusu kugombanishwa na kufanywa kutoaminana kwa faida ya CCM.
 
Naona juhudi za kumchafua Lissu kupitia zito zimeamza hao ni watu wawili tofauti na Tanzania inajua
 
Msingi wa mada yangu ilikuwa ni kuwapongeza Zitto na Lissu kwa kutumia vizuri mitandao tofauti na wenzao ila wewe unaonekana labda una tatizo binafsi na zitto.

Hakuna mahali nimesema ni lazima washirikiane na Zitto ila nimeshauru umuhimu wa wapinzani kushirkiana badala ya kuruhusu kugombanishwa na kufanywa kutoaminana kwa faida ya CCM.
Basi bwana naona tukubaliane kutokukubaliana.
 
Tatizo ni uwezo wa akili mkuu, Zito na Lisu IQ zao ziko juu, Mbowe, Msigwa, Lema,sugu n.k, IQ zao ziko chini mno wanatamani sana watoe uchambuzi kama Zito na Lisu tatizo ndio hivyo tena uwezo wao ni mdogo wanabaki kutoa likes tu

No mkuu..... Lissu na Zitto wako after $$ na umaarufu .... wako tayari kupotosha.
Zitto alikuwa akipewa rushwa na serikali.
Usijisahaulishe sababu za Zitto kufukuzwa chadema.
Hao uliowasifu wanajinufaisha kwa siasa.

Akina Msigwa na Sugu wanafanya siasa za kawaida bila maslahi.... na hawako after daily kikiz na vitisho
 
Back
Top Bottom