Tundu Lissu: Kuna mtu ana ugonjwa mbaya wa kutaka kusifiwa muda wote hata kwa mambo ambayo sio ya kweli

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,898
Kuna mtu ana ugonjwa mbaya wa kutaka kusifiwa muda wote hata kwa mambo ambayo sio ya kweli. Ugonjwa huu nauita 'Attention Deficiency Syndrome' au ADS. Nitoe mfano halisi wa dalili za ADS.

Leo Joe Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa Kanda Emmanuel Masonga wameachiliwa huru baada ya kukaa gerezani miezi mitatu kwa chuki na hila za kisiasa tu.

Mara ghafla tunawasikia wapambe Magufuli wakisema Sugu na Masonga wameachiliwa kwa msamaha wa Rais na jina la Bwana Mtukufu Rais lihimidiwe!!!

Kama kweli wameachiliwa kwa msamaha wa Rais, kwa nini imechukua wiki mbili tangu tarehe 26 Aprili inayodaiwa kuwa ndio siku ya msamaha huo???

Kwa nini Magufuli mwenyewe hakusema ametoa msamaha huo kwa Sugu na Masonga???

Kama kuna mtu anafikiri hilo haliwezekani, akumbuke Rais Ali Hassan Mwinyi alifanya nini kwa wanajeshi waliofungwa maisha kwa kujaribu kuipindua Serikali ya Mwalimu Nyerere.

Mwinyi alitoa taarifa rasmi kwamba amewapa msamaha wahaini hao. Hiyo ilikuwa mwaka '95 kabla ya Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi.

Tuendelee. Kila mfungwa, ukiachia waliofungwa kipindi kirefu kwa makosa makubwa au waliohukumiwa kifo, anastahili kupata automatic remission ya theluthi moja ya kifungo chake.

Remission hii ilikuwa inawahusu Sugu na Masonga vile vile. Je, hawakuipata??? Kama wameipata kama inavyotakiwa na sheria, hiki kinachoitwa msamaha wa Rais ni kitu gani kama sio uthibitisho wa ugonjwa wa ADS???

Lissu, Ubelgiji,
10 Mei 2018.
 
Kuna mtu ana ugonjwa mbaya wa kutaka kusifiwa muda wote hata kwa mambo ambayo sio ya kweli. Ugonjwa huu nauita 'Attention Deficiency Syndrome' au ADS. Nitoe mfano halisi wa dalili za ADS.

Leo Joe Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa Kanda Emmanuel Masonga wameachiliwa huru baada ya kukaa gerezani miezi mitatu kwa chuki na hila za kisiasa tu.

Mara ghafla tunawasikia wapambe Magufuli wakisema Sugu na Masonga wameachiliwa kwa msamaha wa Rais na jina la Bwana Mtukufu Rais lihimidiwe!!!

Kama kweli wameachiliwa kwa msamaha wa Rais, kwa nini imechukua wiki mbili tangu tarehe 26 Aprili inayodaiwa kuwa ndio siku ya msamaha huo???

Kwa nini Magufuli mwenyewe hakusema ametoa msamaha huo kwa Sugu na Masonga???

Kama kuna mtu anafikiri hilo haliwezekani, akumbuke Rais Ali Hassan Mwinyi alifanya nini kwa wanajeshi waliofungwa maisha kwa kujaribu kuipindua Serikali ya Mwalimu Nyerere.

Mwinyi alitoa taarifa rasmi kwamba amewapa msamaha wahaini hao. Hiyo ilikuwa mwaka '95 kabla ya Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi.

Tuendelee. Kila mfungwa, ukiachia waliofungwa kipindi kirefu kwa makosa makubwa au waliohukumiwa kifo, anastahili kupata automatic remission ya theluthi moja ya kifungo chake.

Remission hii ilikuwa inawahusu Sugu na Masonga vile vile. Je, hawakuipata??? Kama wameipata kama inavyotakiwa na sheria, hiki kinachoitwa msamaha wa Rais ni kitu gani kama sio uthibitisho wa ugonjwa wa ADS???

Lissu, Ubelgiji,
10 Mei 2018.

Na yeye Lissu ana ugonjwa kwa kuingilia kila kitu na kujidai mjuaji kwa kila jambo. Augue pole.
 
Ndugu Lissu hayo maradhi uliyoyataja ninkweli yapo, na waathirika wengi ni wanasiasa na waliotajirika haraka ama kifisadi.

Hata wewe mwenyewe umeathirika sana na hayo maradhi, you love attention and praises . Tuna msemo " Nyani hapni kundule"
 
Nyani haoni kinyeo chake!!!
Mwishowe nitaamini maneno ya Barbarosa kuwa Lissu akiona kuna tukio ambalo litamfanya asahaulike anatafuta namna yoyote kuandika chochote ili asisahaulike.
Leo amejua watu tuko busy na mheshiwa "Sugu" kuwa huru kwa hiyo na yeye kaona asibaki nyuma.
Mapovu ruksa.
Well said
Huyo mtu zama zake kwishney kabisa masikini
 
Ndugu Lissu hayo maradhi uliyoyataja ninkweli yapo, na waathirika wengi ni wanasiasa na waliotajirika haraka ama kifisadi.

Hata wewe mwenyewe umeathirika sana na hayo maradhi, you love attention and praises . Tuna msemo " Nyani hapni kundule"
Hahahaha
 
49 Reactions
Reply
Back
Top Bottom