Simba mnyama
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 348
- 129
Mbunge machachari, msema ukweli na muwazi, mheshimiwa Tundu Lissu amesema bungeni jioni hii kuwa madaktari hwakupaswa kufukuzwa bila kuwapa nafasi ya kujitetea kama inasema sheria. Huu ni uonevu mkubwa. Aidha Lissu ameponda kitendo cha kufukuza madaktari hao ambao wamesomeshwa kwa kiasi kikubwa kabisa cha pesa za walipa kodi wa nchi hii na matokeo yake baadhi yao wamekimbia na kwenda nchi nyingine ambako wanalipwa vizuri. Mbunge huyu amesema kuwa inabidi serikali ibadilike na iwalipe vizuri ili kuwafanye madaktari kufanya kazi hapa nchini.
Aidha, Mheshimiwa Tundu ameponda kufungiwa gazeti la Mwanahalisi ambalo kabla ya kuandika chochote hufanya kwanza utafiti. Sauti ya watanzania ni kama imefungwa.
Aidha, Mheshimiwa Tundu ameponda kufungiwa gazeti la Mwanahalisi ambalo kabla ya kuandika chochote hufanya kwanza utafiti. Sauti ya watanzania ni kama imefungwa.