Tundu Lissu: Miradi mikubwa ya Hayati Magufuli ni majanga yajayo ya kiuchumi

Wakati ATCL ilipokuwa imekufa watu walikuwa wanasafiri vizuri na ndege tena kwa bei nafuu.
ATCL hajaongeza tija yoyote kwenye usafiri wa ndege nchini.
Mataifa chungu nzima yaliyoendela na yanayojielewa yameiachia hii biashara sekta binafsi.
Utaniambia walikuwepo Fastjet. Hao hawakuwa na mtandao mpana. Ni kampuni ya nje ilichungulia fursa kwenye route chache wakafanya biashara kwenye hizo route. Wengi wa waliokuwa wadau wa route hizo ndio wanaowasifia . Atcl wana mtandao mpana zaidi..Hii sio opinion ni fact tu hata kwenye mitandao unaweza kuiona..
Wanahitaji kuboresha uendeshaji na kuwa aina ya ndege na idadi yenye tija.
 
Huyo Lissu anajulikana kwa mihemuko....
akili yake bado ya kisekondari....
yy kila kitu cha Magu anapinga....
muda utatuambia ukweli....
Lissu ni wa kupuuza tu hana jipya...
tulimwambia, siku Magu akisepa na siasa zake zitakomea hapo.
We jamaa ulikuwa mtu smart sana humu jamvini! Nini kilukupata mpaka umekuwa mtu wa hovyo iv?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
SAMIA AJICHUNGUZE MWENYEWE NA CCM YAKE? you are not srious broo!
Ndiyo maana huwa nasema Tanzania hatuna upinzani kwa sasa tumebaki na wachumia tumbo na waimba taarabu tu wa kisiasa. Badala ya upinzani kuja na plan B kwamba wao wakipewa nafasi ya kuongoza hii nchi hiyo miradi mikubwa wataendelezaje kwa njia nzuri zaidi ili ilete tija kwa taifa wao wanalaumu tu. Je ni kweli hatuitaji umeme wa uhakika? Hatuhitaji usafiri wa reli wa kisasa?, Hatuhitaji usafiri wa ndege (miaka ya 70s-80s wakati wa Nyerere tulikuwa na ndege 11). Ukiona wapinzani wamebaki kuwa waimba taarabu na mapambio ya kisiasa huwa inasikitisha sana maana hakuna tunamaini madhubuti la kuiondoa CCM madarakani.
 
Muda sasa Umefika wa kujua Lissu anazungumza kama nani? Mwanaharakati? Mbunge? Diwani? au mchambuzi wa Masuala ya Siasa?

Sidhani kwa style anayoenda nayo Lissu, Mbowe atarudia makosa tena kumpa "NAFASI"..ni wakati wa Mbowe kama Mbowe sasa aingie uwanjani 2025
 
Tukiwa na watanzania kama wewe Zaidi ya Million 30. Hii nchi tutaishia kuuza nyanya na mboga mboga tu maana ndio tunaweza fanya na ikakamilika.

Kama unaona kabisa kwamba miradi haitakamilika basi wewe utakuwa unakula ugali wa mama yako. Huna jipya.
utakuwa na kichaa cha mimba
 
Unaweza kumpuuza wewe wala hakuna wa kukushangaa maana hii ndiyo maana ya "Uhuru Wa mawazo" na "Uhuru wa kuchagua"..

Sisi wengine tunamfuata, tunamwamini na kukitilia maanani na umakini kila anachokizungumza...

Tena kwa habari ya Mwendazake usituambie kabisa. Mwache aende zake, alikuwa ni muharibifu tu huyo. Hana legacy yoyote ktk jamii iliyostaarabika...
Mbona huyo Lissu pia ameshirikiana na Mbowe kuharibu michango ya wabunge wa chadema kwa matumizi yasiyoeleweka? Chademu haiweza kuicheka CCM, tofauti ni kwamba CCM ipo madarakani na chedemu wanasubiria mkono udondoke waokote!
 
Ameandika hivyo kupitia twitter:

Nimemsikiliza Prof. Mussa Assad kuhusu ufisadi katika taasisi za umma. Miradi mikubwa ya Magufuli, ndege za ATCL, SGR, Stiegler's Gorge, n.k., ni majanga yajayo ya kiuchumi. Namshauri Rais Samia kuunda Tume ya Uchunguzi kabla mambo hayajaharibika zaidi.
Huo ndio ukweli.
 
Ni hoja nzuri lakini inahitaji maelezo yenye mantiki ili walio wengi tuweze kuelewa.......

Ufisadi kwenye miradi ni jambo lingine na majanga yake kiuchumi ni jambo lingine..........mimi kwa mtazamo wangu ukiweka kando makando kando ya ufisadi kwenye miradi hiyo lakini mingi inatija kiuchumi.......miradi inatakiwa ichunguzwe na kusafishwa mianya yote ya ufisadi ili iendelee kwa manufaa ya taifa kwa ujumla........

NB;
TANZANIA NI YETU SOTE......NA HAPA NDIO TUMEFIKA......
 
Lissu ameanza siasa zamani sana, kwa wanaomfahamu alianza kukinzana na Hayati Benjamin William Mkapa, enzi za uwekezaji wa madini ya dhahabu, (tafuta article inaitwa "The golden opportunity", utajua Lissu hakuanza kupigia kelele rasirimali wakati wa Hayati JPM, mara zote amekuwa against maamuzi yanayoumiza nchi, ukitafakari kwa kina utagundua the guy is smart, ila baadhi ya wanaomsikiliza (kama wewe) hawamuelewi kutokana na uwezo mdogo!



Sent from my Z9 using JamiiForums mobile app
Wewe ni chizi kama yeye tu. Kama alipigania rasilimali za nchi ilikuwaje awe upande wa maadui wakati magufuli alipoamua kuvunja mikataba ya kitapeli ya wazungu badala ya kushirikiana naye?

Unakuwa mnafiki kwa manufaa ya nani? Mmemwua magufuli kwa sababu hizohizo za madini na lisu ndiye mhusika mkuu akitumia mabwana zake wanaomla 071.

Sasa ni hivi, asahau, haitatokea aje awe rais wa nchi hii kwa kuwa Watanzania wenye akili washamfahamu ndani nje na maigizo yake ya kupigwa risasi kushoto akaumia kulia.
 
Ameandika hivyo kupitia twitter:

Nimemsikiliza Prof. Mussa Assad kuhusu ufisadi katika taasisi za umma. Miradi mikubwa ya Magufuli, ndege za ATCL, SGR, Stiegler's Gorge, n.k., ni majanga yajayo ya kiuchumi. Namshauri Rais Samia kuunda Tume ya Uchunguzi kabla mambo hayajaharibika zaidi.
Nakubaliana na Tundu Lissu kwa 100% kuhusu kuunda tume ya kutathmini status ya miradi na kushauri upi tuendelee na upi usubiri.
Kwenye taaluma ya uchumi na biashara inasisitizwa kuwa lazima kila mradi unaofanywa uwe na;
(1) Upembuzi Yakinifu (Feasibility Study)
Hii hukuonyesha kama mradi unaweza kuwapo kijamii na kiu humu (social and economic viability)

(2) Mpango Kazi (Business Plan).
Hii hukuonyesha utapata wapi fedha za mradi, utazalisha nini, utauza wapi, menejimenti itakuwaje na vihatarishi ni vipi na namna vitakavyo epukika

Sasa wakati Mwendazake anaanzisha STIGLERS Gorge, tayari SGR ilikuwa imezinduliwa kule Pugu. Then Mwendazake akajitumbukiza kwenye ma bombardier, barabara za Ubungo, flyover, Busisi nk.

Vingi kati ya hivyo havikuwana feasibility study wala businnes plan hasa Stiglers, ATCL na Busisi.

Kwa hiyo ili kuleta utulivu wa mapato na matumizi ya nchi, huku wafanyakazi wakilipwa stahiki zao lazima Rais SSH ashauriwe nini kianze kwanza, kipi kifuate na kipi kije mwishoni au kifutwe kabisa
 
Wewe ni chizi kama yeye tu. Kama alipigania rasilimali za nchi ilikuwaje awe upande wa maadui wakati magufuli alipoamua kuvunja mikataba ya kitapeli ya wazungu badala ya kushirikiana naye?

Unakuwa mnafiki kwa manufaa ya nani? Mmemwua magufuli kwa sababu hizohizo za madini na lisu ndiye mhusika mkuu akitumia mabwana zake wanaomla 071.

Sasa ni hivi, asahau, haitatokea aje awe rais wa nchi hii kwa kuwa Watanzania wenye akili washamfahamu ndani nje na maigizo yake ya kupigwa risasi kushoto akaumia kulia.
Kama umefunga mwezi Ramdhani, tulia mpaka adhana, pengine njaa inakusumbua. Kama ni mkristu kunywa maji uteremshe munkali. Wewe humjui Tundu Lissu, unachojuwa ni kutukana. Bahati nzuri hakuna matusi mapya ambayo hatujawahi kuyasikia
 
Back
Top Bottom