Tundu Lissu Mungu anakupenda hebu mtumikie...

m2020

JF-Expert Member
Jul 10, 2016
979
1,353
Mheheshimiwa Tundu Lisu,

Tambua kuwa, kuokolewa kutoka katika shambulizi kubwa lenye harufu nzito ya umauti na hatimaye kupata afya, unapaswa kumtumikia mungu wakati wote uliuobaki kuishi duniani badala ya kuzunguka na kulalamika na kuonyesha bado unashindana na wanadamu.

Nakusihi ndugu yangu sisi binadamu hatuna wema kaka rudi nyumbani TANZANIA na kufanya kazi za kitume na kinabii.
 
Kazi anayoifanya TL ni takatifu. Kazi ya kumwumbua shetani ni takatifu. Kazi anayoifanya inaweza kusaidia wengine wasiendelee kushambuliwa, wasitekwe, wasiuawe na kutupwa kwenye viroba, wasifungwe ovyo kwa uonevu.

Huo ndiyo ukristo wa kweli. Yaani kuwa tayari kuteseka, kufungwa na hata kufa kwaajili ya wengine. Walifanya hivyo akina Petro, Paulo, Bartholomayo, Yakobo, n.k.

Ukristo wa kweli ni kuwa tayari kujitoa sadaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu anaitwa ni Bwana wa Majeshi.
Hapendi watu legelege, waoga waoga, wanafki,
 
Kama anachofanya hakina unafiki ndani yake hata nukta,basi ndio utumishi wenyewe kwa Mungu.
 
Kumtumiakia Mungu ni mpaka Mungu mwenyewe amwite kufanya kazi
yake.
Lissu hawezi kujiamlia kuwa mtumishi wa Mungu.Na hapo ndo mitume na manabii mnapofeli na kudondika kabisa.Maana mnafanya kazi kwa akili zenu bila kumshirikisha Mungu.
Tundu lissu ni kwa ajili ya kuwaongoza watu wa Mungu sio Kumtumikia Mungu.kama ni kumtumikia Mungu basi itajulikana tu baadae maadam anaishi tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kushika amri za Mungu ndio kumtumikia Mungu. Lisu anatetea haki yake unadhani hamtumikii Mungu.

Nadhani hujui maana ya kumtumikia Mungu..Kwa ufupi. Kufanya kazi na kuwatumikia watu ndio kumtumikia Mungu. Iwe Mwalimu, Dereva, Daktari na wanasheria wote wanamtumikia Mungu.

Kadanganye wajinga huko
 
Kumutumikia Mungu siyo lazima upande madhabahuni, kuna aina nyingi za kumtumikia Mungu.
 
Kazi anayoifanya Tundu Lissu kwa sasa ni zaidi ya utume..
Tena anaifanya kwa moyo mmoja bila hila kama viongozi wengi wa dini tulionao sasa ...
 
Mheheshimiwa Tundu Lisu,

Tambua kuwa, kuokolewa kutoka katika shambulizi kubwa lenye harufu nzito ya umauti na hatimaye kupata afya, unapaswa kumtumikia mungu wakati wote uliuobaki kuishi duniani badala ya kuzunguka na kulalamika na kuonyesha bado unashindana na wanadamu.

Nakusihi ndugu yangu sisi binadamu hatuna wema kaka rudi nyumbani TANZANIA na kufanya kazi za kitume na kinabii.
Leo mumecharuka na kofia ya unabii kumtisha Lissu. Mfalme Daudi anakumbukwa kwa sifa moja kubwa kuwa alimuua Goliath. Go go go Lissu bring Goliath down.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom