EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Nimeangalia baadhi ya majina ya wateule hawa na kinachoonekana sio tu kwamba Ukuu wa Wilaya ni maalum kwa ajili ya makada wa CCM waliokosa pa kwenda bali pia mwendelezo wa mambo ya kifisadi ndani ya Serikali ya JK. Nitatoa mfano wa wateule wawili, Wilson Elisha Nkhambaku (DC mpya wa Kishapu) na Hassan Mazala (DC mteule wa Kilombero). Mwaka 2010 Wilson Elisha Nkhambaku alitaka kugombea ubunge kwa Kupitia CCM katika Jimbo la Singida Magharibi.
Katika kura za maoni alishinda kwa kishindo cha tufani lakini kama ilivyo jadi ya chama chao, alichakachuliwa kwenye NEC na mpinzani wake aliyemshinda, Mohamed Missanga, ndiye aliteuliwa kuwa mgombea. Baada ya uchakachuaji huo, Nkhambaku alijiuzulu uanachama wa chama chao na kuhamia CHADEMA ambako tulimteua kuwa mgombea wetu wa Jimbo la Singida Magharibi. (Nitazungumzia busara zetu au ukosefu wetu wa busara katika maamuzi yetu hayo wakati mwingine!)
Baada ya kuteuliwa kama mgombea na kampeni kuanza rasmi, Wilson Elisha Nkhambaku alirubuniwa na Lazaro Nyalandu (Mbunge wa Singida Kaskazini na, tulikuja kujua baadae, mlezi wake wa kisiasa wa miaka mingi) na kurudi tena CCM. Kwenye kampeni za uchaguzi huo, Nkhambaku alitumiwa sana kwenye kampeni dhidi yangu katika Jimbo la Singida Mashariki. Wakati ule tuliambiwa kwamba aliahidiwa ama kupewa pesa nyingi sana au kupewa Ukuu wa Wilaya baada ya uchaguzi. Of course hatukupatiwa ushahidi wowote wa kuthibitisha makosa hayo wakati huo.
Uteuzi wa jana wa Wilson Elisha Nkhambaku ni ushahidi tosha kwamba JK na chama chake ni watoa rushwa za uchaguzi wa wazi wazi. Sheria yetu ya Uchaguzi inakataza mtu yeyote kurubuni mgombea ili ajitoe katika kinyang'anyiro cha uchaguzi. Kosa hilo ni moja ya matendo haramu (illegal practices) ambayo adhabu yake ni pamoja na kupigwa marufuku kugombea na kufutwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Aidha, kwa mujibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi, kosa la kutoa hongo (iwe ya kazi ama ajira, fedha, chakula, n.k) kwa mgombea au mpiga kura ni mojawapo ya matendo yaliyokatazwa (prohibited practices) na adhabu yake kwa mujibu wa sheria ni hiyo hiyo ya kufutwa kwenye Daftari na kupigwa marufuku kugombea. Kwa uteuzi huu Waziri Mkuu Pinda ajiandae kukabiliana na maswali ya papo kwa hapo juu ya uteuzi huu na kwenye mijadala itakayofuata Bungeni.
Kuhusiana na uteuzi wa Hassan Mazala, kwa wasiomfahamu bwana huyu, hadi anateuliwa kuwa DC wa Kilombero alikuwa Katibu wa Mbunge wa Singida Mjini kaka Mo Dewji, cheo ambacho amekishikilia tangu Dewji achaguliwe Mbunge mwaka 2005. Bifu langu mimi na yeye ni kwamba kwenye kesi ya kupinga uchaguzi wangu iliyomalizika mwezi uliopita Hassan Mazala ndiye aliyekuwa mgawa ngawila kwa mashahidi wa uongo waliokuja kutoa ushahidi dhidi yangu mahakamani.
Yeye mwenyewe alimpelekea shahidi namba 22 wa upande wa walalamikaji Hussein Musuna Mwangia (Katibu wa CHADEMA Jimbo la Singida Mashariki na wakala wangu kwenye uchaguzi Mkuu wa 2010) shilingi milioni tano cash ili awatolee ushahidi dhidi yangu. Bahati mbaya yao tu ni kwamba hawakujua wanadeal na wanaCHADEMA wa aina gani kwani mahela yaliliwa na wakapigwa bao mbele ya Jaji!
Siku chache tu kabla ya hukumu ya kesi yangu ya uchaguzi, Hassan Mazala na Mwigulu LM Nchemba (Mweka Hazina wa CCM) waliandaa mpango wa kumrubuni Diwani wa CHADEMA Kata ya Mungaa, Jimbo la Singida Mashariki, Bw. Matteo Alex Kiongo ahamie CCM baada ya kulipwa shilingi milioni ishirini! Mpango huo umekwama baada ya Diwani Kiongo kuwataka wampelekee mapesa hayo mchana kweupe nyumbani kwake. Hao tu ni maDC wawili wateule wa JK. Nadhani haitakuwa vibaya kwa wanabidii na wanamabadiliko kutupa taarifa zinazowahusu wengine katika orodha hii ya wateule ili tuhoji busara za uteuzi wao.
Wasalaam,
Tundu
(akiwaandikia WanaMabadiliko)
Source: wavuti - wavuti
Katika kura za maoni alishinda kwa kishindo cha tufani lakini kama ilivyo jadi ya chama chao, alichakachuliwa kwenye NEC na mpinzani wake aliyemshinda, Mohamed Missanga, ndiye aliteuliwa kuwa mgombea. Baada ya uchakachuaji huo, Nkhambaku alijiuzulu uanachama wa chama chao na kuhamia CHADEMA ambako tulimteua kuwa mgombea wetu wa Jimbo la Singida Magharibi. (Nitazungumzia busara zetu au ukosefu wetu wa busara katika maamuzi yetu hayo wakati mwingine!)
Baada ya kuteuliwa kama mgombea na kampeni kuanza rasmi, Wilson Elisha Nkhambaku alirubuniwa na Lazaro Nyalandu (Mbunge wa Singida Kaskazini na, tulikuja kujua baadae, mlezi wake wa kisiasa wa miaka mingi) na kurudi tena CCM. Kwenye kampeni za uchaguzi huo, Nkhambaku alitumiwa sana kwenye kampeni dhidi yangu katika Jimbo la Singida Mashariki. Wakati ule tuliambiwa kwamba aliahidiwa ama kupewa pesa nyingi sana au kupewa Ukuu wa Wilaya baada ya uchaguzi. Of course hatukupatiwa ushahidi wowote wa kuthibitisha makosa hayo wakati huo.
Uteuzi wa jana wa Wilson Elisha Nkhambaku ni ushahidi tosha kwamba JK na chama chake ni watoa rushwa za uchaguzi wa wazi wazi. Sheria yetu ya Uchaguzi inakataza mtu yeyote kurubuni mgombea ili ajitoe katika kinyang'anyiro cha uchaguzi. Kosa hilo ni moja ya matendo haramu (illegal practices) ambayo adhabu yake ni pamoja na kupigwa marufuku kugombea na kufutwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Aidha, kwa mujibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi, kosa la kutoa hongo (iwe ya kazi ama ajira, fedha, chakula, n.k) kwa mgombea au mpiga kura ni mojawapo ya matendo yaliyokatazwa (prohibited practices) na adhabu yake kwa mujibu wa sheria ni hiyo hiyo ya kufutwa kwenye Daftari na kupigwa marufuku kugombea. Kwa uteuzi huu Waziri Mkuu Pinda ajiandae kukabiliana na maswali ya papo kwa hapo juu ya uteuzi huu na kwenye mijadala itakayofuata Bungeni.
Kuhusiana na uteuzi wa Hassan Mazala, kwa wasiomfahamu bwana huyu, hadi anateuliwa kuwa DC wa Kilombero alikuwa Katibu wa Mbunge wa Singida Mjini kaka Mo Dewji, cheo ambacho amekishikilia tangu Dewji achaguliwe Mbunge mwaka 2005. Bifu langu mimi na yeye ni kwamba kwenye kesi ya kupinga uchaguzi wangu iliyomalizika mwezi uliopita Hassan Mazala ndiye aliyekuwa mgawa ngawila kwa mashahidi wa uongo waliokuja kutoa ushahidi dhidi yangu mahakamani.
Yeye mwenyewe alimpelekea shahidi namba 22 wa upande wa walalamikaji Hussein Musuna Mwangia (Katibu wa CHADEMA Jimbo la Singida Mashariki na wakala wangu kwenye uchaguzi Mkuu wa 2010) shilingi milioni tano cash ili awatolee ushahidi dhidi yangu. Bahati mbaya yao tu ni kwamba hawakujua wanadeal na wanaCHADEMA wa aina gani kwani mahela yaliliwa na wakapigwa bao mbele ya Jaji!
Siku chache tu kabla ya hukumu ya kesi yangu ya uchaguzi, Hassan Mazala na Mwigulu LM Nchemba (Mweka Hazina wa CCM) waliandaa mpango wa kumrubuni Diwani wa CHADEMA Kata ya Mungaa, Jimbo la Singida Mashariki, Bw. Matteo Alex Kiongo ahamie CCM baada ya kulipwa shilingi milioni ishirini! Mpango huo umekwama baada ya Diwani Kiongo kuwataka wampelekee mapesa hayo mchana kweupe nyumbani kwake. Hao tu ni maDC wawili wateule wa JK. Nadhani haitakuwa vibaya kwa wanabidii na wanamabadiliko kutupa taarifa zinazowahusu wengine katika orodha hii ya wateule ili tuhoji busara za uteuzi wao.
Wasalaam,
Tundu
(akiwaandikia WanaMabadiliko)
Source: wavuti - wavuti