Tundu Lissu: Magufuli ni cross breed kati ya Sokoine na Mrema

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
May 25, 2015
6,482
20,425
Akiongea katika kipindi cha channel 10,mheshimiwa Tundu Lissu amedai rais Magufuli ni breed kati ya waziri mkuu mstaafu,marehemu Sokoine na waziri wa mambo ya ndani wa kipindi hicho ndg Mrema.

Alipoulizwa kwanini anamfananisha Magufuli na Sokoine ndugu Lissu alidai "Magufuli na Sokoine wanafanana kwa maana wote hawana utaratibu wa kufuata utawala wa sheria kabisa" huku akiendelea kusema "Magufuli na Mrema wote wanafanana kwa kuwa na tabia ya kucheza na vyombo vya habari,akimaanisha kwamba hawa wawili ni watu wanaopenda kuwa kwenye front pages na headlines kwenye magezeti (ujiko),wakifanya vitu hivi kwa manufaa ya vyombo vya habari".

Mdau sijui una lipi la kusema kumhusu hili?
 
Last edited by a moderator:
Waziri wa Magufuli aliniacha hoi siku ile alipoenda kufunga geti pale wizarani saa moja na nusu asubuhi huku kamera za waandishi wa habari zikiwa zinammulika.

Nikashangaa shangaa sana, hao waandishi wa habari na wapiga picha walijuaje kwamba huyu Waziri atalifunga hilo geti?
 
Waziri wa Magufuli aliniacha hoi siku ile alipoenda kufunga geti pale wizarani saa moja na nusu asubuhi huku kamera za waandishi wa habari zikiwa zinammulika.

Nikashangaa shangaa sana, hao waandishi wa habari na wapiga picha walijuaje kwamba huyu Waziri atalifunga hilo geti?
Acha uongo...
 
Akiongea katika kipindi cha channel 10,mheshimiwa Tundu Lissu amedai rais Magufuli ni breed kati ya waziri mkuu mstaafu,marehemu Sokoine na waziri wa mambo ya ndani wa kipindi hicho ndg Mrema.
Alipoulizwa kwanini anamfananisha Magufuli na Sokoine ndugu Lissu alidai "Magufuli na Sokoine wanafanana kwa maana wote hawana utaratibu wa kufuata utawala wa sheria kabisa" huku akiendelea kusema "Magufuli na Mrema wote wanafanana kwa kuwa na tabia ya kucheza na vyombo vya habari,akimaanisha kwamba hawa wawili ni watu wanaopenda kuwa kwenye front pages na headlines kwenye magezeti (ujiko),wakifanya vitu hivi kwa manufaa ya vyombo vya habari"
Mdau sijui una lipi la kusema kumhusu hili?

Kama alidhani anamponda JPM kwa kumfananisha na Sokoine, huenda akwa amempandisha chati bila kujua.
 
Akiongea katika kipindi cha channel 10,mheshimiwa Tundu Lissu amedai rais Magufuli ni breed kati ya waziri mkuu mstaafu,marehemu Sokoine na waziri wa mambo ya ndani wa kipindi hicho ndg Mrema.
Alipoulizwa kwanini anamfananisha Magufuli na Sokoine ndugu Lissu alidai "Magufuli na Sokoine wanafanana kwa maana wote hawana utaratibu wa kufuata utawala wa sheria kabisa" huku akiendelea kusema "Magufuli na Mrema wote wanafanana kwa kuwa na tabia ya kucheza na vyombo vya habari,akimaanisha kwamba hawa wawili ni watu wanaopenda kuwa kwenye front pages na headlines kwenye magezeti (ujiko),wakifanya vitu hivi kwa manufaa ya vyombo vya habari"
Mdau sijui una lipi la kusema kumhusu hili?


Tundu Lisu ni narcist ana kila dalili hizo yeye kila mtu anamuona hafai isipokuwa yeye tu, nakumbuka kuna wakati alimsema sana Mlm.Nyerere kwamba ni mtu muongo na aliyeishi kwa kusema uongo, leo hii tena anamsema W.Mkuu Sokoine sasa kuna kitu mtu unajiuliza kwa maana nijuavyo mimi hawa ndiyo viongozi wawili (Mlm. na Solkoine) ambao sehemu kubwa ya WatanZania wanaowaona kama ndiyo tunu ya nchi kwanza siyo WatanZania tu bali Afrika kwa ujumla kila mahali ukisema Nyerere watu wanamkubali, Uganda mpaka wamefikia kutaka kumfanya mtakatifu lkn Tundu Lisu anasema ni muongo na hakuna alichofanya, sasa watu kama hawa akina Tundu Lisu hata kama mnapenda chama chenu ni wa kuwaangalia sana na kuwaauliza maswali magumu!

Kwa maana Tundu Lisu huyo huyo ambaye leo hii anamwita Mlm.Nyerere muongo ndiyo aliyesema kwamba Lowasa ni fisadi na anapaswa kuwa Jela leo hii anarudi na kusema kwamba Lowasa siyo fisadi na alisingiziwa, sasa hapa kuna tatizo na huyu mtu, iko siku na inakuja atakuja pia kuwageuka chadema!

Kwa maana anaumwa ugonjwa wa akili ni narcist kwamba anajiona na anaamini kwamba ktk nchi nzima ya TanZania yeye ndiyo 100% na yeye ndiyo mjuaji wa kila kitu na kila asemacho yeye ndiyo sawa, sasa hii siyo tabia ya kiongozi bora, CHADEMA kuweni macho na Tundu Lisu ni narcist hili mtakuja kulimbuka!
Tundu Lisu anadharau sana WatanZania anaamini kwamba anaweza akasema chochote akawaambia WatanZania chochote kile hata kama ni cha kutunga halafu baadaye akaja akawaambia vingine tena na kugeuza maneno!
Ogopa sana binadamu asiye na self critic na asiyeweza kukubali kosa na kurudisha maneno aliyoyasema kwa maana kwake yeye wengine wote ni takataka na hawajui kitu na anaweza kuwachezea anavyotaka!

Na watu kama hawa jaribuni kutafuta familia yake muwaulize watawapa majibu mazuri ambayo labda yatawasaidia kuhusu huyu mtu, ni mgonjwa wa akili, fanyeni haraka kabla hajawagharimu!
 
Last edited:
Nimemsikiliza Tundulisu alipokuwa akihojiwa channel ten hakika kwa sasa ameishiwa hoja na nadhani ndyo mwanzo wake wa kupotea katika siasa, yan jimbo lake halina shule za kutosha na madarasa kwa zaid ya miaka mitano unakuja kwenye media na kumlaumu JPM hivi ww mbunge umefanya nini kama ww sio sehemu ya tatizo? Kuna aina ya wabunge wapaswa kupimwa kwanza kabla hawajachaguliwa huyu nae ni jipu pia.
 
Back
Top Bottom