Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Hivi sasa Mashambulizi makali yanaelekezwa kwa Tundu Lissu.Kila hatua anayopiga au kauli anayoitoa inafuatiliwa na kufanyiwa upembuzi na watawala.
Watawala wamejifunza na kutambua hatari ya hatua na kauli za Lissu;Wako bize kujibizana naye moja kwa moja ama kwa kutumia mawakala wao waliowaajiri kwa kazi hiyo.Ukweli ni kwamba,Lissu si hatari kwa taifa hili,bali ni hatari kwa watawala.Watawala watapita,taifa litaendelea kuwepo.
Ukifuatilia Saikolojia ya watawala na hata lugha yao ya picha wanapohutubia wanaotuonesha jambo moja tu:Tundu Lissu ni mwana siasa mwenye nguvu na uwezo katika historia ya upinzani nchini.Mapito aliyopitia kufikia alipo sasa ndicho kilichomzidishia nguvu na uwezo.Lissu amevuka viwango vya mapambano.
Kielelezo cha hili ni heshima anayopewa duniani na coverage inayofanywa na media za kimataifa ili dunia imsikilize.Huyu mwana siasa anayesikilizwa sana na duniani anawapa taabu watawala.Watawala wanataabika na kuteseka.Naam,wataendelea kutabika na kuteseka kwa sababu Tundu Lissu amenusuruka kimuijiza ili kuangusha tawala.
Watu waliopona kimuujiza kama Tundu Lissu Kupona kwao si kwa ajili kuishi kwa ajili yao na familia zao bali ni kwa ajili ya maisha ya kupambana ili ku- achieve Mission yenye faida kwa wengi.
Tundu Lissu anajitambua;kuanzia jinsi alivyojitolea kuishi maisha kufanya struggle.Mapito ya kukamatwa na kuwekwa ndani ni mengi.Lakini Yale Mapito ya political assassination yalikuwa makubwa kwani alikuwa anapoteza maisha.Mungu amekataa asife.
Siku fulani kabla ya kushambuliwa Dodoma Lissu aliwahi sema "tutanyamza tukiwa wafu"
Baada ya kushambuliwa,kule Nairobi alipozinduka kauli ya kwanza aliyoongea ni " I have survived to tell the tale" yaani "nimenusurika ili niwaambie hadithi" (kwa tafsiri yangu).
"To tell tale" bila shaka ni kuendelea na mapambano.Kwa hiyo,Lissu anajua kazi iliyoko mbele yake na hana mpango wa kuiacha kwa sababu yoyote ile.Hiki ndicho kinachotesa watawala na vibaraka wao.
Haya ni maneno ya mtu jasiri yanayothibitisha Lissu ana mambo mengi kwa ajili ya taifa hili.Kunusurika kwake haikuwa bure.Kuna kazi mbele yake.Sasa hakuna wa kumzuia maana Mungu amekataa asife kutokana na kushambuliwa 2017.Hiki ndicho kinachowatesa watawala na vibaraka wao.
Mwanahabari Huru
Magomeni mwembechai
Watawala wamejifunza na kutambua hatari ya hatua na kauli za Lissu;Wako bize kujibizana naye moja kwa moja ama kwa kutumia mawakala wao waliowaajiri kwa kazi hiyo.Ukweli ni kwamba,Lissu si hatari kwa taifa hili,bali ni hatari kwa watawala.Watawala watapita,taifa litaendelea kuwepo.
Ukifuatilia Saikolojia ya watawala na hata lugha yao ya picha wanapohutubia wanaotuonesha jambo moja tu:Tundu Lissu ni mwana siasa mwenye nguvu na uwezo katika historia ya upinzani nchini.Mapito aliyopitia kufikia alipo sasa ndicho kilichomzidishia nguvu na uwezo.Lissu amevuka viwango vya mapambano.
Kielelezo cha hili ni heshima anayopewa duniani na coverage inayofanywa na media za kimataifa ili dunia imsikilize.Huyu mwana siasa anayesikilizwa sana na duniani anawapa taabu watawala.Watawala wanataabika na kuteseka.Naam,wataendelea kutabika na kuteseka kwa sababu Tundu Lissu amenusuruka kimuijiza ili kuangusha tawala.
Watu waliopona kimuujiza kama Tundu Lissu Kupona kwao si kwa ajili kuishi kwa ajili yao na familia zao bali ni kwa ajili ya maisha ya kupambana ili ku- achieve Mission yenye faida kwa wengi.
Tundu Lissu anajitambua;kuanzia jinsi alivyojitolea kuishi maisha kufanya struggle.Mapito ya kukamatwa na kuwekwa ndani ni mengi.Lakini Yale Mapito ya political assassination yalikuwa makubwa kwani alikuwa anapoteza maisha.Mungu amekataa asife.
Siku fulani kabla ya kushambuliwa Dodoma Lissu aliwahi sema "tutanyamza tukiwa wafu"
Baada ya kushambuliwa,kule Nairobi alipozinduka kauli ya kwanza aliyoongea ni " I have survived to tell the tale" yaani "nimenusurika ili niwaambie hadithi" (kwa tafsiri yangu).
"To tell tale" bila shaka ni kuendelea na mapambano.Kwa hiyo,Lissu anajua kazi iliyoko mbele yake na hana mpango wa kuiacha kwa sababu yoyote ile.Hiki ndicho kinachotesa watawala na vibaraka wao.
Haya ni maneno ya mtu jasiri yanayothibitisha Lissu ana mambo mengi kwa ajili ya taifa hili.Kunusurika kwake haikuwa bure.Kuna kazi mbele yake.Sasa hakuna wa kumzuia maana Mungu amekataa asife kutokana na kushambuliwa 2017.Hiki ndicho kinachowatesa watawala na vibaraka wao.
Mwanahabari Huru
Magomeni mwembechai