Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

kweli kabisa Dr.harith ghassany anaelezea mambo mengi sana mabaya yaliyofanywa na Nyerere 1.usanii kwenye muungano 2.kuzorotesa ustawi na maendeleo ya uislamu pale aliporatibu mpango wa kuua jumuiya ya waislam ya afrika mashariki 3.kuchochea vurugu mbalimbali africa mfano mgogoro wa biafra_nigeria , vita ya kagera 4.mgogoro wa burundi 5.kufukuza kazi wazanzibari waliokuwa wanahoji muungano....
nitaendelea
 
Katika mwendelezo wa kupinga mawazo na mfumo wa utawala wa Mwl. Nyerere. Tundu Lissu amepasua jibu ambalo wengi huwa wanaogopa kulipasua pale aliposema kuwa Mwl. Nyerere alikuwa ni "msanii wa kisiasa" kwa sababu aliyokuwa anayasema siyo yale aliyokuwa anayatenda kuhusiana na suala la Muungano. Haya ameyabainisha wakati akitoa hoja kwenye Bunge Maalum.

Mwaka 1984, Wazinzibari walipohoji Muungano, Alhaji Aboud Jumbe akafukuzwa kazi kwa amri ya Mwl. Nyerere na amewekwa kizuizini Mjimwema mpaka leo. Wolfgang Dourado akawekwa kizuizini, Bashiri Swanzy akapakiwa kwenye ndege ya kwanza akapelekwa Ghana.

Mh. Tundu Lissu aliendelea kusema, kwa vile Mwl. Nyerere alizoea vya kunyonga, kwenye Kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Mwl Nyerere alisema, 'huko nyuma baadhi ya viongozi wapinzani wa Muungano wameishawahi kusema tufanye referendum kwa Zanzibar kuhusu Muungano, tukakataa kwa sababu safi kabisa'.

Tundu Lissu anadai, Mwl. Nyerere hakukataa hoja ya Muungano kwa sababu safi kabisa, bali aliwaweka kizuizini wale waliohoji Muungano. Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uwongo na hakuweza kusema kweli.

Kitu muhimu kabisa cha kujiuliza na kufikiria. Kama kweli Mwl. Nyerere alikuwa anaishi kwa uwongo na udanganyifu, ina maana hata hati ya Muungano haipo na kama haipo, ina maana amewaingizwa 'mkenge' wananchi na hasa wanaCCM kwa kusimamia hoja ambayo kiuhalisia haipo. (Muungano wa serikali mbili).

Tukikubaliana na hoja ya Tundu Lissu, inabidi tujiulize, Kwa nini Baba wa Taifa alikuwa anaishi maisha ya uwongo na udanganyifu?. Alikuwa anafanya hivyo kwa manufaa ya nani?.

Kama hoja ya Tundu Lissu ni kweli basi hatuna budi kusema, kweli uwongo hupanda lifti wakati ukweli hutumia ngazi kuwafikia walengwa!.

Hoja hii inanipeleka kwenye angalizo la sababu ya baadhi ya wajumbe wakiongozwa na Leticia Nyerere kushauri bunge kwa nguvu zote liweke mipaka kwenye kanuni za bunge zikiwataka wabunge kutowadharirisha waasisi wa Muungano. Kumbe nyuma ya hoja zao walikuwa wanaogopa ukweli usijulikane!.


Ninadhani kuna kitu hakiko sawa kwenye baadhi ya hoja za Wabunge!.


Kinachoendelea Zanzibar na mtiririko wa hoja ya Lissu kuhusu Nyerere !.Je kuna ukweli kuwa ugonjwa wa kuishi kwa Uongo unazidi au kuelekea kuambukiza kizazi kijacho?

 
kweli kabisa Dr.harith ghassany anaelezea mambo mengi sana mabaya yaliyofanywa na Nyerere 1.usanii kwenye muungano 2.kuzorotesa ustawi na maendeleo ya uislamu pale aliporatibu mpango wa kuua jumuiya ya waislam ya afrika mashariki 3.kuchochea vurugu mbalimbali africa mfano mgogoro wa biafra_nigeria , vita ya kagera 4.mgogoro wa burundi 5.kufukuza kazi wazanzibari waliokuwa wanahoji muungano....
nitaendelea
Na utakaporudi utueleze jinsi Nyerere alivyochochea mgogoro wa Burundi na vita vya Kagera.
 
Ni huyu huyu Tundu Lisu na wenzake mpaka alikuwa anatoka mapovu kwenye kona za midomo yake kuipinga na kuikata Zanzibar, alifikia mahali pa kumtukana Mlm.Nyerere, leo hii maajabu ya Musa ndiyo amegeuka kuwa msemaji Mkuu wa Wazanzibari na kwamba anawapigania ndani ya serikali ya Muungano!

Kama kuna mtu ni opportunitist kwenye hii Dunia basi Tundu Lisu ni mmoja wao, maisha yote Bungeni amekuwa akingombana na Wabunge wa Zanzibar na kuwakebehi leo hii kageuka kuwa mtetezi wao, kweli Duniani kuna watu na viatu!
 
Ni huyu huyu Tundu Lisu na wenzake mpaka alikuwa anatoka mapovu kwenye kona za midomo yake kuipinga na kuikata Zanzibar, alifikia mahali pa kumtukana Mlm.Nyerere, leo hii maajabu ya Musa ndiyo amegeuka kuwa msemaji Mkuu wa Wazanzibari na kwamba anawapigania ndani ya serikali ya Muungano!

Kama kuna mtu ni opportunitist kwenye hii Dunia basi Tundu Lisu ni mmoja wao, maisha yote Bungeni amekuwa akingombana na Wabunge wa Zanzibar na kuwakebehi leo hii kageuka kuwa mtetezi wao, kweli Duniani kuna watu na viatu!

Ni bora lissu kuliko wale waliofuta uchaguzi zanzibar baada ya kuona wameshindwa.
 
Jamani huyo Toto Tundu Lissu msameheni bure tu yeye ni mtu wa mihemko tu,kaingizwa chaka na kushadidia kuwa eti Baba wa Taifa alianzisha vita na Uganda kwa sababu zake mwenyewe za kisanii labda nadhani Kipindi hicho alikuwa hajazaliwa so hajui jinsi vita ilivyoanza,hajui jinsi tulivyoanza kufundishwa namna ya Kuchimba Mahandaki ya L,Y na jinsi ya kukimbilia humo once tukisikia miungurumo mikali ya ndege za kivita,mafunzo ya ulinzi wa mgambo makazini kuchukua Tahadhali kwa mtu yeyote asiyejulikana na mengine meengi.
 
Jamani huyo Toto Tundu Lissu msameheni bure tu yeye ni mtu wa mihemko tu,kaingizwa chaka na kushadidia kuwa eti Baba wa Taifa alianzisha vita na Uganda kwa sababu zake mwenyewe za kisanii labda nadhani Kipindi hicho alikuwa hajazaliwa so hajui jinsi vita ilivyoanza,hajui jinsi tulivyoanza kufundishwa namna ya Kuchimba Mahandaki ya L,Y na jinsi ya kukimbilia humo once tukisikia miungurumo mikali ya ndege za kivita,mafunzo ya ulinzi wa mgambo makazini kuchukua Tahadhali kwa mtu yeyote asiyejulikana na mengine meengi.

Siyo Tundu Lissu tu,hata mkapa aliwahi kusema moja ya mambo yaliyoangusha uchumi ni vita "visivyo na sababu" na nyerere alikuwepo hai.
 
Jamani huyo Toto Tundu Lissu msameheni bure tu yeye ni mtu wa mihemko tu,kaingizwa chaka na kushadidia kuwa eti Baba wa Taifa alianzisha vita na Uganda kwa sababu zake mwenyewe za kisanii labda nadhani Kipindi hicho alikuwa hajazaliwa so hajui jinsi vita ilivyoanza,hajui jinsi tulivyoanza kufundishwa namna ya Kuchimba Mahandaki ya L,Y na jinsi ya kukimbilia humo once tukisikia miungurumo mikali ya ndege za kivita,mafunzo ya ulinzi wa mgambo makazini kuchukua Tahadhali kwa mtu yeyote asiyejulikana na mengine meengi.
zimu wa Mwalimu unamtafuna Lissu, haji aitetee nchi yake au mabwana wanaomtuma.
Haya mabomu yanarindima sasa, hata handaki hajui kuchimba!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom