Wapwa,
Ni ukweli usiopingika kuwa wanawake wamekuwa ndio kimbilio la CCM kujichotea kura lukuki tangu kupatikana kwa uhuru.
Wenzenu wanatumia wasanii kushawishi wakina mama kupigia kura chama chao, hii tumeiona tangu 2015 kwenye kampeni zao kama 'MAMA ONGEA NA MWANAO' ambayo bila shaka ilifanikiwa kwa zaidi ya asilimia 90%. na mwaka huu tena wameamua wapite godoro kwa godoro kuomba kura za akina mama na wanawake
Ningeshauri wagombea wa Chadema na ACT kwa Zanzibari watumie mbinu hizi kupata kura kutoka kwa akina mama
Ila msikengeuke, mkapata madaraka na kuwasau wanawake na akina mama, kama walivyosahauliwa na kudharauliwa ndani ya miaka 5 ya utawala wa mkoloni mweusi
Bado mna nafasi kubwa ya kubadilisha duru ya siasa ndani ya siku 57 zilizobaki.
MAMA MWOKOE MWANAO
Ni ukweli usiopingika kuwa wanawake wamekuwa ndio kimbilio la CCM kujichotea kura lukuki tangu kupatikana kwa uhuru.
Wenzenu wanatumia wasanii kushawishi wakina mama kupigia kura chama chao, hii tumeiona tangu 2015 kwenye kampeni zao kama 'MAMA ONGEA NA MWANAO' ambayo bila shaka ilifanikiwa kwa zaidi ya asilimia 90%. na mwaka huu tena wameamua wapite godoro kwa godoro kuomba kura za akina mama na wanawake
Ningeshauri wagombea wa Chadema na ACT kwa Zanzibari watumie mbinu hizi kupata kura kutoka kwa akina mama
- Nendeni na kauli mbiu, MAMA MWOKOE MWANAO
- Mnaweza kuandaa mikutano ya ndani ya wanawake hata kama ni asubuhi kabla ya mkutano wa kampeni, kuongea na akina mama na wanawake wote ndani ya mkoa husika
- Kama alivyokua anafanya Mama Lowassa 2015, mtumieni mke wa Lissu, apite mikoani kuelezea ushuhuda pamoja na kuongea na akina mama
- Baraza kuu la wanawake ( Halima Mdee na wenzako ), waanze haraka sana kupita mikoani, wajigawe kikanda. hii itasaidia kuongeza ushawishi kwa akina mama
- Tumieni madhaifu ya CCM ya udhalilishaji dhidi ya wanawake, yapo mengi sana.
- Piganieni kwa nguvu zote wagombea wote wanawake waliokatwa warudishwe, hi itaongeza kura zenu maradufu
- Kuna sababu zaidi ya 1000 za kumwambia mama amwokoe mwanae
Ila msikengeuke, mkapata madaraka na kuwasau wanawake na akina mama, kama walivyosahauliwa na kudharauliwa ndani ya miaka 5 ya utawala wa mkoloni mweusi
Bado mna nafasi kubwa ya kubadilisha duru ya siasa ndani ya siku 57 zilizobaki.
MAMA MWOKOE MWANAO