Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,780
Tundu Lissu amesema mali isipokombolewa baada ya kuzuiliwa, itapigwa mnada ili kufidia deni linalodaiwa. Kwa muda gani, inatagemea mkataba Serikali uliongia.
Tundu Lissu alikuwa anajibu swali la mdau aliuliza nini kitatokea kama Serikali itashindwa kulipa deni lililopelekea ndege kukamatwa.
Lissu amesema Serikali inadhani inaweza kuvunja sheria/mikataba na kusiwe na consequences wakati imeingia mikataba ya kimataifa, Lissu amedai Serikali inajiona ina nguvu ndani ya nchi na kudhani inazo nguvu hizohizo nje ya nchi matokeo yake wawekezaji wanasubiri mali zitoke nje ya nchi kwakuwa hawawezi kukamata mali za kidiplomasia kama majengo ya ubalozi.
Kuhusu mtu aliyefariki kushtakiwa, amesema kama kesi ya jinai, kesi za jinai ni kwaajili ya walio hai. Ikiwa ni madai wanaweza kushtakiwa warithi lakini baadhi ya madai yanakufa na aliyekosea.
Tundu Lissu alikuwa anajibu swali la mdau aliuliza nini kitatokea kama Serikali itashindwa kulipa deni lililopelekea ndege kukamatwa.
Lissu amesema Serikali inadhani inaweza kuvunja sheria/mikataba na kusiwe na consequences wakati imeingia mikataba ya kimataifa, Lissu amedai Serikali inajiona ina nguvu ndani ya nchi na kudhani inazo nguvu hizohizo nje ya nchi matokeo yake wawekezaji wanasubiri mali zitoke nje ya nchi kwakuwa hawawezi kukamata mali za kidiplomasia kama majengo ya ubalozi.
Kuhusu mtu aliyefariki kushtakiwa, amesema kama kesi ya jinai, kesi za jinai ni kwaajili ya walio hai. Ikiwa ni madai wanaweza kushtakiwa warithi lakini baadhi ya madai yanakufa na aliyekosea.